TBT ya kibabe: Mabasi na vyombo vya usafiri Tanzania

TBT ya kibabe: Mabasi na vyombo vya usafiri Tanzania

Mzee hauna picha za basi ziliitwa Ilanga moto?? Hatari yake ilikua balaa. Walifungiwa wakati wa lile zoezi la Speed Governor.
 
Mwaka 2004 nilisafiri na basi la SCANDINAVIA kutoka Mwanza-Musoma-Silali-Nairobi-Namanga-Arusha-Moshi-Dar kwa wakati mmoja usiku na mchana
...Unakaguliwa passport usiku na askari wa Kenya.
Tulishakutana na vizuizi vya majambazi mara 3 pori la Namanga ndani ya mpaka.

Akaja huyu Mombasa raha... Naye akawa anapitia njia hiyo hiyo kuja huku Isebania -Sirari
Screenshot_20211224-202903_1.jpg
 
Watu wa kale mlipata sana shida!!!! Kwaio pesa ilikua inatumwa kwa bus[emoji23]
...pesa inatiwa ndani ya bahasha ya kaki, inazungushiwa gundi bahasha yote kisha anapewa dereva.
Sasa jifanye kuchelewa kufika Ubungo stendi kupokea kibahasha chao...utapiga kwata kuwafuata gereji kwao wanakopaki.
Ila walikuwa waaminifu sana madereva wa enzi hizo.
Kongole kwa Scandinavia, Spider, Akamba na Mombasa raha kwa uaminifu wenu kipindi nasoma.
 
Kiswele ilikuwa inatumia masaa mawili tu from Dar to Moro believe me!! ikiwa inashusha mlima kuitafuta msamvu mnaisikia sauti yake hiyooo mnajua kabisa hii ni Kiswele bjnafsi nimefanya kazi Hood Limited kuanzia mwaka 1996 mpaka 2010 mpaka ikafikia kipindi nikawa family friend wa wamiliki ikizingatia kwamba pia walikuwa wanafahamiana na baba yangu before..Nilipiga mzigo pale enzi zile Hood ni Hood hata nilipomaliza chuo sikuona umuhimu wa kuendelea na kazi nyingine kutokana na mavumba yaliyokuwa yanapatikana hapo na mimi ndio nilitoa wazo la kuwa na route ya Nairobi Arusha hapo ndio nikazidi kugongelea msumari wa kuaminiwa lakini kizuri hakidumu niliamua kufanya majukumu yangu mengine kabisa kwa hiyari baada ya kuhitaji changamoto mpya lakini maboss zangu ambao walinilea bado nipo nao karibu mpaka kesho hasa watoto zake..Hood sio kama amefirisika hapana ukweli ni kwamba kulitokea mgogoro mzee mwenyewe akiwatuhumu watoto kuwa wanafuja mali za kampuni kwa kutumia hela kwa starehe hivyo hana nia ya kuendelea na biashara hiyo ingawa bado kampuni ilikuwa top na tulikuwa kwenye process ya kuorder mabasi mapya makaliii so akaifunga taratibu kampuni mabasi kayafungia ndani na mengine anauza kwa bei ya kutupa mgogoro huu ulikuwa hasa kati ya mzee na watoto wake hasa Tiffu na Saidy ambao ni wakubwa na ndio walikuwa wakurugenzi ukiachana na yule mwingine aliyekuwa uarabuni mpaka leo Hood Hood..mzee kaamua kuwekeza kwenye biashara nyingine kama kwenye Real estates na kununua hisa kwa baadhi ya makampuni kama Azania..asante kwa uzi huu

View attachment 2054530
Umbeaaa huoooo.....utasutwaa
 
Super Najimunisa.....Majini 7
Enzi hizo Dodoma Shinyanga ni Vumbi tupu.
Basi Bwana,
Ilikuwa ni Mwaka 1999 natika Zangu Mwanza naenda Shule Morogoro nikaoanda Super najmunisa....Hahahah Acha Kabisa hili basi Sio Basi tuu ni Dereva Anaitwa “Rama Mtoto”
Alikuwa akiendesha Scania.93 ile nadhani!
Unaambiwa Kwanza Mpaka Matrafic walikuwa wanampenda...dogo alikuwa na control ajabu duu!
Basi Nimetoka mwanza tuko na Ligi ya Zuberi,Amit,
Tukaingia Shy chaaap,Hatukukaa sana Chombo Kikaoshwa....Hapo Zuberi na Amit wako mbele yetu[emoji3516][emoji41][emoji851][emoji30][emoji30]
Barabara ni vumbi tuu,Tukaanza Kumtafuta Mmoja baada ya Mwingine,Tunafika Tinde Amit huyu hapa...Chapa Rubber... tukaingia Nzega,Bado Zuberi haonekani...
Dogo anatembea anakuka Karanga tuu!
Mzee niko siti ya Mbele kabisa Nyuma yake,Tena yeye aliniambia Usilipe Nauli hela nipe Mimi! Nikampa.
Tunaingia Igunga...Zuberi huyu hapa nae anatoa Chombo...Sisi tukapaki kwanza...
Dereva Rama mtoto akasema tuondoke jamani,ngoma ikaanza...ni vumbi lakini Imechongwa....Piga piga Mara shelui Zeberi hiyu hapa....Akaombwa site,Overtake akakataa...[emoji3516][emoji3][emoji3][emoji3]Rama katulia tuu na Kitu Scania...
Ngoma Sekenke mlimani pale Rama akaomba tena Kwenye Mlima...[emoji30][emoji30][emoji30]Jamaa kambania kambania ile tunamaliza tuu ile S Rama akaingia kwenye tuta za Viazi[emoji23] Ngoma Imekubali mpaka watu wanashangilia Ile Overtake ya Kibabe! Jamaa Zeberi anachanganya wapi...Rama anatembea na Gia No.5 tuu Break ya Kwanza Singida tumekaa Pale Saa nzima Jamaa wooote mabadi yooote hayajatokea tuu Tukang’o chombo.
No.2 nyingine
Kama Kawaida dogo Rama Mtoto yupo Kwenye Super Najmunisa Tumekwama Manyoni kwenye Tope balaa!Sisi Tunaenda Dar,Tukakutana na Super najmunisa C.I.A ikiendeshwa na George
Wakati sisi tukiwa na NATO chini ya Dereva Mtoto Rama acha Kabisa!
Mlangoni yupo Mhindi Tajiri.
Baada ya Kushindikana Kupita na Magari yote yapo pale...Na Kamvua Kananyesha...Tukaambiwa tushuke tutembee...
Sawa tukashuka...Akabaki Rama peke yake kwenye Usukani....[emoji41][emoji851]
Akaanza Kuitoa Mashine...Kama Unavyojua Mlio wa Scania Mpaka Yule Tajiri Muhindi Akaanza Kutukana Kuionea Huruma Gari yake...[emoji51]
Ngoma Mpaka Imelala....
Rama Akairudisha nyuma eee bwanaeee...
Alipita nayo pale mkukuu inalala Kulia Na Kushoto jamaa yumoo tuu mpaka akaileta Upande wa Pili...
Halafu hao tukapanda tukaenda zetu[emoji851][emoji3516][emoji123][emoji91][emoji91]
Rama mtoto Super Najmunisa...Baadae Zuberi,Baadae nimesahau jina La Basi Alilokuwepo tena...
Alikuwa akishindana na Muhando(Marehemu kwa sasa)
Na Ukitaka Kumjua Ulikuwa unawnda Pale Ubungo Stendi Sehemu Inaitwa madereva Mashuhuru Utampata[emoji119]
 
Back
Top Bottom