TBT ya kibabe: Mabasi na vyombo vya usafiri Tanzania

TBT ya kibabe: Mabasi na vyombo vya usafiri Tanzania

Super Najimunisa.....Majini 7
Enzi hizo Dodoma Shinyanga ni Vumbi tupu.
Basi Bwana,
Ilikuwa ni Mwaka 1999 natika Zangu Mwanza naenda Shule Morogoro nikaoanda Super najmunisa....Hahahah Acha Kabisa hili basi Sio Basi tuu ni Dereva Anaitwa “Rama Mtoto”
Alikuwa akiendesha Scania.93 ile nadhani!
Unaambiwa Kwanza Mpaka Matrafic walikuwa wanampenda...dogo alikuwa na control ajabu duu!
Basi Nimetoka mwanza tuko na Ligi ya Zuberi,Amit,
Tukaingia Shy chaaap,Hatukukaa sana Chombo Kikaoshwa....Hapo Zuberi na Amit wako mbele yetu[emoji3516][emoji41][emoji851][emoji30][emoji30]
Barabara ni vumbi tuu,Tukaanza Kumtafuta Mmoja baada ya Mwingine,Tunafika Tinde Amit huyu hapa...Chapa Rubber... tukaingia Nzega,Bado Zuberi haonekani...
Dogo anatembea anakuka Karanga tuu!
Mzee niko siti ya Mbele kabisa Nyuma yake,Tena yeye aliniambia Usilipe Nauli hela nipe Mimi! Nikampa.
Tunaingia Igunga...Zuberi huyu hapa nae anatoa Chombo...Sisi tukapaki kwanza...
Dereva Rama mtoto akasema tuondoke jamani,ngoma ikaanza...ni vumbi lakini Imechongwa....Piga piga Mara shelui Zeberi hiyu hapa....Akaombwa site,Overtake akakataa...[emoji3516][emoji3][emoji3][emoji3]Rama katulia tuu na Kitu Scania...
Ngoma Sekenke mlimani pale Rama akaomba tena Kwenye Mlima...[emoji30][emoji30][emoji30]Jamaa kambania kambania ile tunamaliza tuu ile S Rama akaingia kwenye tuta za Viazi[emoji23] Ngoma Imekubali mpaka watu wanashangilia Ile Overtake ya Kibabe! Jamaa Zeberi anachanganya wapi...Rama anatembea na Gia No.5 tuu Break ya Kwanza Singida tumekaa Pale Saa nzima Jamaa wooote mabadi yooote hayajatokea tuu Tukang’o chombo.
No.2 nyingine
Kama Kawaida dogo Rama Mtoto yupo Kwenye Super Najmunisa Tumekwama Manyoni kwenye Tope balaa!Sisi Tunaenda Dar,Tukakutana na Super najmunisa C.I.A ikiendeshwa na George
Wakati sisi tukiwa na NATO chini ya Dereva Mtoto Rama acha Kabisa!
Mlangoni yupo Mhindi Tajiri.
Baada ya Kushindikana Kupita na Magari yote yapo pale...Na Kamvua Kananyesha...Tukaambiwa tushuke tutembee...
Sawa tukashuka...Akabaki Rama peke yake kwenye Usukani....[emoji41][emoji851]
Akaanza Kuitoa Mashine...Kama Unavyojua Mlio wa Scania Mpaka Yule Tajiri Muhindi Akaanza Kutukana Kuionea Huruma Gari yake...[emoji51]
Ngoma Mpaka Imelala....
Rama Akairudisha nyuma eee bwanaeee...
Alipita nayo pale mkukuu inalala Kulia Na Kushoto jamaa yumoo tuu mpaka akaileta Upande wa Pili...
Halafu hao tukapanda tukaenda zetu[emoji851][emoji3516][emoji123][emoji91][emoji91]
Rama mtoto Super Najmunisa...Baadae Zuberi,Baadae nimesahau jina La Basi Alilokuwepo tena...
Alikuwa akishindana na Muhando(Marehemu kwa sasa)
Na Ukitaka Kumjua Ulikuwa unawnda Pale Ubungo Stendi Sehemu Inaitwa madereva Mashuhuru Utampata[emoji119]
Daa mkuu umesimulia vizuri, mpaka nina imagine mimi ndio nipo nyuma ya seat ya dereva [emoji4][emoji4][emoji119][emoji1666]
 
Hatari sana
Screenshot_20211128-002826.jpg
 
Mimi simu niliyomnunulia Mzee wangu mara baada ya simu kutoka (ilikuwa Siamen ngapi sijui, ile nyeusi yenye kiantena) niliituma kwa Scandinavia kumpelekea mzee daah..
Siemens C25 maarafu kama twanga pepeta
 
1. TAWAQAL EXPRESS

View attachment 2054358

Pichani ni basi la kampuni ya Tawaqal. Kampuni hii ilikuwa balaa. Njia ya Dar - Mbeya, Dar- Kyela, Dar - Tunduma na Dar - Songea.

Kampuni hii ilikuwa na madereva mahiri kwelikweli. Miongoni mwao alikuwepo GIRIKI.

Jamaa alitoka Dar saa 12 asubuhi akaingia Mbeya saa 7 mchana.

2. SHABAHA EXPRESS

View attachment 2054378

Kampuni hii ilibamba sana miaka ya nyuma ikisafirisha abiria kati ya Dar na Arusha. Jamaa walikuwa wakishindana na wakongwe wa zamani kama Ngorika, Dar EXPRESS nk

3. SCANDINAVIA EXPRESS

Kampuni ya mabasi ya Scandinavia Express ni kampuni pekee ya kitanzania iliyowahi kutokea kwa kuwa na huduma za uhakika na za viwango vya hali ya juu kabisa kulinganisha na huduma zinazotolewa na kampuni za sasa. Kampuni hii ilijijengea jina kubwa na sifa nzuri ndani na nje ya nchi kwa huduma bora walizokuwa wakizitoa kwa abiria wake na pia kuliletea sifa taifa la Tanzania kwa kujulikana kuwa na mabasi ambayo ni quality na high class.

View attachment 2054407
Kampuni ya Scandinavia ilianzishwa zaiidi ya miaka thelathini na tano (35) iliyopita ikiwa na mabasi machache tu aina ya LEYLAND na ilipofika mwaka 1982 kwa mara ya kwanza Scandinavia walinunua basi lao la kwanza la kisasa kutoka kampuni ya SCANIA TANZANIA COACHES aina ya SCANIA ambalo kutokana na ubora wake na uzuri wake kwa kipindi hicho waliamua kulitumia kwa safari yao mpya waliyoianzisha ya Dar es salaam hadi Iringa.


BASI LA KWANZA LA KISASA KUNUNULIWA NA SCANDINAVIA 1982

Kadiri mahitaji ya usafiri yalivyokuwa yakiongezeka ndipo michirizi ya rangi ya BLUU,KIJIVU na NYEKUNDU ikaanza kuonekana katika mabasi mengi zaidi yaliyokuwa yakisafirisha abiria karibia kila kona ya Tanzania.

Ilipofika mwaka 2001 kampuni ya Scandinavia walianzisha safari yao ya kwanza kabisa kutoka nje ya nchi kwa safari ya Dare es salaam hadi Nairobi nchini Kenya,ambapo mafanikio ya ruti hiyo yalipelekea kuzaliwa kwa ruti nyingine kati ya Nairobi hadi Mombasa na Mombasa hadi Dar es salaam. Katika mwaka wa 2002 kampuni ya Scandinavia walipanua wigo wa huduma zao kwa kuanza ruti mpya ndani ya Afrika mashariki kwa safari za Dare es salaam hadi Kampala nchini Uganda.

Ilipofika mwaka 2003 kampuni ya Scandinavia ilipanua wigo zaidi kwa kuanza kwenda katika mji mkuu wa nchi ya Zambia Lusaka.

Wakati huo wote kampuni ya Scandinavia ilikuwa chini ya mkurugenzi na mwanzilishi wake MR.MUHAMED ABDULLAH.



Kampuni ya Scandinavia ilianza kutumia mabasi ya kisasa mwaka 1982 na kuanzia hapo walikuwa wakiongeza mabasi kadili ya mahitaji ya kampuni na abiria pia na kufikia jumla ya mbasi 100 ambayo yalikuwa yakitoa huduma za usafiri ndani na nje ya nchi na mengi ya mabasi hayo yalikuwa ni ya kisasa yaliyonunuliwa kutoka kiwanda cha SCANIA na MARCOPOLO kilichopo nchini BRAZIL

4. KISWELE

View attachment 2054432


Kiswele ndilo basi la kwanza Tanzania kuwa na injini nyuma.

Basi hili likitamba sana siku za nyuma na miongoni mwa njia ilizotamba ni Dar- Mbeya, Dar - Tunduma, Dar- Songea.

Mpaka leo hili basi linakumbukwa

5. SUMRI

View attachment 2054445

View attachment 2054448

Kampuni hii sasa haipo tena. Kampuni hii ilivuma sana ikihudumu njia ya Dar -Mbeya, Dar- Sumbawanga na Mbeya- Sumbawanga.

6. NGORIKA

View attachment 2054451


Kampuni hii kongwe imehudumu miaka mingi ikifanya safari zake kati ya Dar na Arusha.
Sina Picha zote ila kumbuka enzi za
Tanganyika Bus Service pale Mwanza na rangi.za buy mpauko kiaina
Trans Africa na kahawia take kiaina
Songoro bus service
Nzegenuka Nyota ya Bwana
Nyehunge Express ingawa bado wapo wapo
Mashiku Investment
Matema Beach
Mohamed Trans
Bukwaya
.....hao most ni lake zone huko from Mwanza to various destinations
...Wengine ni down hapo...
Kwacha
Safina
Gold Line
Widambe
Mwaafrika
Makete
Siri Yako
Super Star
Railway
Kamata
Bin Klebo Bus Service
Kiswele
Sharuks
Air Msae
Air Chalinze
No Challenge
Air Shen
Bin Klebo Bus Service
Kiswele
Sharuks
Air Msae
Air Chalinze
No Challenge
Air Shengena
Zainab
Scandnavia
Special Video Coach
Tawaqal
Comfort Video Coach
Living Light
Yarabi Salama
Safari Master
Big Mayai
Jupiter
Mbarak
Ruvuma Tours Line
Matema Beach Coach
...

Nb: za chini hapo I.credit JF member mkongwe bwana yutong /yutong

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
+ , Tunyande.
Happy Nation(hili linastahili lingeitwa basi la mashindano).
Na kwa wakazi wa Mbeya kulikuwa na basi maatufu sana,likipiga roote za Mbeya mjini kwenda Rujewa lilitwa "Hot bolt,Mukufwana mukungeta".
[emoji23][emoji23][emoji28][emoji28]hapo mwisho mkuu
 
Kuna basi la Dar-Mbeya liliitwa Scanlink nilipanda mara moja nikajiapiza sipandi tena lilikuwa refu kama treni linasepa sio poa
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji28][emoji28][emoji28]kha basi kama treni?abiria 200[emoji23][emoji28][emoji28]
 
Sina Picha zote ila kumbuka enzi za
Tanganyika Bus Service pale Mwanza na rangi.za buy mpauko kiaina
Trans Africa na kahawia take kiaina
Songoro bus service
Nzegenuka Nyota ya Bwana
Nyehunge Express ingawa bado wapo wapo
Mashiku Investment
Matema Beach
Mohamed Trans
Bukwaya
.....hao most ni lake zone huko from Mwanza to various destinations
...Wengine ni down hapo...
Kwacha
Safina
Gold Line
Widambe
Mwaafrika
Makete
Siri Yako
Super Star
Railway
Kamata
Bin Klebo Bus Service
Kiswele
Sharuks
Air Msae
Air Chalinze
No Challenge
Air Shen
Bin Klebo Bus Service
Kiswele
Sharuks
Air Msae
Air Chalinze
No Challenge
Air Shengena
Zainab
Scandnavia
Special Video Coach
Tawaqal
Comfort Video Coach
Living Light
Yarabi Salama
Safari Master
Big Mayai
Jupiter
Mbarak
Ruvuma Tours Line
Matema Beach Coach
...

Nb: za chini hapo I.credit JF member mkongwe bwana yutong /yutong

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
Teeteeko hili la Songea, DMT/KAMATA, TANGANYIKA BUS, HINDOCHA hii Nzega/Tabora, MAGOMAMOTO hii Dar/ Malawi, A K Nanji Morogoro, RahaLeo, Mamboleo, Manitu / sasa kazi. Dambaya, Wifi.
 
Back
Top Bottom