TCRA: Kipindi cha Shule ya Uongozi cha Humphrey Polepole kinatolewa pasipo kuzingatia misingi, sheria na kanuni za huduma ya utangazaji

[emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1] Ukishika makali yafaa uwe mpole tu.
UNAIJUA VIETE WEWEEEEEE
 
Hapana hizi sheria kali za maudhui ya mtandaoni/sheria ya huduma za habari na takwimu zilipitishwa kipindi polepole ni katibu NEC!!

Je hakujua hizo sheria ni kandamizi kiasi aje kulia lia sahivi? Kipindi anazuia blog zenye mawazo kinzani zisi operate alikua hajui umuhimu wa uhuru wa maoni?

Cha kuchekesha hyu polepole anaweza gombea Urais 2025 kupitia ACT alafu ataanza kulia lia tume huru ilihali alipokua na cheo CCM hakukumbuka umuhimuwa tume huru!!

Fundisho ni kuwa ukipata cheo andaa mazingira mazuri ya kesho yako kwa kutovunja madaraja yote uliyovuka kufikia hapo ulipo; otherwise ukipoteza cheo utashindwa kusimama tena maana atakayerithi kiti chako atatumia sheria hizo hizo mpya kukunyoosha
 
Piga nyundo huyo mpaka akili ikubali kuwa aliyekwenda amekwenda
 
Ungekuwa umemaikiliza vzr Wala usingepata shida na alifafanua, itafute kwenye shule ya uongozi utaona ufafanuzi, usimsikilize ukiwa na chuki nae huwezi kumweelewa
 
Kipindi cha Shule ya Uongozi cha Humphrey Polepole TV kusimamishwa kwa muda mpaka pale atakapofanya yafuaatayo. Kuwa na wafanyakazi wenye taaluma ya uandishi wa habari na utangazi na kuleta tija na ufanisi katika vipindi vyake.
Big up TCRA, huu sasa ni mwanzo mzuri wa kuelekea kwenye professionalism ya utangazaji, sio kila Tom, Dick and Harry, anaweza kuwa mtangazaji hata wa online TV, utangazaji ufanywe na watu wenye taaluma pekee.

Najipanga kufungua shule ya Utangazaji wa Redio na TV, naamini tayari nitapata mwanafunzi wangu wa kwanza wa kuanzia, HP, karibu shule, karibu kwenye fani!.

NB. TCRA pia toeni muongozo kwa Msajili wa Vyama vya Siasa, ahakikishe, wakurugenzi wa habari na uenezi, wa vyama vyote vya siasa, lazima wawe wataaluma wa taaluma husika, na sio wabwabwajaji tuu. Haya mambo ya kupeana tuu vyeo kwasababu mtu anajua sana kubwabwaja, ndio yametufikisha hapa!.
My Take,
Hii ya kuifungia Polepole sasa itaibua hoja ya kizifumua kanuni batili za maudhui mtandaoni, sio kila kinachorushwa mitandaoni ni news contents zinazohitaji kufanywa na professional journalist, lile ni darasa, watu wenye professional nyingine zozote wako huru kurusha mtandaoni contents za issues zao na sio lazima wawe waandishi wa habari.
Pili hii double standards ya TCRA inafurahisha sana!, kwa miaka mitano ya Awamu 5, yule kichaa Musiba, amekuwa kudhalilisha watu na kuwatolea uongo, uzushi na kashfa za ajabu, sikuwahi kusikia akiitwa na TCRA!.
P
 
Kwa hakika ushapata mwanafunzi
 
Hlo kwa mtu yeyote alilitarajia, japo kikiboreshwa kidg tu kiandolewa mapungufu, kikawekwa kitaaluma kabisa, bado naamini kipindi nikizuri,

Japo kimefungiwa ila elim yake imefika mbali Sana, na amesimamia kile anachokiamini, kimsingi Hp Ni 1 tu Ila anawayumbisha zaidi ya vigogo 50, mpka wanajadili uanachama wake, tutafika tu..
 
Polepole nilikwambia siku ileeeee wakati upo na Mbunge wa Bukoba....alipokukodia ndege uende bk.. kufanya yale mafenkeche yako na Bashiru...

Nahisi unakumbuka vzr, mwambie Bashiru zile nyumba zake Chanika muda simrefu tunazibomoa!
 
Polepole ni insignificant katika maslahi ya nchi ni sawasawa wewe unachoma nyumba yako ili kuua kunguni waliomo ndani na unafurahia bila ku-consider hasara ya kupoteza nyumba....

Sikufurahia wakati hizi Sheria zinatungwa.., sikufurahia wakati zinaminya watu na sitafurahia zinavyoendelea kuminya watu (no matter ni nani anaminywa)
 
Nilimkubali sana wakati wa mchakato wa Katiba Mpya uliowekwa kabatini. Baada ya hapo simwamini tena kwa aliyoyasema na kuyaamini baada ya kupewa madaraka makubwa na anayosema na kuyaamini sasa baada ya kutenguliwa. Kwangu amejionesha kuwa na sura tatu zisizofanana; sura ya wakati wa mchakato wa Katiba Mpya, sura ya ukatibu Mwenezi na sura ya ubunge wa kuteuliwa. Nipo njiapanda kumtambu kati ya hao watatu ni yupi alie yeye aliye halisi.
 
Raisi wa marekani Joe Barden aliomba aonane na mwanamziki Lady gaga baada ya kusema yeye hatochanja kwa kuwa rafiki wa binamu yake baada ya kuchanja amepoteza uwezo wa nguvu za kiume na kusababisha uchumba na mchumba wake kuahilishwa.

Sasa tanzania amabapo wamesema kuchanja ni hiali bado viongozi wanatuma TCRA kubana watu kwa hoja za hovyo na ni wasomi wanaotegemewa.

Unashangaa msomi gani anaweza kutoa hoja kama zile?
Viongozi wabadilike ni muda sasa wa kufanya mambo kwa kuheshimu watu na haki zao na pia kuheshimu nafasi walizonazo ili waweze kutumikia nchi kwa uzalendo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…