TCRA yapiga stop wimbo wa Nay wa Mitego kuchezwa kwenye vyombo vya habari

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595


Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imepokea taarifa kutoka Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kuzuiya wimbo uitwao "Amkeni" uliopigwa na mwanamuziki Emmanuel Elibariki (Nay wa Mitego) kutopigwa katika mitandao ya kijamii na vombo vya habari.

Aidha, kwa mujibu wa BASATA, maudhui ya wimbo huo yana melekeo wa kutaka wananchi wasiwe na imani na Serikali, kuchochea wananchi kuwa na mapokeo hasi juu ya utekelezaji wa mipango ya Serikali yao kwa ujumla, na kuwa ni wimbo wa uchochezi baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wananchi wake.

Hivyo, kwa barua hi, TCRA inaelekeza chombo chako cha habari kutopiga wimbo huo.

Tafadhali zingatia maelekezo.

Pia soma: Nay wa Mitego aitwa BASATA. Atuma Wanasheria wake
 
Sirikali isiyopenda kukosolewa. Na kama wananchi wataamua jambo, hawatakumbuka kama na Nay wa Mitego aliwahi kuhamasisha.

Basata, msipime akili zetu kama zinaendeshwa kwa nyimbo za Nay wa Mitego.
 
TCRA kuna vilaza aisee, hawako makini. Hawajui hata waliemfungia anaitwa nani. Ndio maana tunashindwaga kesi mbalimbali kwa kukosa umakini.

Jina halisi la Nay wa Mitego ni EMMANUEL ELIBARIKI MUNISI. Huyo waliemtaja hapo labda ni mbunge wa Singida Magharibi.
 

Nay - Emmanuel Elibariki Munisi
Mb - Elibariki Emmanuel Kingu
 
Uzuri ni kwamba, umeshasambaa mitandaoni, na kwenye kampeni hadema watautumia kwenye majukwaa yao na kwenye magari ya matangazo. ujumbe umeshafika kwa wabongo wenye smartphone, na utafika hata kijijini kwa magari ya matangazo kipindi cha kampeni. dp world kama haitafumuliwa, itawatafuta miaka hii miwili hadi watatamani kuhama nchi.
 
Bonge la Promo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…