desayi
JF-Expert Member
- Aug 27, 2017
- 3,593
- 5,848
Watunga sheria ndo mafisadi unategemea watajifungaWakome Tena hyo adhabu ndogo Kwa wezi, pia adhabu Kali ka hii iletwe Kwa mafisadi ya serikalini
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Watunga sheria ndo mafisadi unategemea watajifungaWakome Tena hyo adhabu ndogo Kwa wezi, pia adhabu Kali ka hii iletwe Kwa mafisadi ya serikalini
Wakome Tena hyo adhabu ndogo Kwa wezi, pia adhabu Kali ka hii iletwe Kwa mafisadi ya serikalini
Huyu hakimuMwananchi
Muktasari:
Watu wanne wamehukumiwa na kifungo cha miaka 30 jela na Mahakama ya Wilaya ya Temeke baada ya kuiba runinga yenye thamani ya Sh400,000.
Dar es Salaam. Wakazi wanne wa eneo la Charambe wamehukumiwa kwenda miaka 30 jela na Mahakama ya Wilaya ya Temeke baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha.
Waliohukumiwa ni Samwel Chacha (20), Haji Ally (24), Athuman Halfan (25) na Sadid Seif (19) wote ni wakazi wa Charambe.
Inadaiwa kubwa Februari 8, 2022 eneo la Charambe kwa Mbiku waliiba luninga yenye thamani ya Sh400,000 mali ya Yahama Ngingile kabla na baada ya kufanya wizi huo walimkata na panga kichwani.
Hukumu hiyo imetolewa leo Aprili 24, 2023 na Hakimu Mkazi Mwandamizi, Jimson Mwankenja amesema ametoa hukumu hiyo baada ya washtakiwa hao kutiwa hatiani kwa kosa hilo ambapo mahakama hiyo imejiridhisha pasipo shaka lolote.
"Jamuhuri walikuwa na mashahidi wanne pamoja na vielezo huku upande wa utetezi washtakiwa hao walijitetea wenyewe,"amesema Mwankenja.
Amesema mahakama hiyo imewatia hatiani kwa kifungu cha 287A ya kanuni ya adhabu kwa kuwa kulikuwa na uthibitisho la wizi, wakati wa tukio walitumia silaha aina ya panga na ilielekezwa kwa mtendewa.
Mwankenja alisema mahakama hiyo imezingatia kifungu cha 287A kinaainisha adhabu pekee ni kifungo cha miaka 30 jela.
Amesema kutokana na kifungu hicho cha sheria mahakama hiyo imewahukumu washtakiwa wote kifungo cha miaka 30 jela na kama hawajaridhika na maamuzi hayo wakate rufaa katika mahakama Kuu.
Wewe utakuwa panya RoadIt's craze mkuu na hawa watawala wanatuchukulia sisi ni mizuzu, hukumu gani hii huu ni ushenzi wa hakimu kwa kuonea vidagaa huku mipapa ikivuruga nchi, hukumu ya kipumbavu
Unashtuka njemba 4 zipo ndani zina mapanga, unapambana ili iweje?Kuna anayetaka achia chake kisepe kindezi?
Hao jamaa ukisema upambane nao either watakuua au kukutia ulemavu wa kudumu vitu kama TV simu Bora uwaachie tu SI vinauzwa.Hicho ndo kimesababisha wale mvua ndefu
Tv laki nne, Bei ya kimtaa inaweza uzwa hta 150000 c unajua tena wazee wa Kazi hawana muda wa kupoteza??Watu wanne mnaenda kumkata mtu mapanga mumuibie tv ya laki 4 kweli?
Mkigawana kila mmoja anachukua laki upumbavu gani huo.
Mnakamatwa mnafungwa miaka 30.
Miaka 30 hao watakula ugali maharage bure kodi zetu.
Bora wanyongwe tu
... waliokwapua billions hawakutumia silaha aina ya panga!Mwendo wameumaliza hao, ripoti ya CAG waliokwapua billions of money wanabadilishwa vitengo wanadunda mtaani
Kabisa hawawezi kuuza laki 4 , ikizidi sana laki 2.Tv laki nne, Bei ya kimtaa inaweza uzwa hta 150000 c unajua tena wazee wa Kazi hawana muda wa kupoteza??
Siyo hoja hi mlitaka nyinyi tu ndio muepoWanyakyusa wamejaa sana kwenye kazi za mahakama