Temeke, Dar: Ili upige muziki kwenye sherehe/shughuli utapaswa kulipia elfu 50 ya kibali

Temeke, Dar: Ili upige muziki kwenye sherehe/shughuli utapaswa kulipia elfu 50 ya kibali

This is hogwash to say the least......

Kwahio kama DJ/MC kapata shughuli ya kulipwa elfu 25 au 10 kwa siku, itabidi atoe kwenye mfuko wake kulipa hio difference..., Au wanataka kusema profit kwa kila kazi kwa hawa watu zinazidi hizo kodi, in short kwa shughuli yoyote mtu inabidi aweke kando 180,000/ kwa ajili ya kodi no matter kama ametumia cost ya laki mbili au bilioni mbili ?
Or anaweza kutoza bei ya juu ili difference inayobaki baada ya kulipia kodi ikawa faida yake
 
Hayo ni maamuzi ya kwenye halmashauri madiwani wengi ni wapya kwenye siasa za maamuzi na wakurugenzi sio wanasiasa.

Isitoshe sio kila maamuzi ya siasa yanayogusa watu moja kwa moja ni sahihi ata kama yanafanywa na CCM.
Tusisingizie uzoefu hapo ni normal common sense tu kumfuraisha mfalme, kwanini wateuliwe watu wasio wazoefu huko
 
Ni sawa kabisa! Unakuta sherehe kwa mfano ya harusi au sendoff watu mnachangishwa kila kichwa elfu hamsini mpaka laki moja,!

Unakuta sherehe moja tu ina gharimu mpaka milioni 10.

Unakuta kwenye bajeti ya sherehe eti
Mapambo milion 1.5
Ukumbi milion 1.2
Mc na music milioni 1.8
Picha na video milioni 1.6
Vinywaji milioni 1.7
Chakuala milion 4

Na hizi ni sherehe tu za uswahilini bado za ushuani ndio balaa

Unakuta mtu ana maisha magumu lakini akipewa kadi ya mchango anajipinda mpaka ipatikane, tena wanakuwekea masharti kabisa single 80,000 double 150,000.


Tena hili suala lilialamikiwa sana humu kwama ifike hatua hawa watu walipe kodi.

Walipe tu kodi aisee.
Walipe kodi hakuna shida, sajili watu wote hao as self employed na walipe kodi kupitia TRA kama biashara zingine that is understandable kwanza wengi mapato yao yanavuka threshold za taxable income kwa sheria na catering services nyingi za hizi sherehe na hayo ma-hall ni walipa kodi wa TRA tayari.

Issue hapa ni tozo za halmashauri ambazo wanataka wananchi ndio walipie zaidi kabla ya sherehe zenyewe.
 
Tusisingizie uzoefu hapo ni normal common sense tu kumfuraisha mfalme, kwanini wateuliwe watu wasio wazoefu huko
Vyanzo vya mapato ya halmashauri vinaanzishwa huko huko kwenye vikao vyao; ata Dr Mpango anaweza asijue kila halmashauri imekuja na tozo gani, let alone the president.

Na kama wanajua this is a bad one.
 
Walipe kodi hakuna shida, sajili watu wote hao as self employed na walipe kodi kupitia TRA kama biashara zingine that is understandable kwanza wengi mapato yao yanavuka threshold za taxable income kwa sheria.

Issue hapa ni tozo za halmashauri ambazo wanataka wananchi ndio walipie kabla ya sherehe zenyewe.

Mitano tena.
 
Safi sana but mbona viwango vipo chini hivyo?

Hivi hapa ndivyo vyenyewe sasa...

Ukumbi malaki 5
Chakula malaki 4
MC malaki 3
DJ malaki 2

Badala ya kuchangianaga kwenye mambo muhimu kama elimu, tiba, nk watu wanashobokeaga masherehe. Hiiiiiiiiiii!

Wacha wakomage kabisa kabisa wakufwage huko!
 
You knew Sengerema was going to set the precedent.

Sometimes wacha yawakute tu aiwezekani watu wajiamulie mambo na sheria ipo; halafu wahusika kwao iwe hewala tu.

Kesho watasema mechi za ndondo cup kuchezwa lazima walipie tozo ya laki moja ili kuwe na kiingilio.

Kikubwa kwao chochote kinachompa mtanzania starehe nchi ambayo wananchi wake wanatakiwa wawe na manung’uniko according global happiness index lazima kiangaliwe upya na kuitoa hiyo furaha maana ilo jambo ni anasa.

Haya ndio madhara ya kuwa na waziri wa fedha asie mwanasiasa na kura za ushindi aziitaji ushawishi; vinginevyo waziri mwingine yeyote asingekubali huu upuuzi.

Mwisho wa siku anaelipa ni wenye sherehe sio mpishi, MC, mwenye ukumbi wala photographer; just pathetic watu wakikubali huu upuuzi.

Mtu mwanawe kafaulu shule, mzazi amefurahi anataka kumfanyia ka part inabidi aachane na hilo Waco maana kuna tozo za halmashauri zinamsubiri; aisee na wananchi wanadhani this is OK ili swala likipita bila makash kash sasa ndio ntaamini watanzania ni kama kondoo.
Tulia sindano ziingie ndg proMagufuli regime.
 
dah mbona hizo gharama za kodi ni ndogo sana kwa baadhi ya wahusikaa !

Ni jambo jema kwa namna moja ama nyingine kutafanya jamii kupunguza baadhi ya matukio ya sherehe na kuelekeza fedha kwenye mambo mengineyo ya kujenga familia / uwekezaji
Mkuu umeongea point.Walichofanya siyo kutanua uwanda wa kodi bali wamezifunga shughuli tajwa hapo juu kwa sababu ukitaka kutanua uwanda wa kodi inabidi kwanza uje na mbinu za kuongeza/kuimarisha pato la mwananchi halafu ndiyo uje na kodi.Ukileta kodi bila kuimarisha kipato cha mlengwa maana yake ni kuifunga shughuli husika ya mlengwa halafu kinachofuata ni economic colapse.Imagine hawa MC watakula wapi kama shughuli lengwa hizi zikifungwa/zikifa?Maana yake unemployment rate itaongezeka mara dufu halafu kutakuwa hakuna expenditures na hatimae uchumi unacolapse.Mimi huwa najiuliza serekali huwa haina wataalam wa kodi?!
 
Wanachomaanisha ni kuwa wamepandisha gharama za hizi shughuli.Yaani kama MC alikuwa analipwa TZS 25,000/= akienda kweye shughuli ya mnyonge kama vile kipaimara sasa itabidi alipwe TZS 75,000/= ili yeye aweke mfukoni 25,000/= na 50,000/= alipie kodi.Tafsiri yake ni kwamba wanyonge hawataweza kuwafanyia wapendwa wao sherehe tena!
Kuweka kiwango flat ni tatizo. Hao wanaolipwa wawe na efd kisha wanapopokea watoe risiti itozwe kodi
 
Back
Top Bottom