Tenzi za rohoni

Kijito cha utakaso
Ni salama rohoni mwangu

Kwa SDA wao wana nyimbo za kikrustu kuna wimbo no 158 U MWENDO GANI NYUMBANI? huwa unanipa nguvu sana
 
Sahihi kabisa
 
Mbele ninaendelea
Bwana uliyewaita
Nasikia kuitwa
Hizi za chini ndio zangu dahh, Hiyo nasikia kuitwa wakati nahangaika na uzinzi na ujana ilikuwa inasema nami sana Moyoni Mwangu. Uliyewaita dah, hiyo ninlazima nitoe machozi nikiisikia na huwa najitahidi sana nisiisikilize mbele za watu.

Nilikuta mtu anasikiliza hiyo tenzi huwa naondoka kwani huwa nataka sana machozi. Naipenda sana na Marehemu mzee wangu alikuwa anaipenda sana. Kwenye msiba wake, watoto tuliomba tuombe huo wimbo kama kumbukumbu yake.
 
Kwa Kalvari:

Muda mwingi nilipotea,
Sikufahamu msalaba,
Wala aliyenifilia,
Kwa Kalvari.

Rehema bure na neema,
Samaha nalo nilipewa,
Ndipo aliponifungua
Kwa Kalvari.


Kwa neno lake Bwana Mungu,
Nilijiona mimi mwovu,
Nikageuka na kutubu,
Kwa Kalvari.

Rehema bure na neema,
Samaha nalo nilipewa,
Ndipo aliponifungua
Kwa Kalvari.


Yote kwa Yesu namtolea,
Ndiye mfalme wa pekee sasa,
Kwa furaha nitamwimbia,
Wa Kalvari.

Rehema bure na neema,
Samaha nalo nilipewa,
Ndipo aliponifungua
Kwa Kalvari.


Jinsi pendo lilivyo kuu,
Neema ilishuswa toka juu,
Alitufanyia wokovu
Kwa Kalvari.

Rehema bure na neema,
Samaha nalo nilipewa,
Ndipo aliponifungua
Kwa Kalvari.
 
Hii ni ya kusemehea madeni unakuta unamdai mtu mpaka unajihisi utafika mahali unaweza mkosea Mungu ,basi unakumbuka jinsi Mungu alivyokusamehe dhambi zako bila kikwazo unajikuta unabubujika na hii nyimbo alafu unamwambia mdeni wako uende kwa amani Bwana atanilipa
 
Kimsingi, kanisa linalazimishwa kufuata ulimwengu. Sisi tunapoabudu, bado tumesimama kwenye ule uimbaji wa zamani.
hawa waabudishaji wa kisasa ndio wanaharibu nyimbo asilia. Tenzi zinaimbwa tune za ajabu na wachungaji wao hawawakemei
 
Siwezi kulala bila kuimba au kusikilizaa hizi hymnal zinabariki sana .its nice moment kwa kweli..ndio maana Paulo na sila waliimba hadi milango ya gereza ikafunguka..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…