Tetesi: Rwanda yanunua madini kwa siri nchini Tanzania na kuyauza tena kwa kampuni ya Apple

Tetesi: Rwanda yanunua madini kwa siri nchini Tanzania na kuyauza tena kwa kampuni ya Apple

Kuna tetesi madini yamekuwa yakinunuliwa kwa kasi ktk mikoa ya Geita na Shinyanga na wafanyabiashara wasio wazalendo.

Wafanyabiashara hao hupewa mitaji na serikali ya Rwanda japo wao ni watanzania.
Wanachofanya ni kununua almasi na dhahabu kutoka kwa wachimbaji wadogo na kuiuza nchini Rwanda kimagendo kwa siri kubwa sana. Jengo la ununuzi lipo jijini Kigali na Rushwa hutumika pakubwa kuwazima mamlaka za mipakani.

Inadaiwa wafanyabiashara hawa hufanya biashara nyingine halali kati ya kanda ya ziwa na Rwanda huku lengo fiche ikiwa ni madini ya Tanzania.

Haikubainika ikiwa kampuni ya APPLE ambayo huyanunua madini hayo kutoka serikali ya Rwanda kama inayo habari kuwa madini hayo hutoka nchini Tanzania.

Source: Wachimbaji wadogo Geita na Shinyanga.
Naona umeamua ama kupotosha au kuandika masuala ambayo huyafahamu uzuri kwa undani.

Habari za kijasusi zilizopo ni kwamba Apple wanunua madini yale ya T3s ambayo (kwa kufahamu au kutokufahamu) huibwa na kutoroshwa kutokea Kivu huko Goma na kuishia Kigali.

Na moja ya sababu kubwa ya Tshisekedi kuwa Paris wakati huu ni kujadili hilo maana M23 ndo wasadikiwa kuwa mkono wa kulia wa Rwanda.
 
Mama anawaza uchaguzi tu na mambo ya kijinga, sasa unategemea nini..?
Acha wajipigie tu
 
Acha wauze biashara huria maana wakisema wayauza hapa hakuna watakachopata badala ya siasa tu, maana siasa imeharibu nchi yetu ,kwenye taaluma siasa imaingizwa wacha tupige hatua kurudi nyuma na acha wenye akili waende mbele tutaishia hivi hivi tu
 
kama ananunua shida ik wapi? Si seikali yenu imeshindwa? Mibantu stupid sana.
 
Nilisikiaga stori kahama kipindi flani kuna vijana wa kitusi huwa ndio biashara yao(Direct connection na Kagame) na wanapiga hela chafuu
Ila wanapitia njia halali
Nenda kahama mzee katafute chanel
MADINI YANALIPA ILA USIKURUPUKE
 
Sioni tatizo kama wananunua na kuuza, ni biashara. Ingekuwa tatizo kama wangekuwa wanaiba
 
Huyu Mama tunajiendea tu. Na Ukifika hadi 2030 warahi hii nchi itakuwa ishagawiwa yote. Tutampa kazi Rais ajae kuvunja mikataba na kurudisha Mali zilizopolwa.
Kila raia ana wajibu wa kujilinda, kuilinda nchi na kuhakikisha sheria zinafuatwa. Timiza wajibu wako au toa taarifa upate msaada kutoka ngazi mbalimbali za serikali.
Mlaumu Mama kama umefanya hivyo bila matokeo chanya kwenye ngazi zote.
 
Kuna tetesi madini yamekuwa yakinunuliwa kwa kasi ktk mikoa ya Geita na Shinyanga na wafanyabiashara wasio wazalendo.

Wafanyabiashara hao hupewa mitaji na serikali ya Rwanda japo wao ni watanzania.
Wanachofanya ni kununua almasi na dhahabu kutoka kwa wachimbaji wadogo na kuiuza nchini Rwanda kimagendo kwa siri kubwa sana. Jengo la ununuzi lipo jijini Kigali na Rushwa hutumika pakubwa kuwazima mamlaka za mipakani.

Inadaiwa wafanyabiashara hawa hufanya biashara nyingine halali kati ya kanda ya ziwa na Rwanda huku lengo fiche ikiwa ni madini ya Tanzania.

Haikubainika ikiwa kampuni ya APPLE ambayo huyanunua madini hayo kutoka serikali ya Rwanda kama inayo habari kuwa madini hayo hutoka nchini Tanzania.

Source: Wachimbaji wadogo Geita na Shinyanga.
Kwani ni waziri gani alikuwa na dhamana na wizara hiyo wakati hayo yote yakitokea? Ukijuwa ni nani, unaweza kuunganisha 'dots' zako kirahisi Wahenga husema "Damu ni nzito kuliko maji," na ni kweli hata kisayansi.

Nchi hii inaviongozi mabwege sana.
 
Sioni tatizo kama wananunua na kuuza, ni biashara. Ingekuwa tatizo kama wangekuwa wanaiba
Hii ni biashara nje ya utaratibu wa kibiashara, bado wewe huoni tatizo? Bila shaka unayo kadi ya kijani mfukoni mwako.
Umeisoma hiyo taarifa na kuielewa kweli kabla ya kuandika haya uliyoweka hapa?
 
Hii ni biashara nje ya utaratibu wa kibiashara, bado wewe huoni tatizo? Bila shaka unayo kadi ya kijani mfukoni mwako.
Umeisoma hiyo taarifa na kuielewa kweli kabla ya kuandika haya uliyoweka hapa?
Ngoja nikasome
 
Tunaweza kuilaumu Rwanda lakini makosa ni sisi Tanzania, naomba kutoa ushuhuda km mfano kwa hili... Ukienda mikoa wa Kagera... Wilaya ya Missenyi, Karagwe na Kyerwa wakati wa msimu wa mavuno ya kahawa kuna jambo utalishangaa....
Serikali unawahimiza wananchi kuuza kahawa kwenye vyama vya Msingi
Taratibu ni kama ifuatavyo
1. Ujisajiri kwanza... Huu ni mchakato wenye kila aina ya usumbufu
2.Uandae kahawa yako.. Uipembue kutoa kila aina ya uchafu baada ya kukauka
3. Uipeleke hadi kwenye eneo husika kwa gharama zako
4. Usubiri hatua zote za kupokelewa.. Usisahau namba ya NIDA na Account Bank.. Au namba ya simu ya kupokelea pesa zako
5. Kilo moja watakulipa hata 1200
6. Pesa unaweza lipwa baada ya miezi 2 au mitatu na kuendelea.
7. Pesa itakuwa na makato ya hapa na pale hata miamala pia ina makato.
Lakini kuna njia ya pili... Njia hii inaitwa MAGENDO njia hii ni kama ifuatavyo
1. Anakuja Waganda hadi nyumbani kwako au hata shambani
2. Wananunua kahawa yako kilo elf 1500/1600
3. Wanakupa pesa yako yote sekunde hiyo hiyo
4. Hawana muda wa kukagua km kahawa imepembuliwa au ni chafu
5. Wanaondoka na mnakuwa mmemalizana wala hakuna cha makato wala nini
_TUTAFAKARI KWA PAMOJA
1. Sasa ungekuwa Mtanzania wa kawaida ungeuza kahawa yako wapi? Kwenye chama cha msingi au kwa Waganda?
2. Je, serikali ya Tanzania wao kahawa wanaenda kuuzia soko gani na Waganda wanapeleka soko lipi? Ambako kwa Serikali ya Tanzania inapata bei ndogo na Waganda bei kubwa?
3. Kazi ya Usalama wa Taifa ni nini katika kipengele cha uchumi? Au wako kushughulikia masuala ya siasa za majukwaani kuliko masuala nyeti ya kitaifa.?
#Wanyarwanda km wanatoa pesa inayowaridhisha wachimbaji au wauzaji wa madini hapa Tanzania unategemea nini?
 
Kwamba Apple wakafate dhahabu hapo Rwanda wakati huko Marekani ipo yakutosha tu
Usikatae mkuu, hata Rais wa CONGO mh Tshisekedi amelalamika juzi juu ya suala hili, amesema Rwanda wamesaini mikataba na Makampuni ya Apple kuwauzia madini ambayo Rwanda haina bali inatumia waasi Kuyaiba Congo na Nchi Jirani ( yamkini Tanzania) na kuyauza. Ameomba mataifa ya Ulaya yasaidie kusitisha mikataba hiyo kwani inaendelea kuchochea Vurugu katka Taifa la Congo... Kampuni ya Apple haikukanusha bali imesema hayo madai hayana msingi wowote km wao wananunua ki halari madini hayo kutoka Rwanda.... Hii ni taarifa ya Juzi tu.
Sisi km Tanzania viongozi wetu wako kwenye siasa... Akina Muliro wako bize kusikia ni nani hajamsifia Rais ili wamshughulikie
 
Hali ya kukosa uzalendo imeasisiwa na viongozi wa chama tawala. Wafanyabishara kazi yao ni kuunga juhudi kile CCM inafanya. Hao Rwanda akili kubwa, nyie tiss yenu kazi yake kubwa kuilinda CCM while wenzetu wanawaza mambo ya maana ya kiuchumi
 
Kila raia ana wajibu wa kujilinda, kuilinda nchi na kuhakikisha sheria zinafuatwa. Timiza wajibu wako au toa taarifa upate msaada kutoka ngazi mbalimbali za serikali.
Mlaumu Mama kama umefanya hivyo bila matokeo chanya kwenye ngazi zote.
Toa analysis Sasa tusome.
 
Kuna tetesi madini yamekuwa yakinunuliwa kwa kasi ktk mikoa ya Geita na Shinyanga na wafanyabiashara wasio wazalendo.

Wafanyabiashara hao hupewa mitaji na serikali ya Rwanda japo wao ni watanzania.
Wanachofanya ni kununua almasi na dhahabu kutoka kwa wachimbaji wadogo na kuiuza nchini Rwanda kimagendo kwa siri kubwa sana. Jengo la ununuzi lipo jijini Kigali na Rushwa hutumika pakubwa kuwazima mamlaka za mipakani.

Inadaiwa wafanyabiashara hawa hufanya biashara nyingine halali kati ya kanda ya ziwa na Rwanda huku lengo fiche ikiwa ni madini ya Tanzania.

Haikubainika ikiwa kampuni ya APPLE ambayo huyanunua madini hayo kutoka serikali ya Rwanda kama inayo habari kuwa madini hayo hutoka nchini Tanzania.

Source: Wachimbaji wadogo Geita na Shinyanga.
Una maanisha nini unaposema wafanyabiashara wasio wazalendo?

Ninachokifahamu mimi mfanya biashara anatafuta faida na kama mteja anampa malipo mazuri hawezi kulikimbia hilo soko.
 
Back
Top Bottom