Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
MOE United Republic Of Tanzania - Ministry of Education and Vocational Training naona wamerudi labda ndiyo wanajiandaa kuweka matokeo muda si muda.
labda ngoja tusubiri
Munyaaaazi mungu subana wa taala,ha ha ha
Mi nashauri wapewe A wote,wapige pointi saba wote kuzuia uvunjifu wa amani
Mwaka jana yalitoka tar 16 january ila haya ya mwaka huu mbona utata mwingi au kuna janja janja hapo?
Matokeo ya kidato cha nne kwa mitihani iliyofanyika October mwaka jana yanakaribia kutoka. Katika matokeo hayo ambayo vikao vyake vya mwisho ndio vinafanyika,ufaulu umnaonekana kushuka.Nyaraka zinaonesha kuwa Shule za Seminari,kama ilivyo ada,zinaoongoza.Baadhi ya Shule za Serikali zinajikongoja ingawa ufaulu katika Shule zetu za Kata ni wa utata mtupu.
Matokeo hayo ambayo nimefanikiwa kuyachungulia kiintelijensia yanaonesha kuwa wanafunzi wa Sayansi ndio waliofaulu zaidi ya wale wa masomo ya Sanaa. Wasichana,katika ufaulu wa kitaifa,wameng'ara kuliko wavulana. Hali katika Shule zetu za Serikali hasa za Kata si nzuri hata kidogo. Yakitoka,hapatatosha!
Matokeo hayo yanatarajiwa kutangazwa muda wowote hasa kuanzia tarehe 1/2/2013.
ANGALIZO: Siwezi kutaja kwa majina Shule za kwanza na za mwisho na wanafunzi wa namna hiyo kwakuwa matokeo rasmi hutangazwa na Serikali.
Madogo sasa hizi post zenu humu zinaboa si msubiri; kwani kwa kupost humu ndio mtayaharakisha au?!
Sio lazma ufungue thread znazohusu matokeo. Kama hazikuhusu na zinakuboa unafungua za nin?