Tetesi: Tetesi za usajili wa dirisha dogo ligi kuu Tanzania bara 2023/2024

Fujo tupu ....usajili huu...huyu huku huyu kule.....
 
Edwin Balua wa Tanzania Prison kutua simba hivi karibuni

Sent using Jamii Forums mobile app
Hii inaitwa fujo ya kusajili mawinga, nahisi simba tunakosea, kuna haja ya kufanya timu iwe na balance, tuna shida viungo wakabaji, tuna shida beki za kati, tuna shida na beki za pembeni, tuna shida strikers lakini hii ya kuwa na winga timu nzima naona sio sahihi sana ! Kamati ya usajili ina shida mahala
 
Ndani ya miaka 3 ijayo kwa janjajanja za viongozi wa Simba nina uhakika hatutapata kombe lolote tofauti na Mapinduzi cup.

Linapokuja suala la usajili wanajimbwambafai sana lakini mwisho wa siku kinachofanyika ni upuuzi uleule wa kila dirisha la usajili.


cc Hichilema

Kwa sasa wote wapenzi na mabosi wa Simba tunapitia wakati mgumu, mashabiki mioyo ina sonona na mabosi biashara zao za jezi, viingilio getini, kuchangia app n.k nako mapato yameshuka.
 
Kuna haja kubwa ya kuwa na mkurugenzi wa ufundi pale, yaani usajili wetu umekuwa wa kihunihuni sana kwakweli, sijui kamati ya usajili inafanya nini? Mashabiki wanaona viongozi wanakosea ila hawajirebishi kutokana na ubishi wao! Hatuna viongozi wenye weledi zaidi ya wizi tu
 
Reactions: K11
Hafiz Konkoni Konki master anahitajika na bechem United ya Ghana .
Sasahivi Yupo njiani kuelekea Ghana
 
Golden boy Chasambi....jamaa anajua mpaka anajua tena. Ni muda mrefu simba tumekosa mbadala wa chama katika kuhakikisha strikers wanapata assists za kutosha .
Ana Kasi? Au ndo Yale Yale mambo ya Slow motion
 
Count me in Mkuu
 
Nduo, Boko kijana amepewa nafasi.
 
Kombe liko karibu mkuu, kama si msimu huu basi ujao. Kilichoikumba Simba sio janjajanja wala nini bali ni harakati za kuanza kutengeneza kikosi kipya baada ya kilichokuwepo kusnza kuisha kitu ambacho kilichelewa kuanza. Wachezaji wengi waliozeana na kuitengeneza Simba bora umri ulikuwa unawatupa mkono e.g Kagere, Bocco, Mugalu, Nyoni, Wawa, Kahata, Kotei, Lwanga etc.
 
Yanga lzm tumfikirie pia coz ndio mshindani wetu
 
Msimu wa ngapi huu maneno ya viranja yakiwa yaleyale?
 
Yanga alimaliza misimu mingapi?
Alikuwa kapuku mfukoni, aliishi kwa msaada wa bakuli, tangu aishi kwa nguvu ya beberu GSM balaa tunaliona.

Sisi tunaambiwa daily timu inavuna mabilioni ya kutosha huku na kule, kwa minajili hiyo hatukutegemea kufanya sajili za kuokoteza kiasi hicho.

Unaleta rundo la wachezaji wa bei chee wakifika badala ya kuingia kwenye mfumo wanaishia asilimia kubwa kwenye mbao ndefu au kucheza chini ya kiwango kuliko waliopo.


Kwa sasa silaumu sana maana hata mabosi kibiashara huenda malengo yenu yasifikiwe kutokana na mashabiki kususia bidhaa za timu kwa asilimia flani.
 
GSM Yanga kaingia lini?
 
Wanaofanya usajili Simba sidhani kama wana uelewa wa mpira kabisa. Nildhani kwenye dirisha hili dogo ndio ungekuwa muda sahihi wa THANK You kwa Boko na Saidoo lakini badala yake eti wanambembeleza Saidoo akubali kusaini mwaka mmoja. Mapungufu makubwa mawili kati ya mengi yaliyopo kwa sasa Simba ni kiungo mkabaji na mshambuliaji wa kati anayejua kufunga kwa kutumia nafasi nyingi zinazotengenezwa na viungo na mawinga. Hayo mapungufu mengine achananeni nayo siyo makubwa sana yatazibwa wakati wa dirisha kubwa. Nilitegemea mpaka sasa hivi Simba ingekuwa imeshawapeleka kambini kiungo mkabaji na mshambuliaji wa kati ili waanze kuzoeana na wenzao.
 
Ngoja tuone, nahisi watakuwa wanafinalize baadhi ya vitu ili hayo maeneo yaletewe watu
 
Wazee wa 10 percent hawawezi kukubali boko na said waondoke maana ndio vitega uchumi vyao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…