TFF hakikisheni Simba inakuwa ya pili ili iungane na Yanga kuiletea nchi heshima. Sio Azam

hizi ndizo akili za watanzania kwenye swala la Simba na Yanga....leo hii miaka nenda miaka rudi timu pinzani ni mbili kwenye taifa lenye watu milioni 60,hamtaki mabadiliko hadi mnaomba kupangiwa matokeo.....maana ya kuwepo ligi ni nini sasa,ndio maana soka letu halikuwi kwa ujinga kama huu.
 
Azam wana matatizo yao ambayo yana wafelisha ndani na kimataifa ila naamini iko siku watafika mbali kwenye ramani ya soka la hapa ndani na kimataifa.

Si busara kutoa maoni yasiyokuwa na mashiko kila timu ina haki ya kutumia nafasi iliyoipigania katika ligi hata hao simba wamefanya nini msimu huu,leo hii Yanga ni bora kuliko simba kwa nini asiende yanga peke yake kimataifa kwa sababu atafanya vizuri kuliko simba.
 
Ndio maana nimetoa mifano hai, Liverpool 2005 na 2006 mwaka mmoja walichukua ubingwa wa Ulaya na mwaka Final bila kuwa bora katika league ya nyumbani, kwanini? experiance inawabeba. Simba mwaka huu sio wazuri lakini hawakufanya vibya Africa, kwanini? experiance. Azam nafasi zote huko Africa waliambulia knockout round za mwanzo tu. Azam haiwezi kubadilika japo wana kila kitu kuifanya team ishindane na wakubwa na sababu viongozi wanazi wa hizi team kubwa. Azam abaki kucheza na kina Mashujaa tu ndio level yake.
 
Watanzania akili huwaruka kwenye usimba na uyanga,unaona hata mziki una mabadiliko lakini sio mpira wa miguu wa Tanzania hata mtoto wa 2007 anazaliwa kisha batizwa usimba na uyanga,leo Azam fc ingekuwa na mashabiki wengi waliozaliwa miaka ya juzi juzi lakini wapi,natamani sana ligi yetu iwe na top 4 kama wengine lakini haiwezekani,hata ukiangalia uwezo wa wachezaji wa wazawa wanaocheza timu zingine za ligi kuu tofauti na simba,Yanga na Azam uwezo wao unasikitisha sana kwenya maamuzi.....watu wameweka nguvu kubwa sana kwa simba na yanga hawajui kama wanadidimiza soka letu.
 
Kama Itatokea Simba kupewa nafasi hiyo ligi yenu itakuwa ni taka taka
itakuwa haina maana,leicester city walienda kushiririki Uefa na wakiwa hawana uzoefu wowote wakaliwakilisha taifa kubwa lenye timu zenye uzoefu mkubwa katika mashindano ya ulaya?
 
Narudia tena Liverpool hakupewa mbeleko na chama cha soka England kushiriki klabu bingwa bali wao wenyewe UEFA waliamua kurekebisha sheria kwavile ndio kwa mara ya kwanza michuano ya UEFA champions league ingecheza pasipo kuwepo kwa bingwa mtetezi tokea yaanzishwe. Hivyo wakarekebisha sheria kuwa bingwa wa UCL atakuwa ame qualify moja moja kucheza UCL msimu unaofuata bila kujali kwenye ligi kuu atashika nafasi ya ngapi
 
Kama Itatokea Simba kupewa nafasi hiyo ligi yenu itakuwa ni taka taka
itakuwa haina maana,leicester city walienda kushiririki Uefa na wakiwa hawana uzoefu wowote wakaliwakilisha taifa kubwa lenye timu zenye uzoefu mkubwa katika mashindano ya ulaya?
Shida ndio hapa unataka kufananisha integrity ya EPL na NBC yetu, vitu viwili tofauti. Mimi sijasema wapewe unless kama sheria inaruhusu kuteuwa basi aende Simba lakini kwenye hili wala usiumize kichwa ni AZAM wenyewe watampa Simba kwa maelekezo ya juu watapoteza point tu katika mechi 2 hizi kwa makusudi kabisa. Kama kweli wako serious kipimo chao mechi hizi mbili.
 
Nimekuelewa vizuri na wala sibishi, ila nakwambia atakempa Simba wala sio TFA ni Azam wenyewe sababu wanajijuwa hawana malengo yoyote. Huu mwaka tunajuwa Azam wako vizuri kuliko Simba kwenye league yetu iweje Azam katika ubora wao wanagombania nafasi ya pili na Simba team inayo struggle. Na nafasi hii ya pili watampa Simba tu watadondosha point kusudi tu. Unafungwa 3 bila na Simba, Simba mbovu kuliko miaka ya nyuma na wewe ndio unasema uko katika ubora. Team inacheza utasema hawana wanachogombania.
 
Kama Itatokea Simba kupewa nafasi hiyo ligi yenu itakuwa ni taka taka
itakuwa haina maana,leicester city walienda kushiririki Uefa na wakiwa hawana uzoefu wowote wakaliwakilisha taifa kubwa lenye timu zenye uzoefu mkubwa katika mashindano ya ulaya?
Huko kwa Leicester city umeenda mbali sana, angalia wa Afrika wenzetu Kaizer chief, Orlando Pirates, Zamalek, n.k wanaweza kukosekana kwenye kuwakilisha nchi zao pamoja na kuwa na uzoefu.
 
Hapo sawa kama Azam fc ataachia mwenyewe sina tatizo.
kuiga kilicho bora sio dhambi mkuu....binafsi napenda ligi yenye upinzani sio anacheza Yanga na Dodoma jiji unajua laizma yanga ashinde.
 
Maisha yanaenda Kasi Leo mnyama anabebeleza ushindi wa pili
 
Mkuu baada ya mechi kumalizika urudi hapa Azam anamaliza nafasi ya pili msimu huu.
 
Mpaka sasa wenye advantage ya nafasi ya pili ni Azam kwa idadi ya magoli. Ngoja tuone mechi mbili zilizobakia. Mechi inayofuata Azam anacheza na Kagera Chamazi na uzuri raundi ya 29 na 30 mechi zote zinachezwa kwa wakati mmoja.
 
Mpaka sasa wenye advantage ya nafasi ya pili ni Azam kwa idadi ya magoli. Ngoja tuone mechi mbili zilizobakia. Mechi inayofuata Azam anacheza na Kagera Chamazi na uzuri raundi ya 29 na 30 mechi zote zinachezwa kwa wakati mmoja.
Ushindani kwenye league na integrity(uadilifu kama sijakosea) ndio ubora wa mashindano. Mimi na uhakika Azam watafanya nini najuwa maana hata kama wanacheza muda sawa shida ya Azam ni ile ile kushabikia team kubwa anaoshindana nao. Azam wanajuwa nini cha kufanya, dondosha point na Simba anajuwa funga magoal. Hizi mechi 2 ndio zitaonesha uadilifu wa league yetu. Kufungwa kupo lakini vita ionekane.
 
Lakin wanenda wasiokuwepo Super League.. Kina Azam hao
Hapana wanaenda timu zilizochukua ubingwa na timu zinazoshika nafasi ya pili endapo shirikisho la soka husika wamekidhi vigezo vya kuingiza timu mbili klabu bingwa. Timu zitakazoshika nafasi ya tatu na nne zitaenda CAFCC kwa mashirikisho yenye vigezo vya kuingiza timu nne
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…