The Buzwagi Saga: Karamagi aenda kusaini Mkataba wa ULAJI London

System ya Tanzania ilivyo huwezi hata kuwasiliana na wabunge kwa e-mail sababu majority yao hawajui hata what is email. Sasa how you gonna complain?

Magazeti makubwa kama Nipashe, Majira and others will not take your complain and publish in the front page, sababu editor ana kadi ya kijani ndani. So, system is so complicated.

One thing i can demostrate is to consult Mr Zito that Tanzania siasa ni kichwa cha mwenda wazimu, go back to school and earn your PhD, then just utilize your knowledge to your fellow Tanzanian. I know if we can't stand then who will stand, but rememember we are fighting with CCM (chama cha Majambazi), and on top of that Zito hana waku msupport sababu wapinzani ni wachache na wote wanatunza viti vyao.

Smart move, iandikwe barua ya wazi ambayo itafanyiwa petition na majina atleast 500 humu JF kisha ichapishwe kwenye magazeti makubwa mawili amabyo itamuuliza kikwete yeye kama Mweneyekiti wa Chama Cha Mapinduzi nini msimamo wake katika swala la Zito, na spika sitta nini msimamo wake.
 
Mtanganyika,

Mbona baadhi ya maandiko yako ya kiingereza ngumu sana kuyaelewa?

Najua kila mtu ana matatizo kwenye hizi lugha, ila kwa ushauri wangu jitahidi kuyapunguza hayo makosa kwa ku review posts zako kabla ya kutuma.

Pia naona tatizo ni kuandika, sijui uko wapi lakini jitahidi kuchukua course hata ya miezi michache ili kuongeza ufanisi katika maandishi yako.

Naomba usichukie na badala yake take it as a challenge. Wote tuna matatizo na wakati mwingine ngumu kujua mpaka mtu mwingine akuambie.
 
Chakaza
[QUOTE Malecela anapewa heshima sana ndani ya CCM katika kuendesha mambo kihuni.Angalia hata katika kuchangia hoja za kumfungia Zito,yeye kapangwa kuwa msemaji wa mwisho na kabla hajazungumza eti anaitwa Zito azungumze kama ana lolote la ziada(kuomba radhi) kabla HAKIMU mkuu Malecela hajapitisha hukumu.
Hii ni aibu sana. Hata hivyo kama ilivyotegemewa na wengi SHUJAA KIJANA WA KITANZANIA ZITO KABWE hakubembeleza wanafiki na wasaliti wa nchi hii bali aliwaambia wafanye vile watakavyo na kuwa fikra za kimapinduzi zitadumu.Wazee kama hao wasubiri aibu mwisho wa safari kisiasa[/QUOTE]

Kwa kweli sababu ya MAlecela, ambaye ni Makamu MWenyekiti wa CCM, na Spika wakati anampa nafasi alirudia mara mbili kusema, Meheshimiwa Mbunge Malecela, Mheshimiwa Mbunge Malecela..." hii ni kujaribu kufuta akilini mwaka mkakati wa kichama uliomopanga Malacela kusema mwisho... Na ndio maana badala ya kuacha wote waseme ndio amuulize Zitto kaama ana cha kusema, anamuuliza kabla ya "mtu anayetakiwa kuhitimisha mkakati wao wa Kijambazi"

Lakini watu kama "Mugongo Mugongo" na Jamaa yangu wa Pwani... kwanza majina yao yana maana mbaya sana na ashakum si matusi naomba tuwaombee dua kwa Mungu awape ufahamu wa kutambua wayafanyayo hata kama ni ile ya "Mtumikie Kafiri" lakini wazinduke na kuibua hoja za kutetea taifa maana nawaona ni watu waliozaliwa na uwezo mkubwa wa kujenga hoja lakini wanapindisha makusudi kama walivyofanya mabosi wao ndani ya Bunge jana usiku
 

sidhani mahala nilipo panasaidia nini kuhusu kuandika kwangu. I don't think at this point any course will make any life easy.

I don't take things personal, but we differ on tones, probably you find hard to understand my tone for some reasons. I wish i could help, but at this point i'm sorry.

third, i used kiswahili almost the entire post, however english is the second language so keep up with it.

Thanks for concern
 
Mtanganyika,

Sawa, post niliyoongelea ni ile ya kwanza ambayo umetumia kiingereza kwenye post yote.

Pili suala la uko wapi, lililenga kwenye kuonyesha urahisi wa kupata course ya kukusaidia. Najua TZ ni ngumu na aghali sana
kwa mtu kujiendeleza kuliko sehemu zingine. Samahani kama kuuliza hivyo ulinielewa vibaya.

Lilikuwa ni wazo tu na njia ya kusaidiana na kuelemishana.
 
GAzeti la Mtanzania la leo story yao imeandikwa na "Mwandishi Maalumu" wakati wana mwandishi wao kule Dodoma anaitwa Dilunga,lina kichwa kisemacho, "Zitto Kabwe hoi bungeni" likiwa na habari ya mapema yaani imeandikwa na wenyewe na kupelekwa.. walijaribu kufanya hivyo katika magazeti mengi ikashindikana ila hapo kwa sababu ni la kwao wakaweka. Hiyo imewadhalilisha sana. Inaonekana Mhariri amewaumbua kwa kuweka "mwandishi maalumu' kukwepa kuwajibika kitaaluma kwa wanaaaluma wenzake ambao wameona dhahiri kuwa si ya mwandishi wa gazeti hilo.

Huo ndio UTATU MTAKATIFU unajidhihirisha.. EL alikua akiishi nyumba moja na Rostam.. alipopanda akamwachia nyumba Rostam na KAramagi akakaribishwa na Rostam... Iko kazi hapo.. hayo ni makoti ya hali halisi, ukweli uko ndani ya hayo makoti
 
Wanasheria wawili wamenipigia simu wanasema, wa kwanza "jana usiku nilitamani kumaliza hasira katika TV yangu., lakini nikavumilia kabla ya kuamua kwenda kulala... Nina hasira na kuanzia leo niko tayari kwa gharama zote kuhakikisha hii vita inaendelea. Sina ushabiki na chama chochote" , mwingine akasema, "nilikasirika sana na ujinga wa kupita kiasi ulioonyeshwa na wabunge wetu wa CCM, lakini nadhani huu si wakati wa kukasirika ila ni wakati wa kutafakari HATMA YA TAIFA LETU... Tunakwenda wapi? Je, nani atazuia UFISADI ikiwa PCCB inasafisha wala rushwa, inafunga midomo waandishi wa habari na Bunge linegeuka mtetezi wa ufisadi... AMANI YA TANZANIA INAELEKEA KUTOWEKA SIKU SI NYINGI"
 

Spot on bro!
 
HAya mwingine anakuja na kusema, "HUyu Zitto hajui kwamba anataka kumharibia KAramagi katika mbio zao za kuwa Waziri wa Fedha? kama THISDAY walivyomharibia Dr Dau kushika TRA?" aache kabisa kuwagusa wenzake ambao wako busy kupanga safu
 
Mi nadhani hoja ya msingi iwe ni mkataba huu aliosaini Mh. Karamagi kama una maslahi ya kweli kwa nchi na tushawishiwe na tujiridhishe kuwa huu mpya wa mwezi feb. 2007 ni tofauti na ile mingine ambayo wajanja wachache walijipatia 10% zao wakawaingiza Watanzania mkenge!
Sasa basi na mimi kwa kuchelea kutoka kwenye hoja ya msingi napendekeza, napigia debe na nataka mkataba huu mpya uwekwe wazi bungeni ujadiliwe ili na sisi wananchi tupate kujua yaliyomo na niliyogusia hapo awali tuyapambanue.
Bado nakubaliana na hoja ya Hayati Mwl. Nyerere kuhusu kuyaacha madini mpaka ambapo sisi wenyewe tutajenga uwezo wa kuyachimba. Pili nilifarijika jiasi na taarifa aliyoitoa Mh. Rais ya kwanza, kusitisha uingiaji mpya wa mikataba na pili, mapitio ya mikataba ya zamani.
Nisingependa tena kupata aibu ya viongozi wangu wa nchi wakienda kutudhalilisha Watanzania nje ya nchi kwa kuwaomba waanze kulipa kodi ya mapato..aibu! Wakati mikataba waliingia wenyewe wakiangalia matumbo yao tu na kuwatoa kafara Watanzania!

Ya zitto kusimamishwa vikao vya bunge naomba nitakapopata majibu ya Mh. Karamagi hapa JF, niyapitie kama ambavyo napitia hoja Mh. Kabwe, ndo nitoe maoni yangu
 
Mtanzania,
Nisaidie kunitafutia hiyo kozi 🙂
Gagnija,
Hapa nilipo zipo nyingi tu ila tatizo ni muda na mapesa ya kulipa.

Haina maana matatizo yote yataisha ila kuna makosa ambayo ni very obvious, hayo yanaweza kutatuliwa kwa course moja tena ya bei poa kabisa. Vipi huko uliko hakuna Open University? Ungelikuwa UK, ningekuambia jaribu OU au kwenye chuo chochote kwenye mji wako. Uzuri wa nchi za wenzetu kila palipo na mapungufu unaweza kwenda kusoma.

Siku moja nilikuwa bored nikaamua kusoma kupika kwa wiki mbili kwa pounds 50. Nikifurahi nawapikia wanangu.
 
Mtanzania,
Hapa nilipo tunayo OUT, lakini katika kona ya nchi ninayoishi sidhani kama itakuwa rahisi. Hata hivyo nashukuru sana kwa ushauri.
 
EL alikua akiishi nyumba moja na Rostam.. alipopanda akamwachia nyumba Rostam na KAramagi akakaribishwa na Rostam... Iko kazi hapo.. hayo ni makoti ya hali halisi, ukweli uko ndani ya hayo makoti

This is such a monumental discovery! Enhe, leta habari za mabibi zao sasa.
 

PCCB = Preventing and Cleaning Corrupt Burglers
PCCB = Previnting and Cleaning Corrupt Bandits
 
Malecela sawa na Kingunge wana mawazo finyu na ya kizamani , wamejewa fitina na usongo sawa na Mudhihiri nk lazima asimame aonyeshe u CCM kuwa mbele.

Zitto is a hero maana hakuna maisha bila ya historia . Tanzania we had Mwalimu, Kenya D Kimathi, SA -Mandela, Ghana -Nkrumah nk .Huwezi kuchimba dhahabu ama almasi bila kwanza kuingia machafuni uzoe taka then upate dhahabu ikiwa safi baada ya kutoka jasho . Zitto kaza uzi historia na sisi Watanzania tuna angalia, hongera sana na usijute kusimamishwa maana Sitta alionyesha nia ya kutaka usimamishwe tangia mwanzoni akiwa na wapambe wenzake akina Buriani.
 
Uwe unasoma kwanza kabla ya kupost. Hiyo habari imeshajadiliwa sana kwenye thread nyingine.

Siyo rahisi kama unavyodhani kupitia threads za JF ili kuhakikisha kwamba thread unayotaka kutuma imeshatumwa au la. Halijaharibika neno kwani hii inaweza kuunganishwa na ili nyingine au ikafutwa.
 
Bunge la chama kimoja halitatufikisha popote Watanzania! Yaani ishu zote Bungeni Watanzania zaidi ya milioni 35 tubategemea wabunge wanne au watano ambao ndio wanao ongea kila siku...Zitto Kabwe, Halima Mdee, Dr Slaa, Ndesamburo basi! Wengine wako wapi?

Sheria ya chama kuwa na mamlaka ya kumfuta uachama mbunge na akawa si mbunge tena kwa kufukuzwa uachama kunafanya wabunge wa CCM wawe mabubu!!

Kwa kifupi mfumo mzima wa utawala wa nchi hii una walakini mkubwa sana na umepitwa na wakati. Katiba inatakiwa kuandikwa upya au la basi ifanyiwe reshuffle kubwa sana!

Yote ni yote, adui yako muombee njaa. Viongozi wetu wanahahakikisha Watanzania ni wenye njaa muda wote, wasio na elimu ya kutosha ili iwe rahisi kuwarubuni na hata kuwaibia kura kipindi cha uchaguzi! Niliwahi kusema hapa kwamba kizazi hiki hakitashuhudia mabadiliko nchi hii, labda kizazi kijacho! LABDA!!
 

Hii haitusaidi chochote bila kujua majibu ya waziri. Ungeambatanisha majibu ya waziri ndipo tungeweza kulinganisha hoja na jibu na hivyo kujua wapi hoja zilizidi majibu na wapi majibu yalipozidi hoja.
 
Mapak kieleweke shukrani kwa kutuwekea hoja za Zitto, ngoja nizipitie.

Mzee Lunyungu
Good to see you back!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…