The Buzwagi Saga: Karamagi aenda kusaini Mkataba wa ULAJI London

The Buzwagi Saga: Karamagi aenda kusaini Mkataba wa ULAJI London

Ndugu,
Place of signing kisheria is an issue, kwa sababu inabidi kufuata sheria za mahali mkataba ulipo sainiwa! Poor Tanzanian what a shame waziri mzima anakimbia na mihuri yetu kwenye brief case/rambo/Koti???? ili akasaini mkataba Ulaya???

Insane!

Wewe, ni mizito hiyo wanavyosema; inawezekana iliwekwa kwenye kikapu au tenga kabla ya kupakizwa kwenye ndege ya Tanzania inayo PAA kuelekea Great Britain!!🙂

SteveD.
 
Ndugu,
Place of signing kisheria is an issue, kwa sababu inabidi kufuata sheria za mahali mkataba ulipo sainiwa! Poor Tanzanian what a shame waziri mzima anakimbia na mihuri yetu kwenye brief case/rambo/Koti???? ili akasaini mkataba Ulaya???

Insane!

Thank you, I was not aware of this; however, I knew of the need to be specific so that the alibi of signatories at the time of signing is made clear. That is why the place, day, date, year and the time of signing must be stated.
 
let me leave for now so that you can have time to prepare for preparation for purchase of fuel helicopter for country tour!!!

Hata kama ni kutumia helikopta kwani shida iko wapi? Cha msingi ni walala hoi wafikiwe na ujumbe wazinduke usingizini watumie nguvu yao ya kura kuwaondoa wezi hawa!

Hapa ndugu ni kume kucha hao wezi lazima suruali ziwabane.. AROBAINI YAO INAKARIBIA.

Nani ajuaye? Labda Mungu aliamua wapiga upofu wabunge wooooote wa CCM waka kosa hekima ili haya yatimie. Kwa wale wamuaminio MUNGU, Hujibu maombi kwa njia mbali mbali.
KAWAPIGA UPOFU WA AKILI WAKALEWA MADARAKA NA KUJISAHAU.. SASA WANA STUKA MAJI YAMEISHA MWAGIKA!!!

kaa tayari!
 
Sidhani kabisa kama kusaini mkataba nje ya nchi ni tatizo. In fact hata JK na Mkapa wameshasaini mikataba nje ya nchi kama vile
ule wa Microsoft na serikali ambao kama sikosei JK alisaini kule South Africa.

Tatizo hapa ni kwamba kwanza walisimamisha kusaini mikataba ya madini, pili hata waliposaini walifanya kimya kimya bila kutangazia umma na baada ya hapo wakalificha hata bunge. Hapo ndipo panaponuka hasa.

Zitto aliposema hawakwenda hata kusainia kwenye ubalozi wetu naona hapo ndipo aliwamaliza. Kuna mambo mengi bado wanaficha kuhusu hili jambo.
 
Nimeona hii MOU na Microsoft nayo haina mahali pa kusainia japo ilisainiwa Cape Town,SA.

http://www.tanedu.org/MOU_between_Microsoft_and_Tanzania_(signed_CapeTown_11th_July_2006).pdf


A memorandum of understanding (MOU) is a legal document describing a bilateral or multilateral agreement between parties. It expresses a convergence of will between the parties, indicating an intended common line of action and may not imply a legal commitment. It is a more formal alternative to a gentlemen's agreement, but in some cases, depending on the exact wording, lacks the binding power of a contract.
 
Guys!!! Let me ask, assume IPTL and RICHMOND was signed in Statehouse or Kwenye nyumba za dini, does it make a good contract,,,? naomba tujadili kama mkataba ni fake and not where it has been signed guys, let THINK BIG...

It is still doesn't click to me, if this is real issue unless you are saying the contract itself is fake and in addition to that it has been signed in HOTEL...

Kili,

I agree a contract is a contract regardless of premises where it wil be inked. however what Zitto is implying between the lines is that even Ubalozi had no idea of this contract and the signing!

Then the question becomes why such secrecy on the contract and the signing? This is where Karamagi appears to be in violation with Presidental decree to suspend all signing of mining contracts unless JK alitulaghai wananchi kwenye Tovuti!
 
Kichuguu,

Nakubaliana nawe kwamba kuna tofauti kati ya MOU na contract ila tu njia zinazotumika kusaini MOU na contract sitegemei ziwe tofauti.

Kuna uwezekano mkubwa kabisa kwamba hata contracts nyingi kuandika sehemu iliposainiwa sio muhimu sana. Hata mikataba yangu ya kazi naona hakuna sehemu inayoonyesha wapi ilisainiwa ila tarehe ya kusaini ndio muhimu.

Labda wanasheria watusaidie kutuelezea umuhimu wa kuandika sehemu ambapo mkataba ulisainiwa.
 
Kali nyingine hii hapa. CCM imejifunga bao!!!!.
kp2wa4.jpg

Kichuguu,

I like this one, it was a massive own goal! Who should be blamed for the goal?
 
Sidhani kabisa kama kusaini mkataba nje ya nchi ni tatizo. In fact hata JK na Mkapa wameshasaini mikataba nje ya nchi kama vile
ule wa Microsoft na serikali ambao kama sikosei JK alisaini kule South Africa.

Ok, Hoja hiyo hapo juu tumekubaliana tuiachie hapo,,, twende mbele.

Tatizo hapa ni kwamba kwanza walisimamisha kusaini mikataba ya madini, pili hata waliposaini walifanya kimya kimya bila kutangazia umma na baada ya hapo wakalificha hata bunge. Hapo ndipo panaponuka hasa.
Hoja mbili...

KWANZA: Walishasimamisha, tupate sehemu ilipoandikwa ili twende vizuri, samahani probably I'm slow learner msiniache wenzio nimesoma shule ya KALUMANZIRA

PILI: (a) Ilisainiwa kimnya kimnya, well done, kuna kanuni inayolazimisha mikataba isainiwe kwa kishindo?
(b) Walificha hata bunge! Mbona Waziri alijibu siku ya kwanza kwamba kweli alisaini ulaya/uingereza.

Zitto aliposema hawakwenda hata kusainia kwenye ubalozi wetu naona hapo ndipo aliwamaliza. Kuna mambo mengi bado wanaficha kuhusu hili jambo.

What changes ukisaini kwenye ubalozi? Kuna vifungu vinabadilika, well hii ni sawa na hoja ya kwanza ambayo tumekubaliana juu... twende mbele
 
Dua Kwa nini unaruka ruka, nimekuomba url ya Hotuba ya JK ya mei mosi... sasa huleti nisome mwenyewe na mimi sitaki kuambiwa na JF member nataka from original source... kama huna tulia wengine wataniletea...

JF,,, aliyo nayo aniletee please.

jaribu website ya serikali
 
Ni nani anakumbuka mjadala wa "waTanzania, au wapiga kura wa Tanzaniakuwa ni wajinga?"

Kwa maoni yangu, "Viongozi wa Ushindani" ndio bado ni wajinga. Hawajajua namna ya kuutumia ushindani wao kuwashawishi wananchi ambao ni 'welevu' sana; ili wawaunge mkono.

Linalosikitisha ni kuwasikia akina Mbowe wakati huu tena wakitilia msisitizo kutumia "Helikopta" kutembelea mikoa. The entire important message gets lost in trivialties of the helcopter!
Kalamu,

Nadhani wewe hukuwa kwenye maandamano na mkutano, la sivyo usingeandika haya. naona wewe umandika kutokana na ulichosoma magazetini au mtandaoni. Kwa taarifa yako viongozi wamezungumza mambo ya maana sana ambayo yametukuna sisi waandamanajimagazeti ambayo yaliona helikopta ni laini yua kuuzia message yao. Lakini katika hotuba nzima ya Mbowe hilo ni neno lililosemwa kwenye sentensi moja tu.
Jihadhari kufanya uchambuzi kwa kutumia tu message za magazeti.

Sisi tulio 0nthe ground tunajua kinachoendelea sasa. Vuta subira mdogo wangu siyo wewe tu mwenye kuona mbali katika hili. Wapo wengi na kazi imeanza, usianze kulaumu kabla ya hata kujua kinachoendelea.
Kichwamaji:
Nyinyi mliopo 'on the ground' na mnaosoma hisia za wananchi ni mhimu pia muwatahadharishe viongozi wawe na uangalifu katika matumizi ya maneno na vitendo. Kama magazeti yamerukia hiyo sentensi moja tu ya helikopta, wewe hapo huoni kuwa hayo maneno hayakuwa na umhimu wowote katika ujumbe aliotaka kuufikisha Mbowe? Hayo maneno yameongezea uzito gani katika hoja yake, licha ya kuondoa uzito katika jambo lililosababisha maandamano hayo? Ma-Hummer, ma-Helikopta yanaongeza nini. Of course, waandishi wa habari had all the right to zoom-in on these distractors; what do you expect? Na kama mimi ni mwanakijiji kule Ikwiriri I will certainly take note of these symbols na kuziunganisha na wanasiasa wenyewe.

Sipendi kulaumu, lakini ninaamini kuwa kazi ni kubwa mno inayowakabili hao viongozi uliowaona hapo Jangwani. Pengine wewe katika kuwasoma wananchi waliohudhuria maandamano hayo unaweza kuwa na matumaini ya mageuzi katika mwenendo mzima wa siasa katia nchi yetu, mimi sijui. Ndio maana ninaogopa kulaumu, ila niko radhi nivute subira nione hao viongozi watakavyoitumia nafasi kama hii aliyoianzisha Kabwe katika kutuonyesha kuwa kweli tunaweza kuwaamini na kuwapa kura zetu, badala ya zimwi lile lile tulilolizoea miaka yote. Zimwi ambalo nadhani sasa limeishiwa na subira kabisa katika kuwaibia waTanzania urithi wao waliojaliwa na Mwenyezi Mungu.

Hatuhitaji kiongozi malaika; lakini nadhani wananchi tunahitaji kuona dalili za uadilifu na upenzi wa dhati kabisa kwa nchi yetu hii Tanzania.
 
Tatizo hapa ni kwamba kwanza walisimamisha kusaini mikataba ya madini, pili hata waliposaini walifanya kimya kimya bila kutangazia umma na baada ya hapo wakalificha hata bunge. Hapo ndipo panaponuka hasa.

Extract ya Hotuba ya Mh. Rais, kwenye mei mosi 2007, paragraph zinazohusu madini

Mikataba ya Madini,

Ndugu Wananchi;

Jambo lingine ambalo nililizungumzia mwaka jana lilihusu mikataba ya madini. Katika hotuba yangu ya Shinyanga nilizungumzia haja ya nchi yetu kutazama

upya mikataba hiyo ili tuweze kunufaika na rasilimali ya madini aliyotujaalia Mwenyezi Mungu. Nilisema pamoja na kuthamini sana mchango wa Makampuni ya madini yaliyowekeza hapa nchini, bado kuna haja ya kuweka utaratibu mzuri utakaotuwezesha sisi wenye rasilimali nao tufaidike.

Aidha, niliagiza Wizara ya Nishati na Madini ishirikiane na Wizara ya Sheria na Katiba, Wizara ya Uchumi, Mipango na Uwezeshaji na Wizara ya Fedha na makampuni husika kuangalia upya Sheria yetu ya Madini na mikataba tuliyowekeana kwa lengo la kufanya marekebisho stahiki.

Katika kutekeleza agizo hilo , Agosti 10, mwaka wa jana Kamati Maalum ya majadiliano ya mikataba ya madini iliundwa. Kamati hiyo ilikuwa na jukumu la kufanya mashauriano na Tanzania Chamber of Minerals and Energy (TCME) kuhusu mfumo wa kodi katika sekta ya madini. Pia ilikuwa na jukumu la kufanya majadiliano na makampuni ya madini yenye mikataba ya madini na serikali kwa lengo la kurekebisha kasoro zilizopo.



Ndugu Wananchi;

Nafurahi kuwafahamisha kuwa, majadiliano kati ya serikali na makampuni makubwa ya madini hapa nchini yamekuwa na mafanikio. Tayari kampuni ya Barrick Gold Tanzania Limited na Resolute Mines Tanzania Limited zimekubali kuondoa kipengele cha kivutio cha asilimia 15 kwenye salio la gharama ya uwekezaji katika migodi yao . Hatua hii itayafanya makampuni haya sasa kulipa kodi ya mapato miaka michache ijayo tofauti na ilivyokuwa kabla ya hapo ambapo yasingelipa kodi kwa uhai mzima wa migodi yao .

Mazungumzo yanaendelea na makampuni mengine kufanya kama ilivyokuwa kwa makampuni haya mawili. Muda si mrefu nchi yetu nayo itaanza kunufaika ipasavyo na utajiri mkubwa wa dhahabu tuliyojaaliwa na Mwenyezi Mungu.

Kampuni ya Barrick Gold pia imekubali kuilipa serikali kiasi cha dola za Kimarekani milioni 7.0 kwa mwaka kwa kila mgodi inaoumiliki kuanzia mwezi





Desemba, 2006 hadi mwaka 2010. Malipo hayo ni mbali na dola za Kimarekani 200,000 ambazo kampuni hiyo na ile ya Resolute itazilipa kila mwaka Halmashauri za wilaya ambako kuna migodi yake.

Hivi sasa tunapitia Sera na Sheria yetu ya madini kwa lengo la kuzifanyia marekebisho stahiki katika muda si mrefu ujao. Nia yetu ni kuwa na sheria ya madini itayohakikisha kuwa pande zote mbili zinanufaika sawia yaani sisi wenye rasilimali ya madini na makampuni ya uwekezaji yenye fedha na teknolojia. Tunataka Sheria hiyo ituwezeshe kuwa na mazingira ambayo Waingereza wanayaita ¡°win¨Cwin situation¡±, yaani wao wanapata na sisi tunapata.

Inawezekana nina makengeza,,, naomba kuona sehemu mikataba iliposimamishwa!
 
Article nyingine kuhusu Mambo ya Mikataba ya Madini:

Kwa uelewa huu kipengele cha 15% kiliondolewa tangu 2004... hivyo tunahitaji data kama kipengele hicho bado kiko kwenye mkataba wa sasa huu unaoleta utata!

Serikali inafanya marekebisho katika sekta ya madini ili kupata faida na mapato zaidi kwa ajili ya wananchi wake.

Katika marekebisho hayo, Serikali imeshafanya majadiliano na kukubaliana na kampuni za Barrick Tanzania Limited (inayomiliki migodi ya Bulyanhulu ulioko wilayani Kahama, Tulawaka ulioko wilayani Biharamulo; na North Mara ulioko wilayani Tarime) na Resolute Tanzania Limited (inayomiliki mgodi wa Golden Pride ulioko wilayani Nzega) ili kuyawezesha kampuni hizi kulipa kodi na ushuru stahili kwa Serikali.

Katika majadiliano hayo kampuni hizi zimekubali kuondolewa kwenye mikataba baadhi ya vivutio vya ziada ikiwa ni pamoja na nyongeza ya asilimia 15 kwenye mtaji wa uwekezaji ambao haujarejeshwa/kukombolewa (15% additional capital allowance on unredeemed qualifying capital expenditure). Hatua hii itawezesha kampuni hizi kukomboa gharama zao za uwekezaji mapema na hivyo kulipa kodi ya mapato (corporate tax). Endapo kipengele hicho kisingeondolewa, kungekuwa na uwezekano mkubwa wa kampuni hizo kutolipa corporate tax.

Serikali bado inaendelea na majadiliano na kampuni ya Geita Gold Mine Limited inayomiliki mgodi wa Geita ili nayo ikubali kufuta kipengele hiki kwenye mkataba wake. Hata hivyo, Serikali tayari ilisharekebisha kipengele hiki cha 15% additional capital allowance on unredeemed qualifying capital expedicture, kilichokuwa kwenye Sheria ya Kodi ya mwaka 1973 ambayo ilifanyiwa marekebisho. Sheria ya Kodi ya mwaka 2004 haina kipengele hicho tena, hivyo mikataba mipya ya madini haitakuwa na kipengele hiki.

Pamoja na suala la ulipwaji kodi ya mapato (corporate tax), kampuni hutakiwa kulipa kodi na ushuru mbalimbali ikiwemo mrabaha. Mrabaha wa asilimia 3 kwa madini ya dhahabu na madini mengineyo; na asilimia 5 kwa madini ya almasi na vito hulipwa Serikalini bila kujali kama kampuni inapata hasara au faida tofauti na kodi ya mapato (corporate tax) ambayo hulipwa baada ya kampuni kupata faida kwa kuondoa gharama za uendeshaji na uzalishaji. Kodi nyingine zinazolipwa na kampuni za madini ni pamoja na kodi ya zuio (withholding taxes) kodi za ajira (PAYE); ushuru wa forodha, stamp duty; ambapo ushuru ni pamoja na ada ya pango (annual rent), ada ya maombi na utayarishaji wa leseni za utafutaji (application and preparation fee); na ada za leseni mbalimbali za biashara ya madini.

Katika jitihada za Serikali za kuhakikisha sekta ya madini inachangia ipasavyo kijamii na kiuchumi inafanyia marekebisho Sera ya Madini ya mwaka 1997. Aidha, Sheria ya Madini ya mwaka 1998 nayo inafanyiwa marekebisho ili kuhakikisha usimamizi wa sekta ya madini unaihakikishia Serikali na wananchi wake mapato zaidi kutokana na rasilimali ya madini.
 
Katuni nyingine hii hapa. Spika wa Bonge la utukufua, Zito kashonwa mdono anaondoka na brief case yake yenye hoja nzito.


By kichuguu at 2007-08-19
 
Kuna mtu hapa JF anayeweza kuelezea hii "..........15% additional capital allowance on unredeemed qualifying capital expedicture,........" kwa lugha nyepesi kidogo what does it mean in real terms........ maana wananchi tunahitaji lugha nyepesi ati!!
 
Kutoka wikipedia

Capital Cost Allowance (CCA) is effectively the means by which Canadians may claim depreciation expense. Depreciable items are deemed to belong to different classes which depreciate at different rates and are subject to different rules. For the most common classes the value of all assets belonging to that class are accumulated in a pool, and the designated percentage for that class may be claimed on the balance in that class at the end of the taxation year. To prevent a flurry of tax motivated purchases in the dying days of a taxation year only half of net additions to the class are considered purchased in the year for purposes of the current year's calculation.

Some examples of asset classes are,

Class 1(Rate 4%): Buildings acquired after 1987 Class 3(Rate 5%): Building acquired before 1987 Class 8(Rate 20%): Assets not included in other classes Class 10(Rate 30%): Cars costing less than 30 000 Class 12(Rate 100%): Small equipment and tools costing less than 500 Class 13🙁no specific rate): Improvements made to leased premises Class 14🙁no specific rate): Franchises, Concessions, and Licences Class 17(Rate 8%): Parking lots Class 43(Rate 30%): Machinery and equipment used for production Class 45(Rate 45%): Patents acquired after April 26, 1993 Class 46(Rate 30%): Database and network equipment

In contrast to the practice followed in the United States for depreciation there is no penalty for failing to claim Capital Cost Allowance. Where a taxpayer claims less than the amount of CCA to which he is entitled the pool remains intact, and available for claims in future years. Unclaimed amounts are not subject to recapture.


Hii ni njia mojawapo ya kukwepa ulipaji kodi kwa madai kwamba unapata hasara etc.
 
Kilitime,

You have a point. na ndio maana tunataka kujua the content ya mkataba wenyewe (which is impossible), kuna mikataba nimewahi shuhudia na baadhi ya clauses zinatamkia sheria mahala ambapo imesainiwa ndio zitachukua mkondo in case kuna dispute...........only tume ndio ingetuambia au ndio ingetupa confidence level kuwa mkataba huo una maslahi kwa taifa na wananchi tusiwe na wasiwasi.........

I mean.....hivi kweli kati ya swala la Mengi Vs Malima na hili tunalozungumza hapa ni lipi lenye maslahi kwa wananchi ambalo linahitaji kuundiwa tume!! do we really need ku-spend money kwenye umbeya/kujipendekeza kwa malima/mengi than hili suala??

Note: katika majibu ya msingi ya Karamagi kwa hoja ya Zitto hivi kuna sehemu alikanusha kuwa mikataba ilisitishwa kusainiwa.........!!!!, nafikri kama ningekuwa Karamagi ningeanza na Kukanusha kuwa KWANZA MIKATABA HAIJASITISHWA KUSAINIWA and then bla blah blah blah..........waraka unapopita serikalini sio lazima wananchi mtangaziwe na JK kuwa nimepitisha waraka kusitisha signing ya new contracts hadi hapo negotiations zitapokamilika..........may be i overlooked that........i stand to be corrected
 
Kilitime,
Pamoja na maelezo yako hapo juu, nakuomba usome vizuri kipengele cha mwisho wa maelezo yote hayo ambacho kinasema hivi:-

Katika jitihada za Serikali za kuhakikisha sekta ya madini inachangia ipasavyo kijamii na kiuchumi inafanyia marekebisho Sera ya Madini ya mwaka 1997. Aidha, Sheria ya Madini ya mwaka 1998 nayo inafanyiwa marekebisho ili kuhakikisha usimamizi wa sekta ya madini unaihakikishia Serikali na wananchi wake mapato zaidi kutokana na rasilimali ya madini.

Na hili ndilo lilikuwa swali la Mheshimiwa Zitto isipokuwa Waziri wetu Karamage alijaribu kuepa swali kwa kuunganisha sheria ya Kodi ambayo imetajwa mwanzoni kutokana na mazungumzo kati ya serikali na Barricks.
Kwa kuelewa kwangu sheria hii ya madini ndiyo rais iliizungumzia ktk mahojiano ya VOA na kwingineko achana kabisa na makubaliano kati ya serikali na kampuni husika. Hii ni sheria (policy) ya nchi ktk sekta ya madini na haina makubaliano kama alivyokuwa akizungumzia Karamage.
Kwa hiyo Zitto hakuchanganya vitu kabisa ila waziri wetu ndiye aliyekwepa swali kwa kutaja sheria tofauti kabisa nje ya swali la Zitto.
Labda tukuulize wewe Je, hii sera na sheria ya madini zimekwisha rekebishwa?
 
Back
Top Bottom