Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,771
- 41,027
Taarifa zilizoingia muda mfupi ulipita ni kuwa Rais Kikwete amezuiwa na wananchi kuingia Buzwagi, na msafara wake umegeuza njia kurudi Bulyanhulu (ambako tayari alishatembelea). Mbunge anayewakilisha eneo la Buzwagi anaitwa James Lembeli. Huyu bwana alizungumza kabla ya Zitto, na Zitto hakujua kuwa hili suala lilishaletwa Bungeni na Mbunge huyo.
Hili hapa swali lake:
Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.
(a) Kwa kuwa hivi sasa mchakato wa mgodi mpya wa dhahabu wa Buzwagi ulioko nje kidogo ya mji wa Kahama unaendelea ikiwa pamoja na zoezi la kulipa fidia wananchi na wachimbaji wadogo wadogo waliokuwa wakifanya kazi katika eneo hilo, zoezi la kulipa wananchi linaonekana kuendelea vizuri lakini zoezi la kuwalipa wachimbaji wadogo wadogo waliokuwa wakifanya kazi katika eneo hilo hasa eneo la Mwime, Mwendakulima na Chapulwa linaelekea kuwa na matatizo makubwa kiasi kwamba Serikali inatumia nguvu.
Je, Waziri anaweza kulihakikishia Bunge lako Tukufu kwamba wananchi hao wachimbaji wadogo wadogo hawanyanyaswi na walipwe pesa zao kabla ya mashimo yao kufukiwa?
(c) Kwa kuwa utafiti wa madini katika eneo la Mwabomba katika Kata Idahina umeendelea kwa muda mrefu hivyo kuleta usumbufu mkubwa kwa wananchi wa eneo hilo ambao walikuwa wakitumia maeneo hayo kwa ajili ya kilimo na ufugaji.
Je, Serikali inaweza kuwahakikishia wananchi wa kata hii kwamba watafiti hao kama hawajagundua hayo madini wanaondoka?
ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION #
Answer From Hon. Ngeleja , William Mganga ENERGY AND MINERALS
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI :
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa James Lembeli, kama ifuatavyo.
Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa James Lembeli, kwa jinsi ambavyo amekuwa akifuatilia hatma ya wananchi wake katika jimbo lake kutokana na matarajio ya kuanzishwa mgodi wa Buzwagi katika eneo la jimbo lake.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza naomba kumhakikishia Mheshimiwa James Lembeli kwamba wachimbaji wadogo watapata haki zao kama inatarajiwa lakini pia kama alivyokiri mwenyewe kwamba zoezi la kuwafidia wananchi linaendelea vizuri na kwa kweli katika hili ni pamoja na wachimbaji wadogo, fedha kadhaa imeshalipwa na tunaendelea vizuri na tunaomba tu Mheshimiwa James Lembeli tuzidi kushirikiana naye ashirikiane na ofisi yetu na Wizara yetu kwa ujumla ili kuhakikisha kwamba wale wananchi wachache ambao bado hawajachukua na hawajaanza kupokea fidia zao tuwashawishi waanze kupokea.
Mheshimiwa Spika, la pili, utafutaji kama tulivyoeleza kwenye jibu la msingi unafuata sheria, naomba nizidi kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini kwamba Serikali haitaruhusu utafutaji au uchimbaji ufanyike kinyume cha sheria kwa hiyo tunazidi kuwahakikishia wananchi wa Jimbo la Kahama na hasa maeneo ya Mwabomba pamoja na Idahina kwamba watafutaji wa madini walioko pale wanafuata sheria na Serikali inafuatilia kuhakikisha hawakiuki sheria zilizopo ambazo zinawezesha kufanya hizo shughuli.
Hili hapa swali lake:
Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.
(a) Kwa kuwa hivi sasa mchakato wa mgodi mpya wa dhahabu wa Buzwagi ulioko nje kidogo ya mji wa Kahama unaendelea ikiwa pamoja na zoezi la kulipa fidia wananchi na wachimbaji wadogo wadogo waliokuwa wakifanya kazi katika eneo hilo, zoezi la kulipa wananchi linaonekana kuendelea vizuri lakini zoezi la kuwalipa wachimbaji wadogo wadogo waliokuwa wakifanya kazi katika eneo hilo hasa eneo la Mwime, Mwendakulima na Chapulwa linaelekea kuwa na matatizo makubwa kiasi kwamba Serikali inatumia nguvu.
Je, Waziri anaweza kulihakikishia Bunge lako Tukufu kwamba wananchi hao wachimbaji wadogo wadogo hawanyanyaswi na walipwe pesa zao kabla ya mashimo yao kufukiwa?
(c) Kwa kuwa utafiti wa madini katika eneo la Mwabomba katika Kata Idahina umeendelea kwa muda mrefu hivyo kuleta usumbufu mkubwa kwa wananchi wa eneo hilo ambao walikuwa wakitumia maeneo hayo kwa ajili ya kilimo na ufugaji.
Je, Serikali inaweza kuwahakikishia wananchi wa kata hii kwamba watafiti hao kama hawajagundua hayo madini wanaondoka?
ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION #
Answer From Hon. Ngeleja , William Mganga ENERGY AND MINERALS
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI :
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa James Lembeli, kama ifuatavyo.
Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa James Lembeli, kwa jinsi ambavyo amekuwa akifuatilia hatma ya wananchi wake katika jimbo lake kutokana na matarajio ya kuanzishwa mgodi wa Buzwagi katika eneo la jimbo lake.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza naomba kumhakikishia Mheshimiwa James Lembeli kwamba wachimbaji wadogo watapata haki zao kama inatarajiwa lakini pia kama alivyokiri mwenyewe kwamba zoezi la kuwafidia wananchi linaendelea vizuri na kwa kweli katika hili ni pamoja na wachimbaji wadogo, fedha kadhaa imeshalipwa na tunaendelea vizuri na tunaomba tu Mheshimiwa James Lembeli tuzidi kushirikiana naye ashirikiane na ofisi yetu na Wizara yetu kwa ujumla ili kuhakikisha kwamba wale wananchi wachache ambao bado hawajachukua na hawajaanza kupokea fidia zao tuwashawishi waanze kupokea.
Mheshimiwa Spika, la pili, utafutaji kama tulivyoeleza kwenye jibu la msingi unafuata sheria, naomba nizidi kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini kwamba Serikali haitaruhusu utafutaji au uchimbaji ufanyike kinyume cha sheria kwa hiyo tunazidi kuwahakikishia wananchi wa Jimbo la Kahama na hasa maeneo ya Mwabomba pamoja na Idahina kwamba watafutaji wa madini walioko pale wanafuata sheria na Serikali inafuatilia kuhakikisha hawakiuki sheria zilizopo ambazo zinawezesha kufanya hizo shughuli.