Timu ya uchunguzi wa Makosa makubwa kutoka ofisi ya DCI yatumwa kuchunguza Mauaji ya Ali Kibao wa CHADEMA

Timu ya uchunguzi wa Makosa makubwa kutoka ofisi ya DCI yatumwa kuchunguza Mauaji ya Ali Kibao wa CHADEMA

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Snapinsta.app_459089460_864579895776057_82654367666808998_n_1080.jpg

Timu ya uchunguzi wa matukio makubwa toka Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai toka Makao Makuu imetumwa kuongeza nguvu ili kuhakikisha waliofanya mauaji ya Ali Kibao Kada wa CHADEMA wanakamatwa na kufikishwa mahakamani.

Jana Septemba 7, 2024 Jeshi la Polisi lilitoa taarifa juu ya Ally Mohamed Kibao kuhusishwa kutoka kwenye basi la Tashrif na kuchukuliwa na watu ambao hawakuweza kutambuliwa na kwamba uchunguzi ulianza baada ya kupokelewa taarifa hiyo.

Baada ya kutolewa taarifa za kuonekana mwili wa mtu mwanaume ambaye hakuweza kutambuliwa kwa wakati huo ni mwili wa nani huko Ununio Jijini Dar es Salaam, utambulisho umefanyika kwa mujibu wa taratibu na kubainika ni mwili wa Ally Mohamed Kibao.

Soma Pia:
Aidha, uchunguzi wa mwili wa marehemu (postmortem) umefanywa leo tarehe 08/09/2024 na Madaktari bingwa kwa kushirikisha familia.

Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa tukio hili la kusikitisha na timu ya uchunguzi wa matukio makubwa toka Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai toka Makao Makuu imetumwa kuongeza nguvu kwenye timu ya awali ili kuhakikisha waliofanya mauaji haya wanakamatwa na kufikishwa mahakamani.
 

Timu ya uchunguzi wa matukio makubwa toka Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai toka Makao Makuu imetumwa kuongeza nguvu ili kuhakikisha waliofanya mauaji ya Ali Kibao Kada wa CHADEMA wanakamatwa na kufikishwa mahakamani.
Huu ni utani mwingine kwa watanzania. Polisi wana tuhumiwa halafu ati wana tuma kikosi kuchunguza.. We are not serious. Halafu alie tuma ni Kingai ambae historia yake ina julikana.
 
Najiuliza hivi mtu gani anaweza kushika silaha nzito ya kivita na kuingia nayo ndani ya basi mchana kweupe na kumfunga pingu raia na kisha kuindoka naye kwa kutumia Toyota Landcruiser HardTop.
Jibu nalopata huyo mtu lazima awe wa Serikali na Serikali lazima inamjua.
Ingekuwa vyema Serikali ikajitoa kwenye hili iwaite scotland yard waje wafanye uchunguzi ili ukweli ujulikane
 
Back
Top Bottom