Tishio la Wakenya kuitaka ardhi yetu ni zaidi ya Wachina na wazungu

Tishio la Wakenya kuitaka ardhi yetu ni zaidi ya Wachina na wazungu

Si bora hao wakenya waje tu ili wanunue hiyo ardhi maana haina faida yoyote kwa watu wengi wanaoimiliki. Nenda huko vijijini utakuta mtu anamiliki sio chini ya heka tano, lakini ni masikini wa kutupwa. Mtu wa hivyo si bora amuuzie huyo mkenya apate mtaji wa kufanyia biashara?
Duuh we jamaa....
 
Huko nchi nyingine ardhi hakuna wakachukue nini ?
Mkuu, Somalia ardhi ni tele. Sudan Kusini ardhi nyingi tu. Hata Uganda ardhi ipo.

Ambako hakuna ardhi ni Rwanda na Burundi.

Naona sasa wananyemelea DRC, sijui kama watafanikiwa huko, pengine watupe ahueni sisi.
 
Kihistoria tuko tofauti na KENYA...

Hatuwezi kuishi kama wakenya katika nchi yetu....

Hivi tuishivyo....yako mazuri zaidi ya hizo "hurstles" za Wakenya nchini kwao na wakiwa nchi za wengine.....


#TaifaKwanza
#TanzaniaKwanza
#KaziIendelee
 
Duuh we jamaa....

Mkuu huo ndio uhalisia, unakuta mtu ni barmaid hapa mjini na anakaa nyumba ya kupanga, lakini ndio anawasaidia ndugu zake huko kijijini ambao wanamiliki mashamba kibao. Hapo mtu wa namna hiyo ardhi kwake ni laana. Vinginevyo serikali iwekeze kwenye kilimo ili hiyo ardhi iwe mkombozi kweli wa hao wanaoimiliki.
 
Ardhi ya Tanzania ni mali ya Rais.

Unaweza kufanya mbwembwe zote kama mhamiaji ila siku wakiitaka wanaichukua na hata wewe wanaweza kukuchukua ukaozea mahabusu na hutakuwa na kitu cha kufanya.
Nyakati hubadilika.

Jana alikuwepo Magufuli, leo yupo Samia.

Sijui kama unanielewa.

Kwa hali ya nchi yetu ilivyo, mtawala yeyote anaweza kubadili kitu chochote bila ya pingamizi. Hilo la ardhi kuwa ya rais, tena hapo ndipo inakuwa rahisi kabisa kwa mtu huyo kurasimisha ardhi hiyo kwa watu anaopenda waichukue.
 
Yan watanzania waoga ukijumlisha na hangover za ujamaa unapata viumbe vya ajabu kabisaaa
"Ujamaa" hauna lolote na jambo hili, sema tu inakupendeza kutaja "ujamaa" hata kama hujui maana yake ni nini.
 
Nyakati hubadilika.

Jana alikuwepo Magufuli, leo yupo Samia.

Sijui kama unanielewa.

Kwa hali ya nchi yetu ilivyo, mtawala yeyote anaweza kubadili kitu chochote bila ya pingamizi. Hilo la ardhi kuwa ya rais, tena hapo ndipo inakuwa rahisi kabisa kwa mtu huyo kurasimisha ardhi hiyo kwa watu anaopenda waichukue.
Ardhi siyo kitu rahisi Mkuu. Ardhi ndio nchi na ndio urithi wa watu.

Ukigusa ardhi umegusa damu ya mtu. Hata mababu zetu walipigana na wakoloni kulinda ardhi.

Pita sehemu zenye migogoro ya ardhi kama Kiteto na Moro ndio utajua ardhi nini.

Usidhani lile azimio la EAC kuhusu ardhi limeshindikana kwa makusudi.

Watu hawawezi kuandamana kwasababu ya katiba mpya au tume huru ya uchaguzi lakini mtu hawezi kujiuliza mara mbili linapokuja suala la kupigania ardhi yake.

Kama wanasiasa wanadhani nibrahisi sana wabadilishe tu sera ya ardhi.

Angalia tu kwanza namna ilivyo ngumu kumiliki ardhi Zanzibar.
 
Mkuu, Somalia ardhi ni tele. Sudan Kusini ardhi nyingi tu. Hata Uganda ardhi ipo.

Ambako hakuna ardhi ni Rwanda na Burundi.

Naona sasa wananyemelea DRC, sijui kama watafanikiwa huko, pengine watupe ahueni sisi.
Ni nani alitunga lile Azimio kwamba raia yeyote ndani ya Jumuiya ya Afrika Masharti aruhusiwe kumiliki ardhi na kuishi sehemu yoyote ndani ya jumuiya ?
 
Wakenya ni majirani zetu na ndio nchi pekee duniani ambayo naweza kusema tunachangia vitu vingi sana. Kwa mfano, tunaongea lugha moja, chakula chetu kinafanana na kuna makabila mengi ambayo yapo Kenya na Tanzania.

Pamoja na ujirani wetu na mila na tamaduni kufanana lakini pia kuna tofauti kubwa sana baina yetu. Tofauti hizo ni kama Wakenya kuendekeza ukabila na uchu wa mali kupita kiasi.

Hoja kubwa ninayotaka kuijadili hapa ni kuhusu ardhi yetu.

Kenya kuna uhaba wa ardhi kutokana na ardhi kubwa kumilikiwa na matajiri wachache. Hali hiyo imepelekea Wakenya kuja kwa wingi Tanzania ili kutafuta fursa za kupata ardhi. Wakenya wanafanya hivyo kupitia mahusiano ya kimapenzi na dada na kaka zetu wa Kitanzania. Wakenya wanawarubuni ndugu zetu kimapenzi ili wapate urahisi wa kutumia ardhi yetu. Kitu cha kuogopa zaidi hawa watu wana rangi za ngozi na kuongea kama sisi kwahiyo ni vigumu kujua wameenea kwa kiasi gani (bila kutumia takwimu za uhamiaji) tofauti na wazungu.

Hivi ninavyoandika ndugu yangu ambaye ni wakili anamuwakilisha dada mmoja wa Kitanzania ambaye alirubuniwa kimapenzi na jamaa wa Kikenya na kuacha ardhi yake itumiwe lakini yule dada hapati chochote ilhali wameingia ubia kwenye mkataba wa uwekezaji. Kitu kinachonipa faraja ni kwamba ndugu yangu ananiambia licha ya kuwa anamuwakilisha mteja wake lakini hii kesi ni "personal " na atapigana kufa na kupona ili ashinde kesi! Ndugu yangu anafanya hivyo kwasababu anajua Wakenya hawana utu.
Tuwe wakweli tunahitaji nguvu kazi ya kutosha kujenga Tanzania yetu nikimaanisha nguvu za watu kujidanganya eti tuzaane ndipo tupate nguvu kazi ya kutosha ni ujima,ubaguzi wa hata na majirani zetu ,ni wa kiwango Cha juu.lengo la jumuia ya afrika mashariki ni kujenga nchi kubwa ya uchumi mkubwa .lengo hilo liliasisiwa mwishoni mwa miaka ya 1950 ,Leo hii mtu anajitokeza na kuogopa wakenya pole yake. ubaguzi hujawahi kuleta maendeleo, afrika ya kusini ilishamiri kwa ubaguzi iakatengwa pamoja na maendeleo waliyo kua nayo walikwama wakasalimu amri,wakakubali kuwathamini watu wote taifa lisilo lakibaguzi likaunuka na kua taifa la uchumi imara.kwa kua ilikubaliwa kushirikiana na nchi nyingine
Taifa linalo ongoza kwa uchumi duniani ni Marekani , taifa la mchanganyiko wa mataifa karibu yote duniani
Sisi tuna rasilimali za kutosha, lakini uchumi wetu ni wa kipato Cha Kati Cha nchini wakenya uchumi wao ni wa Kati wa juu, ni kwa kua Wana maarifa na mbayo tunayahitati mbinu wanazo tatua changamoto huenda zikatusaidia
Hebu fanya utafiti mdogo mijini Kuna maendeleo unajua ni kwa Nini,ni kwakua Kuna mchanganyiko wa makabila . na mikoa yenye makabila mengi Toka sehemu tofauti zinapiga hatua.
Hivi Sasa Canada inabembeleza wahamiaji imegundua Siri ya urembo na sisi wakijilengesha Kuna kosa gani .
kwanza wameoa au kuolewa unadhani watarudi kwao labda Sio Tanzania nakutabiria siku wakikubali uraia pacha mitaji italetwa na wageni kutafuta ulowezi
Pia tujifunze historia sisi tunaojiita watanzania ni miaka ya 1844 ndipo afrika ikagawanyika haijafika hata miaka 200
sisi wasukuma historia Ina sema tulitokea Uganda kwenye Dora la buchwezi ndio maana utakuta tamaduni za kichwezi tukiwatuhumu waganda ni kutokujua chimbuko letu wadigo wasambaa wamasai wamburu wachaga nk ni makabila yaliyotokea Kenya wayao wamakua wamwela nk walitokea msumbiji Vivyo hivyo wamanda wanyakyusa baadhi Yao walitokea Malawi na Zambia Kuna watanzania asiri Yao ,na Kongo Burundi Rwanda Uganda Hadi sudani (wajaluo)
Najalibu kuonesha jinsi tulivyo kua tunatoka sehemu mbali mbali na hata Sasa Kama watu wanakuja na kuoleana huo ni mpango wa MUNGU
Mbona hujahoji watu waliokuja na kugoma kuoleana nasi vipi hao wao unawachukuliaje poa tu,na inawezekana ndo wenye ukwasi mkubwa
Kubali falsafa ya marasta afrika moja isiyo na mipaka ndiyo ita kayo kua na maendereo
 
Wakenya ni majirani zetu na ndio nchi pekee duniani ambayo naweza kusema tunachangia vitu vingi sana. Kwa mfano, tunaongea lugha moja, chakula chetu kinafanana na kuna makabila mengi ambayo yapo Kenya na Tanzania.

Pamoja na ujirani wetu na mila na tamaduni kufanana lakini pia kuna tofauti kubwa sana baina yetu. Tofauti hizo ni kama Wakenya kuendekeza ukabila na uchu wa mali kupita kiasi.

Hoja kubwa ninayotaka kuijadili hapa ni kuhusu ardhi yetu.

Kenya kuna uhaba wa ardhi kutokana na ardhi kubwa kumilikiwa na matajiri wachache. Hali hiyo imepelekea Wakenya kuja kwa wingi Tanzania ili kutafuta fursa za kupata ardhi. Wakenya wanafanya hivyo kupitia mahusiano ya kimapenzi na dada na kaka zetu wa Kitanzania. Wakenya wanawarubuni ndugu zetu kimapenzi ili wapate urahisi wa kutumia ardhi yetu. Kitu cha kuogopa zaidi hawa watu wana rangi za ngozi na kuongea kama sisi kwahiyo ni vigumu kujua wameenea kwa kiasi gani (bila kutumia takwimu za uhamiaji) tofauti na wazungu.

Hivi ninavyoandika ndugu yangu ambaye ni wakili anamuwakilisha dada mmoja wa Kitanzania ambaye alirubuniwa kimapenzi na jamaa wa Kikenya na kuacha ardhi yake itumiwe lakini yule dada hapati chochote ilhali wameingia ubia kwenye mkataba wa uwekezaji. Kitu kinachonipa faraja ni kwamba ndugu yangu ananiambia licha ya kuwa anamuwakilisha mteja wake lakini hii kesi ni "personal " na atapigana kufa na kupona ili ashinde kesi! Ndugu yangu anafanya hivyo kwasababu anajua Wakenya hawana utu.
Wakenya wakawaida sana,wenyewe tu wanakimbizwa na wanageria hatari,
Sasa hv vijana kutoka china wanakuja kwa kasi hatari,Kazi zote za IT,watafanya wao,kwanza Wana backup kubwa kutoka kwenye serikali yao
 
Ardhi siyo kitu rahisi Mkuu. Ardhi ndio nchi na ndio urithi wa watu.

Ukigusa ardhi umegusa damu ya mtu. Hata mababu zetu walipigana na wakoloni kulinda ardhi.

Pita sehemu zenye migogoro ya ardhi kama Kiteto na Moro ndio utajua ardhi nini.

Usidhani lile azimio la EAC kuhusu ardhi limeshindikana kwa makusudi.

Watu hawawezi kuandamana kwasababu ya katiba mpya au tume huru ya uchaguzi lakini mtu hawezi kujiuliza mara mbili linapokuja suala la kupigania ardhi yake.

Kama wanasiasa wanadhani nibrahisi sana wabadilishe tu sera ya ardhi.

Angalia tu kwanza namna ilivyo ngumu kumiliki ardhi Zanzibar.
Mkuu, nimekusoma hapa, na tunaweza kuandika mengi juu yake.

Lakini kabla hata hatujaenda mbali, nikakuta unauliza swali hili:
Ni nani alitunga lile Azimio kwamba raia yeyote ndani ya Jumuiya ya Afrika Masharti aruhusiwe kumiliki ardhi na kuishi sehemu yoyote ndani ya jumuiya ?
Hili tu linakuonyesha ni jinsi gani hali ya nchi yetu isivyokuwa na mwelekeo.

"Ni nani aliyetunga lile azimio"?

Na kwa hali ninavyoiona kwa sasa, huenda tukapiga hatua ndefu zaidi safari hii kuelekea huko tusikokuelewa.
 
Sisi tuna rasilimali za kutosha, lakini uchumi wetu ni wa kipato Cha Kati Cha nchini wakenya uchumi wao ni wa Kati wa juu
Andiko lako lote linaweza kuhojiwa kwa usahihi wake; lakini katika mstari huu hapa unakuonyesha kwamba hujui unachokiandika juu yake.
 
Ardhi siyo kitu rahisi Mkuu. Ardhi ndio nchi na ndio urithi wa watu.

Ukigusa ardhi umegusa damu ya mtu. Hata mababu zetu walipigana na wakoloni kulinda ardhi.

Pita sehemu zenye migogoro ya ardhi kama Kiteto na Moro ndio utajua ardhi nini.

Usidhani lile azimio la EAC kuhusu ardhi limeshindikana kwa makusudi.

Watu hawawezi kuandamana kwasababu ya katiba mpya au tume huru ya uchaguzi lakini mtu hawezi kujiuliza mara mbili linapokuja suala la kupigania ardhi yake.

Kama wanasiasa wanadhani nibrahisi sana wabadilishe tu sera ya ardhi.

Angalia tu kwanza namna ilivyo ngumu kumiliki ardhi Zanzibar.
Pointi nzuri.
 
Mkuu huo ndio uhalisia, unakuta mtu ni barmaid hapa mjini na anakaa nyumba ya kupanga, lakini ndio anawasaidia ndugu zake huko kijijini ambao wanamiliki mashamba kibao. Hapo mtu wa namna hiyo ardhi kwake ni laana. Vinginevyo serikali iwekeze kwenye kilimo ili hiyo ardhi iwe mkombozi kweli wa hao wanaoimiliki.
Laana ya Aridhi ni jambo kubwa sana mkuu! Lakini unacho Sema ni kweli, hata hawa watetezi wa Aridhi wengine humu, Aridhi watakayo kuja kumiliki ni hatua mbili kwa tatu za kaburi tu!
 
Awamu hii hawaioni kenya kama tatizo ni rafiki na mpaka gesi wameamua kuwauzia,
Yaani badala ya kuhakikisha Raia wanapata nishati hii Kwa Bei rahisi,

Wanakwenda kuwauzia wakenya.

Ajabu sana hii.
 
Ardhi ya Tanzania ni mali ya Rais.

Unaweza kufanya mbwembwe zote kama mhamiaji ila siku wakiitaka wanaichukua na hata wewe wanaweza kukuchukua ukaozea mahabusu na hutakuwa na kitu cha kufanya.
Rais wa sasa anaweza kuwanyang'anya ardhi waarabu wa Loliondo?
 
Back
Top Bottom