Tishio la Wakenya kuitaka ardhi yetu ni zaidi ya Wachina na wazungu

Tishio la Wakenya kuitaka ardhi yetu ni zaidi ya Wachina na wazungu

Naona huwa hunisomi.

Mimi niwahofie Kenya. Kwa lipi hasa?

Mimi nawahofia watu kama wewe, waTanzania wenzangu wasiojuwa hili wala lile; ikiwa ni pamoja na hawa viongozi wanaoyumba kama bendera wasiojuwa kuwaongoza wananchi wao wanufaike na utajiri mkubwa sana wa nchi yao; badala yake wanajiuza...
We unajifanya unajua hili na lile lkn nikisoma fikra zako nakuona umejaza uhafidhina kichwani mwako? Sawa Mie sijui hili wala lile na viongozi wetu ndo walewale, swali je tusubiri miaka mingapi mpaka tuseme sasa tunaweza kufanya biashara na Kenya bila kuwahofia?
 
We unajifanya unajua hili na lile lkn nikisoma fikra zako nakuona umejaza uhafidhina kichwani mwako? Sawa Mie sijui hili wala lile na viongozi wetu ndo walewale, swali je tusubiri miaka mingapi mpaka tuseme sasa tunaweza kufanya biashara na Kenya bila kuwahofia?
Kwani tulikuwa hatufanyi biashara na Kenya? Huoni walivyoanza kuhaha na kuzuia mahindi yetu kwa visingizio vya kipuuzi kabisa?

Watu mnaoikuza Kenya hamjui matatizo yao ni makubwa sana. Angalia ilivyokuwa ikifurahia kuilalia Uganda miaka na miaka. Uganda kakosa la kufanya kwa sababu ya utegemezi wake kwa Kenya kupitishia mizigo yake. Sasa Uganda kaanza kujitutumua kwa kuzalisha kwa wingi na kupunguza anavyonunua Kenya..., Kenya kaanza vitimbi, anazuia Maziwa ya Uganda, anazuia sukari na mengine..., wewe haya huyajui!

Analeta kuuza viperemende na biskuti vyake hapa, kwa udanganyifu wa sukari iliyoingizwa bila kulipia ushuru; Tanzania ikihoji, analia lia na kuzuia vioo na vigae visiuzwe kwake!
Hivi hujui jinsi gani Kenya anavyohangaika sana sasa, hadi hapa tunapoingia na kumpa mwanya mpya?

Halafu unakuja hapa na kusema kuihofia Kenya, kwa kitu gani?
 
Kwani tulikuwa hatufanyi biashara na Kenya? Huoni walivyoanza kuhaha na kuzuia mahindi yetu kwa visingizio vya kipuuzi kabisa?

Watu mnaoikuza Kenya hamjui matatizo yao ni makubwa sana. Angalia ilivyokuwa ikifurahia kuilalia Uganda miaka na miaka. Uganda kakosa la kufanya kwa sababu ya utegemezi wake kwa Kenya kupitishia mizigo yake. Sasa Uganda kaanza kujitutumua kwa kuzalisha kwa wingi na kupunguza anavyonunua Kenya..., Kenya kaanza vitimbi, anazuia Maziwa ya Uganda, anazuia sukari na mengine..., wewe haya huyajui!

Analeta kuuza viperemende na biskuti vyake hapa, kwa udanganyifu wa sukari iliyoingizwa bila kulipia ushuru; Tanzania ikihoji, analia lia na kuzuia vioo na vigae visiuzwe kwake!
Hivi hujui jinsi gani Kenya anavyohangaika sana sasa, hadi hapa tunapoingia na kumpa mwanya mpya?

Halafu unakuja hapa na kusema kuihofia Kenya, kwa kitu gani?
Tumekuwa tukifanya biashara na Kenya miaka na miaka nakubali, hili la Uhuru kuzuia mahindi mchokozi alikuwa ni magufuli na Uhuru alireact kujibu shambulizi la magufuli make magufuli alikuwa anakiuka mikataba ya jumuiya na pia ktk janga la corona misimamo ya magufuli ilikuwa inahatarisha sekta ya utalii Kenya ndo chanzo cha migogoro yote hiyo.
 
Tumekuwa tukifanya biashara na Kenya miaka na miaka nakubali, hili la Uhuru kuzuia mahindi mchokozi alikuwa ni magufuli na Uhuru alireact kujibu shambulizi la magufuli make magufuli alikuwa anakiuka mikataba ya jumuiya na pia ktk janga la corona misimamo ya magufuli ilikuwa inahatarisha sekta ya utalii Kenya ndo chanzo cha migogoro yote hiyo.
Sasa unamsingizia Magufuli na mengine asiyohusika nayo. Sioni kwa nini umwingize Magufuli hapa.
Mimi simtetei kwa mambo mengi maovu aliyokuwa akiyafanya, lakini siyo kwa hayo unayomsema na huyo mnafiki ndumila kuwili ambaye hata humujui vizuri.
Magufuli alikuwa anahatarisha vipi utalii wa Kenya, kwa mfano! Sasa Samia ndipo wanapotaka kupandia kwake na utalii wao au siyo; hilo ndilo unaloona ni jambo zuri? Miaka na miaka utalii wetu wameudumaza hao jamaa, sasa umeanza kuinukia kwa kasi kubwa, halafu Samia anakwenda kujadili nao kitu gani juu ya utalii; hebu nieleze.

Mambo yale yale ya gesi, tulikoanzia kujibishana hapa. Bado huoni picha ilivyo?

Blac kid, haya mambo usiyaendee kwa pupa na kuamini 'propaganda' zinazoenezwa na hao wanaotuuza na wanaotafuta kutununua pamoja na kwamba uwezo hawana.
 
Watanzania tumejaa Kenya, South Africa, Uganda, Botswana, Namibia ULAYA NA AMERIKA NDIYO USISEME. TUJITAHIDI KUWA WAVUMILIVU NA KUWAKUBALI WATU WENGINE!
Ila watanzania tuwe makini sana. Kuna kaugonjwa fulani kanaingia kwa kasi mno. Tunahisi umasikini wetu uneletwa na watu wengine, tunaacha kupambana na maadui wa kweli wa maisha yetu tunalazimishwa kuamini kuwa mara tunaonewa, mara watu wa nje wanatamani vitu vyetu, mara mabeberu tupo nao kwenye vita nk. Hawa si maadui zetu, adui zetu ni ujinga, uzembe, siasa za hovyo na IQ pungufu.

Mleta mada una mifano mingapi ya wakenya waliowahulumu wadada wa kitanzania? Una mifano mingapi ya wakaka wa kitanzania waliowadhulumu ndugu zao wa damu ardhi?

Ishu ni kujitambua tu mkuu. Watanzania tufike mahali tujitambue, hii ya kuwaza wakenya wanataka ardhi yetu mara mabeberu wanataka utajiri wetu haitatufikisha popote. Tusimame tupambane
 
Kwani tulikuwa hatufanyi biashara na Kenya? Huoni walivyoanza kuhaha na kuzuia mahindi yetu kwa visingizio vya kipuuzi kabisa?

Watu mnaoikuza Kenya hamjui matatizo yao ni makubwa sana. Angalia ilivyokuwa ikifurahia kuilalia Uganda miaka na miaka. Uganda kakosa la kufanya kwa sababu ya utegemezi wake kwa Kenya kupitishia mizigo yake. Sasa Uganda kaanza kujitutumua kwa kuzalisha kwa wingi na kupunguza anavyonunua Kenya..., Kenya kaanza vitimbi, anazuia Maziwa ya Uganda, anazuia sukari na mengine..., wewe haya huyajui!

Analeta kuuza viperemende na biskuti vyake hapa, kwa udanganyifu wa sukari iliyoingizwa bila kulipia ushuru; Tanzania ikihoji, analia lia na kuzuia vioo na vigae visiuzwe kwake!
Hivi hujui jinsi gani Kenya anavyohangaika sana sasa, hadi hapa tunapoingia na kumpa mwanya mpya?

Halafu unakuja hapa na kusema kuihofia Kenya, kwa kitu gani?
Nani walichoma Vifaranga????🤣🤣🤣🤣
 
Sasa unamsingizia Magufuli na mengine asiyohusika nayo. Sioni kwa nini umwingize Magufuli hapa.
Mimi simtetei kwa mambo mengi maovu aliyokuwa akiyafanya, lakini siyo kwa hayo unayomsema na huyo mnafiki ndumila kuwili ambaye hata humujui vizuri.
Magufuli alikuwa anahatarisha vipi utalii wa Kenya, kwa mfano! Sasa Samia ndipo wanapotaka kupandia kwake na utalii wao au siyo; hilo ndilo unaloona ni jambo zuri? Miaka na miaka utalii wetu wameudumaza hao jamaa, sasa umeanza kuinukia kwa kasi kubwa, halafu Samia anakwenda kujadili nao kitu gani juu ya utalii; hebu nieleze.

Mambo yale yale ya gesi, tulikoanzia kujibishana hapa. Bado huoni picha ilivyo?

Blac kid, haya mambo usiyaendee kwa pupa na kuamini 'propaganda' zinazoenezwa na hao wanaotuuza na wanaotafuta kutununua pamoja na kwamba uwezo hawana.
Maghufuli hakutaka Kenya wauze Vitu Tanzania Ila alitaka Tanzania iuze vitu Kenya,Alichoma Vifaranga,Akakataza Maziwa ya Brookside na mengine mengi,Ungekuwa President Uhuru ungefanyaje????
 
Kwa Sasa hatuwezi kushindana na Kenya kiuchumi ingawa kuwaogopa si sawa!Tatizo la mtanzania ni kuwa hajawekeza kwenye elimu,tubadilishe huu Mfumo wa elimu yetu,tuachane na hii elimu ya kizungu,tuandae mtaala unaoendana na mazingira yetu afu tujipe muda.
Nna Imani after 30 years WAKENYA WATATUKIMBIA!!
 
Sasa kama huo sio ujamaa Kenya unawahofia wa nini kama sie wenyewe tulikubali kuunda nao jumuiya ya EAC?
Tunashare vitu ambao sote tunavyo. Kama serikali inapenda hili kwanza ihakikishe kila mtu amegawiwa ardhi kwamaana tugawane ardhi yote kama ilivyo Kenya na then kila mmoja ndio ataamua kurithisha watoto wake au kuiuza kwa wahamiaji.
 
Wakenya ni majirani zetu na ndio nchi pekee duniani ambayo naweza kusema tunachangia vitu vingi sana. Kwa mfano, tunaongea lugha moja, chakula chetu kinafanana na kuna makabila mengi ambayo yapo Kenya na Tanzania.

Pamoja na ujirani wetu na mila na tamaduni kufanana lakini pia kuna tofauti kubwa sana baina yetu. Tofauti hizo ni kama Wakenya kuendekeza ukabila na uchu wa mali kupita kiasi.

Hoja kubwa ninayotaka kuijadili hapa ni kuhusu ardhi yetu.

Kenya kuna uhaba wa ardhi kutokana na ardhi kubwa kumilikiwa na matajiri wachache. Hali hiyo imepelekea Wakenya kuja kwa wingi Tanzania ili kutafuta fursa za kupata ardhi. Wakenya wanafanya hivyo kupitia mahusiano ya kimapenzi na dada na kaka zetu wa Kitanzania. Wakenya wanawarubuni ndugu zetu kimapenzi ili wapate urahisi wa kutumia ardhi yetu. Kitu cha kuogopa zaidi hawa watu wana rangi za ngozi na kuongea kama sisi kwahiyo ni vigumu kujua wameenea kwa kiasi gani (bila kutumia takwimu za uhamiaji) tofauti na wazungu.

Hivi ninavyoandika ndugu yangu ambaye ni wakili anamuwakilisha dada mmoja wa Kitanzania ambaye alirubuniwa kimapenzi na jamaa wa Kikenya na kuacha ardhi yake itumiwe lakini yule dada hapati chochote ilhali wameingia ubia kwenye mkataba wa uwekezaji. Kitu kinachonipa faraja ni kwamba ndugu yangu ananiambia licha ya kuwa anamuwakilisha mteja wake lakini hii kesi ni "personal " na atapigana kufa na kupona ili ashinde kesi! Ndugu yangu anafanya hivyo kwasababu anajua Wakenya hawana utu.
Mama alishasema watanzania wanaenda pewa mimba kipindi nae kaenda kenya kisha wanatudi jifungulia Tz....acha nchi wapewe hao wanaoweka mimba
 
Sasa unamsingizia Magufuli na mengine asiyohusika nayo. Sioni kwa nini umwingize Magufuli hapa.
Mimi simtetei kwa mambo mengi maovu aliyokuwa akiyafanya, lakini siyo kwa hayo unayomsema na huyo mnafiki ndumila kuwili ambaye hata humujui vizuri.
Magufuli alikuwa anahatarisha vipi utalii wa Kenya, kwa mfano! Sasa Samia ndipo wanapotaka kupandia kwake na utalii wao au siyo; hilo ndilo unaloona ni jambo zuri? Miaka na miaka utalii wetu wameudumaza hao jamaa, sasa umeanza kuinukia kwa kasi kubwa, halafu Samia anakwenda kujadili nao kitu gani juu ya utalii; hebu nieleze.

Mambo yale yale ya gesi, tulikoanzia kujibishana hapa. Bado huoni picha ilivyo?

Blac kid, haya mambo usiyaendee kwa pupa na kuamini 'propaganda' zinazoenezwa na hao wanaotuuza na wanaotafuta kutununua pamoja na kwamba uwezo hawana.
Simsingizii magu lkn utakubaliana Nami ktk jumuiya yetu hii ya EAC ipo ktk muundo wa common market, na moja ya mkataba wa common market ni free movement of labour and capital, so kama utakumbuka sakata la MD wa Vodacom, serikali ya magu ilimwekea figisu yule mkenya mpaka akaukosa u-md hapo tuliingia doa kideplomasia na Kenya ingawaje Uhuru aliamua kufunika kombe mwanaharamu apite, kuhusu suala la corona unataka kujua magu alitaka kuhatarisha Vp sekta ya utalii Kenya? Kenya inapokea sana wazungu kwa ajili ya utalii na unajua wale watu ni wanajali sana precaution, so Uhuru aliwasoma na kuwazuga kuweka half kafyuu/ lockdown na vitu kama uvaaji wa barakoa na nk, upande wa tz magu alipuuzia kabisa suala la corona ikafikia hatua akawa anawanga hata wanaovaa barakoa, so kwa Sababu ya muingiliano kibishiara tz na Kenya, wazungu walianza kuigopa Kenya coz inaingiza watz ambao hawana habari na corona, kuona hivyo Uhuru akazipiga pini ndege za tz kuingia Kenya na mipikani akajaza vipimo na kuweka watz kantini 2 weeks, magu naye akajibu mapgo kibabe, so muvi zote hizo za magu zilimfanya sasa Uhuru naye apige kombora tata la kuzuia mahindi, ukweli ni kwamba tz na Kenya tunategemeana kwa mengi ila cha ajabu watz wengi mnawapga vita wakenya kwa vijisababu uchwara na ndo mana Mie nasema hizo ni hangover za ujamaa.
 
Nani walichoma Vifaranga????🤣🤣🤣🤣
Hujui kwa nini vifaranga walichomwa moto, au huna uelewa na maswala ya namna hiyo?
Nenda kajielimishe ni nini hufanyika wakati sheria inapokiukwa kwenye maswala ya namna hiyo kabla hujaja hapa kuuliza swali la namna hiyo.
 
Maghufuli hakutaka Kenya wauze Vitu Tanzania Ila alitaka Tanzania iuze vitu Kenya,Alichoma Vifaranga,Akakataza Maziwa ya Brookside na mengine mengi,Ungekuwa President Uhuru ungefanyaje????
Wewe ni Mkenya?

Ninakuuliza hivyo kwa sababu ndivyo wanavyojitetea wao wenyewe kiupotofu kabisa.

Uliwahi kusikia Brookeside walivyonunua kampuni ya maziwa Arusha na kung'oa mitambo yake na kuipeleka Ruiru? Arusha ikabaki ni eneo la kukusanya maziwa na kupekwa Ruiru kwenda kusindikwa kabla ya kuletwa kuuzwa Tanzania?

Kama wewe ni mTanzania, hilo ndilo linalokufurahisha?
 
Simsingizii magu lkn utakubaliana Nami ktk jumuiya yetu hii ya EAC ipo ktk muundo wa common market, na moja ya mkataba wa common market ni free movement of labour and capital, so kama utakumbuka sakata la MD wa Vodacom, serikali ya magu ilimwekea figisu yule mkenya mpaka akaukosa u-md hapo tuliingia doa kideplomasia na Kenya ingawaje Uhuru aliamua kufunika kombe mwanaharamu apite, kuhusu suala la corona unataka kujua magu alitaka kuhatarisha Vp sekta ya utalii Kenya? Kenya inapokea sana wazungu kwa ajili ya utalii na unajua wale watu ni wanajali sana precaution, so Uhuru aliwasoma na kuwazuga kuweka half kafyuu/ lockdown na vitu kama uvaaji wa barakoa na nk, upande wa tz magu alipuuzia kabisa suala la corona ikafikia hatua akawa anawanga hata wanaovaa barakoa, so kwa Sababu ya muingiliano kibishiara tz na Kenya, wazungu walianza kuigopa Kenya coz inaingiza watz ambao hawana habari na corona, kuona hivyo Uhuru akazipiga pini ndege za tz kuingia Kenya na mipikani akajaza vipimo na kuweka watz kantini 2 weeks, magu naye akajibu mapgo kibabe, so muvi zote hizo za magu zilimfanya sasa Uhuru naye apige kombora tata la kuzuia mahindi, ukweli ni kwamba tz na Kenya tunategemeana kwa mengi ila cha ajabu watz wengi mnawapga vita wakenya kwa vijisababu uchwara na ndo mana Mie nasema hizo ni hangover za ujamaa.
Blac kid, unahitaji darasa muhimu ili ufunguke akili vizuri kwa sababu naona una maluweluwe mengi, pamoja na kwamba akili yako inaonyesha kuwa wazi.

Swala la MD, hata mimi ningekuwa Magufuli ningekataa. Huyo binti hana 'qualifications' zozote za kuletwa hapa kama MD wa kampuni hiyo. Mbona hapo tu kwao kwenye kampuni hiyo 'Safaricom' hakupewa nafasi hiyo kama anastahiri nafasi ya namna hiyo? Na bado hujauliza kwa nini Bob Collimore alipofariki, kwa nini wenye kampuni yao (Safaricom) walilazimishwa wamtafute Mkenya kushika hiyo nafasi ---, unalo jibu juu ya hilo?

Swala la Corona, hata hapa unaliunganisha na utalii kimakosa kabisa na uhusika wa Magufuli juu yake.

Hata mimi sikupenda Magufuli alivyoichukulia corona hapa nyumbani, na michango yangu mingi mno imo humu humu JF juu ya hilo, lakini nilijua maana yake ya kufanya vile, hata kama ilikuwa ni kufanya kwa upotofu. Msukumo wake mkubwa ulikuwa ni kulinda uchumi, akidhani kwamba kutangaza uwepo wa corona utawatia watalii uoga wasije kutembelea hapa (Tanzania); pili, kwamba kuweka 'lockdown' (kujifungia kutasababisha hali ngumu kwa wananchi, kama wamachinga na wengine wanaopata pato lao kwa siku na kulitegemea pato hilo kuendesha maisha yao. Alitaka kuepuka gharama za matumizi juu ya msaada kwao.

Huo ndio ulikuwa msukumo wa maamuzi yake kuhusu corona.

Sasa wewe niambie, Kenyatta pamoja na yote aliyoyafanya utalii kwake umemletea neema gani? Hapa utamlaumu Magufuli juu ya kutokuja kwa watalii huko Kenya? Mbona dunia nzima utalii ulisimama!
Sasa wewe hapa, utaendelea vipi kuamini kwamba Magufuli alikuwa anamfanyia mbinu Kenyatta ili avuruge utalii wa Kenya?

Hilo la mwisho la Tanzania na Kenya "kutegemeana kwa mengi" nalo ni la kipropaganda tu. Sema Kenya wanaitegemea sana Tanzania, na ndiyo sababu hawaishi malalamiko kila mara juu ya Tanzania.

Tanzania haina sababu hata kidogo ya kuitegemea Kenya. Bandari tunazo, na majirani tunao wengi sana, mbona hatujishughulishi nao ili tuendeleze uchumi wetu huko, kwa nini tuitegemee Kenya kwa kuuza mahindi yetu na kumbe kuna sehemu chungu nzima za kuuza mahindi hayo! Kama mtumishi wa serikali kama mkuu 'Blac kid' ndiye anahusika na kutafuta masoko kwa wakulima wetu, anaacha kufanya kazi kwa kutegemea tu kuwa Kenya ndilo soko pekee, nchi hii itakwenda wapi?
 
Unaniuliza tena Mimi? Mie nakiri kweli kama taifa kwa miaka 60 tumeshindwa kuwa na kiwanda cha nguo ili hali malighafi tunazo je kipi ni bora tuendelee kutokuwa na viwanda na pia tusiuze malighafi Kenya au tuendelee kutokuwa na viwanda na angalau tuuze malighafi Kenya? Swali la nyongeza je unajua dhumuni la kuunda jumuiya ya EAC?
Ndiyo.
Jumuia hiyo haikuundwa kuifanya Tanzania ndilo liwe soko la Kenya na mahali pa kupeleka uchafu uliopo huko Kenya.
 
Watanzania are scared of Kenyans..... what kind of nonsense is this? I have never met a single Kenyan scared of anyone from Tanzania

if watanzania are bad at doing business blame it on yourselves not others. Take responsibility for your failures.
 
Si bora hao wakenya waje tu ili wanunue hiyo ardhi maana haina faida yoyote kwa watu wengi wanaoimiliki. Nenda huko vijijini utakuta mtu anamiliki sio chini ya heka tano, lakini ni masikini wa kutupwa. Mtu wa hivyo si bora amuuzie huyo mkenya apate mtaji wa kufanyia biashara?
Aiuze kwa mgeni kutoka nje au aingie mkataba wa kuwekeza!?!!

Kuuza mali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mtu asiye mzawa?
Rais kama msimamizi wa ardhi yote ya JMT, anasemaje juu ya hilo?


Sheria za ardhi No.4 na No.5, Zinasemaje juu ya hilo?
 
Kihistoria tuko tofauti na KENYA...

Hatuwezi kuishi kama wakenya katika nchi yetu....

Hivi tuishivyo....yako mazuri zaidi ya hizo "hurstles" za Wakenya nchini kwao na wakiwa nchi za wengine.....


#TaifaKwanza
#TanzaniaKwanza
#KaziIendelee
Kazi ya kutekana ausio
 
Back
Top Bottom