Simsingizii magu lkn utakubaliana Nami ktk jumuiya yetu hii ya EAC ipo ktk muundo wa common market, na moja ya mkataba wa common market ni free movement of labour and capital, so kama utakumbuka sakata la MD wa Vodacom, serikali ya magu ilimwekea figisu yule mkenya mpaka akaukosa u-md hapo tuliingia doa kideplomasia na Kenya ingawaje Uhuru aliamua kufunika kombe mwanaharamu apite, kuhusu suala la corona unataka kujua magu alitaka kuhatarisha Vp sekta ya utalii Kenya? Kenya inapokea sana wazungu kwa ajili ya utalii na unajua wale watu ni wanajali sana precaution, so Uhuru aliwasoma na kuwazuga kuweka half kafyuu/ lockdown na vitu kama uvaaji wa barakoa na nk, upande wa tz magu alipuuzia kabisa suala la corona ikafikia hatua akawa anawanga hata wanaovaa barakoa, so kwa Sababu ya muingiliano kibishiara tz na Kenya, wazungu walianza kuigopa Kenya coz inaingiza watz ambao hawana habari na corona, kuona hivyo Uhuru akazipiga pini ndege za tz kuingia Kenya na mipikani akajaza vipimo na kuweka watz kantini 2 weeks, magu naye akajibu mapgo kibabe, so muvi zote hizo za magu zilimfanya sasa Uhuru naye apige kombora tata la kuzuia mahindi, ukweli ni kwamba tz na Kenya tunategemeana kwa mengi ila cha ajabu watz wengi mnawapga vita wakenya kwa vijisababu uchwara na ndo mana Mie nasema hizo ni hangover za ujamaa.
Blac kid, unahitaji darasa muhimu ili ufunguke akili vizuri kwa sababu naona una maluweluwe mengi, pamoja na kwamba akili yako inaonyesha kuwa wazi.
Swala la MD, hata mimi ningekuwa Magufuli ningekataa. Huyo binti hana 'qualifications' zozote za kuletwa hapa kama MD wa kampuni hiyo. Mbona hapo tu kwao kwenye kampuni hiyo 'Safaricom' hakupewa nafasi hiyo kama anastahiri nafasi ya namna hiyo? Na bado hujauliza kwa nini Bob Collimore alipofariki, kwa nini wenye kampuni yao (Safaricom) walilazimishwa wamtafute Mkenya kushika hiyo nafasi ---, unalo jibu juu ya hilo?
Swala la Corona, hata hapa unaliunganisha na utalii kimakosa kabisa na uhusika wa Magufuli juu yake.
Hata mimi sikupenda Magufuli alivyoichukulia corona hapa nyumbani, na michango yangu mingi mno imo humu humu JF juu ya hilo, lakini nilijua maana yake ya kufanya vile, hata kama ilikuwa ni kufanya kwa upotofu. Msukumo wake mkubwa ulikuwa ni kulinda uchumi, akidhani kwamba kutangaza uwepo wa corona utawatia watalii uoga wasije kutembelea hapa (Tanzania); pili, kwamba kuweka 'lockdown' (kujifungia kutasababisha hali ngumu kwa wananchi, kama wamachinga na wengine wanaopata pato lao kwa siku na kulitegemea pato hilo kuendesha maisha yao. Alitaka kuepuka gharama za matumizi juu ya msaada kwao.
Huo ndio ulikuwa msukumo wa maamuzi yake kuhusu corona.
Sasa wewe niambie, Kenyatta pamoja na yote aliyoyafanya utalii kwake umemletea neema gani? Hapa utamlaumu Magufuli juu ya kutokuja kwa watalii huko Kenya? Mbona dunia nzima utalii ulisimama!
Sasa wewe hapa, utaendelea vipi kuamini kwamba Magufuli alikuwa anamfanyia mbinu Kenyatta ili avuruge utalii wa Kenya?
Hilo la mwisho la Tanzania na Kenya "kutegemeana kwa mengi" nalo ni la kipropaganda tu. Sema Kenya wanaitegemea sana Tanzania, na ndiyo sababu hawaishi malalamiko kila mara juu ya Tanzania.
Tanzania haina sababu hata kidogo ya kuitegemea Kenya. Bandari tunazo, na majirani tunao wengi sana, mbona hatujishughulishi nao ili tuendeleze uchumi wetu huko, kwa nini tuitegemee Kenya kwa kuuza mahindi yetu na kumbe kuna sehemu chungu nzima za kuuza mahindi hayo! Kama mtumishi wa serikali kama mkuu 'Blac kid' ndiye anahusika na kutafuta masoko kwa wakulima wetu, anaacha kufanya kazi kwa kutegemea tu kuwa Kenya ndilo soko pekee, nchi hii itakwenda wapi?