TLS kumsaidia aliyefungwa Miaka 22 kisa nyama ya Swala

TLS kumsaidia aliyefungwa Miaka 22 kisa nyama ya Swala

James Hadley Chase

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2020
Posts
1,984
Reaction score
3,695
28aeada3704aff46b4aab83218d33adc
CHAMA cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) Kanda ya Iringa wameanzisha kampeni ya kumsaidia kisheria mjane Maria Emirio Ngoda aliyehukumiwa na Mahakama ya Mkoa wa Iringa kifungo cha miaka 22 kwa kosa la kukutwa na ndoo yenye vipande 12 vya nyama ya swala kinyume na sheria.

Hukumu hiyo ilitolewa Novemba 3, mwaka huu na Hakimu Mkazi Mkuu Mkoa wa Iringa, Said Mkasiwa baada ya kujiridhisha pasipo na shaka kuwa ni kweli mjane huyo mwenye watoto wanne alikutwa na ndoo iliyokuwa na nyama hiyo yenye thamani ya Sh 900,000.

17ab033562d668ed4cafa45cc0e59e27

Kwa kupitia taarifa yao waliyoitoa mapema leo, Mwenyekiti wa TLS Kanda ya Iringa, Wakili Moses Ambindwile pamoja na Wakili Cosmas Kishamawe wamesema kwa kushirikiana na mawakili wengine wa mkoani Iringa tayari wameanzisha mchakato wa kumsaidia kisheria mjane huyo.

Mawakili hao wamesema tayari mchakato wa kukata rufaa dhidi ya hukumu ya Mahakama ya Mkoa wa Iringa umeanza rasmi leo asubuhi ikiwa ni muendelezo wa mpango wao wa kutoa msaada wa ushauri na utetezi wa kisheria kwa makundi mbalimbali ya kijamii yasio na uwezo.

Ambindwile alisema tangu waanzishe mpango wa kutoa msaada wa ushauri wa kisheria mkoani Iringa, wameendelea kupokea maombi kutoka kwa makundi ya watu wasio na uwezo kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya mkoa wa Iringa.

“Tuishukuru sana kampuni ya Asas kwa ahadi yake iliyotolewa na mmoja wa wakurugenzi wake, Ahmed Asas kwa kujitokeza kushirikiana nasi ili tuweze kuwafikia watu wengi zaidi wasio na uwezo hususani wale waishio vijijini,” alisema.
 
Huyo hakimu aliyetoa hiyo hukumu kasababisha mahakama ziendelee kuonekana hazitumii weledi na ziko kwa ajili ya maskini tu. Au alimaanisha siku 22 akakosea.maana adhabu gani ambayo haiendani na uhalisia.ata kama nikukomoa uko kumezidi.Afadhali kama kapata msaada.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hakimu kathibitisha kua sheria ni kwa ajili ya makapuku tu. Yule mdogo wake Rosti Tamu alikamatwa na silaha kabisa za kuwindia hayo mazaga lakini kesi yake iliisha kimazabe mazabe
 
Back
Top Bottom