TLS kumsaidia aliyefungwa Miaka 22 kisa nyama ya Swala

Hili suala lazima liibue hiisia coz haiwezekani mtu anaitia hasara serikali ya bilioni 71 halafu anapewa hukumu ya miaka minne jela au kulipa faini milioni 7 wakati huo huo huyo mama kakamatwa na vipande vya nyama ya swala anafungwa miaka 22

Sasa hapo chief huoni kuna unafiki mkubwa wa kisheria hapo? Sheria ni msumeno lakini cha ajabu unakata upande wa watu maskini tu! Hilo halikushangazi?

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Reasoning capacity watu tunatofautiana sana, wenye uelewa hawalalamikii sheria,bali wanalalamikia double standards za hizo sheria, kwa nini sheria iwe kali kwa masikini tu,na kwa watu hi class iwe na huruma, wakati wote tunajua sheria ni msumeno unakata huku na huku!!?
 
Unafiki upo lakini si vyema kuibua emotions kwenye mambo kama haya kwani wakati mwingine hisia zinaweza kutufanya tumuhukumu asiyekuwa na hatia na kumuacha mwenye hatia........

Rejea kesi ya yule mwanafunzi aliyedai kudhurumiwa matokeo yake....watu waliibuka Kwa hisia na kutoa maneno makali kwa walimu baadae ikaja kugundulika kuwa ni muongo.......
 
Kwani vibali vya uwindaji kwa mtu aliefuata utaratibu huwa ni kiasi ???, Ni formula gani kupata thamani ya hivyo vipande kadha vya nyama ya swala. Welevu naomba ufafanuzi na mimi nielewe
 
Sio Maria tu jela Kuna watu wengi tu hawajui hata wamefikaje huko hukumu nyingi za kihuni
 
Kuna wale wahuni waliingiza mpaka twiga kwenye ndege ... Wapo tu mtaaani.....
 

“Tuishukuru sana kampuni ya Asas kwa ahadi yake iliyotolewa na mmoja wa wakurugenzi wake, Ahmed Asas kwa kujitokeza kushirikiana nasi ili tuweze kuwafikia watu wengi zaidi wasio na uwezo hususani wale waishio vijijini,” alisema.
Msambatavangu jiandae,jamaa anakuja kasi sana siku hizi. Inaonesha hili jimbo analitaka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…