TLS pamoja na Mwabukusi waziombe radhi Simba na Yanga hadharani kwa kuzitolea kauli za hovyo

NAKAZIA📌

Hata hivyo Mashaabiki kindakindaki wa mpira hasa wa Simba na Yanga wengi au wote ni vichwa Panzi wakiongozwa na wewe muandishi.
Na mnajulikana kwa kutamba na kuzurura hovyo na Jersey utafikiri mnaiishi uwanjani muda wote.

Nchi ina mengi ya kujadili sio huo uchizi wenu kila dakika utasikia Tumesajili..., Nimemfunga mflan..., Goli la Mama..., Mobeto vile... na upuuzi mwingine.

#STUPID.
 
Leo kweli umeongea points za maana. Mwambukusi nae Leo kateleza sana. Soka itabaki soka na siasa zitabaki siasa.

Siasa ya Tanzania kwa pande zote, sio nzuri. Kwa, upinzani vyama ni vya watu binafsi. Mfano CUT, Lipumba mpaka Leo ni mwenyekiti zaidi ya miaka 25 iliyopita. CDM Mbowe pia ni mwenyekiti wa kudumu. ACT wazalendo pia ni cha Zitto.

Upande wa CCM pia bado kuna kasoro nyingi. Watanzania sio wajinga washabikie siasa za kijinga huku baadhi ya watu wakijinehemesha.
 
Kwani uongo hapo ni upi? Au unajitoa ufahamu? Mala ngapi hawa watu wameandamana kwaajili ya Simba na Yanga lakini mambo ya msingi hawataki? Siku nzima kubishana mpira kwa wendawazimu
 
Mara nyingi tu mashabiki wa Simba na Yanga huandamana uchi na hata wachezaji wao huvuaga Jezi uwanjani

Tatizo unaishi Rombo Ndani Ndani huko 😂😂
 
Nani kawazuio kuimarisha SACCOSS yenu ya Chadema?
Wewe hukuona kinachozuia CHADEMA wasiandamane? Au unajitoa ufahamu. Serikali imetumia mabavu na fedha nyingi za wananchi kuzima maandamano ambayo ni haki kikatiba na kisheria. Nimeshuhudia maandamano makubwa ya hizi timu mbili na uharibifu mkubwa ukitokea lakini serikali na jeshi letu limekaa kimya. IPO SIKU!
 
Bro kinachopiganiwa hapa ni kikubwa kuliko hata huo mpira Amani ikikosekana kwa watu kuendelea kupotea na kuuawa huo mpira hautakuwa na maana …Sema wa Tanzania tuna ugonjwa wa Afya ya Akili Kwene mambo ya Maana tunakua nyuma nyuma Maandamano ya aman kupinga mauaji ila wa Tanzania tulivo wapumbavu et tunaogopa kuchafua aman sasa amani gani inayoruhusu mauaji na utekaji hii nchi ukiachana na uongozi kuendesha hata raia tuna percent kubwa ya kuiongoza sbb kuna wakat nchi inakua na viongozoli wenye akili zinazofanana wanaongoza kwa maslahi yao tu …mwananchi ukiumia njia pekee ya kuleta mapinduzi au kufikisha ujumbe ni kwa njia ya maandamano ila sbb sisi ni kama mazuzu mtu ana mmaindi Mwabukusi et kisa Kawasema vibaya Simba na yanga ila haoni kama kuna point ya maandamano Wachungaji, Mashehe, Mapadri wakat wa mabubiri hutumia kauli hii “Uwanjani goal la simba au Yanga likiingia mnapiga sana makofi na kuruka kuruka ila nyumba za ibada hamfanyi hivyo” nao hawa waziombe msamaha club? hata mzazi kuna wakati anakukataza usiangalie mpira uingie chumbani kwako ukasome nae au ukafanye kazi ni mjinga …Kutawaliwa upya muhimu sana sbb sisi ni mazuzu sana
 
Ha ha ha ha we ulikuwa wapi mkuu ktk maandamano kuonesha hujamsalit MBOWE na chadema yake?
 
Ni ukweli wala hakuna haja kuomba msamaha. Watu wameacha kufuatilia kuhusu mambo ya msingi ya maisha yao wanafuatilia mpira na usanii. Watawala nao wamegundua kuwa washabikia huko hawana muda wa kuhoji kinachoendelea kwenye matumizi ya Kodi zao kwa maendeleo ya Nchi na huduma kwa wananchi.
 
pongezi kwa Mwabukusi kuusema UKWELI MCHUNGU ambao baadhi ya wapenda mpira(wajinga) hawapendi kuusikia.
 
Chakushangaza wote humu mnao comment kumuunga mkono Mwambukusi hakuna hata mmoja aliye jitokeza kwenye maandamano.
 
Ww unaye zingatia mambo ya msingi kwenye maandamano ulikuwepo ili kudai hizo haki?
 
Ulevi wa madaraka na ulimbukeni. Utadhani yeye ndiye rais wa TLS wa kwanza na wa mwisho
 
Kwani Mwabukusi nini alichoongea ambacho siyo sahihi?

Watanzania "wamelogwa" Kwa ushabiki wa Yanga na Simba.
Full Stop
Wasiwapangie watanzania maisha
 
Jamaa amejichanganya sana.
 
Hakuna mwenye akili timamu atakayekubaliana na binaadamu kumteka mwenzie na kumtesa au kumuua lakini bado havizuii watu kuendelea na wanavyovipenda. Tatizo la Chadema ni kutaka kutuaminisha watanzania kuwa matatizo yao ni matatizo yetu.
Daa; uzi unahusu TLS, wewe umeingiza masuala ya Chadema tena. Halafu lini Chadema walituomba Watanzania tuandamane kwasababu ya matatizo yao? Hivi watu kutekwa, kuuawa ni matatizo ya Chadema? Halafu bado tunamsema Mwambukusi anatutukana? Kwa maandishi haya, Mwambukusi anakua kakosea wapi?
 
Chakushangaza wote humu mnao comment kumuunga mkono Mwambukusi hakuna hata mmoja aliye jitokeza kwenye maandamano.
Hahaaaa, keyboard warriors.
 
Kasema kweli ndiyo zinatumika kupumbaza watu wanakuwa wajinga
Sasa Wacha tujiulize sisi wengine tumepumbazwa.. huyo rais wenu wa TLS mbona hatukumuona magomeni pale? Na nyinyi humu madomo kaya wa Jamii Forums mbona hatukuwaona? Kwanza kabla ya kuwadhihaki wananchi wa kawaida jiangalieni nyinyinajiita waelewa na wajuaji mbona mmeishia kuwa keyboard worrier hapa JF
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…