Kuna mtendaji wa kijiji cha Rung'abure anaitwa Sendy, huyu jamaa ni dizaini ya wale mchwa wakubwa tena wala vyuma.
Amekuwa na rekodi mbaya sana toka aingie kazini amesimamishwa mara nne kwa makosa tofauti.
Mwaka 2012 akiwa kijiji cha Bonchugu alikamatwa baada ya kuuza vocha za ruzuku ya pembejeo za wakulima na kupiga mpunga, baadae kesi ikaunguruma na kutokana na magumashi zilizokuwepo kipind kile anachokaga na kurudishwa kazini.
2. Mwaka 2014 baada ya kurudishwa kazini akapangiwa Ngoreme, huko akampa mwanafunzi wa shule mimba na akasimamishwa kazi, ajabu baadae akarudishwa kazini na kupangiwa Kijiji cha Nyamerama kama VEO. Huko nako alituhumiwa kwa kuuza ardhi /shamba la kijiji na baadae wakagombana na Mwenyekiti wa kijiji kabla ya kusogea kijiji cha Rung'abure . Hapa napo amefanya madudu mengi. Kwanza amejipa madaraka ya kugawa fedha za TASAF kinyume na taratibu na amekula Ile asilimia inayobaki kijijin na amekutwa na DC - Serengeti akikiuka huo utaratibu, pili DC amemkuta akikiuka taratibu za kazi, siku hiyo DC alifika ofisini kwake ikiwa saa tano asubuhi na kwenye daftar la mahudhurio alikuta huyo VEO amesaini ameingia kazin saa moja na nusu asubuhi na kuandika ametoka saa kumi jioni. Mda huo DC anashuhudia hayo ilikuwa saa tano asubuhi.
Juzi tarehe 28/3/2016 tena huyo VEO amedai vocha za ruzuku ya pembejeo za wakulima zimepotea tena.
Huyo ndo Jacob Sendy almaarufu John Sulusi anaetumia cheti cha mtu mwingine Jacob Tuguro kufanya figisufigisu serikalini. Na hapa ndipo Serengeti ambapo DC anashuhudia uozo kama huu halafu anapiga kimya.
Tuone kama Mh Magesa Mulongo atayaweza haya.