Toyota Crown Athlete - ‘the Japanese Benz’

Sasa unafikiri kwa uongozi huu wa nani kama mama na machawa wanavyopambana akalie kiti hadi 2030 unafikiri Petroli itakuwa bei gani? Kama kila mwezi inaongezeka Tsh. 150
Mi nafikiri tukiangalia suala la demand and supply, demand itakuwa ndogo na supply itakuwa kubwa kwa sababu Europe na USA watakua wamepunguza matumizi makubwa ya mafuta, hivyo wauzaji wa mafuta watashusha bei cause shehena ya mafuta itakuwa kubwa kuliko watumiaji(supply and demand).

Hapa kwetu wapiga deal wakiamua kutufanyia roho mbaya ndo hivyo, lakini natarajia mafuta yatapungua bei unless mama na chawa zake waamue kuzingua. lakini sikukatalii maono yako.

Tujiandae kisaikolojia dunia inakwenda ku transform katika hali nyingine kabisa, kuna ambao wata tajirika kupitia fursa zitakazo kuwepo na kuna ambao watashuka.

Ushauri kwa mafundi wa bongo, wajiandae kujifunza kuhusu mifumo ya gari za umeme. kama ulivyosema kuna watu watazinunua.
 
Dah! mzee hio ya mafuta lita 1 itakuwa 6000 imetokea wapi? 🤣 hayo mahesabu umepigaje?
Ongeza 400 tu kila mwaka utapata jibu.

Mwaka huu tunafunga na TZS 3400 per litre, 2024 itakuwa TZS 3800... 2025 ni TZS 4200....2026 ni TZS 4600.... 2027 ni TZS 5000.....2028 ni TZS 5400.... 2029 ni TZS 5800...2030 ni TZS 6200.
 
Hivi navyoongea kuna gari moja ya umeme mtu alishea humu iko Serengeti mbugani. Ni chinese Brand moja kalii inaitwa Li L8 Suv sasa imagine bongo watu wakiamua kuzinunua hata miaka 3 haishi zitakuwa chungu tele barabarani.

CCM hawawezi shusha mafuta hata mapipa yakigawiwa bure huko duniani. Magufuli tu ndio aliweza shusha bei when barrel price dropped to USD 0 kipindi cha Corona bei ikawa na statutory charges tu. Ila nina hakika nchi ingekuwa chini ya kiongozi mpiga dili bado enzi za Covid wese lingebakia 2300 na kuzidi kupanda bila huruma.
 
Ongeza 400 tu kila mwaka utapata jibu.

Mwaka huu tunafunga na TZS 3400 per litre, 2024 itakuwa TZS 3800... 2025 ni TZS 4200....2026 ni TZS 4600.... 2027 ni TZS 5000.....2028 ni TZS 5400.... 2029 ni TZS 5800...2030 ni TZS 6200.
Dah mzee hio kali, kikubwa uhai na hii platform iendelee kuwepo, kuna siku tutarudi kuhakikisha hapa tulichoandika tukijaaliwa uhai.

Sema bongo hasa kwa sie car enthusiast ni kama wazazi kuna mistake walifanya 🤣, US unachukua chuma kwa mkopo unalipa taratibu, halafu chuma ya maana.
 
Sasa shida ipo kwa hao wanakijiji elimu Yao na ufahamu wao sio kama wako. And why uishi wanavyokudhania wewe -na usiishi wewe kama wewe?
 
Kuna Crown Royal Ile Sasa ndio moto ProMax. Hata bei sio yake YAP.
 
Hivi navyoongea kuna gari moja ya umeme mtu alishea humu iko Serengeti mbugani. Ni chinese Brand moja kalii inaitwa Li L8 Suv sasa imagine bongo watu wakiamua kuzinunua hata miaka 3 haishi zitakuwa chungu tele barabarani.
Sahihi, watu watazivuta, wabishi wapo, tena kama hio battery uliosema ina charge 15 min na kwenda 1200 km , serikalini zitanunuliwa sana, hilo naliona kabisa.
 
Bongo nchi ya laana hii basi tu tumezaliwa hapa ila Ulaya ndio sehemu sahihi ya binadamu kuishi
 
Sahihi, watu watazivuta, wabishi wapo, tena kama hio battery uliosema ina charge 15 min na kwenda 1200 km , serikalini zitanunuliwa sana, hilo naliona kabisa.
Yani kinachotatiza watu ni charging time tu na capacity ya kutunza umeme. Benchmark ya 1000kms per charge ikifikiwa wengi watahamia kwenye fully EV. Sahizi transformation kwenda hybrid imeanza kufanyika kwa kasi sana. Naona watu kibao wananunua Prius Hybrids uoga umeisha.

Kwa ujio wa Solid state batteries solution ya 1000kms per charge itafanikiwa na ndipo watu watanunua gari za umeme kwa kasi. Kero ya mafuta wengi washaichoka sema basi tu gari za umeme ni aghali kwa sasa.
 

Nahisi ndio huu unyama, dah imetulia balaa.

Dah, ebwanaeeh, hivi wazungu kwa nini wanatufanyia hivi, hio infotainment screen ni ya dunia nyingine kabisa.
 
Sahihi sana, kama kawaida yetu, mchina muokozi wetu hawezi kutuacha tuwe wanyonge ndugu zake lazima atafanya jambo.

Ngoma ni umeme tu, watu wanapenda gari powerful na luxury lakini sema ndio hivyo mafuta! mafuta! mafuta!, mtu yupo traffic light anazima gari... 🤣.
 
Kuna Crown Royal Ile Sasa ndio moto ProMax. Hata bei sio yake YAP.
Ile Hybrid Max Platinuma unaiweka mkononi kwa 180M kwa sasa ila ile ya LIMITED edition unaipata kwa 145M tu mkononi. Zote ni za 2023 sema Hybrid Max ndio kiboko ina 340HP while Limited ni 236HP
 
Mchina kashaovertake makampuni yote ya EV kwa mauzo duniani. 🤣 Anatoa vyuma vya kwenda yani kwa kasi ya mwanga
 
Tesla anajamba kwenye maji, mchina na kampuni lake la BYD kashatoa gari kali ya ku compete na Tesla. Inakula mauzo yake tayari ndio maana Marekani anamuandama sana mara asiuziwe semi conductor mara asiuze marekani ilimradi mshike mshike tu
Dah! Chinese hawachelewagi, tayari walishachungulia EV za tesla na kufanya yao
 
Ile Hybrid Max Platinuma unaiweka mkononi kwa 180M kwa sasa ila ile ya LIMITED edition unaipata kwa 145M tu mkononi. Zote ni za 2023 sema Hybrid Max ndio kiboko ina 340HP while Limited ni 236HP
Hizi Sasa unaendesha Gari...
 
Tesla anajamba kwenye maji, mchina na kampuni lake la BYD kashatoa gari kali ya ku compete na Tesla. Inakula mauzo yake tayari ndio maana Marekani anamuandama sana mara asiuziwe semi conductor mara asiuze marekani ilimradi mshike mshike tu
Kwa kweli binafsi nimefarijika mno kusikia jamaa tayari wanatoa EV, hawa ndugu zetu wanajua hali zetu, naamini hawatotusahau, kikubwa tuwaombee tu.
 
Dunia inaenda mbali Sana na technology yake ... WAJUKUU zetu watakuja kuishi kwenye dunia ya ajabu Sana Kwa mfano hizi electronic vehicle sio Ile Raha yake kuendesha gari isiyotoa mlio na yenye single pedal.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…