Tozo Mpya: Kwa tabia za Watanzania, Rais Samia kazia hapohapo

Tozo Mpya: Kwa tabia za Watanzania, Rais Samia kazia hapohapo

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Kwa namna nikienda kwenye maduka ninavyoona Wafanyabiashara wanafanya mauzo bila kutoa risiti na Wananchi wananunua bidhaa bila kudai risiti napenda kusisitiza, Mama yangu Samia kazia hapo hapo.

Nchi inahitaji kodi ili huduma za maendeleo ziweze kutolewa na kama wananchi hawako tayari kushiriki kwenye njia za kawaida kabisa katika kuhakikisha wanalipa kodi stahiki ili nchi ipate mapato basi njia hizi zingine kama kuweka kodi kwenye miamala ya kibenki hazina budi kutumika ili tupate mapato

Niliandika uzi humu kwa namna gani Watanzania hawajali suala la kuhakikisha wanalipa kodi ili kuhakikisha nchi yao inapata mapato kwa ajili ya miradi ya maendeleo. Leo hii mfano mdogo tu mtu kwenye duka ana bidhaa zenye thamani ya milioni zaidi ya 5 au 10 ila hana mashine ya efd, kama anayo mashine basi kaiweka uvunguni imejaa vumbi anauza bidhaa za mamilioni mwezi mzima ila hakuna hata risiti anayotoa.

Kwa wananchi pia, pamoja na matangazo kibao ya TRA kwenye radio na television kuwa wanaponunua wadai risiti ila unamkuta mtu anafanya manunuzi na hajali kama anatakiwa kudai risiti ili nchi ipate mapato kwa shughuli za maendeleo.

Siku ya mwisho wanaishia kuumizwa wafanyakazi kwa kukatwa kwenye mishahara yao kwa sababu wananchi hawataki kutimiza wajibu wao kwenye kulipa kodi

With wangu, Rais wangu Mama Samia usicheke na nyani utavuna mabua, wanataka bima ya afya kwa wote, elimu bure hadi form six, madaraja yajengwe, barabara zijengwe sasa wasipolipa kodi utapata wapi hela za kufanya yote hayo?

Kazia hapo hapo Mama yangu!
 
Halafu kila siku hizo kodi mnazichezea tu kwenye matumizi ya kipuuzi. Na kwa taarifa yenu tutakwepa sana tu. Kama ni huko benki, hatuweki tena hela.
Kama barabara hazijengwi na kama wanafunzi wanasoma kwa kulipa ada hadi form six basi kweli kodi zinachezewa
 
images76543.jpeg
 
Kama barabara hazijengwi na kama wanafunzi wanasoma kwa kulipa ada hadi form six basi kweli kodi zinachezewa
Na hizo hela mnazokopa kila siku mnafanyia nini? Halafu suala la elimu bure ni hitaji la Watanzania, au ni kieherehere chenu?
Kuna Mtanzania anaweza kukosa kweli elfu 20 au elfu 70 ya ada kwa mtoto wake?

Nyinyi ni wezi tu na mafisadi mlio kubuhu! Na hata asilimia kubwa ya makusanyo ya hizo kodi mnatumia tu kwenye matumizi yenu ya kifahari na ufisadi! Hivyo nakuhakikishia kabisa, Wazalendo wengi tutaendelea kukwepa kodi kadiri iwezekanavyo! And we are proud of that.
 
Na hizo hela mnazokopa kila siku mnafanyia nini? Halafu suala la elimu bure ni hitaji la Watanzania, au ni kieherehere chenu?
Kuna Mtanzania anaweza kukosa kweli elfu 20 au elfu 70 ya ada kwa mtoto wake?

Nyinyi ni wezi tu na mafisadi mlio kubuhu! Na hata asilimia kubwa ya makusanyo ya hizo kodi mnatumia tu kwenye matumizi yenu ya kifahari na ufisadi! Hivyo nakuhakikishia kabisa, Wazalendo wengi tutaendelea kukwepa kodi kadiri iwezekanavyo! And we are proud of that.
Unadhani hayo madeni ya hizo hela zinazokopwa yanalipwa na yatalipwa kwa pesa gani wakati hutaki kushiriki vizuri katika kulipa kodi ili nchi ipate mapato?
 
Hivi unajua kuwa GSMs ndio kinara wa ukwepaji kodi na hata hao viongozi wako wanajua

Wastani wa kwenye kila kontena kumi za GSMs zinazolipiwa kodi ni mbili tu
 
Unadhani hayo madeni ya hizo hela zinazokopwa yanalipwa na yatalipwa kwa pesa gani wakati hutaki kushiriki vizuri katika kulipa kodi ili nchi ipate mapato?
Acheni kuendekeza rushwa na ufisadi! Punguzeni matumizi yasiyo na ulazima wowote serikalini! Kila mwaka mnanunua magari ya kifahari ya kutembelea!
Kuna watu wanalipwa mamilioni ya mishahara kila mwezi huku vyeo vyao vikiwa havina tija yoyoye ile, maana ni vya kisiasa!

Nakuhakikishia mimi ni mmoja ya watu wanaofurahia kukwepa kodi katika nchi ambayo haijielewi! Mimi mfanyabiashara akiandika hata laki 1 kwa bidhaa niliyonunua laki 5, nakubali kwa moyo mkunjufu kabisa.
Muhimu tu aniuzie kwa bei rafiki.


Kamwe sitokuja kudai risiti kwenye nchi iliyojaa ufisadi na upigaji. Yaani watu wanatafuta juani, halafu nyinyi mnakula kivulini!
 
Hivi unajua kuwa GSMs ndio kinara wa ukwepaji kodi na hata hao viongozi wako wanajua

Wastani wa kwenye kila kontena kumi za GSMs zinazolipiwa kodi ni mbili tu
Kama GSM anakwepa kodi kuna mjinga mmoja anamsaidia hivyo ni sawa nae huyo mjinga aonjwe kulipa tozo kwa kupitia miamala ya kibenki
 
Acheni kuendekeza rushwa na ufisadi! Punguzeni matumizi yasiyo na ulazima wowote serikalini! Kila mwaka mnanunua magari ya kifahari ya kutembelea!
Kuna watu wanalipwa mamilioni ya mishahara kila mwezi huku vyeo vyao vikiwa havina tija yoyoye ile, maana ni vya kisiasa!

Nakuhakikishia mimi ni mmoja ya watu wanaofurahia kukwepa kodi katika nchi ambayo haijielewi! Mimi mfanyabiashara akiandika hata laki 1 kwa bidhaa niliyonunua laki 5, nakubali kwa moyo mkunjufu kabisa.
Muhimu tu aniuzie kwa bei rafiki.


Kamwe sitokuja kudai risiti kwenye nchi iliyojaa ufisadi na upigaji. Yaani watu wanatafuta juani, halafu nyinyi mnakula kivulini!
Na wewe anza kudai risiti kila unaponunua bidhaa na kutoa risiti kila unapouza bidhaa ili kusiwe na tozo
 
Na wewe anza kudai risiti kila unaponunua bidhaa na kutoa risiti kila unapouza bidhaa ili kusiwe na tozo
Nyinyi siku zote si mnatuona hatuna akili! Tutaelewana tu. Yaani kutoka moyoni huwa najisikia raha kweli nikikwepa kodi, au nikumona mjasiriamali mwenzangu naye akikwepa kodi!

Maana hiyo kodi yenyewe ikilipwa, inaenda kuliwa tu na watu wenye midomo mirefu.
 
Kwa namna nikienda kwenye maduka ninavyoona Wafanyabiashara wanafanya mauzo bila kutoa risiti na Wananchi wananunua bidhaa bila kudai risiti napenda kusisitiza, Mama yangu Samia kazia hapo hapo.

Nchi inahitaji kodi ili huduma za maendeleo ziweze kutolewa na kama wananchi hawako tayari kushiriki kwenye njia za kawaida kabisa katika kuhakikisha wanalipa kodi stahiki ili nchi ipate mapato basi njia hizi zingine kama kuweka kodi kwenye miamala ya kibenki hazina budi kutumika ili tupate mapato

Niliandika uzi humu kwa namna gani Watanzania hawajali suala la kuhakikisha wanalipa kodi ili kuhakikisha nchi yao inapata mapato kwa ajili ya miradi ya maendeleo. Leo hii mfano mdogo tu mtu kwenye duka ana bidhaa zenye thamani ya milioni zaidi ya 5 au 10 ila hana mashine ya efd, kama anayo mashine basi kaiweka uvunguni imejaa vumbi anauza bidhaa za mamilioni mwezi mzima ila hakuna hata risiti anayotoa.

Kwa wananchi pia, pamoja na matangazo kibao ya TRA kwenye radio na television kuwa wanaponunua wadai risiti ila unamkuta mtu anafanya manunuzi na hajali kama anatakiwa kudai risiti ili nchi ipate mapato kwa shughuli za maendeleo.

Siku ya mwisho wanaishia kuumizwa wafanyakazi kwa kukatwa kwenye mishahara yao kwa sababu wananchi hawataki kutimiza wajibu wao kwenye kulipa kodi

With wangu, Rais wangu Mama Samia usicheke na nyani utavuna mabua, wanataka bima ya afya kwa wote, elimu bure hadi form six, madaraja yajengwe, barabara zijengwe sasa wasipolipa kodi utapata wapi hela za kufanya yote hayo?

Kazia hapo hapo Mama yangu!
ishu sio kulipa kodi!ishu ni kodi zetu hatuoni zikitumika ipasavyo,watu tuliowapa dhamana hawasimamii ipasavyo kodi zetuu!ndo maana wananchi hawataki kulipa kodi
 
Nyinyi siku zote si mnatuona hatuna akili! Tutaelewana tu. Yaani kutoka moyoni huwa najisikia raha kweli nikikwepa kodi, au nikumona mjasiriamali mwenzangu naye akikwepa kodi!

Maana hiyo kodi yenyewe ikilipwa, inaenda kuliwa tu na watu wenye midomo mirefu.
Huwezi kukwepa kodi lazima Serikali itaipata tu hela yako kwa hii mikakati kabambe labda ukaishi porini kama Chui
 
Unadhani hayo madeni ya hizo hela zinazokopwa yanalipwa na yatalipwa kwa pesa gani wakati hutaki kushiriki vizuri katika kulipa kodi ili nchi ipate mapato?
Wewe ni mwehu kweli. Madeni hayo yameleta tija gani ya kushawishi mtu alipe tozo? Kama lengo ni mradi mradi gani uliokamilika na kuleta tija hadi sahizi ya kumfanyia ahueni mtanzania?Tozo ni kwa ajili ya madarasa, misaada ya CoVid nayo ni kwa ajili ya madarasa. Hicho kipaumbele cha kwenda kuzalisha majobless wenye vyeti badala ya kuimarisha sekta za uzalishaji na viwanda ni upuuzi uliotukuka.

Magufuli alitukamua makende ila hatime safari ya buguruni mwenge ilibadilika toka masaa 3 hadi dakika 25! Hivi ndio vitu vitatupa moyo wa kutoa tozo bila kulalamika.
 
ishu sio kulipa kodi!ishu ni kodi zetu hatuoni zikitumika ipasavyo,watu tuliowapa dhamana hawasimamii ipasavyo kodi zetuu!ndo maana wananchi hawataki kulipa kodi
Huoni zikitumika ipasavyo barabara zinajengwa kwa hela yako? Gharama za ada form five na Six zinafidiwa kwa hela yako? Madeni ya mikopo yanalipwa kwa pesa yako?
 
Back
Top Bottom