Tozo zinaweza kugeuka na kuwa wizi wa dola dhidi ya Wananchi

Tozo zinaweza kugeuka na kuwa wizi wa dola dhidi ya Wananchi

Yeah chochote ukihalalisha kinakuwa halali, uzalendo unauhimiza kwa wananchi tu wanaoathirika na hizo tozo ila hao viongozi wanaolipwa mishahara mizuri na kuishi vizuri kwa gharama za hizi tozo zetu wewe huna cha kuwahimiza uzalendo.
Nimewahimiza Sana juu ya usimamaizi mzuri wa pesa za umma, nimewahimiza na kuwashauri Kama mwananchi na kijana wa kitanzania kuwa waziogope pesa za umma Kama ukoma, wasiziguse na kuzitumia kwa maslahi yao binafsi
 
Unapotunza pesa bank harafu unakatwa unakuwa umezalisha nini?
Unajua wewe The Sunk Cost Fallacy unahitaji kuelimishwa tu ili kukamua ujinga wako huo...

Unapaswa kuelewa taxation cycle inavyokwenda. Serikali haiwezi tu kunyang'anya watu fedha zao eti kwa sababu imewaona wana fedha. This is stupidity of high quality...!

1. MOSI; Fedha inapokuwa benki, maana yake imezalishwa huko na serikali imeshachukua kila chake kwa mujibu wa sheria..

E.g mshahara wa mtu. Si utakuwa umekatiwa PAYE?. Au mauzo ya mfanyabiashara fulani. Je anakuwa hajakatwa kodi mbalimbali..? Sasa kwanini serikali izifuate pesa hizo hizo benki ili kutaka kodi tena?? Ndugu The Sunk Cost Fallacy unaweza kuwa honest ingalau kwa dakika moja ili ujibu swali hili kwa usahihi...?

2. MBILI; Mimi ninapopeleka pesa benki, ni kwa ajili kutunziwa na ofcoz at first place nakuwa najua kuwa, nitakwenda kulipa gharama ya kutunziwa. Kwa hiyo ni haki nilipe gharama hiyo. Hii kwa ajili ya benki. Maana yake benki inaingiza kipato...

3. TATU; Kumbuka pia benki naye ni tax payer. Analipa kodi na tozo kutoka kwenye mapato ya faida anayokusanya kutoka kwa wateja....

4 NNE; Serikali haipaswi kuingia benki kwa watu walewale wa mlango wa nyuma kudai tena kodi toka kwa pesa ileile ambayo imekwisha kulipiwa kodi lakini mtu ameipeleka benki tu ili kutunza...

Serikali inatakiwa kuitoza benki hiyo kodi na si wateja tena...!!
 
Kodi au tozo haziwahi kuwa wizi ndio maana nilikuuliza kama ni wizi hizi pesa zinaenda kutumika wapi? Hukujibu..pesa inatumika kuboresha huduma mbalimbali kama hizi 👇
What rubbish! Kumbe ndio maana wengi wa mamilionea wanaotuhumiwa kwa wizi hukimbilia kuichangia CCM na hivyo kujitakasa!

Wizi ni wizi, hata ukiitwa tozo ni wizi tu. Hakuna wizi mbaya kama wizi wa kidola...kwamba
serikali inatafuta njia ya kuwaibia wananchi wake, kweli!

Ingawa CCM imejengwa kwenye misingi ya rushwa na wizi, sikujua watakuja na sera ya kuwaibia wananchi wa Tanzania kupitia hiyo inayoitwa tozo!

Tozo ni wizi, hakuna serikali hapa duniani inaweza kutafuta hela kwa kubariki wizi kwa njia tunazozishuhudia zikitendeka hapa kwetu Tanzania, hakuna!

Cha ajabu sasa, wananchi wametulia kama kondoo wanaopelekwa machinjoni. Taasisi zetu nyingi zinaongozwa na vijana waliozaliwa na kukulia ndani ya CCM!

Wengi wana tuhuma za wizi toka utotoni...ama waliiba majina, waliiba mitihani, waliiba vyeti na yawezekana wengine wametumika katika wizi wa kura!

Hapana, umefika wakati wa kuita wizi kwa jina lake halisi na si kuipamba kwa majina ya ajabu ajabu.
1661162547424.png

You can put lipstick on a pig, it is still a pig, fullstop!
 
Unajua wewe The Sunk Cost Fallacy unahitaji kuelimishwa tu ili kukamua ujinga wako huo...

Unapaswa kuelewa taxation cycle inavyokwenda. Serikali haiwezi tu kunyang'anya watu fedha zao eti kwa sababu imewaona wana fedha. This is stupidity of high quality...!

1. MOSI; Fedha inapokuwa benki, maana yake imezalishwa huko na serikali imeshachukua kila chake kwa mujibu wa sheria..

E.g mshahara wa mtu. Si utakuwa umekatiwa PAYE?. Au mauzo ya mfanyabiashara fulani. Je anakuwa hajakatwa kodi mbalimbali..? Sasa kwanini serikali izifuate pesa hizo hizo benki ili kutaka kodi tena?? Ndugu The Sunk Cost Fallacy unaweza kuwa honest ingalau kwa dakika moja ili ujibu swali hili kwa usahihi...?

2. MBILI; Mimi ninapopeleka pesa benki, ni kwa ajili kutunziwa na ofcoz at first place nakuwa najua kuwa, nitakwenda kulipa gharama ya kutunziwa. Kwa hiyo ni haki nilipe gharama hiyo. Hii kwa ajili ya benki. Maana yake benki inaingiza kipato...

3. TATU; Kumbuka pia benki naye ni tax payer. Analipa kodi na tozo kutoka kwenye mapato ya faida anayokusanya kutoka kwa wateja....

4 NNE; Serikali haipaswi kuingia benki kwa watu walewale wa mlango wa nyuma kudai tena kodi toka kwa pesa ileile ambayo imekwisha kulipiwa kodi lakini mtu ameipeleka benki tu ili kutunza...

Serikali inatakiwa kuitoza benki hiyo kodi na si wateja tena...!!
Tozo ni malipo ya uzalendo Wala haiitwi Kodi..

Wazazi wetu walichapwa bakora kuchangia maendeleo by physical na Kwa kutoa Kodi na michango mbalimbali..

Watu wamebomolewa majumba yao tena wengine bila fidia kwa ajili ya maendeleo.

Hatuna wajomba wa kutuletea maendeleo zaidi ya kujichanga wenyewe..

Utaumia in short run ila uta enjoy maisha in long-run..

Kuwa mzalendo changia maendeleo ya Nchi yako.
 
What rubbish! Kumbe ndio maana wengi wa mamilionea wanaotuhumiwa kwa wizi hukimbilia kuichangia CCM na hivyo kujitakasa!

Wizi ni wizi, hata ukiitwa tozo ni wizi tu. Hakuna wizi mbaya kama wizi wa kidola...kwamba
serikali inatafuta njia ya kuwaibia wananchi wake, kweli!

Ingawa CCM imejengwa kwenye misingi ya rushwa na wizi, sikujua watakuja na sera ya kuwaibia wananchi wa Tanzania kupitia hiyo inayoitwa tozo!

Tozo ni wizi, hakuna serikali hapa duniani inaweza kutafuta hela kwa kubariki wizi kwa njia tunazozishuhudia zikitendeka hapa kwetu Tanzania, hakuna!

Cha ajabu sasa, wananchi wametulia kama kondoo wanaopelekwa machinjoni. Taasisi zetu nyingi zinaongozwa na vijana waliozaliwa na kukulia ndani ya CCM!

Wengi wana tuhuma za wizi toka utotoni...ama waliiba majina, waliiba mitihani, waliiba vyeti na yawezekana wengine wametumika katika wizi wa kura!

Hapana, umefika wakati wa kuita wizi kwa jina lake halisi na si kuipamba kwa majina ya ajabu ajabu. You can put lipstick on a pig, it is still a pig, fullstop!
Sio wizi ndio maana watu wametulia..

Huu ukiwa ndio wizi acha uendelee 👇
 

Attachments

  • Screenshot_20220816-203211.png
    Screenshot_20220816-203211.png
    87.3 KB · Views: 2
  • Screenshot_20220812-104856.png
    Screenshot_20220812-104856.png
    259.9 KB · Views: 2
  • Screenshot_20220812-104841.png
    Screenshot_20220812-104841.png
    268.4 KB · Views: 2
  • Screenshot_20220812-104925.png
    Screenshot_20220812-104925.png
    305.9 KB · Views: 2
  • Screenshot_20220713-194118.png
    Screenshot_20220713-194118.png
    155.5 KB · Views: 2
Hapana, bado wewe ni mpumbavu tu...!!

Kwa kuwa unataka kununua gari nyumbani kwako, ina maana utauza chakula cha watoto wako na nyumba yako ili ukanunue gari...?

Kwani kununua gari ni jambo baya? La, hasha!

Bali mtu huyu anatumia njia yenye madhara kwake mwenyewe kujipatia kitu chema vilevile...

Ndivyo zilivyo fikra zako wewe..

Na huu ndiyo utetezi wako. Kwamba, it's okay kwa serikali kuwanyang'anya watu vya kwao hata baada ya kuwa imeshalipwa cha kwake inachostahili. Huu ni wizi..

Sasa kwa kuwa wewe huyatafakari vyema mambo haya na umeamua uwe mjinga kwa sababu una uelewa wa upande mmoja (one way traffic understanding), kwamba ni LAZIMA KILA MTU ALIPE KODI lakini hutaki kujiuliza kodi zipi na kwa namna gani...

Hawa hawatafuti kodi hizi kwa maendeleo yetu kwa sababu kwa miaka 60 tangu uhuru wameshakusanya kodi nyingi sana lakini kilichofanywa na kodi hizi hakifanani kabisa...

Ndo kusema kubwa, wanakusanya TOZO HIZI ZA KIWIZIWIZI ili hawa watu CCM ambao ni highly privileged tayari, wagharamie gharama ya kubaki kwenye mamlaka na madaraka yao ya kiserikali na pia kutumia kwenye anasa zao...

Narudia tena kukuambia kwamba, kama unadhani kwa miaka hii miwili hawa nduguzo watakujengea barabara au watakuletea maji kila kijiji, basi wewe The Sunk Cost Fallacy ni mjinga na mpumbavu wa kiwango cha juu kabisa...!!
Ukiondoa lugha chafu, hoja yako ina mashiko.
 
Nimewahimiza Sana juu ya usimamaizi mzuri wa pesa za umma, nimewahimiza na kuwashauri Kama mwananchi na kijana wa kitanzania kuwa waziogope pesa za umma Kama ukoma, wasiziguse na kuzitumia kwa maslahi yao binafsi
Wenzetu hao wana mishahara mikubwa na bado serikali inawagharamia bure kwenye huduma muhimu na bado wana nafasi za kupiga pesa, sisi huku pamoja na kwamba hakuna cha bure tunaunga unga ndio tunahimizwa uzalendo kwa kuwekwa utitiri wa tozo na tukilalamika tunaonekana tunapenda bure bure tu hatuna uzalendo.
 
Kama na wao wangekuwa wanalipa Kodi, nadhani wasingekuwa wanaumiza wananchi namna hiyo
 
Wewe ndio mpumbavu kwa kujenga hoja Kwa kufanya reference ya Waziri unaemtaja..

Tuambie basi wewe hizi tozo ni Kwa ajili gani Ili na mimi nikuwekee ushahidi wa nachosema..

Mwisho CCM kushindwa miaka mingine haimaanishi itashindwa na leo,Leo Rais ni Mwanamama na miaka hiyo Marais walikuwa Wanaume ambao kwa hulka huwa ni wezi..

Nasisitiza Rais Samia ataweza hayo ndio maana mwaka mmja tuu kajenga vituo vya afya 252,taja Rais mwingine aliyewahi weza?

Rais Samia Ataweza ndio maana mwaka mmja huu kahamisha bajeti ya barabara Vijijini kutoka bil.252 hadi bil.802 Ili kutimiza hiyo azma..

Rais Samia ataweza ndio maana kwa mwaka mmja Katia bajeti ya Maji kutoka bil.334 hadi bil.787 na maelfu ya miradi inaendelea..

Hivyo hivyo na sekta zingine zote kama kilimo nk..So Usilete ujinga wa kujenga hoja yako kwa failures.
Fedha za COVID ndio unajivunia kujengea Madarasa na vituo vya Zahanati??. Tozo ni za akini Mwigulu kula bata na kujitajirisha tu...
 
Fedha za COVID ndio unajivunia kujengea Madarasa na vituo vya Zahanati??. Tozo ni za akini Mwigulu kula bata na kujitajirisha tu...
Wewe acha umbumbu wako,hakuna pesa ya covid imejenga vituo vya afya bali imejenga majengo ya EMD kwenye hospital za Mikoa na Wilaya na hospital za Rufaa..

Zahanati na Vituo vya afya vinajengwa kwa pesa ya tozo na Mapato ya serikali Kuu..

Kwani kabla ya pesa ya covid madarasa yalikuwa hayajengwi? Madarasa ya uviko yalikuwa mahsusi Ili kuhakikisha maelfu ya watoto wa Elimu bure waliomaliza mwaka juzi hawakosi nafasi.
 
Msingi wa kodi, tozo au ushuru ni mapato. Kutokana na mapato uliyoyaingiza, sehemu ya hayo mapato, wewe uliyeingiza unastahili kutoa sehemu ya hayo mapato kama kodi, ushuru, tozo au jina jingine lolote utakalopenda kuita lenye lengo la makato yanayyoenda kwenye mamlaka za Serikali. Hii ni kanuni mama ya kodi.

Kanuni kuu ya pili, mapato yalikwishalipiwa kodi, tozo au ushuru hayastahili kulipishwa tena kwa mara ya pili. Double taxation inazuiwa.

Wizi ni kuchukua kitu chochote ambacho siyo stahili yako. Wizi huu unaweza kuwa wa mtu mmoja dhidi ya Serikali, taasisi, mtu mwingine au kikundi au Serikali dhidi ya wananchi wake au dhidi ya mwananchi mmoja.

Serikali inapomtoza mwananchi kodi zaidi ya kiwango halali au zaidi ya mara moja kwa mapato yale yale, huo ni wizi wa dola dhidi ya mwananchi.

Maswali muhimu ya kujiuliza:

1) Kwa mfano, mfanyakazi au mfanyabiashara amepata mshahara au pesa ya mauzo, ameilipua kodi tayari, ikawekwa benki, benk amelipia gharama ya huduma, na benki inalipa kodi kwa mapato yanayotokana na utoaji huduma, huyu mteja anapotaka kuichukua pesa yake, akatozwa tena na Serikali, ni mapato gani ameyapata kule benki?

2) Kwa mfano, mfanyakazi, kwenye mshahara wake amekatwa PAYE, pesa imeenda benki, anatoa kwenye ATM, anakatwa kodi kwa mara ya pili, anaweka kwenye simu, pesa ile ile anaituma kwa mama yake kijijini anakatwa kodi, mama yake anaenda kwa wakala kuchukua ile pesa, anakatwa kodi.

Pesa siyo chakula, lazima huyu mama ataitumia, anaenda kununua chumvi anakatwa kodi. Yaani makato mara 5 kwa mapato yale yale, hii ni halali? Lakini ikumbukwe kwamba, benki kutokana na mapato yake yanayotokana na utoaji huduma imekatwa kodi, mtandao wa simu kutokana na mapato ya utoaji huduma ya usafirishaji fedha, nao umekatwa kodi, na muuzaji wa chumvi naye amekatwa kodi.

Tax regime ya Tanzania ni lazima iangaliwe upya. Siyo regime rafiki kwa wananchi wala wawekezaji.

Siku zote kodi utitiri au kubwa huua uwekezaji. Hakuna nchi hata moja Duniani iliyokuwa maskini ambayo iligeuka kuwa tajiri kwa haraka kwa kuwa na kodi utititiri au kodi kubwa.

Dubai, ilipata maendeleo makubwa, na kubadilika kabisa ndani ya miaka 15 tu kwa kufuta kabisa kodi nyingi na kubakia na kodi chache sana. Mpaka leo Dubai ni kituo cha biashara Duniani.

Anayehamasisha Tanzania kuwa na kodi utitiri na kodi kubwa ni adui mkubwa wa maendeleo ya nchi yetu.

Nchi hii inahitaji sana uwekezaji ili watu wetu wapate ajira, na Serikali iwe na vyanzo vingi vya mapato, na siyo kuongeza kodi kwa vyanzo vile vile.

Wazalendo wa nchi hii, wanaoitakia mema Tanzania tukatae mambo yote yanayoua uwekezaji katika Taifa letu.

Tukiwa na sera na sheria ambayo inachochea uwekezaji kivitendo, kama uwekezaji utasababisha japo watanzania milioni 15 kupata ajira za uhakika, na hao milioni 15 angalao kila mmoja kwa wastani akalipa kodi ya sh milioni 4 kwa mwaka, PAYE pekee yake itaipatia Serikali 4,000,000×15,000,000 = 60,000,000,000,000 (trillion 60).

Haya ni mapato ambayo ni karibu 50% ya makusanyo ya Serikali kwa sasa. Na haya ni mapato ambayo Serikali itayapata, na huku mlipa kodi akifurahi kwa kuwa ana ajira inayompa kipato cha uhakika.
Halafu pesa ikipatikana inatumika katika matanuzi ya viongozi fake walioingia madarakani kwa wizi wa kura chini ya mwehu mwendazake. Singida big stars ni kati ya wanufaika wa ufisadi huu
 
Kodi au tozo haziwahi kuwa wizi ndio maana nilikuuliza kama ni wizi hizi pesa zinaenda kutumika wapi? Hukujibu..pesa inatumika kuboresha huduma mbalimbali kama hizi [emoji116]
Wizi wa kidola dhidi ya wananchi, kwa kiasi kikubwa kinachoibwa hupelekwa kuhudumia dola.

Fikiria mwananchi anayetuma mchango wa kumtibu ndugu yake au maziko ya ndugu yake kwa njia ya simu, yeye mwenyewe ameshindwa kusafiri kwa sababu hana nauli, analipishwa tozo ili tozo ikamlipe posho na kumnunulia gari la kifahari Waziri au mkuu wa mkoa, au kugharamia mbwembwe za misafara ya viongozi wakuu wa nchi.

Kama wananchi wana mapato duni, na Serikali yao ni lazima iendane na uduni wa wenye Serikali. Lakini unapokuwa na walipa kodi walio duni kimapato, lakini watendaji wakuu wa Serikali wanataka mbwembwe sawa au hata kuzipita mbwembwe za mataifa yenye vyanzo vingi vya mapato, kwa kuwarundikia walipa kodi tozo nyingi, siyo sahihi, na siyo halali.
 
Mtapiga makelele wewe ila come 2025 mtakapokuta kila Kijiji kina maji,kina barabara,kina Zahanati na vituo vya afya ,kina umeme nk mtajua kwamba kumbe mlikuwa wajinga.
Hayo yote siyo hisani, ni wajibu wa Serikali, na yanastahili kufanywa kwa kutumia kodi halali zinazolipwa na wananchi. Na yanaweza kufanyika mengi zaidi ya hayo, huku wananchi hawanyanyasiki kwa tozo utitiri, alimradi tuwe na sheria rafiki za kodi, sera nzuri za uwekezaji, na mipango mizuri ya Serikali katika kutengeneza mazingira mazuri ya kujenga uchumi.
 
Msingi wa kodi, tozo au ushuru ni mapato. Kutokana na mapato uliyoyaingiza, sehemu ya hayo mapato, wewe uliyeingiza unastahili kutoa sehemu ya hayo mapato kama kodi, ushuru, tozo au jina jingine lolote utakalopenda kuita lenye lengo la makato yanayyoenda kwenye mamlaka za Serikali. Hii ni kanuni mama ya kodi.

Kanuni kuu ya pili, mapato yalikwishalipiwa kodi, tozo au ushuru hayastahili kulipishwa tena kwa mara ya pili. Double taxation inazuiwa.

Wizi ni kuchukua kitu chochote ambacho siyo stahili yako. Wizi huu unaweza kuwa wa mtu mmoja dhidi ya Serikali, taasisi, mtu mwingine au kikundi au Serikali dhidi ya wananchi wake au dhidi ya mwananchi mmoja.

Serikali inapomtoza mwananchi kodi zaidi ya kiwango halali au zaidi ya mara moja kwa mapato yale yale, huo ni wizi wa dola dhidi ya mwananchi.

Maswali muhimu ya kujiuliza:

1) Kwa mfano, mfanyakazi au mfanyabiashara amepata mshahara au pesa ya mauzo, ameilipua kodi tayari, ikawekwa benki, benk amelipia gharama ya huduma, na benki inalipa kodi kwa mapato yanayotokana na utoaji huduma, huyu mteja anapotaka kuichukua pesa yake, akatozwa tena na Serikali, ni mapato gani ameyapata kule benki?

2) Kwa mfano, mfanyakazi, kwenye mshahara wake amekatwa PAYE, pesa imeenda benki, anatoa kwenye ATM, anakatwa kodi kwa mara ya pili, anaweka kwenye simu, pesa ile ile anaituma kwa mama yake kijijini anakatwa kodi, mama yake anaenda kwa wakala kuchukua ile pesa, anakatwa kodi.

Pesa siyo chakula, lazima huyu mama ataitumia, anaenda kununua chumvi anakatwa kodi. Yaani makato mara 5 kwa mapato yale yale, hii ni halali? Lakini ikumbukwe kwamba, benki kutokana na mapato yake yanayotokana na utoaji huduma imekatwa kodi, mtandao wa simu kutokana na mapato ya utoaji huduma ya usafirishaji fedha, nao umekatwa kodi, na muuzaji wa chumvi naye amekatwa kodi.

Tax regime ya Tanzania ni lazima iangaliwe upya. Siyo regime rafiki kwa wananchi wala wawekezaji.

Siku zote kodi utitiri au kubwa huua uwekezaji. Hakuna nchi hata moja Duniani iliyokuwa maskini ambayo iligeuka kuwa tajiri kwa haraka kwa kuwa na kodi utititiri au kodi kubwa.

Dubai, ilipata maendeleo makubwa, na kubadilika kabisa ndani ya miaka 15 tu kwa kufuta kabisa kodi nyingi na kubakia na kodi chache sana. Mpaka leo Dubai ni kituo cha biashara Duniani.

Anayehamasisha Tanzania kuwa na kodi utitiri na kodi kubwa ni adui mkubwa wa maendeleo ya nchi yetu.

Nchi hii inahitaji sana uwekezaji ili watu wetu wapate ajira, na Serikali iwe na vyanzo vingi vya mapato, na siyo kuongeza kodi kwa vyanzo vile vile.

Wazalendo wa nchi hii, wanaoitakia mema Tanzania tukatae mambo yote yanayoua uwekezaji katika Taifa letu.

Tukiwa na sera na sheria ambayo inachochea uwekezaji kivitendo, kama uwekezaji utasababisha japo watanzania milioni 15 kupata ajira za uhakika, na hao milioni 15 angalao kila mmoja kwa wastani akalipa kodi ya sh milioni 4 kwa mwaka, PAYE pekee yake itaipatia Serikali 4,000,000×15,000,000 = 60,000,000,000,000 (trillion 60).

Haya ni mapato ambayo ni karibu 50% ya makusanyo ya Serikali kwa sasa. Na haya ni mapato ambayo Serikali itayapata, na huku mlipa kodi akifurahi kwa kuwa ana ajira inayompa kipato cha uhakika.
Zungu alisema ni kodi ya uzalendo.

Mtamrudisha bungeni 2025?
 
Hayo yote siyo hisani, ni wajibu wa Serikali, na yanastahili kufanywa kwa kutumia kodi halali zinazolipwa na wananchi. Na yanaweza kufanyika mengi zaidi ya hayo, huku wananchi hawanyanyasiki kwa tozo utitiri, alimradi tuwe na sheria rafiki za kodi, sera nzuri za uwekezaji, na mipango mizuri ya Serikali katika kutengeneza mazingira mazuri ya kujenga uchumi.
Lipa tozo subiria huduma
 
Wizi wa kidola dhidi ya wananchi, kwa kiasi kikubwa kinachoibwa hupelekwa kuhudumia dola.

Fikiria mwananchi anayetuma mchango wa kumtibu ndugu yake au maziko ya ndugu yake kwa njia ya simu, yeye mwenyewe ameshindwa kusafiri kwa sababu hana nauli, analipishwa tozo ili tozo ikamlipe posho na kumnunulia gari la kifahari Waziri au mkuu wa mkoa, au kugharamia mbwembwe za misafara ya viongozi wakuu wa nchi.

Kama wananchi wana mapato duni, na Serikali yao ni lazima iendane na uduni wa wenye Serikali. Lakini unapokuwa na walipa kodi walio duni kimapato, lakini watendaji wakuu wa Serikali wanataka mbwembwe sawa au hata kuzipita mbwembwe za mataifa yenye vyanzo vingi vya mapato, kwa kuwarundikia walipa kodi tozo nyingi, siyo sahihi, na siyo halali.
Lipa tozo dai huduma
 
Back
Top Bottom