DOKEZO TRA mulikeni hawa Wachina, wanahujumu uchumi wetu. Hawalipi kodi ipasavyo

DOKEZO TRA mulikeni hawa Wachina, wanahujumu uchumi wetu. Hawalipi kodi ipasavyo

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Salamu wakuu:
Hili nimekutana nalo jana, japo imekuwa sio ngeni ila hii niliipokea kwa uchungu mkubwa sana (sijui kwa vile ni Wachina).... kama mzalendo ikabidi ‘nipachimbe’ sana.

Wanauza bidhaa kwa kile wanachoita ‘bei ya kiwandani’ hivyo mteja unategemea unafuu wa bei, na kwa kuzingatia hilo nilifika hadi kiwandani kupata ofa hii (godoro).... ila masharti niliyopewa ni kwamba stakabadhi (risiti) itaandikwa NUSU ya kiasi ninayolipia mzigo.

Nilipoonesha kutoafiki kwanza ‘wahudumu’ wakanishangaa kwamba mi wa wapi sijui utaratibu huo ni wa siku zote, na kauli za vitisho kuwa wataacha kuuzia ‘watumiaji’ ili kuepusha usumbufu na ujuaji badala yake wauzie wafanyabiashara tu ambao wao wanaelewa.... nami kwa vile sikutaka kukosa kilichonipeleka ikabidi kukubaliana na masharti nishiriki kwenye hujuma.

Mamlaka zina mkono mrefu, mnajua yanayoendelea kukwepa VAT za EFD.... huu ni mfano tu ila picha ni kubwa sana TRA kuweni macho.
Kituoo. KINACHOFWATA
 
Sio unakataa kitu bila kua na hona za msingi we ungewaambia tu nyie niandikie risiti halisi maana risiti nikiipeleka ofisini naenda kurudishiwa hela yangu..ila kama hujawahi fanya biashara huwezi elewa umuhimu wa wanachokifanya hao wachina..pia hata ukinunua mzigo i.e china invoice hua haiandikwi bei halisi uliotoa
Alitaka mtelezo anunue kwa bei ya kiwandani. Actually angeenda kwa retailers angepata risiti ya full price ila kitonga kitamu [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Uko sahihi.
Nimeamua kutumia jukwaa hili kutoa dukuduku nikiamini TRA pia wako humu, uongo na unoko wangu uko wapi ndugu nimeweka sehemu ya risiti hapo.... huko police wala sikuwa na lengo la kukukamatisha endelea kuhujumu tu.
Yes but do you have proof of the real purchase price kuwa 188k x2?
 
Kuna kamchezo kameingia, risiti zinazotoka sheli baada ya kununua mafuta kuna baadhi ya watu huwa wanaziacha.... Juzi kati Kuna boda boda nilipanda akaniambia hizo huwa watu wa sheli wanaziuza kwa wafanyabiashara.....
Sijajua kama kuna ukweli katika hilo.
Si zimeandikwa Petrol au Diesel?

Kuna ukakasi hapa...

Yani umenunua nguo za 30,000 afu u apewa risiti ya EFD ya Diesel ya 30,000?
 
Wanaozinunua ni wafanya biashara ambao wanaenda kuzijumlisha kwenye expenditure zao ili matumizi yaonekane mengi na faida kidogo hence kodi inakua ndogo..
Si zimeandikwa Petrol au Diesel?

Kuna ukakasi hapa...

Yani umenunua nguo za 30,000 afu u apewa risiti ya EFD ya Diesel ya 30,000?
 
Wanaozinunua ni wafanya biashara ambao wanaenda kuzijumlisha kwenye expenditure zao ili matumizi yaonekane mengi na faida kidogo hence kodi inakua ndogo..
I thought so too kwa mbali.

Kwahiyo accounts zinazokuwa audited ni tofauti na zinazoenda TRA for tax purposes
 
Yes but do you have proof of the real purchase price kuwa 188k x2?

I don’t have to prove that, nilichoweka hapa ni kuonesha tu jinsi mchezo unavyofanyika.... suala sio langu binafsi na wala sina personal interest.

Mamlaka zikiona linafaa ni jukumu lao kwenda kuprove, naweza kusaidia jina la hiyo kampuni na hata location ya kiwanda then mtu anaenda as simulated client.... shida ni pale ninavyoshambuliwa humu kama kwamba nimeleta kitu cha ajabu wakati huko mtaani wanaita ‘ndio utaratibu wetu’.
 
Soma vizuri mkuu wangu, nilitishiwa kuwa nikileta ujuaji bora niache kununua nikanunue dukani.... nikawaza kuhusu punguzo na nimechapa mwendo hadi kiwandani nikaamua kuihujumu serikali.
....Mkuu, hapo unatumia vibaya neno 'vitisho'. Hapo walikupa option tu sio kutishiwa!
Ama ununue bidhaa uliyofuata kiwandani kwa masharti yao ama ukanunue dukani kwa bei ya dukani! Umetishiwaje hapo???
 
....Mkuu, hapo unatumia vibaya neno 'vitisho'. Hapo walikupa option tu sio kutishiwa!
Ama ununue bidhaa uliyofuata kiwandani kwa masharti yao ama ukanunue dukani kwa bei ya dukani! Umetishiwaje hapo???

Kwani bei ya dukani risiti wanaandika kiasi kamili..? Mi kwangu ilikuwa vitisho kunipa ‘option’ hizo, risiti ni haki kwa kila manunuzi wala sio kuzingatia masharti.... UKIUZA TOA RISITI.
 
Nonsense , nchi hii hamna faida ya kulipa kodi , it doesn't make any difference . Mijitu inakwapua trillions haiwajibishwi halafu inapambana kupata Mia mbili Mia mbili za wachina . ****
Ulitumbuliwa vyeti fake au nini brother!
 
Back
Top Bottom