TRA yadaiwa kuvamia Waturuki na kufunga Ofisi jioni ya Leo (Desemba 14, 2020)

TRA yadaiwa kuvamia Waturuki na kufunga Ofisi jioni ya Leo (Desemba 14, 2020)

Jioni ya leo, TRA imevamia na kufunga ofisi moja ambayo ilikuwa bado haijaanza kufanya kazi wakidai kodi. Hii ni kampuni ya waturuki inayohusika na kutengeneza tiles za majengo. Mashine zililetwa lakini kwa bahati mbaya jamaa walishindwa kuanza kufanya kazi kutokana na mtaji kutokutosha.

Waturuki walitegemea kupata mkopo kwenye moja ya mabenki ya ndani, kitu ambacho kimechelewa. Mategemeo yao ilikuwa ni kupata mkopo mwezi wa 4 lakini hadi December mkopo ulikuwa bado haujapitishwa. Kwa maana hiyo hawakuwa na jinsi ya kuanza operations zao.

Hii kampuni hipo maeneo ya Mbezi Afrikana, na kwa bahati mbaya, magari ya TRA wamevamia jioni hii na kufunga ile ofisi na kumchukua mtu anayesimamia ile mali maana wengine inaonekana wako nje ya nchi. Na kwa sababu hakuna kazi, ni mmoja wao amebakia pale kulinda mali.
TRA wa sasa wapo tayari hata kufunga A/C bank mfanyabiashara ashindwe kuzungusha pesa ashindwe hata kurejesha mkopo kwa visingizio vya kishamba haramu na vya kishetani
 
Jioni ya leo, TRA imevamia na kufunga ofisi moja ambayo ilikuwa bado haijaanza kufanya kazi wakidai kodi. Hii ni kampuni ya waturuki inayohusika na kutengeneza tiles za majengo. Mashine zililetwa lakini kwa bahati mbaya jamaa walishindwa kuanza kufanya kazi kutokana na mtaji kutokutosha.

Waturuki walitegemea kupata mkopo kwenye moja ya mabenki ya ndani, kitu ambacho kimechelewa. Mategemeo yao ilikuwa ni kupata mkopo mwezi wa 4 lakini hadi December mkopo ulikuwa bado haujapitishwa. Kwa maana hiyo hawakuwa na jinsi ya kuanza operations zao.

Hii kampuni hipo maeneo ya Mbezi Afrikana, na kwa bahati mbaya, magari ya TRA wamevamia jioni hii na kufunga ile ofisi na kumchukua mtu anayesimamia ile mali maana wengine inaonekana wako nje ya nchi. Na kwa sababu hakuna kazi, ni mmoja wao amebakia pale kulinda mali.
Jua matumizi ya lugha. Unajua maana ya neno "vamia?" Lini mamlaka halali kisheria ikiwa inatekeleza majukumu yake kisheria useme imevami?
 
Pamoja na mapungufu ya TRA Ila wachangiaji wengi hapa wanakimbilia kuleta Siasa. Wewe kama mtanzania unaweza kwenda uturuki au nchi yoyote hata Kenya bila mtaji wa kutosha ukitegemea benki zao zikukopeshe na ukaachwa tu!?

Hao sio wawekezaji ni wababaishaji tu Ila Kama ilivyo kawaida wale wanaoipinga serikali ya awamu hii tayari wataleta story za CCM na CDM. Naona kuna mpumbavu ameshaanza kutamka Lissu, sijui anaingiaje.
Kweli hujui unachoandika kwa sababu unakula bure! Hawa waturuki wameleta Equipment, zenye gharama ambayo inaweza kuwa collateral kwenye mkopo, wanaruhusiwa kuomba mkopo. Nenda kaona pale TIC, siyo kukaaa na kwa shemeji na kula bure tu. Na nchi nyingi zinafanya aina ya uwezeshaji huo.
 
Jua matumizi ya lugha. Unajua maana ya neno "vamia?" Lini mamlaka halali kisheria ikiwa inatekeleza majukumu yake kisheria useme imevami?
Acha kutetea uonevu kwa kisingizio cha mamlaka halali wakati hizo hizo mamlaka baadhi huwabambikia wafanyabiashara kodi bandia na hata kuwabambikia kesi na uonevu mwingineo kibao
 
Pamoja na mapungufu ya TRA Ila wachangiaji wengi hapa wanakimbilia kuleta Siasa. Wewe kama mtanzania unaweza kwenda uturuki au nchi yoyote hata Kenya bila mtaji wa kutosha ukitegemea benki zao zikukopeshe na ukaachwa tu!?

Hao sio wawekezaji ni wababaishaji tu Ila Kama ilivyo kawaida wale wanaoipinga serikali ya awamu hii tayari wataleta story za CCM na CDM. Naona kuna mpumbavu ameshaanza kutamka Lissu, sijui anaingiaje.
Mkopo hauna Uraia yeyote anakopa tu na TRA wanapaswa kutumia njia za kistarabu kudai kodi siyo ubabe wa kishamba kwa njia haramu za kishetani kutengeneza mazingira ya Rushwa
 
Kweli hujui unachoandika kwa sababu unakula bure! Hawa waturuki wameleta Equipment, zenye gharama ambayo inaweza kuwa collateral kwenye mkopo, wanaruhusiwa kuomba mkopo. Nenda kaona pale TIC, siyo kukaaa na kwa shemeji na kula bure tu. Na nchi nyingi zinafanya aina ya uwezeshaji huo.
TRA sasa wamewafanya hata Bank kukosa pesa nyingi tokea kwa wafanyabiashara baada ya kuanza kukosa imani na mabenk kwa kuwa TRA huenda kufunga A/C za wafanyabiashara kihuni huni tu kuwapora pesa zao kwa visingizio vya VAT na mengineyo ambayo hayaeleweki,huwa wakiwa wamedhamilia Rushwa hujitoa fahamu na kuwabambikia kodi bila kujali takwimu za wakaguzi wenzao waliopita awali kwa wafanyabiashara.
 
Hiki kitu nakifahamu lakini ni unyanyasaji tunafanyiwa wewe haujaanza biashara ukajua faida yake halafu ukadiriwe kodi means wanakadiria kodi kwenye mtaji wakati uhalisia wanatakiwa kukadiria kodi kwenye Faida, unapokadiria kodi kwenye mtaji unaandaa mazingira ya kuua mtaji.
TRA ifumuliwe isukwe upya na wale maofisa vinara wa kufunga kampuni, kufunga account za wafanyabiashara wote watajwe majina yao wapate kuchunguzwa na Takukuru juu ya mali zao
 
Nilifungua biashara nikapewa makadirio kama kawaida nikalipa awamu ya kwanza, biashara haikufanya vizuri kutokana na eneo awamu ya pili wakaendelea kunidai, biashara ikafa kwa kulipa mikodi na nadaiwa mpaka sahivi mapato mengine, nimefunga biashara, sijui kwanini TRA wasiwe USER FRIEND na walipa kodi, sahivi nataka kufungua biashara ingine mkoa mwingine naambiwa maliza kwanza deni la awali na uombe maombi ya kuhamisha TIN

Mkichekewa hamuwezi kulipa kodi. Hakuna binadamu anayependa kodi siku zote. Halafu nashangaa kwa nini wanaokwepa kodi hawabanwi? Kampuni ya mzee wangu hatulipi kodi lakini sijawahi kuona wamekuja [emoji23][emoji23]..
 
Kabla hujafanya biashara ya halali, ufanye utafiti kwanza! Usishindwe wewe, ukaanza kulaumu TRA. Umesema biashara haikufanya vizuri kwa sababu ya eneo! Je! Na hilo ni kosa la TRA?
TRA wakidhamilia Rushwa hata uwe malaika tokea kwa mungu hawakosi kisingizio lazima watakubambikia chochote ili kutimiza lengo lao, wewe usikute ni mnufaika wa uonevu wa TRA ndiyo maana unatetea uovu wao.
 
Jua matumizi ya lugha. Unajua maana ya neno "vamia?" Lini mamlaka halali kisheria ikiwa inatekeleza majukumu yake kisheria useme imevami?
Umejua maana ya neno ila ume fail kuitafsiri....wote tunajua wafanyabishara ndiyo wanailisha hii nchi unaanzaje kuanza kumfungia virago instead ya kumuita offisini na kufanya mazungumzo na kufikia muafaka, wafanyabisahara sio wahalifu wanatakiwa wachukuliwe serious na sio mzaha mzaha, kuwa nao karibu wengi wanapitia magumu unakuta mtu amechukua mkopo faida haioni bado uje umfungie ofisi huo mkopo ataulipaje na kodi atalipaje?
 
Kiongozi ukifungua biashara alafu ikafa unaandika barua kuwajulisha kuwa biashara yako umeifunga hivyo wasiendelee kukudai tena kodi, lakini biashara ikifa alafu ukakaa kimya wao wanaendela kuhesabu tu kodi yao.
TRA walianzisha utaratibu wa kudai kodi ya magari yote bila kujali kama liko barabarani au la. Kama gari lako lilipata ajali au liliharibika miaka 20 iliyopita ukaliweka juu ya mawe lakini hukuwaambia, jamaa walikuletea invoice. Mheshimiwa Rais akazuia upuuzi huo. Bahati mbaya watu huwa tunalisahau jambo hili jema alilofanya na hatumpi sifa anazostahili kwa kuchukua uamuzi ule.

Amandla...
 
Unalipaje kodi haujaanza biashara? Hua nasema TRA watakuja kutuua na kiharusi kodi idaiwe kwenye faida hapo sawa unadai vipi kodi kwenye mtaji?
Hujawahi kadiriwa kodi na huku hujaanza biashara?.Tatizo linaanzia hapo mifumo yetu inawafanya TRA kutazama kodi kwanza kabla ya kuijali na kuikuza biashara yeneyewe ili iweze kutoa kodi.

Kwetu mtu kuwa na TIN number tu ya baishara tayari unatazamwa kama mdaiwa wa kodi kumbe kuna nchi mtoto akishazaliwa anapewa TIN akifikisha 18 ndipo wanaanza kuangilia kama ana kipato.

Mazingira ya kuanza biashara bado hayako favaourable sana hasa kwa weneye mitaji midogo inayowafanya kuchukua muda mrefu kuanza uzalishaji au kupata return ya uwekezaji
 
Jioni ya leo, TRA imevamia na kufunga ofisi moja ambayo ilikuwa bado haijaanza kufanya kazi wakidai kodi. Hii ni kampuni ya waturuki inayohusika na kutengeneza tiles za majengo. Mashine zililetwa lakini kwa bahati mbaya jamaa walishindwa kuanza kufanya kazi kutokana na mtaji kutokutosha.

Waturuki walitegemea kupata mkopo kwenye moja ya mabenki ya ndani, kitu ambacho kimechelewa. Mategemeo yao ilikuwa ni kupata mkopo mwezi wa 4 lakini hadi December mkopo ulikuwa bado haujapitishwa. Kwa maana hiyo hawakuwa na jinsi ya kuanza operations zao.

Hii kampuni hipo maeneo ya Mbezi Afrikana, na kwa bahati mbaya, magari ya TRA wamevamia jioni hii na kufunga ile ofisi na kumchukua mtu anayesimamia ile mali maana wengine inaonekana wako nje ya nchi. Na kwa sababu hakuna kazi, ni mmoja wao amebakia pale kulinda mali.

Ni sawa kabisa, Yani uje huku uchukue mkopo humu? Fungeni tu!
 
Na wasiporudi hao Waturuki itakuwaje?

READ! Taarifa inasema Waturuki wamekosa mkopo wa benki za ndani

Maana yake hawakuja na mtaji!

Ndio haya Marehemu Mengi alikuwa anayasema wakati ana bifu na Wahindi, walikuwa wanamwambia tumekuja na briefcase la makaratasi ya business plan za kutajirikia hapa hapa kwenu! Yani sisi ni vichwa panzi.

Magufuli fukuza hao Waturuki!

Thank God Almighty tumepata kichaa mzalendo Ikulu hapapatikii wazungu, hafagilii wageni!

ALHAMDULLILAH ALA KULLI HAAAL HADHA MIN FADLI RABBI
Wewe wa wapi hakuna mwekezaj anakuja na mtaji, wanakuja na kuchukua mikopo kwenye bank ndo biashara zinazofanywa, tofauti na hapo utaambiwa unatakatisha fedha
 
Back
Top Bottom