TRA yadaiwa kuvamia Waturuki na kufunga Ofisi jioni ya Leo (Desemba 14, 2020)

TRA yadaiwa kuvamia Waturuki na kufunga Ofisi jioni ya Leo (Desemba 14, 2020)

Mkuu umenena kitu cha maana sana. Kinachotokea ni elimu duni itolewayo na TRA na hao TRA kushindwa kuwa na common sense. Mtu kama hafahamu aelimishwe then afuate utaratibu. In fact TRA inahitaji mtu kama Dkt Magufuli, yaani mbunifu na mwenye maono.
Sodata yani mambo haya hayahitaji nguvu wala ubabe, TRA ina wafanyakazi wakutosha mambo ya kodi sio kila mfanyabiashara kasomea mambo ya kodi huko shule, wanachotakiwa ni kutupa elimu ili watu wajifunze na kujua anawajibika mpaka wapi kwenye maswala ya ulipaji kodi, wengi hawana ufahamu huo yani ni kuchukulia mambo as business as usual kwamba kila mtu anajua
 
Unalipaje kodi haujaanza biashara? Hua nasema TRA watakuja kutuua na kiharusi kodi idaiwe kwenye faida hapo sawa unadai vipi kodi kwenye mtaji?
Et wanakukadiria kwanza. Unatoa kodi ya mwaka mzima, upumbavu. Nishawai kuwauliza kwa nini mnafanya hivi? Majibu waliyotoa mpaka leo sjaelewa.
 
Kiongozi ukifungua biashara alafu ikafa unaandika barua kuwajulisha kuwa biashara yako umeifunga hivyo wasiendelee kukudai tena kodi, lakini biashara ikifa alafu ukakaa kimya wao wanaendela kuhesabu tu kodi yao.
Kwahyo nasie tudai hela tuliyowapa..manaa kama mtu hujapata faida maana muamala unakua negative .

Mauzo-matumiz=faida...sasa ...washachkua percent ya faida yangu kabla sjaanza kaz...wamejuaje ntapata faida...yaan kiufup hii scenario ni ya kipumbavu
 
duh kiingoz naona umeikubal move. ila nauliza je kwa sisi nao tukitaka kufanzia beshara uturuki na wao je na mtaji ukawa huna unaruhusiwa kuweka ofisi zako wakat unahangaikia mkopo bila kukatwa kodi?
Hao waturuki hawana kosa yawezekana maofisa wa TRA hayo mambo ya kodi na biashara waliyoyasomea hawakuelewa ila wamekariri tu

Kama waturuki walileta machine zao kwa njia za halali wakatafuta sehemu wakazihifadhi huku wakiwa katika mchakato wa kutafuta mtaji ili waanze production hilo sio kosa katika nchi zote duniani ukiondoa Tanzania

TRA ilitakiwa wadai kodi baada ya kuanza production kama hakuna production ina maana hakuna biashara yoyote inayofanyika sasa hiyo kodi itatoka wapi wakati hakuna mapato yoyote yanaingia

Na hao waturuki kutafuta mkopo wa mtaji wakiwa hapa Tanzania sio kosa na ndio maana hata mabenki yaliopo hapa Tanzania mengine ni ya kigeni
 
Jioni ya leo, TRA imevamia na kufunga ofisi moja ambayo ilikuwa bado haijaanza kufanya kazi wakidai kodi. Hii ni kampuni ya Waturuki inayohusika na kutengeneza tiles za majengo. Mashine zililetwa lakini kwa bahati mbaya jamaa walishindwa kuanza kufanya kazi kutokana na mtaji kutokutosha.

Waturuki walitegemea kupata mkopo kwenye moja ya mabenki ya ndani, kitu ambacho kimechelewa. Mategemeo yao ilikuwa ni kupata mkopo mwezi wa 4 lakini hadi Desemba mkopo ulikuwa bado haujapitishwa. Kwa maana hiyo hawakuwa na jinsi ya kuanza operations zao.

Hii kampuni hipo maeneo ya Mbezi Afrikana, na kwa bahati mbaya, magari ya TRA wamevamia jioni hii na kufunga ile ofisi na kumchukua mtu anayesimamia ile mali maana wengine inaonekana wako nje ya nchi. Na kwa sababu hakuna kazi, ni mmoja wao amebakia pale kulinda mali.
Unachosema ni kuwa muwekezaji toka Uturuki, kaja toka huko akitegemea mtaji wa mkopo toka Local Bank? Tuwe serious!
 
Basi kabla hawajaja wangetumia hizo equipment zao zenye thamani ya collateral kuomba mkopo KWAO!

Hawakopesheki kwao wanadhani watakuja kupeta kwenye mabenki ya wendawazimu wa Afrika.

Wamekutana na ngoma ngumu Ikulu...

Julius Nyerere, aliyekuwa hatetemeki mbele ya Mzungu, Mwarabu na Mkenya, amefufuka katika wafu.
Labda akili yako haifanyi kazi. Investor anasoma TIC incentives ndiyo anakuja kuwekeza Tanzania. Unafikiri angejua hayo yote angekuja kuwekeza huko ujimani? Moja ya incentive ya kuwekeza ni kukopeswa (kuwezeshwa) kama una equipment. Watu kama nyie huwa mnajielewa kweli mnaishi dunia gani?

Viongozi wanaotuongoza kweli ni watu wasio na akili timamu, kwa namna hii wanatesa watu wa nchi zao wenyewe kwa kukosesha ajira na huduma muhimu, investor wengi wangekuja lakini tatizo ni kama hawa viongozi vilaza
 
Jioni ya leo, TRA imevamia na kufunga ofisi moja ambayo ilikuwa bado haijaanza kufanya kazi wakidai kodi. Hii ni kampuni ya Waturuki inayohusika na kutengeneza tiles za majengo. Mashine zililetwa lakini kwa bahati mbaya jamaa walishindwa kuanza kufanya kazi kutokana na mtaji kutokutosha.

Waturuki walitegemea kupata mkopo kwenye moja ya mabenki ya ndani, kitu ambacho kimechelewa. Mategemeo yao ilikuwa ni kupata mkopo mwezi wa 4 lakini hadi Desemba mkopo ulikuwa bado haujapitishwa. Kwa maana hiyo hawakuwa na jinsi ya kuanza operations zao.

Hii kampuni hipo maeneo ya Mbezi Afrikana, na kwa bahati mbaya, magari ya TRA wamevamia jioni hii na kufunga ile ofisi na kumchukua mtu anayesimamia ile mali maana wengine inaonekana wako nje ya nchi. Na kwa sababu hakuna kazi, ni mmoja wao amebakia pale kulinda mali.
Kwa hiyo tufanyeje kama hawajalipa kodi yetu?
 
Swala la kukopesha ni swala mahususi linalohusu benki wana haki ya kumkopesha yeyote hata awe mgeni provided sera yao inasema hivyo.

Kama mwekezaji ana mtaji kwa maana ya Capital Goods na anataka kuwekeza ili uwekezaji wake uongeze mtaji wa benki basi kuna mabenki yanatoa mikopo kwa mazingira hayo.

Haieleweki TRA walitumia sheria ipi kukamata mali za hao waturuki na huyo mtu wao ilhali hawajaanza hata uzalishaji.

All in all, mazingira ya uwekezaji katika nchi hii kwa sasa ni magumu mno kwa wawekezaji wa ndani na nje vile vile na ndio maana ukuaji wa uchumi tayari umeshaanza kushuka japo wapishi wa takwimu hawataki watu wajue.
 
Unalipaje kodi haujaanza biashara? Hua nasema TRA watakuja kutuua na kiharusi kodi idaiwe kwenye faida hapo sawa unadai vipi kodi kwenye mtaji?
TRA ya awamu hii ni ya ajabu sana, nadhani tangu kuumbwa kwa dunia hii. Wanatumai nguvu nyingi mno kukusanya mapato, badala ya kutumia akili (sheria na miongozo iliyopo).
 
Et wanakukadiria kwanza. Unatoa kodi ya mwaka mzima, upumbavu. Nishawai kuwauliza kwa nini mnafanya hivi? Majibu waliyotoa mpaka leo sjaelewa.
TRA kuna shida kubwa wao wenyewe hawajielewi ndiyo maana hata wafanyabiashara hawawaelewi
 
TRA ya awamu hii ni ya ajabu sana, nadhani tangu kuumbwa kwa dunia hii. Wanatumai nguvu nyingi mno kukusanya mapato, badala ya kutumia akili (sheria na miongozo iliyopo).
Njaa na kupenda Hongo ndiyo Tatizo lao kubwa
 
Unachosema ni kuwa muwekezaji toka Uturuki, kaja toka huko akitegemea mtaji wa mkopo toka Local Bank? Tuwe serious!
Kutoka Uturuki si kigezo cha TRA kufanya mambo ya hovyo lazima tukemee vitendo vya hovyo pasipo kuangalia chochote
 
Jioni ya leo, TRA imevamia na kufunga ofisi moja ambayo ilikuwa bado haijaanza kufanya kazi wakidai kodi. Hii ni kampuni ya Waturuki inayohusika na kutengeneza tiles za majengo. Mashine zililetwa lakini kwa bahati mbaya jamaa walishindwa kuanza kufanya kazi kutokana na mtaji kutokutosha.

Waturuki walitegemea kupata mkopo kwenye moja ya mabenki ya ndani, kitu ambacho kimechelewa. Mategemeo yao ilikuwa ni kupata mkopo mwezi wa 4 lakini hadi Desemba mkopo ulikuwa bado haujapitishwa. Kwa maana hiyo hawakuwa na jinsi ya kuanza operations zao.

Hii kampuni ipo maeneo ya Mbezi Afrikana, na kwa bahati mbaya, magari ya TRA wamevamia jioni hii na kufunga ile ofisi na kumchukua mtu anayesimamia ile mali maana wengine inaonekana wako nje ya nchi. Na kwa sababu hakuna kazi, ni mmoja wao amebakia pale kulinda mali.
Hivi kweli wawekezaji gani wanakuja kukopa ndani
 
Nilifungua biashara nikapewa makadirio kama kawaida nikalipa awamu ya kwanza, biashara haikufanya vizuri kutokana na eneo awamu ya pili wakaendelea kunidai, biashara ikafa kwa kulipa mikodi na nadaiwa mpaka sahivi mapato mengine, nimefunga biashara, sijui kwanini TRA wasiwe USER FRIEND na walipa kodi, sahivi nataka kufungua biashara ingine mkoa mwingine naambiwa maliza kwanza deni la awali na uombe maombi ya kuhamisha TIN
😃😃😃 TRA waangalie maana hata nyuzi zao kibao humu.. kuna mahala hapako sawa, huenda wakawa wana muhujumu Rais
 
Unachosema ni kuwa muwekezaji toka Uturuki, kaja toka huko akitegemea mtaji wa mkopo toka Local Bank? Tuwe serious!
Mtu kama wewe ukiajiriwa TRA ndio unaenda kufunga ofisi za wawekezaji kwa sababu ya umbumbu wako

Nani aliyejuambia muwekezaji toka nje ya nchi haruhusiwi kukopa katika local bank

Lakini pia hapa Tanzania zipo bank za nje zimefungua matawi hapa Tanzania

Bank Huwa zinaangalia faida hivyo zinamkopesha mtu yoyote endapo wakiona watapata faida
 
Kwa kweli mifumo ya ulipaji kodi ni ya kipuuzi, halafu kutwa tunaambiwa na kushauriwa jiajirini kujenga uchumi wa taifa, ajira itabaki kuwa tamu aisehh kuliko unajiajiri na kuacha ajira ukitegemea ajira itafanya vizuri unajikuta unakua masikini zaidi, serikali waliangalie hili.
Leo nimeamka asubuhi nime tengeneza CV . Nasubiri mchongo tu.. 😀😀😀 kujiajiri inahitaji moyo sana. Badala ya kupata suport kwao..wana kukalia kooni..
 
Back
Top Bottom