Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kama taifa hii ni kasoro kubwa, tumerithi mfumo wa kodi kandamizi kutoka mfumo wa kijamaa, mpaka leo kumiliki gari inatafsiriwa (Sheria ya kodi)kuwa ni anasa.Kodi karibu na bei uliyonunulia, yaani upumbavu wetu umetufanya tuwe watumwa kwa misheria ya kijinga tuliyojiwekea wenyewe, kila kona ni hivyo hivyo tuu na mitozo isiyo na akili ndio maana hakuna siku tutaendelea
Unaagizaje G Guard Brabus wakati una pesa ya kulia katanga? Kama gari limemshinda kutoa bandarini aseme tumrudishie gharama zake zote, pamoja na riba na hela ya usumbufu na ya kifuta machozi wanaume tuchukue hiyo ndinga, alisikika kaka Mshana Jr akihojiwa na vyombo vya habari vya njeView attachment 2353083
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imesema mfanyabishara maarufu wa Zanzibar, Toufiq Salum Turky, bado hajalipa Sh. milioni 308.5 za kodi kutokana na kuingiza gari la kifahari aina ya Benzi, Januari, mwaka huu.
Naibu Kamishina wa TRA Zanzibar, Juma Bakary Hassan, aliwaambia waandishi wa habari jana ofisini kwake, Kinazini, Unguja kuwa gari hilo ilingizwa na mfanyabishara huyo kupitia kampuni yake ya Mifuko Turky ya Zanzibar.
Juma alisema, kiwango hicho cha kodi kinatakiwa kulipwa baada ya maombi ya masamaha wa kodi kukataliwa mara mbili na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar, Dk. Saada Mkuya Salum.
View attachment 2353084
“Baada ya maombi ya msamaha wa kodi kukataliwa mara mbili na kutakiwa alipe, waliomba kufanyike tathmini upya baada ya kutia shaka kiwango walichokuwa wanatakiwa kulipa kwamba ni kikubwa lakini hesabu ilikuja ile ile ya mwanzo kulingana na thamani ya gari,” alisema Juma.
Alisema, baada ya kutakiwa alipe, aliomba wapewe muda wa kulipa kidogo kidogo kwa madai hali ya kifedha si nzuri na kulazimika kupewa miezi mitatu kuanzia Mei hadi Agosti, mwaka huu.
“Mpaka muda unamalizika Agosti, amelipa Sh. milioni 138 na bado wanadaiwa Sh. milioni 170 kati ya Sh. milioni 308 .5 alizopaswa kulipa. Tunajiandaa kuhakikisha fedha hizo zinalipwa kupitia bodi ya dhamana aliyokuwa ameweka kwa kutumia taasisi moja ya fedha,” alisema.
Barua mbili za maombi ya msamaha wa kodi zilizotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa wa Mamlaka ya Uwekezaji Zanzibar (ZIPA), Sheriff Ali Sharif, ziliweka wazi kwamba, mdaiwa anapaswa kunufaika na msamaha wa kodi kupitia Kampuni ya Mifuko Turky kama mwekezaji.
Hata hivyo, maombi hayo yalikataliwa na Waziri Mkuya kwa sababu muda wa kunufaika kisheria ulikuwa umemalizika baada ya ujenzi wa kiwanda cha mifuko kuwa umekamilika na uzalishaji kuanza muda mrefu.
“Unaweza kunufaika na msamaha wa kodi kama mwekezaji wakati wa ujenzi wa mradi na si baada ya ujenzi kukamilika na uzalishaji unaendelea kufanyika,” alisema ofisa mmoja mwandamizi wa ZIPA.
Wakati hayo yakiendelea, Bodi ya Mapato Zanzibar ilishasajili gari hilo la kifahari na kutoa namba Z-1 kwa malipo ya Sh. milioni 15, na kuonekana likitembea barabarani kabla ya kukamilisha malipo ya kodi.
“Sisi tumesajili na kutoa namba kwa masharti gari lisitembee mpaka wakamilishe taratibu za kodi tukazo kutoa kibali cha umiliki wa gari,” alisema Meneja Uhusiano na Huduma kwa Walipakodi ZRB, Makame Mohammed Khamis.
Gari hilo lenye thamani ya Dola za Marekani 214,668.71, liliingizwa kupitia bandari ya Malindi na kampuni ya uwakala wa mizigo ya Kimataifa HT Motors Group LTD (UK) kwa kushirikiana na kampuni ya uwakala wa mizigo ya ZARA Freight Forwaders ya Malindi, Zanzibar.
Nenda kwenye calculator, tena hapo wamempunguzia. Mara nyingi thamani ya kununulia gari inakuwa sawa na thamani ya kodi, hao ndio TRAKwamba hiyo USD 214,660 ambayo ni kama tsh 500,607,430 ndio iwe na kodi tsh 308,000,000?
Nenda kwenye calculator, tena hapo wamempunguzia. Mara nyingi thamani ya kununulia gari inakuwa sawa na thamani ya kodi, hao ndio TRA
Kama taifa hii ni kasoro kubwa,tumerithi mfumo wa kodi kandamizi kutoka mfumo wa kijamaa,mpaka leo kumiliki gari inatafsiriwa (Sheria ya kodi)kuwa ni anasa
Hahaha[emoji23] Buji umeuwaaaUnaagizaje G Guard Brabus wakati una pesa ya kulia katanga? Kama gari limemshinda kutoa bandarini aseme tumrudishie gharama zake zote, pamoja na riba na hela ya usumbufu na ya kifuta machozi wanaume tuchukue hiyo ndinga, alisikika kaka Mshana Jr akihojiwa na vyombo vya habari vya nje
Na Passo, unakuta baba zima na likitambi lake limejikunja kwenye PassoNdio mana bongo zimekaa starlet tu
Plivate jet yao ndo iliyompeleke Tundu Lisu Nairobi alipopigwa Risasi na WasiojulikanaHuyo ni mbunge,mtoto wa marehemu Turky aka Mr White alirithi ubunge wa baba yake,baada ya baba yake kufa ,yeye na wabunge wenzake wanatakiwa walitazame hilo suala la kodi.Kodi haitakiwi iwe sawa au ikaribiane na thamani ya bidhaa.Wakati wa kutunga sheria wao wanapiga makofi tu na kupongeza matokeo yake ndiyo hayo.
Unaweza kukuta kodi ya ku import Plivate jet ni ndogo kuliko kodi ya ku import hiyo BrabusPlivate jet yao ndo iliyompeleke Tundu Lisu Nairobi alipopigwa Risasi na Wasiojulikana
Inawezekana lakini Bado TRA kwenye kodi ya Gari hawapo sawa! Burundi japo awana uchumi kama sisi Kodi za Gari ni chini mno- kama vipi akalisajili Burundi kisha hapa analipia kibali cha mwaka mwaka ainjoyUnaweza kukuta kodi ya ku import Plivate jet ni ndogo kuliko kodi ya ku import hiyo Brabus
Halafu mwaka ukiisha anarudi Burundi tena halafu analiingiza tena nchini na kuliombea kibaliInawezekana lakini Bado TRA kwenye kodi ya Gari awapo sawa! Burundi japo awana uchumi kama sisi Kodi za Gari ni chini mno- kama vipi akalisajiri Burundi kisha hapa analipia kibali cha mwaka mwaka ainjoy
this is weirdHebu ona hapa chiniView attachment 2353107hiyo gari inauzwa usd 14,000 sawa na 32,000,000 lkn ushuru ni 41,00,00View attachment 2353108
Hili nalo mwanangu Kamishina Mkuu Kidata muende mkalitizame wewe na timu yako,mkandamizeni mpaka gari alisuse,na akisusa lileteni Chamwino nami nitembelee Benzi,nimechoka kutembelea mijigari ya Toyota".