TRA yaendelea kumkaba koo Toufiq Salum Turky kodi ya gari milioni 308.5

TRA yaendelea kumkaba koo Toufiq Salum Turky kodi ya gari milioni 308.5

Mimi na baiskeli yangu nawaangalia tu usoni, Mnavyolalamika. Nia ya serikali ni nzuri kuhakikisha sisi wenye baiskeli tunaheshimika. Fikiria kila mtu awe na gari, tutajificha wapi siye? Nani atakubali kuolewa na kuoa mtu asiye na gari.
 
Kama umeweza nunua gari ya dola laki mbil nje why usilipe kodi kwani hujuwi starwhe gharama mjomba..
Ukumbuke serikali inakusanya kodi ili iendeshe nchi, unaposhindwa kukusanya sababu umeweka ushuru mkubwa unajiua mwenyewe. Fikiri kama kodi ingekuwa shilingi milioni 3 kwa gari za cc1500, si watu wengi sana wangepambana kumiliki magari, serikali ingekusanya kodi nyingi pasipo kuchukiwa na wananchi wake.
 
Huyo ni mbunge,mtoto wa marehemu Turky aka Mr White alirithi ubunge wa baba yake,baada ya baba yake kufa ,yeye na wabunge wenzake wanatakiwa walitazame hilo suala la kodi.Kodi haitakiwi iwe sawa au ikaribiane na thamani ya bidhaa.Wakati wa kutunga sheria wao wanapiga makofi tu na kupongeza matokeo yake ndiyo hayo.
Uko sahihi. Wabunge wengi wako tu bungeni kuuza sura na kusubiri posho, hawajui hata hizo sheria wanazozipitisha. Kumbuka wabunge hawalazimiki kuwa na elimu kubwa wanatakiwa tu wajue kusoma na kuandika. Sheria nyingi zinaandikwa kitaalamu na kwa kiengereza, ni ngumu kwa wabunge wetu kuzielewa, na hata wakizielewa Chama kinawabana na kwa kulinda ugali inabidi wapitishe. Lakini hili liwe funzo what goes around comes around
 
Kama taifa hii ni kasoro kubwa,tumerithi mfumo wa kodi kandamizi kutoka mfumo wa kijamaa,mpaka leo kumiliki gari inatafsiriwa (Sheria ya kodi)kuwa ni anasa.

Gari ni vyombo muhimu katika kuharakisha shughuli za kiuchumi.

Wizara ya fedha ione UMUHIMU wa kutafsiri gari kuwa sio anasa Bali ni muhimu hata mwananchi wa kawaida kumiliki.

Tujifunze kwenye boda boda, zimesaidia ajira,mafuta kununuliwa na hivyo kuchangia kodi kwa wingi.

Makusanyo ya Kodi kutokana na uagizaji magari haijawahi kuzidi makusanyo ya kodi ya bia na sigara bado TRA hamjifunzi kuwa tupunguze kodi magari yaagizwe kwa wingi ili tupate kodi mara 2(kodi kwenye uagizaji na kodi ya mafuta wakati matumizi ya gari).

Tulivyokubali kuruhusu boda boda uchumi wa vijana na ajira uliongezeka.Umeme na maji tunapeleka vijijini kinachofuata ni kuendelea kumletea mwananchi unafuu wa kumiliki vyombo vya moto(punguzo la kodi iwe kwa magari chini ya cc 3000).

Wizara ya fedha rekebisheni viwango vya tozo(import duty),ili tufikie uchumi wa kati mapema zaidi.

Fanyeni tathimini idadi ya wamiliki wa magari ikiongezeka na matumizi ya mafuta ya kiongezeka,pato litaongezeka!
1.Angalau kwenye kila kijiji chenye kaya 200 ,kaya 30 zimiliki gari, kwanini hatuangalii namna ya kuleta unafuu wa maisha hadi kijijini lengo ni kupata mchango wa kiuchumi utokee kijijini kwa kumiliki na kutumia vyombo vya moto.
2.Hizi nchi za kiafrika zinazotuzidi kiuchumi,wao kodi ya uagizaji magari ipo vipi?
3.Kwa nini kodi na tozo zilingane na gharama ya kununua gari?hii ni aibu kwa zama hizi za sasa,hii ifanyiwe kazi tuondoe aibu hii,tunaonekana kama hatuna ubunifu na mbinu sahihi za kutoza kodi.
Hiyo ni kodi ya gari moja au magali 100 duuh😂
 
60% tunapeleka mazamwamwa wao ni kupiga makofi Tu wanasubiri kutoka wakanywe kahawa
 
Hivi ndio inafaa kipato kikubwa na kodi kubwa na hivi ndio ilivyo katika nchi zote zilizo endelea!
Sio kuwauwa wana nchi wa kipato cha chini kwa uchwara tozo kibao walahi [emoji3062]
Boss hiyo kodi haichagui maskini au tajiri, wewe ingiza IST utapigwa hiyo hiyo 100% na zaidi, na kwa taarifa yako maskini ndio wanalipa kodi kuliko matajiri, usidanganyike na rate za kwenye makaratasi
 
Back
Top Bottom