TRA yafungulia akaunti zote za Wafanyabiashara zilizokuwa zimefungwa kutokana na madeni ya kodi

TRA yafungulia akaunti zote za Wafanyabiashara zilizokuwa zimefungwa kutokana na madeni ya kodi

Wewe ni mtu deluded mwenye cognitive bias ya hali ya juu.
Hilo wala halina ubushi, hila sio muda mrefu utaelewa kukopesheka bila idhini ya IMF na WD sio jambo rahisi.

Wakopaji walikuwa wanamuamini Magufuli anauwezo wa kulipa, tuombe na mama apewe imani ile ile waliyokuwa nayo kwa hayati.
 
Ni vizuri maana wengine mkishika hapo ina maana kila kitu kinasimama ajira za watu hata kile kidogo cha kodi nacho kinapotea kabisa maana kama umefreeze acc...biashara itaendeleaje kwa kulipa kidogo kidogo wanaepusha mengi....hongera
Yule Bwana alituharibia Sana nchi.check mfano ishu ya mishahara ya watumishi sio rahisi kuibalance ije ikae sawa.
 
Truth be told, mazoea mabaya ya muda mrefu yamewafanya wafanyabiashara wengi wawe na kasumba ya kutoridhia kutii sheria bila shurti --- lugha ya kutoa kodi kwa hiari hawaielewi kamwe.

Wamejifunza njia ya mikato, ujanjaujanja, wiziwizi, rushwarushwa, dilidili and the like. Sasa wakiletwa kwenye mstari, by definition, wao wanadhani wanaonewa. What!???

TRA walikuwa wanafunga account za wafanya biashara kisha dhalimu anazunguka na fedha za kupora kugawa huko mitaani, wakati yeye alikuwa halipi kodi. Eti sheria inawaruhusu TRA kushikilia account za watu baada ya njia zote kushindikana, je sasa hivi baada ya dhalimu kuelekea kuzimu hizo njia ndio zimerejea?
 
Umeongea pumba tu uyo jk aliekua akilipa mishahara mwezi unaofata tarehe 5 kwenda huko ndio WA kumuongelea hapa? nchi ilichoka kila sehemu umeme kukatika hovyo,panya road Leo mnajitia kusahau hii nchi Ina viumbe WA ajabu Sana,Bila Kodi Hakuna maendeleo lipa Kodi ili usiingie matatizoni

Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
Wewe hukuwa mfanyakazi wa Serikali. Hakuna mfanyakazi wa Serikali alikuwa anapata mshahara tarehe 5/ mwezi unaofuata
 
OK nimekupata; tatizo bado unachanganya utaratibu wa jinsi ivyo vitu vinavyodaiwa.

Sijachanganya, nisamehe nitakupa maelezo marefu kwann TRA walionekana wanyang'anyi 2015-2020.

Ukishajikadiria una namna tatu za kulipa. Ulipe yote, ulipe mara mbili au ulipe mara nne. Baada ya hapo utapeleka hesabu zilizokaguliwa na CPA(T) PP kuonyesha kuwa ulichojikadiria kilikuwa sahihi hujaiibia serikali na ww hujaibiwa. TRA watafanya kitu kinaitwa examination of books of accounts. Kama kuna kodi hukuilipa watakuambia ilipe.

Tatizo limekuja TRA wanajisahau wanakaa muda mrefu hawafanyi examination, halafu wakifanya wanakucharge penalty na interest ya muda mpaka kufikia wakati wa ukaguzi ulipofanyika. Hapo sasa ndio dhana ya unyang'Anyi inapokuja.

Mfano, assume umepeleka hesabu za 2014 june 2015. TRA wakakaa nazo mpaka april 2021, wakagundua ulilipa kodi pungufu kwa 30m.
Kutegemeana na aina ya kodi utachajiwa adhabu ya miezi approx 60 na interest. Kama adhabu ni 225,000 then itakuwa:
30m+ (225,0000 ×60) plus interest kila mwezi. Hapo ni mwaka 2014, watafanya hivyo hivyo 2015, 2016, 2017,2018,2019. Kila mwaka na adhabu zake na penalt zake. Ndo unasikia mtu anadaiwa M800 na TRA.

Sasa unajiuliza kwann ukae na hesabu miaka mingi uzilimbikize na hesabu nyingine ili umwadhibu mtu na kumcharge interest? Halafu kwann kama examination yako imeonyesha nimelipa pungufu kwann hukunieleza mwaka husika ili kama umefanya makosa ya examination nyaraka ziletwe, kwann unasubiri pale ambapo kuna uwezekano sitakuwa na nyaraka kukuprove wrong?

Ukumbuke mwaka wa biashara ukimpa mfanyabiashara tax clearence certificate ni wafanyabiashara wachache sana ni watunzaji wa nyaraka kama marisiti, bank slips n.k.

Baada ya yote hayo Wanafunga acc, wanachukua hela bila kujali hiyo hela ni mkopo au ya mauzo ya manunuzi ya mteja. Hapo ndo neno unyang'anyi linapokuja.
 
Pia kuna fedha na vifaa vilivyoporwa kwenye bureau de change virudishwe kwa wenyewe. Mwendazake alikuwa mtu mwovu sana. Kinachonishangaza kuna watu watu walikuwa wanampenda! Mungu mwema sana!
Ukiwa na mawazo ya chapchap huwezi kuelewa kwanini mwendazake alipendwa kwa ubaya na uzuri.Utamaduni wa Mtanzania ni kukwepa deni ndiyo anajiona mjanja.
 
Acha upumbavu wewe unaongea usichokijua. Yaani JK aliyekua anakusanya bil.750 kwa mwezi ndiye bora kulikonhuyu aliekua anakusanya karibu tril. 2 kwa mwezi. Hebu tukumbushe ni mradi gani wa maana wa kimkakati uliofanywa na JK.
Wewe ndiye mpumbavu kwa kukurupuka kwa kudhani kuwa Mwendazake alikuwa anakusanya sana kuliko JK, nitakupa sababu ;
1. Takwimu za Mwendazake zilikuwa za kuchakachua. Alikuwa mwongo kwa kila kitu. Anasema tunajenga kwa hela zetu za ndani halafu kesho unakuta KM Fedha na Waziri wa Fedha wanakopa AfDB au Stan chart

2. Kama alikuwa anakusanya sana kwa nini alishindwa kuongea mishahara ya wafanya kazi kwa miaka 5

3. Wakati wa JK Halmashauri zilikuwa zinakusanya mapato zenyewe hivyo basi zikikuwa hazihesabiwi kwenye kapu kubwa la Hazina. Wakati wa Mwendazake fedha zinazotangazwa na Hazina zinahusisha na za Halmashauri

4. Population wakati wa JK mpaka 2015 ilikuwa 55 Million, wakati wa Mwendazake ilipanda hadi 60 Milion mwaka 2020
 
Mama anifumua vizuri sana legacy.
Samia futa na masheria ya hovyo aliojitungia yule Muovu.
 
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA), imezifungulia akaunti zote za wafanyabiashara ilizokuwa zimeshikiliwa kutokana na madeni ya kodi

Hayo yamesemwa leo mjini Morogoro na Mkurugenzi wa Elimu kwa Umma wa (TRA), Richard Kayombo, wakati akitoa mada kwenye Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Jukwaa la Wahariri (TEF).

Kayombo amesema hivi sasa mamlaka hiyo inaingia mikataba ya makubaliano na wafanyabiashara hao wenye madeni ili walipe kwa utaratibu maalum.

Amesema sheria inairuhusuTRA kushikilia akaunti ya mtu yeyote ambaye anadeni la kodi kama njia ya kupata fedha ambazo serikali inadai.

Lakini Kayombo amesema uamuzi wa kushikilia akaunti ya mfanyabiashara huwa ya mwisho kabisa baada ya njia zingine zote kama majadiliano kushindikana.

"Sikawaida kushikilia akaunti ya mfanyabiashara na uamuzi huu mara nyingi unakuwaga wa mwisho kabisa baada ya jitihada zingine kushindikana ikiwemo majadiliano na mhusika," amesema Kayombo

"Tumeamua kuziachia hizi akaunti ili sasa tuwe tunakaa mezani na kujadiliana na wafanyabiashara wenye madeni namna bora ya kulipa taratibu taratibu na tunaachana na ule wa kushikilia akaunti zao," amesema Kayombo

Chanzo: NIPASHE
IMG-20210522-WA0058.jpg
 
Wewe unashangilia upumbavu. Kama umesoma vizuri taarifa ya aTRA ni kwamba hatua ya kushikilia akaunti ya mtu ni ya mwisho kabisa, baada juhudi nyingine kushindikana.

Yaani mtu akwepe kodi kwa makusudi halafu muanze kubembelezana. Kukwepa kodi ni uhalifu kama uhalifu mwingine. Nendeni kwenye nchi za watu muone kama kuna mtu anabembelezana na wakwepa kodi. Ninachojua kwa uhakika hizo kodi hazitalipwa na TRA hawatakua na meno tena ya kuwafanya wafanyabiashara walipe kodi. Kwa ufupi IMEISHA HIYO
Mke wangu acha kupaniki,hujawahi kufanya biashara ndio maana huwezi kuelewa TRA ilichokua inakifanya.

We tulia hapo nyumbani wanaume tutakuletea mahitaji ya nyumbani upike,ila haya mambo ya Tra achana nayo maana huyajui.
 
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA), imezifungulia akaunti zote za wafanyabiashara ilizokuwa zimeshikiliwa kutokana na madeni ya kodi

Hayo yamesemwa leo mjini Morogoro na Mkurugenzi wa Elimu kwa Umma wa (TRA), Richard Kayombo, wakati akitoa mada kwenye Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Jukwaa la Wahariri (TEF).

Kayombo amesema hivi sasa mamlaka hiyo inaingia mikataba ya makubaliano na wafanyabiashara hao wenye madeni ili walipe kwa utaratibu maalum.

Amesema sheria inairuhusuTRA kushikilia akaunti ya mtu yeyote ambaye anadeni la kodi kama njia ya kupata fedha ambazo serikali inadai.

Lakini Kayombo amesema uamuzi wa kushikilia akaunti ya mfanyabiashara huwa ya mwisho kabisa baada ya njia zingine zote kama majadiliano kushindikana.

"Sikawaida kushikilia akaunti ya mfanyabiashara na uamuzi huu mara nyingi unakuwaga wa mwisho kabisa baada ya jitihada zingine kushindikana ikiwemo majadiliano na mhusika," amesema Kayombo

"Tumeamua kuziachia hizi akaunti ili sasa tuwe tunakaa mezani na kujadiliana na wafanyabiashara wenye madeni namna bora ya kulipa taratibu taratibu na tunaachana na ule wa kushikilia akaunti zao," amesema Kayombo

Chanzo: NIPASHE
Yafaa TRA iachwe kufanya kazi kwa mujibu wa sheria sio shinikizo hata kutoka kwa rais ambaye anawayumbisha kwenye kutekeleza wajibu wao. Malalamiko ya wafanyabiashara yasiwe ndio hoja ya kutiliwa manani bila kuangaliwa sababu ya kuwepo sheria na taratibu za ukusanyaji kodi zilizowekwa.
 
Awamu iliyopita ilikuwa ya kupika data sana ,nani ana uthibitsho kwamba tulikuwa tunakusanya trilioni 2 kwa mwezi? Kama tulidanganywa kwamba ATCL inapata faida,vipi kuhusu mambo mengine? Kudai kodi kibabe ndio chanzo cha kupiga mweleka kwa uchumi wetu maana TASK force walikuwa wanapora mali na si kukusanya kodi.
Data za uchumi huwezi kuzipika. Zinakusanywa na IMF na ndiyo waliotuingiza kwenye nchi za uchumi wa kati. Muda utaongea kama tutaendelea kuwemo kwenye hizo nchi za uchumi wa kati au tutarudishwa tulikotoka. Kuwa na subira. Ninawajua sana watanzania aka wabongo; hawawezi kupata maendeleo bila kuwarusharusha kichura. Ukiwachekea chekea tu utavuna mabuwa.
 
Hongera kwa kitabu mkuu, lakini nina maswali machache

1. Soko kubwa unalolenga wanunuzi wa kitabu ni watu wa nje au wa Tzania?

Nimeuliza kwa kuwa nimeona suala hili sana mtu analenga kitu kiuzwe Tzania kama hicho kitabu hlf anaandika kw Eng wakati asilimia 99% ya watz wote tunaongea kiswahl tu.
Swali zuri sana nimeandika kitabu mama vingine vitafuata nimeangalia pia soko la nchi zinazoendelea siyo kwa Tanzania peke yake Tanzania being a source of local knowledge
 
Back
Top Bottom