kissa anyigulile
JF-Expert Member
- Apr 21, 2017
- 1,550
- 1,742
Enzi hizo, watu walikuwa huru sana kujiongeza. Hazina ikaishiwa hela kabisa. Nakumbuka Walimu wetu walipata shida sana kwenye mishahara. Kunusuru ikabidi "Sur tax" ianzishwe kwenye magari.Mashine ni ya ofisi, sio ya dereva, na dereva kajiongeza, na huku kujiongeza ndio hufanya vyakula viwe bei nafuu hata wanyonge wanaweza kumudu kula, sasa tukikaza kila kona hadi kwenye vyakula tutaumiza wanyonge, busara iwe inatumika
Mkuu utofautishe kati ya kodi ya mazao inayomhusu mkulima na kodi ya biashara ya usafirishaji (transportation) kitu chochote bila kujali aina ya kitu inayo mhusu mmiliki wa gari au kampuni ya usafirishaji.Rais alisema kama mzigo wako haijavuka tani moja usilipe kodi.
Na karudia rudia mara kibao.
Kwa hio sijaelewa.
Au yale yalikuwa maneno ya majukwaani???
Maelezo yamesema kwakuwa hakua na risiti ya mzigo. Au kuna kitu sijaona?Mkuu unaweza kujua kwa nini alipigwa faini?
Chief nini huangaliwa mpaka mzigo wa thamani hiyo ukapigwa faini kama hiyo?Mkuu iwe Tandam , singo au canter Dereva unapopakia mzigo ni Lazima umkatie risiti mteja wako . na Hayo magari ni Lazima yawe na EFD mashine. Kwa mfano ukiwa unatoka mikoa ya mwanza ,shinyanga ,tabora , Singida na manyara kuja Arusha na moshi utakutana na TRA pale makuyuni. Bila hiyo risiti hampiti hapo.
Na Wewe kama mwenye mzigo pia unakaguliwa kama una risiti ya ushuru yenye jina lako pamoja na leseni ya biashara unayofanya. Bila hivyo vitu hupiti hapo
Mkuu naongea hivi vitu kwa uzoefu hapa.Wakulima nao Wana EFD?.
Mzigo unatoka shamba efd inatoka wapi?
Ni kweli, kama ni hivyo, awe anamuomba tajiri yake juu ya jambo hilo, nadhani wataelewana tu.Ni kweli, kwa 300k lazima dereva aangalie namna ya kupata pesa ya ada na matibabu, serikali iwe na huruma jamanii...!
Mkuu naongea hivi vitu kwa uzoefu hapa.
Ni hivi watendaji wote kule vijijini wana mashine za EFD na ni Lazima ukatiwe risiti yenye jina lako sambamba na leseni ya biashara. Mkuu ukikosa hiyo risiti au kwa Bahati mbaya ukapoteza. Trust me kama unatoka Singida Basi hata pale kateshi hufiki maana kutoka Singida Mpaka babati kuna geti kama nane hivi , na zote zinakagua risiti.
Kwenye suala la faini chief kweli sina ushahidi nalo ni kiwango gani unatakiwa ulipe.Chief nini huangaliwa mpaka mzigo wa thamani hiyo ukapigwa faini kama hiyo?
Tunakoelekea, bei ya mazao yanayoharibika kwa haraka itapanda sana, kula vitu kama nyanya na vitunguu itakuja kuwa ni anasa, serikali ichukue hatua sasa juu ya hili, ikiwezekana pawe na exemption kwa mazao ya chakula yanayoharibika kwa haraka na yasiyozidi kiwango flani kudaiwa risiti za usafirishaji, lazima tutumie akili, tutaua wakulima na wananchi njaa bila sababu za msingi, ahsante kwa mchango wako mzuri sana, tutaufanyia kazi. Ngoja nijadiliane na mbunge hapa.Hili ni Kati ya masuala tata sana.
Kodi muhimu na kodi hii ipo kisheria.
Lakini upande wa pili wa shilingi kodi hizi kwenye usafiri wa mazao ya chakula utaongeza ugumu wa maisha na kushusha kipato cha wakulima wa mazao ya chakula, matunda na mboga mboga, maana madereva sasa hawatathubutu kubeba mizigo midogo kama hiyo njiani. Mazao yata waharibikia na masokoni kutakuwa na upungufu wa bidhaa kisha bei zitapanda kama ilivyo uzwa 1kg ya vitunguu kwa 10,000/- wakati wa Corona.
Lakini tujiulize, kama mwenye mgahawa anatakiwa atoe risiti ya EFD akiuza kitu cha chini ya 30,000 mfano kahawa cupuccino au juice au kuku nusu au Samosa(sambusa) kwanini mwenye kusafirisha mzigo na kutoza 70,000/- au 100,000/- asitoe risiti ya EFD?
Hapa madereva waongee na matajiri wao watembee na EFD na hii pesa ya mizigo ya juu kwa juu wapawe commission kubwa nje ya mishahara yao ili kuwaongezea kipato na kupunguza ugumu wa maisha.
Au
Njia ya pili ambayo mmiliki wa gari si lazima ahusishwe au ajue gari yake ilibeba mzigo wa juu kwa juu.
Kuwe na maafisa wa TRA ambao si wala rushwa wakikutana na mzigo kama huo wanakata kodi halali (yenye uwiano sahihi) kwa huo mzigo, wanatoa risiti ya EFD na gari inaendelea safari.
Kurahisisha zoezi hili na kuepuka udanganyifu wa madereva kuhusu bei walitoza kusafirisha mizigo inabidi TRA waweke vituo vidogo kama check-points au mfano wa vile vya maliasili barabarani kila Kijiji au umbali flani ambapo hapo wenye mizigo na madereva watapakilia hii mizigo na mbele ya hao afisa wa forodha.
TRA inaweza kuweka hata mawakala kwenye vituo hivi kupunguza gharama za kuajiri watu wengi.
Hakuna haja ya ku- centralize kila kitu.
Hivi vituo pia vinaweza kuwa kama vile masoko ya madini Kika wilaya.
Mkulima kazi yako kutoa mzigo wa mazao shamba na gari ndogo kisha kufikisha kwenye vituo hivi. Iwepo na miundombinu ya kusaidia baadhi ya mazao haya yasiharibike yakirubiria usafiri.
Serikali isihusike kabisa kupanga bei ya usafiri wa hii mizigo, hiyo iwe mapatano ya mwenye mzigo na dereva.
Nafikiri haya ndiyo mawazo yangu ambayo si lazima niwe sahihi.
Kwa mfano ukiwa na tenga mia za nyanya Basi kila tenga ni shilingi 1000 tu kwa hiyo kwa tenga 100 ni shilingi laki moja.inakuwa risiti ya Bei gani?
Kwa mfano ukiwa na tenga mia za nyanya Basi kila tenga ni shilingi 1000 tu kwa hiyo kwa tenga 100 ni shilingi laki moja.
NARUDIA TENA KAMA UNAFANYA BIASHARA ZA MIKOANI KUBEBA MAZAO BASI HAKIKISHA UNA RISITI NA PIA IPIGE PICHA.
WAKUU WALE JAMAA WA TRA WANA NYODO KISEN*E KAMA UKIKOSA HIVYO VITU
Dah! Alikua kiserikali kabisa, maana akivaaga mashati ya kijani anaakuaga haaminiki ila hapo kila kitu alichoongea ni amri huyu dereva apaze sauti yake mpaka imfikie au kama wana umoja wasaidiane kupiga kelele maana kazi ya udereva wa maroli bila kucheza ndondo hamnaga kitu paleAngalia post iliyofuata baada ya hii post yangu uliyoi quote.
Jamaa katuma video kabisa
Ndio maana kuna sehemu nimesema sina uhakika na hiyo faini labda jamaa atuletee ushahidi.Kwa hyo tenga 27 Ni elfu 27.
Sasa mbona faini Ni milioni 3
Ndo mana kuna sehem nimesema sina uhakika na hiyo faini labda jamaa atuletee ushahidi.
Mara nyingi unaweza kupigwa faini ya laki tatu Mpaka tano ila inategemea na mzigo.
Mimi bado kwenye hiyo faini Niko kama TOMASO. Mpaka niione ndo ntaamin
Risiti ni rahisi sana kuipata, kama nilivyokuambia wanakatisha risiti ni hao watendaji wa vijiji. Maana watendaji wana EFD MACHINE na pia huwa kuna mawakala wa vipimo wanazungukagaFaini hyo NI kwa wale wenye maduka.
Na hyo risiti sio risiti ya mzigo Ni risiti za viongozi wa vijiji.
Ila risiti yenyewe ya mzigo Ni ngumu kuipata maana mzigo unatoka shamba hautoki sokoni.
Kosa linakuwa ni kutotumia mashine ya Efd, swala la ni nini na cha thamani gani ulibeba haliwahusu Tra, faini ya kutotumia Efd ni kuanzia mil 3 Hadi 4.5Kwa hyo tenga 27 Ni elfu 27.
Sasa mbona faini Ni milioni 3
Unachanganya mada, unachoeleza hakihusiani na nilichoandika, tafadhali soma tena vizuri.Rais alisema kama mzigo wako haijavuka tani moja usilipe kodi.
Na karudia rudia mara kibao.
Kwa hio sijaelewa.
Au yale yalikuwa maneno ya majukwaani???
Risiti ni rahisi sana kuipata ,kama nilivyokuambia wanakatisha risiti ni hao watendaji wa vijiji. Maana watendaji wana EFD MACHINE na pia Huwa kuna mawakala wa vipimo wanazungukaga