TRA yotoa ufafanuzi wa madai ya kutengeneza mfumo wa kuingiza mizigo nchini usio halali

TRA yotoa ufafanuzi wa madai ya kutengeneza mfumo wa kuingiza mizigo nchini usio halali

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inapenda kutoa ufafanuzi juu ya taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu malalamiko ya Bw. Emmanuel Gadi kuwa, TRA imetengeneza mfumo wa kuingiza mizigo nchini nje ya mfumo halali wa Serikali kinyume na Sheria ya Forodha.

Tunapenda kuufahamisha umma na jamii kwa ujumla kuwa, Mamlaka haina mfumo wowote mwingine inaouendesha wa kuingiza mizigo nchini nje ya mfumo wa Forodha wa TANCIS ambao unatumika kwa mujibu wa Sheria ya Usimamizi wa Forodha ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EACCMA).

Bw. Emmanuel Gadi alifikisha malalamiko yake kwa njia ya barua tarehe 27 Februari, 2023 akidai kupewa uthibitisho na TRA wa kuingiza mzigo wa vifurushi 471 vya “Toner Cartridges’’ kupitia kampuni ya Tosh Logistics Ltd. TRA ilifanya uchunguzi wa kutosha na kuthibitisha kwamba, hapakuwa na mzigo wowote ulioingizwa nchini kwa jina la Wintech Tanzania Ltd wa vifurushi 471 vya “Toner Cartridges” kupitia kadhia yenye namba TZDL-22-1382193 ya tarehe 18 Agosti 2022 kama anavyodai.

Hivyo, TRA ilimjibu mhusika kupitia barua yenye kumbukumbu namba CF 8/92/01 ya tarehe 25 Julai 2023 ikimjulisha kuwa, kutokana na kukosekana kwa ushahidi wa “House Bill of Lading” na kutoonekana kwa mzigo huo kwenye kadhia iliyowasilishwa na kampuni ya Tosh Logistics Ltd, TRA isingeweza kuthibitisha kuingizwa kwa mzigo huo nchini.

Kupitia taarifa yake aliyoitoa kwenye vyombo vya habari tumebaini kuwepo viashiria vya ukwepaji kodi kwani ni dhahiri kuwa mzigo huu uliingizwa kwa njia za magendo. TRA inamtaka mlalamikaji kuwasilisha nyaraka na uthibitisho wa kampuni yake kuingiza mzigo huo nchini mara moja ili hatua stahiki zichukuliwe.




===========
Video ya Mfanyabiashara akiituhumu TRA
Nimempenda bure huyu Mtanzania mzalendo
 
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inapenda kutoa ufafanuzi juu ya taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu malalamiko ya Bw. Emmanuel Gadi kuwa, TRA imetengeneza mfumo wa kuingiza mizigo nchini nje ya mfumo halali wa Serikali kinyume na Sheria ya Forodha.
Mtu aandike barua Feb ajibiwe Aug?? Mie?i 7 baadae. Hapa iko shida kubwa
 
Hili ni bomu ambalo inatakiwa kitu cha kwanza Wazziri wa Fedha, Makamishnana, manaibu Kamishna, vyombo vya usalama vyote waliopo TRA wanaohusiana na bandarin, wote wasimamishwe kazi wawekwe wengine haraka sana, uchunguzi wa kina ufanyike.


Hawa ndiyo wanaochelewessha maendeleo.

Huyo Mfanyabiashara apewe ulinzi wa saa 24, watamfinya.

Wameshaonesha wanataka kumgeuzia kibao. Barua ya kujibiwa ndani ya muda mchache kwanini ikae miezi kujibiwa?

Tena inaonesha imejibiwa ile "ficha kombe mwanaharamu apite).


Mama aSamia, nnauhakika hili limeshafika mezani kwako.
Hongera wewe ni mzalendo sana madam, hakika hili Jipu kubwa sana trillions of money a stolen hatari sana
 
Mizigo ya loose cargo nikuwa mizigo ya watu tofauti inakusanywa kwenye kontena moja na kampuni ya usafirishaji inasafirisha kama mali yao.Ndiyo maana unachajiwa kwa CBM na unalipa kwenye kampuni ya usafirishaji bila kwenda mwenyewe forodha.

I think baada ya TRA kupata hili zengwe la huyu jamaa wakaja na mfumo wa kila mtu alipie forodha,ambapo kwenye mgomo wa Kkoo kipindi kile watu waliupinga huu utaratibu.Maana ilikuwa let’s say kontena ina mizigo ya watu 100,kila mmoja inatakiwa akalipie ushuru forodha.

Kitu ambacho hawakujua ndio kama sasa hivi inakuwa ngumu bima kulipa bila nyaraka za uingizaji mzigo.TRA walilijua hili ila kwa kuwa walikuwa wananeemeka bila kesi wakapuuzia.
Kuna mtu atatolewa mbuzi wa kafara kwenye hili.
Maelezo yako ndugu Dreams LLC LLC yana make sense kwa kiasi kikubwa..

Yaani watu wanatengeneza mfumo ulio na lopeholes za kuji - corrupt ili waibe mapato..

Pia Mjomba Fujo naye kajiuliza maswali ya msingi tu.

Na maelezo yako haya yanajibu hoja zote za Mjomba Fujo..

CC: Mjomba Fujo
 
Hongera wewe ni mzalendo sana madam, hakika hili Jipu kubwa sana trillions of money a stolen hatari sana
Kwa sababu TRA inatetea msimamo wake sitashangaa wachangiaji wengi hapa ni ama wa TRA au wana uhusiano wa karibu na TRA kwa hiyo wana maslahi yanayosigana. Hoja yangu ni kuwa TRA ina wajibu wa ziada wa kulinda sheria na taratibu zake zisitumike kuathiri kusudi la Serikali,pamoja na kuwaelimisha wadau . TRA katika hoja yao inaonekana hilo suala la wafanyabiashara wadogo ambao hawawezi kujaza content haliwahusu hususan kutoa utaratibu unaofaa, madhara ya kutofuata utaratibu na wajibu wa Clearing and Forwarding Agent ambaye ni wakala wa TRA kumwakilisha TR ipasavyo.

TRA katika hoja yake hajamgusa mwakilishi wake Clearing and Forwarding Agent inakimbilia kumtuhumu mfanyabiashara ambaye aliihusisha TRA tangu mwanzoni na siyo kwamba TRA imegundua kuwa amekwepa kodi! Watanzania tunatakiwa tujue, hata katika kuchangia, wajibu wa kila Tassisi ni nini? Hili siyo suala la ushabiki. TRA ni taasisi kubwa na inatakiwa iendeshwe na mtu mwenye uelewa mpana. Hili suala lilipelekwa kwake amekaa nalo mpaka sasa linapelekwa kwa Mhe. Rais ndipo anatoa utetezi wake wakati umma unasubiri uamuzi wa Rais! Je, huu ndiyo utaratibu?

Sasa TRA inataka Rais amwambie nini Gadi? Huu utaratibu unafanya kazi ya Rais iwe ngumu sana. Sijui kama wengi mnanielewa ninachoandika. Vinginevyo naomba msamaha.
 
Cha kushangaza KIZIMKAZI yy hajui lolote na yuko majuu n stive Nyerere. Kwake hili nalo litapita bila hata kuhoji
 
Waziri wa uchukuzi ni Mzanzibar, KM wa uchukuzi ni Mzanzibar, CEO wa bandari ni mzanzibar(wote dini moja), Mwigulu anahusikaje kwenye bandari? upigaji ni mfumo ovu wa serikali nzima, kuna kuwaje na wizi na wakati hapo bandarini kuna polisi na TISS?
Kwa hiyo wa Uchukuzi ndo ana mfumo wa forodha? Hebu acha chuki na Wazanzibar.
 
Ngoja nichanganue hili sakata kwa nilivyoelewa mimi.

Mfanyabiashara Ameingiza bidhaa zake nchini kupitia kampuni ya tosh cargo

Tosh cargo amesafirisha na kukamilisha taratibu zote za forodha na kukabishi mzigo kwa mteja wake.

Shida inaanzia hapo kwenye (Amesafirisha na kukamilisha taratibu zote za forodha)

Wakati mfanyabiashara anapelekea mzigo wake huko unapotakiwa kwenda gari ikapata ajali na kusababisha uharibifu na upotevu wa mali.

Kwakua mfanyabiashara alikua na bima, akaanza mchakato kufatilia ili apate fidia ya mali yake iliyoharibiwa na tukio la ajali.

Kampuni ya bima inawajibika kumlipa mteja wake, lakini kabla hawajamlipa lazima wapate nyaraka zote muhimu kuhusu mali zilizopotea, ikiwa ni pamoja na nyaraka zote halali za kikodi na mengineyo ili wapate uhakika wa thamani na uhalali wa wanachoenda kulipa.

Sakata linaanzia hapa kwenye nyaraka.

TRA hawatambui mali ya mlalamikaji, kwanini hawaitambui na hawajaiona kwenye mfumo?

Kuna mawili hapa;

1. Tosh cargo wameingiza mzigo kama mali yao, hivyo mteja mwenye mzigo hatambuliki na mfumo mzima wa TRA.

2. Rejea namba moja [emoji23], kama mfumo haukusomi basi unamsoma aliekamilisha clearance ya mzigo.


Kama Nyaraka za TRA hazikutambui kampuni ya Bima itakufidia vipi na umeshindwa kutoa vielelezo vya uhalali wa mali iliyoharibika, vipi kama umekula njama na mtu baki utumie mgongo wa mali yake iliyoharibika kujipatia bima kwa njia ya udanganyifu?


Swali jingine la msingi kwa mfanyabiashara.
Asijekua anataka huruma ilhali nayeye anajua fika changamoto ambazo zingejitokeza.

Je kabla ya kupata matatizo yote ya ajali n.k, aliridhika na nyaraka zote alizokabidhiwa baada ya kupewa mizigo yake, au akili imekuja kukaa sawa baada ya matatizo?
Safiii
 
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inapenda kutoa ufafanuzi juu ya taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu malalamiko ya Bw. Emmanuel Gadi kuwa, TRA imetengeneza mfumo wa kuingiza mizigo nchini nje ya mfumo halali wa Serikali kinyume na Sheria ya Forodha.

Tunapenda kuufahamisha umma na jamii kwa ujumla kuwa, Mamlaka haina mfumo wowote mwingine inaouendesha wa kuingiza mizigo nchini nje ya mfumo wa Forodha wa TANCIS ambao unatumika kwa mujibu wa Sheria ya Usimamizi wa Forodha ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EACCMA).

Bw. Emmanuel Gadi alifikisha malalamiko yake kwa njia ya barua tarehe 27 Februari, 2023 akidai kupewa uthibitisho na TRA wa kuingiza mzigo wa vifurushi 471 vya “Toner Cartridges’’ kupitia kampuni ya Tosh Logistics Ltd. TRA ilifanya uchunguzi wa kutosha na kuthibitisha kwamba, hapakuwa na mzigo wowote ulioingizwa nchini kwa jina la Wintech Tanzania Ltd wa vifurushi 471 vya “Toner Cartridges” kupitia kadhia yenye namba TZDL-22-1382193 ya tarehe 18 Agosti 2022 kama anavyodai.

Hivyo, TRA ilimjibu mhusika kupitia barua yenye kumbukumbu namba CF 8/92/01 ya tarehe 25 Julai 2023 ikimjulisha kuwa, kutokana na kukosekana kwa ushahidi wa “House Bill of Lading” na kutoonekana kwa mzigo huo kwenye kadhia iliyowasilishwa na kampuni ya Tosh Logistics Ltd, TRA isingeweza kuthibitisha kuingizwa kwa mzigo huo nchini.

Kupitia taarifa yake aliyoitoa kwenye vyombo vya habari tumebaini kuwepo viashiria vya ukwepaji kodi kwani ni dhahiri kuwa mzigo huu uliingizwa kwa njia za magendo. TRA inamtaka mlalamikaji kuwasilisha nyaraka na uthibitisho wa kampuni yake kuingiza mzigo huo nchini mara moja ili hatua stahiki zichukuliwe.




===========
Video ya Mfanyabiashara akiituhumu TRA
Waulizeni wafanya biashara wa Kariakoo kama kuna hata mmoja ana karatasi ya importation ya mali walizo nazo dukani. Mizigo yote inasafirishwa na kutolewa na GSM. Siri ndio iko hapa GSM na TRA wakanushe na hii kwani ni ya miaka yote
 
Back
Top Bottom