FRANCIS DA DON
JF-Expert Member
- Sep 4, 2013
- 38,920
- 44,970
Hizi ni hujuma za wenye maabasi kukorofisha mifumo ya umeme kwa makusudi..
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Watusamehe aisee, inawezekana wameweka timu ya vijana wao kwenye vituo vyote vya kupoozea umeme, ikifka usiku tu wanafanya yao.., kwanini hitilafu zitokee zaidi usiku?!Abood na Shabiby tusameheni wakuu. Madam president alikuwa anatania tu mbona
Mnafanya hujuma halafu mnaleta vijiushauri vyenu hapa, hatutaki!TRC ifanye Kazi na sekta binafsi, wenye uwezo wa kuleta vichwa na mabehewa Kwa standard za TRC waluhusiwe na Wao kuleta wapewe utaratibu, hii itaondoa hisia za kuwa matajiri wa Mabus wanahujumu reli!
Hiyo imekaa vizuri, akina Abood mbona wanalalamika SGR imeua biashara yao ya mabasi, si waingie tu kwenye gemu sasa.Wameishaambiwa wanakaribishwa kuwekeza vichwa na mabehewa harafu watalipia tozo za miundo mbinu
Hiyo imekaa vizuri, akina Abood mbona wanalalamika SGR imeua biashara yao ya mabasi, si waingie tu kwenye gemu sasa.Wameishaambiwa wanakaribishwa kuwekeza vichwa na mabehewa harafu watalipia tozo za miundo mbinu
Hiyo imekaa vizuri, akina Abood mbona wanalalamika SGR imeua biashara yao ya mabasi, si waingie tu kwenye gemu sasa.Wameishaambiwa wanakaribishwa kuwekeza vichwa na mabehewa harafu watalipia tozo za miundo mbinu
Si imefika kituoni kwa mwenyee muhusika imepumzika? Kwani kituo gani?
Rais Samia Suluhu Hassan leo Alhamisi amezindua rasmi huduma za usafiri wa reli ya kisasa (SGR), treni iliyokuwa imebeba wageni walioshiriki uzinduzi huo wakiwamo mabalozi na viongozi mbalimbali wa kiserikali kutokea mkoani Dodoma, imepata tena hitilafu karibu na Stesheni ya Morogoro kwa zaidi saa moja sasa.
Pia soma: Morogoro: Treni ya SGR (Dar-Dodoma) yakwama Kidete Kilosa kwa zaidi ya saa 4, sababu Hitilafu ya Umeme
Mmoja wa abiria aliyemo kwenye treni hiyo amesema:"Tumetoka vizuri tu Dodoma lakini tulipofika katikati ya Mkata na Moro stesheni ikiwa kama saa 4:33 usiku ikasimama ghafla hadi na kuzima kabisa, hadi sasa saa 5:33 usiku bado tupo hapa."
Mmoja wa wahariri, Peter Nyanje katika ukurasa wake wa Instagram ameandika:"Ni saa tano usiku tulitoka Dodoma kwenye uzinduzi wa SGR. Wakati tunakaribia station ya Morogoro treni imesimama ghafla njiani, air conditions zimezima, milango haifunguki. Tumekwama hapa sasa ni zaidi ya nusu saa. Tupo takribani watu 1,000 humu ndani."
Hata hivyo, ilipofika saa 5:35 usiku, treni hiyo ilianza safari.
Juhudi za kuupata uongozi wa Shikika la Reli Tanzania (TRC) zinaendelea.
Hayo yanajiri ikiwa zimepita siku mbili baada shirika hilo kuomba radhi kwa treni yake iliyokuwa ikisafiri kutoka Dar es Salaam kuelekea Dodoma kusimama kwa muda wa saa mbili kati ya stesheni ya Kilosa na Kidete mkoani Morogoro juzi tarehe 30 Julai 2024.
Pia soma: TRC yatolea ufanunuzi kuzimika kwa treni ya SGR Julai 30, 2024 katikati ya Stesheni ya Kilosa na Kidete
“Taarifa za awali zinaonesha kuwa hitilafu za aina hiyo husababishwa na wanyama (ngedere) au ndege (bundi) wanapogusa nyaya za umeme zilizotandazwa juu ya reli (overhead catenary system),” amesema.
Mwananchi
View attachment 3059048
Bindi aligonga boda ya afisa kilimo Tanga ikawa written off
Rais Samia Suluhu Hassan leo Alhamisi amezindua rasmi huduma za usafiri wa reli ya kisasa (SGR), treni iliyokuwa imebeba wageni walioshiriki uzinduzi huo wakiwamo mabalozi na viongozi mbalimbali wa kiserikali kutokea mkoani Dodoma, imepata tena hitilafu karibu na Stesheni ya Morogoro kwa zaidi saa moja sasa.
Pia soma: Morogoro: Treni ya SGR (Dar-Dodoma) yakwama Kidete Kilosa kwa zaidi ya saa 4, sababu Hitilafu ya Umeme
Mmoja wa abiria aliyemo kwenye treni hiyo amesema:"Tumetoka vizuri tu Dodoma lakini tulipofika katikati ya Mkata na Moro stesheni ikiwa kama saa 4:33 usiku ikasimama ghafla hadi na kuzima kabisa, hadi sasa saa 5:33 usiku bado tupo hapa."
Mmoja wa wahariri, Peter Nyanje katika ukurasa wake wa Instagram ameandika:"Ni saa tano usiku tulitoka Dodoma kwenye uzinduzi wa SGR. Wakati tunakaribia station ya Morogoro treni imesimama ghafla njiani, air conditions zimezima, milango haifunguki. Tumekwama hapa sasa ni zaidi ya nusu saa. Tupo takribani watu 1,000 humu ndani."
Hata hivyo, ilipofika saa 5:35 usiku, treni hiyo ilianza safari.
Juhudi za kuupata uongozi wa Shikika la Reli Tanzania (TRC) zinaendelea.
Hayo yanajiri ikiwa zimepita siku mbili baada shirika hilo kuomba radhi kwa treni yake iliyokuwa ikisafiri kutoka Dar es Salaam kuelekea Dodoma kusimama kwa muda wa saa mbili kati ya stesheni ya Kilosa na Kidete mkoani Morogoro juzi tarehe 30 Julai 2024.
Pia soma: TRC yatolea ufanunuzi kuzimika kwa treni ya SGR Julai 30, 2024 katikati ya Stesheni ya Kilosa na Kidete
“Taarifa za awali zinaonesha kuwa hitilafu za aina hiyo husababishwa na wanyama (ngedere) au ndege (bundi) wanapogusa nyaya za umeme zilizotandazwa juu ya reli (overhead catenary system),” amesema.
Mwananchi
View attachment 3059048
Pesa za raia zimetumika nyingi halafu watu wanasema mwanzo mgumu ,wakati ni uzembe na hujuma tuu ndio tatizo linalo lelewaUkute unahangaika na Abood.Kajificha kwenye kijineno- Kasikazini hapo.Ndiyo wabunge wa CCM..eti Mwanzo mgumu, utafikiri wanafanya biashara ya nyanya, hawajui wajibu wao kwa watu wanaowaongoza.
Wewe kama mimiMmmh ngoja nisipande kwanza acha nipambane na usafiri mwingine.
Nimesikia A/C zilizima na milango ikawa haifunguki nilivyo muoga ngoja nisubiri kwanza.
HahaaaaAbood na Shabiby tusameheni wakuu. Madam president alikuwa anatania tu mbona
Inatia hasira sana baasi tuSisi hatuna ugeni. Vitu vyote vinavyofanywa na kusimamiwa na Serikali hii ya kwetu huwa havina perfection hata siku moja. Hiyo ndiyo kawaida ya miradi yote ya Serikali. Kukiwa na perfection ndiyo itakuwa ajabu.
Tulianzisha viwanda, viliishia wapi? Tulianzisha mashirika ya usafirishaji kwa kila.mkoa, yaliishia wapi? TANESCO utendaji kazi wake upoje? Hospitali zetu za umma, zipoje?
Watu wazoee tu, hiyo SGR itakuwa inakwenda hivyo hivyo, cha kuombea isipate hitilafu ya kuleta maafa. Hiyo kukwamakwama itakuwa ndiyo utendaji wake wa kawaida.
Hivi Rais anashindwa kufukuza hao viongozi jamaniiSiamini kama ni hujuma. Uwezekano mkubwa ni uzembe na kukosa umakini. Ndivyo utendaji kazi wa serikali na taasisi zake zote, ulivyo.
Yaani kaka angu usemayo yawez akua saihiUsikute umoja wa wamiliki wa mabasi wameanza kupenyeza rupia wahujumu, abiria warudi kwenye mabasi maana trip 1 ni abiria wa mabasi 15, trip 4 basi. I mabasi 60,unadhani wao wanafurahi!!!!?
Lakini pia usikute kuna wasenge wanataka waharibu iwe kama mwendokasi kesho na keshokutwa wabinafsishe
Ama uzembe tu wa wabongo makazinj, wabongo tuna kaujinga fulani ka kutokujali, kila kitu kwetu ni poa poa... Nina mashaka hata pale tren zinaposimama na kusubiri zipishane ipo siku utatokea uzembe vyuma vitaingiana uso kwa uso. (mungu aepushe mbali)
Wafungue viwanda sasa waajiri watu wengi zaidiHiyo imekaa vizuri, akina Abood mbona wanalalamika SGR imeua biashara yao ya mabasi, si waingie tu kwenye gemu sasa.