Treni yaleta ‘kilio’ usafiri wa mabasi Dar - Moshi

Yaani treni inaenda Moshi mara 3 kwa week, trip moja inabeba watu 150 kwa hiyo hadi mwezi uishe itakuwa imebebeba abiria kama 2000 tu ndiyo imeua biashara ya mabasi msimu wa Christmas?

Get outta here.
Hili la treni kubeba abiria 150 kwa trip moja umelitoa wapi mkuu? Nadhani umeshindwa hata kufikirisha ubongo wako. Treni ina mabehewa mangapi na kila behewa lina uwezo wa kubeba abiria wangapi?

Hii uloyoleta ni uzandiki tu na haukubaliki kwa maendeleo ya taifa.
 
hivi kwani wauzaji wa vyakula pale korogwe hawalipagi kodi mkuu
 
Nenda China kuna train kila route na mabasi yapo yanajaa
 

Kweli kabisa Mkuu
Tunahitaji mipangilio mizuri na utaratibu mzuri
Tatizo viongozi wanapokuja nchi zilizoendelea wao wanalala tu na kula bata na kununua suits tu
Wanayaona yote haya na wengi wamesoma Ulaya na kuona miundombinu yao ila hawana mikakati kabisa ya kuiga


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
huo ni mzuka tu! mikoa ya Njombe,Mbeya na morogoro ni watumiaji wakubwa wa Treni ya Tazara tena ukiwa ndani ya Makuba Express ni nzuri kuliko Hiyo ya Moshi-Dar au Reli ya kati.Pia Tazara ina utulivu kwa kua Reli yake ni standard kuliko hiyo ya Moshi Dar lakini miaka yote hii Imeshindwa kuyapiku mabasi sababu kuu ni kama mbili au tatu hivi kama ifuatavy.
1. usafiri wa treni Tanzania unasafari chache sana kwa wiki nje na matarajio ya abiria hususani wafanyabiashara ambao wanatamani kutembea twenty four hours yaani atoke NjOMBE/MBAYA aende DSM afanye shughuli zake siku ya pili arudi nje ya usafiri wa mabasi hakuna huo mfumo kwenye Treni sababu ni uduni wa hudumu na uwekezaji.
2. usafiri wa treni Tanzania Unagharama pengine tofauti na nchi nyingine.Ikifika Disemba ndio usiseme kwa abiria anayeshukia makambako analipa zaidi ya 30000 wakati kwenye basi nako amabapo anondoka asubuhi na kufika jioni nauli 30000 au chini tofauti na treni amabpo atatoka IJUMAA saa tisa na dakika 55 dasm na kuingia makambako Jumamosi alfajiri.
3. usafiri wa treni Tanzania bado hauja wa uhakika ndio na hauna mbadala kama kwenye mabasi.

Hivyo MAONI yangu usafiri wa mabasi hauwezi athiriwa na usafiri wa treni ni watu mia nne ndio wamerudi na treni Juzi tujiulize ni watu wangapi wanasafiri kwa siku toka Arusha,Kilimanjaro,Tanga kuja DSM.
 
mimi ni mfuasi wa chama pinzani lakin katika sala la treni namuunga mkono raisi kwa asilimia zote
treni hii imegusa maisha ya watu wa hali ya chini i wish ingekuwa inafanya safari kila siku ya wiki
 


Uchambuzi mzuri lakini ukisema treni haitaathiri usafiri wa mabasi sio sawa. Itaathiri ila sio kwa kiwango kikubwa. Kumbuka hata iwe abiria 10 au 20, tayari wameshaanza kugawana tofauti na awali hao wote walikua wanalazimika kutumia usafiri wa mabasi.

Nnaowahurumia zaidi ni wale wenye mabasi ya Dar Moro pindi reli ya SGR ikikamilika, kwanza itakua na mwendo na ya kisasa.

Kingine usumbufu wa maaskari wa usalama barabarani unafanya mabasi yatembee mwendo mdogo sana na kusababisha abiria kuchelewa zaidi.

Wengi wanaona bora wapoteze muda wa usiku kwenye treni ili siku inayofuata waendelee na kazi zao, ikumbukwe ajali za treni zipo lakini zinatokea mara chache sana.

Ule uhuru wa kuamua kulala na kupatikana kwa huduma muhimu kama chakula na vyoo napo kunaleta hamasa kwa wasafiri.

Usafiri wa treni kwa namba moja ama nyingine unaathiri wamiliki wa mabasi.

Nnachojiuliza baada ya kipindi cha krismas watapunguza idadi ya safari na mabehewa?
 
Acha mabasi yafe kabisa,maana walikuwa wajinga na wapuuzi mwisho wa mwaka wanaongeza nauli kitoto toto kabisa,acha walie kilio cha Paka mwizi
 
NIKOOO MOSHII HALI N TETE WAPENDWA MABASI YANAENDA DAR KWA SABABU TU YANATAKIWA KWENDA

MABASI HATA NUSU AYAJAI BEI N ZAKUTUPA KURUDI DAR HADI 18000 LWENDA MPAKA 22000 WACHA TUNYOOOKE MUDA WA KUINGIA KANNAN YA MAGUFULI NDIOO HUU

MLIFIKIRI YULE DOGO ALIUZA MALORI 300+ ALIKUWA FALA NA MABASI AKAISHIA KUUZA KABISA ATAKI SHIDA
 
Kiukweli mlikuwa wanyanyasaji sana kwa abiria wa kanda hiyo... yani kipindi hiki mlikuwa mnaringa kupita maelezo... MUOSHA HUOSHWA...dawa ya moto ni maji 😂😂😂
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…