True story: Babu yangu kama mshikaji wangu

...105
Bibi alikuwa ananitazama kama ananisoma nini nawaza, nilipokutanisha nae macho alibabaika na kuangalia pembeni, niliwaza huenda kuna ishara inamfanya kuwa na wasiwasi na mimi.
Baada ya kufungua vinywa babu alimtaka bibi waondoke wakaone yatayojili huko msibani kwani kulikuwa na vioja vya aina yake, waliondoka huku babu akinitaka nisivuke mpaka wa pale nyumbani, nilikubali huku moyoni nikilaani zuio lile kwani lilinichelewesha kupata ukweli wa ndoto niliyoota usiku huku yunge mdogo akinambia haikuwa ndoto.
Nilitamani niende nyuma ya nyumba ya nyasi (jikoni) ili nimwite yunge mdogo, lakini nijijizuia kutokana na huenda kulikuwepo na wazazi wake, basi niliingia getoni mwangu nikachukua kiredio changu, pia nikakumbuka ndani ya begi palikuwa na game (tetri) nilichukua nikaenda navyo nje ambapo nilifungulia clouds fm, mda ule wa saa 5 kulikuwa na top 20, hivyo nilienjoy good myuzik huku nikifurahia game langu, mpaka saa 6:55 yunge mdogo hakuwa ametokea.
Spooorts roundup, ilisikika sauti kutoka redioni...!
 

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Keep up the good work brother...
 
...106
Ilikuwa imetimu saa 7 kamili mchana, nilikuwa nimenogewa na game lile na sasa nilishahau kama mda mfupi ulipita nilikuwa namngoja yunge mdogo kwa hamu.
Nilishtuka baada ya kuzibwa uso na viganja vya mikono ya mtu, niliwaza atakuwa nani huyu, mbona viganja kama vimekomaa sana atakuwa nani huyu?
Jumaa! Niliita nikifikiri atakua yule captain wa timu, lakini ikawa kmya.
Nilijipa asilimia nyingi kwamba viganja vile vilikuwa vya kijeba.
Nilirudisha mikono kwa nyuma na kupapasa miguuni ili nijue aliepo pale alikuwa kavaa nguo ya kike ama ya kiume, bahati haikuwa yangu kwani alinikwepa nisifanikiwe kumgusa.
Yaani wewe huwezi hata kutambua harufu ya mkeo kweli? Alikuwa yunge mdogo akiongea kwa bashasha.
Sasa wewe mikono imekomaa kama ya mwanaume mie ningejuaje kama ni wewe? Nilitania.
Mwone! Kwahiyo ndo ukaniita juma kisa mikono yangu imekomaa? Aliniuliza.
Ee mie nikajua ni juma tu.
Tulicheka kisha akasema hii mikono kuwa hivi ni kwasababu ya kilimo cha mkono.
Najua yote hayo mama, naomba twende ndani kwanza.!
 
Tupia vitu mkuu pamoja sana ✌️🙌
 
Toka kugonga dem mara ya kwanza mpaka sports round-up??? Kabla ya hapo ilikua ni top 20, tena ni asubuhi hiyo??!! Ayseee [emoji119][emoji119][emoji119]

Hii safari nimejitahidi kujishikilia lakini naona tunarudi kulekule kwa jirani bonge..... [emoji849][emoji849][emoji849]
 
Punguza kiherehere soma vizuri ukiona hauelewi achana nayo mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
...107
Nilimwomba twende geto, kwani nilitaka nimjuwemo kwanza kabla hajanipa stori nzima ilikuwaje mimi niote napaa halafu yeye aje kunambia nilikuwa napaa kweli, japo nilianza kuyazoea mauzauza ya pale kijijini, mengine yalinitia shaka mno.
Hapana tusiingie ndani naona watakuja watu muda si mrefu hapa hivyo naomba niondoke, alisema yunge mdogo.
Wanakuja kina nani na wapo wapi? Nilimwuliza.
Elewa nimekwambia watakuja hapa watu muda si mrefu, tena naona kutakuwa na kazi pevu hapa, aliongea yunge mdogo huku akiaga na kuondoka kwa haraka sana, alipoishilizia tu nikasikia hodi hapa, ilikuwa sauti yenye mamlaka, yaani utafikiri jamaa anabisha hodi kwake, karibuni wazee wenzangu, ilikuwa sauti ya babu akiwakaribisha wazee wapatao watatu, nilipowaona tu, wawili kati yao walisimama kwa mshtuko, walinikazia macho nami pasipo wasiwasi wowote niliwatazama kwa kujiamini mno kwani nilihisi watakuwa vigagula tu.
Huyu mtoto ni mchawi na ndo kasababisha mkeo apatwe na madhira yale yote, alilopoka mzee mmoja mwenye mvi tele.
 
Kama hujaelewa uliza ueleweshwe, kwani top 20 ilikuwa inaanza muda gani na sports roundup ilikuwa muda gani? Na wapi nimesema siku hiyo niligonga dem?
Vichwa vingine bwana mafi kbs.
 
Kama hujaelewa uliza ueleweshwe, kwani top 20 ilikuwa inaanza muda gani na sports roundup ilikuwa muda gani? Na wapi nimesema siku hiyo niligonga dem?
Vichwa vingine bwana mafi kbs.
Mkuu kuanzia sehemu ya kwanza hadi 20 hukua unajibizana na K kama hizi..

please maintain the acceleration & status
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…