.....!
Niliwasha moto pale nje(shikome) kisha nikachukua kiti na kukaa karibia na moto, muda kidogo alikuja yule binti akiwa kabeba rufuria na kisu, ndani ya sufuria kulikua na yule kuku alienyonyolewa manyoya, basi binti kwa ustaarabu akaniomba nimshikie ili amkate vipande vipande yule kuku kwani anakazi nyingine ya kufanya nyumbani kwao,
Nilimshikia akaianza kazi ile mara moja.
Unaitwa nani? Aliniuliza yule binti huku anaendelea na kazi yake,
Naitwa Buhabhi jina la babu, ila nitapenda ukinita nzehe, nilijibu,
kwanini unapenda jina la nzehe (mzee) aliuliza tena,
Napenda jina hilo kwa sababu ndo jina ambalo mama hupenda kuniita kwa kuhofia kulitaja jina la baba mkwe wake (babu kizaa baba) nilimjibu.
Nikweli sio vizuri kutaja jina la mkwe, alisema yule binti na kuongeza,
Sasa mbona hujaweka kuni kubwakubwa (shitinde) kwenye moto wako? Aliuliza huku akinitazama usoni,
Mie sijui bwana, nilimjibu,
Kuni kubwa ndo uhai wa moto ule, yani bila hizo moto hautodumu, basi nilisogeza magogo mawili makubwa nikachochea