Trump alivyolea wanawe ni changamoto kubwa kwa dunia inatakiwa tuige mfano wake

Trump alivyolea wanawe ni changamoto kubwa kwa dunia inatakiwa tuige mfano wake

Kwenye masuala ya ndoa Trump anakwama; sio mfano bora sana wa kuigwa. Mke mmoja, mume mmoja hadi kifo kiwatenganishe ameshindwa kuiishi hiyo doctrine!
Kubadilisha wanawake ni msingi wa imani ya Kikristo kweli?
 
Kwenye masuala ya ndoa Trump anakwama; sio mfano bora sana wa kuigwa. Mke mmoja, mume mmoja hadi kifo kiwatenganishe ameshindwa kuiishi hiyo doctrine!
Kuna mda hii ya mke mmoja hadi kifo kiwatenganishe naona Ina ukakasi kwa maisha ya sasa.
Kuwa na mke mmoja ni sahh ila kung'ang'ania ndoa na mwanandoa (mke /mme) asiefaa ni upumbavu na ni sumu inayomaliza watu wengi kihisia na kiimani na kiakili mpaka kupelekea kushindwa kusimamia watoto wao.
Si shauri ndoa za wake wengi ila mkishindwana usiongeze bali ondoa utafte mpya anaeweza kutembea kwenye njia uitakayo
 
Kuna mda hii ya mke mmoja hadi kifo kiwatenganishe naona Ina ukakasi kwa maisha ya sasa.
Kuwa na mke mmoja ni sahh ila kung'ang'ania ndoa na mwanandoa (mke /mme) asiefaa ni upumbavu na ni sumu inayomaliza watu wengi kihisia na kiimani na kiakili mpaka kupelekea kushindwa kusimamia watoto wao.
Si shauri ndoa za wake wengi ila mkishindwana usiongeze bali ondoa utafte mpya anaeweza kutembea kwenye njia uitakayo
Kuna wimbo mmoja huwa nasikiaga dhehebu fulani wanaupenda sana; BWANA kama ungehesabu maovu yetu, nani angesimama?

Swali; utafukuza na kuoa wangapi? Kwa njia ya waovu yaweza kuonekana jambo jema ila kwa Mungu ni machukizo.
 
Kuna wimbo mmoja huwa nasikiaga dhehebu fulani wanaupenda sana; BWANA kama ungehesabu maovu yetu, nani angesimama?

Swali; utafukuza na kuoa wangapi? Kwa njia ya waovu yaweza kuonekana jambo jema ila kwa Mungu ni machukizo.
Usijifananishe na Mungu, yeye ana tusikilizia tu anajua Kuna hukumu yake inakuja ila mwanzo na yeye alikuwa anauwa na kuanza upya mfano sodoma na gomora, gharika la nuhu nk.
Sasa ww binadam uvumilie ujinga ambao unaona unaenda kiathiri na wengne kwa kigezo gani? Je una mda wa kuja ku-amend kama Mungu?

Tusipende kujifananisha na Mungu kwenye kila kitu ili hali approach zetu na zake ni tofauti
 
Trump hana maadili yoyote kama Elon musk tu wote n wahuni
Muhuni amepewa dhamana ya kuongoza taifa kubwa na tajiri sana duniani na maamuzi yake yoyote yanakuathiri hata ukiwa kijijini kwenu Kung'ombe, Bunda.

Tuanze na Trump. Amepewa urais na watu waliotengeneza chombo hichohicho unachotumia kumpondea humu mtu huyo waliyemchagua kuwa rais wao. Huyu ndiye mtu ambaye kwenye urais wake amekataa mshahara mnono wa dola 400,000 (Tshs. 2,4000,000/-) kwa mwaka na kuamua kupokea dola moja (1) sawa na shilingi 2,600 kwa mwaka kwa sababu tu ya kwamba alichokifuata ikulu ni zaidi ya mshahara.

Twende kwa Musk, ndiye mtu tajiri sana duniani na ambaye kwa "sekunde" moja tu hutengeneza dola za kimarekani 43,000 sawa na shilingi za kitanzania milioni 111,800,000 pesa ambazo ukipewa sasa hivi hapo ulipo wewe, unaweza hata ukamtukana baba yako mzazi kwa kibri tu.

Tuje kwako, wewe Kalumekenge aliyekataa kwenda shule, hakuna hata anayekufahamu hata ktk kijiji chako na hata kwenye kitongoji chako ikitokea msiba mama moja mtoto kafia tumboni na utaratibu wa maziko unafanywa, kwenye hicho kikao wewe hapo hata huwezi kuteuliwa kuwa hata mwenyekiti wa muda tu ili uendeshe kikao cha huo msiba.

Sasa mpaka hapo na kwa mujibu wa uchambuzi mwanana wa hapo juu, wana jukwaa wataamua wenyewe kati yenu watatu nani muhuni na nani sio muhuni.

Sidhani kama utanielewa ninachokimaanisha hapo juu na kama ikitokea ukanielewa sidhani kama utakuwa na hamu ya kuendelea kubaki kwenye hili jukwaa. Sidhani.
 
Usijifananishe na Mungu, yeye ana tusikilizia tu anajua Kuna hukumu yake inakuja ila mwanzo na yeye alikuwa anauwa na kuanza upya mfano sodoma na gomora, gharika la nuhu nk.
Sasa ww binadam uvumilie ujinga ambao unaona unaenda kiathiri na wengne kwa kigezo gani? Je una mda wa kuja ku-amend kama Mungu?

Tusipende kujifananisha na Mungu kwenye kila kitu ili hali approach zetu na zake ni tofauti
Kujifananisha na Mungu? Sijakuelewa.
 
Kujifananisha na Mungu? Sijakuelewa.
Kuna wimbo mmoja huwa nasikiaga dhehebu fulani wanaupenda sana; BWANA kama ungehesabu maovu yetu, nani angesimama?
Nilimaanisha hicho. Sio kwamba hahesabu bali anasamehe pale unapotubu na kuanza upya na atahukumu mwisho wa siku pale atakapo kukuta una madhambi yako
Swali; utafukuza na kuoa wangapi? Kwa njia ya waovu yaweza kuonekana jambo jema ila kwa Mungu ni machukizo.
Kuna mda uvumilivu wa baadhi ya tabia unaweza kusababisha ukajikuta unafanya machukizo zaidi kwa Mungu
 
Hi ipo kwenye kitabu gani? Basi sulemen,Daudi,ibrahimu baba wa imani alikuwa na wake 3,yacobo baba wa Israeli alioa mtu na dada take baadaye ya kuchunga miaka 14 na masulia 2...…Hiyo ya mke 1 Ni upuuzi tu wa kanisaaa
Mke moja inaua ufanisi na maboresho ya familia
 
Je, Donald Trump ni mtu wa namna gani na familia yake ikoje..!!??

Ukiangalia jinsi Trump alivyowalea watoto wake watano kwa kweli utashangaa sana na hii ndio maana hata jumuiya ya makanisa yenye nguvu na ushawishi mkubwa nchini Marekani ya Evangelical Christian Churches of America hupenda kumpigia debe sana kila anapogombea urais ili awe rais wao.

Popote pale duniani unapotaka uongozi watu hupenda sana kujua una familia ya namna gani na umeileaje hiyo familia yako kwa sababu jamii hupenda kuona una familia ambayo itawapa familia zao changamoto ya kuiga uzuri wanayoiona kwa familia yako.

Leo hii familia nyingi sana duniani zimekosa malezi mazuri toka kwa wazazi na jamii yote kwa ujumla na ndio maana leo hii dunia imejaa maovu mengi ya kutia huzuni tofauti kabisa na ilivyokuwa zamani.

Leo hii uhalifu umekuwa ni sehemu ya maisha yetu ya kila siku Ubadhirifu, Ufisadi, Utapeli, Uzinzi, Uwizi, Ujambazi, Ubakaji, Ushoga, Usagaji, Ugaidi, Umbeya, Unafiki, Udhulumati na mengine mengi ni sehemu ya maisha yetu ya kila siku.

Leo hii unakuta familia nyingi za watu wenye uwezo hazina kabisa maadili na unakuta zinawaona wenzao wa familia ambazo kidogo maisha ni changamoto kama takataka tu kitu ambacho ni matokeo tu ya malezi mabaya.

Kwa kweli ukiona Trump, pamoja na utajiri mkubwa alionao, alivyowalea watoto wake kwa imani ya kidini inakushawishi kwamba na wewe kuna kitu unaweza ukaifanyia familia yako na ikawa kama urithi wa maana kabisa katika maisha yao kuliko hata urithi wa mali na kwa kweli hapa hata sisi waafrika tuna changamoto kubwa sana kwa namna leo hii tunavyoshindwa kuwalea watoto wetu kimaadili.

Well done Mr. Trump for raising your offsprings in way that is a source of admiration and envy to all men and women of goodwill and may the people of your great country and the whole world at large borrow a leaf from your endeavours. Bravo Don.


View: https://youtube.com/shorts/Wo8KtX_BOg4?si=uAx3PllHSJ8Nb0Kd

Trump
 
Back
Top Bottom