Tuheshimu Katiba. Uchaguzi Mkuu ufanyike 2026

Tuheshimu Katiba. Uchaguzi Mkuu ufanyike 2026

Kwani Samia si alikuwa mgombea mwenza wa Magufuli?na walipoapishwa Magufuli kuwa Rais na Samia Makamu inamaana kipindi chao cha pili kilikuwa kiishe Oktoba 2025;baada ya Magufuli kufariki Samia anaapishwa kumalizia muda uliobaki wa Magufuli;sasa Machi 2026 umeitoa wapi?

Sasa kwa nini sa 100agombee tena wakati muda wao umeisha sa100 atakaa pembeni ccm tutapate mtu mwingine
 
.....Katiba imeweka bayana kuwa Rais ataacha Urais kwa (1) kufariki
(2) Kuumwa na kushindwa kutekeleza majukumu yake na (3) kwa kujiuzulu. Katiba haisemi kwamba Rais akipatwa na hayo matatu let's say ndani ya miaka minne basi atakayemrithi atamalizia awamu yake (marehemu)........

mkuu umesoma katiba ya nchi au unaongea sauti unazozisikia kichwani kwako?

Rais akifariki na ikawa kifo kimetokea ndani ya miaka 3+ kabla ya miaka yake 5 basi mrithi anaapishwa na anahudumu hiyo miaka 3+ iliyobaki kwa kuhesabika amehudumu muhula mzima. Baada ya hapo anaruhusiwa kugombea muhula mmoja kukamilisha awamu yake aliyoianza baada ya kumrithi marehemu

Iwapo rais amefariki na kubakiza muda chini ya miaka mitatu yaani -3 basi anayerithi kijiti anaruhusiwa kugombea mara mbili kwa sababu katiba inasema anamalizia muda mchache uliosalia ili aanze awamu yake uchaguzi unaofuata na atagombea mihula miwili.

Mlipokuwa mnamalizana na Mwendazake mlipaswa kuzingatia muda uliowekwa Kikatiba....
 
Hizo AWAMU zipo kwenye katiba? au ni vitu tu vya kujitungia, yaani hilo neno AWAMU limeandikwa kwenye katiba kuwa AWAMU ya kwanza itakuwa hivi na hivi na yapili .......
Mambo ya awamu ni miongozo ya ccm, ambayo hayawahusu WaTz wote. Katiba inaongelea kipindi cha miaka mitano, bila ya kujali aliyechaguliwa yu hai ama mbadala wake unamalizia hicho kipindi
 
Wajumbe, aliyekuwa Rais wa JMT Dk. John Pombe Magufuli alifariki tarehe 17/3/2021 hapo Mzena kisha Samia Suluhu Hassan kutangaza kifo chake saa 5:57 usiku "akiwa ziarani Tanga".

Baada ya hapo aliyekuwa Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan alitawazwa kuwa Rais wa JMT. Katiba yetu inaelekeza kuwa Rais atakuwa madarakani kwa miaka 5 (si minne wala sita) na kama atataka kugombea tena kwa awamu ya pili na ya mwisho basi ataomba ridhaa kwa chama chake.

Katiba imeweka bayana kuwa Rais ataacha Urais kwa (1) kufariki
(2) Kuumwa na kushindwa kutekeleza majukumu yake na (3) kwa kujiuzulu. Katiba haisemi kwamba Rais akipatwa na hayo matatu let's say ndani ya miaka minne basi atakayemrithi atamalizia awamu yake (marehemu).

Naamini hii ndiyo maana uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan umetambuliwa kama Awamu ya Sita na si ya Tano. Kama ni hivyo basi, tutakuwa hatujamtendea haki Rais Samia Suluhu Hassan endapo tutafanya uchaguzi Mkuu Oktoba mwakani Jumapili ya mwisho maana haitokidhi matakwa ya Katiba ya miaka mitano madarakani.

Kwa hiyo tuheshimu Katiba na haki ya Samia tufanye uchaguzi mwezi machi 2026 siku aliyoapishwa. Ova!
Mkuu;

Tafadhali kwanza, Kasome Katiba ya JMT ya mwaka 77, sura ya 2, sehemu yake ya 1, ibara ya 37 kufungu kidogo cha 5:

Ambacho kinazungumzia kumalizia awamu inayoendelea, kwa hapa Rais Samia anamalizia kipindi cha pili cha awamu ya 5! Kwa hapa sio awamu ya 6!

Pili, Kasome sura hiyo hiyo ya 2, ibara ya 40 kifungu kidogo cha 4 ambacho kina rejea ibara ya 37/5; Hapo, kinazungumzia ukomo wa awamu ya urais kwa Rais aliyepatikana kwa mujibu wa ibara ya 37/5:

Kwa hapa Rais Samia atachaguliwa kwa awamu moja tu maana mpaka mwaka wa 2025 atakuwa amehudumu kwa zaidi ya miaka 3 ya kipindi cha pili cha awamu Mwendazake!

Mkuu usipotoshe watu!
 
Huwezi kujificha, kosa la maudhui yanakuhusu. Kama hujui mabadiliko ya sheria ya mtandao hili unalo hata uwe Mbinguni tutakufikia ueleze maudhui Yako. Mwenzio aliyetumia ghost account humu Leo yuko Keko. Hauko salama udhaiavyo.
Usitishe watu
 
Samia aligombea Uwenza ili hatimaye aje kuwa Makamu wa Rais si Rais. Samia hamalizii Awamu ya Jiwe mbona hamuelewi? Kwa nini ni AWAMU YA SITA? JPM alitawala awamu ya ngapi?

Mbona kwenye kupiga kura kulikuwa na picha ya magufuri na samia ukiweka tiki kwa magufuri sawa ukiweka tiki kwa samia sawa saaa kwa nini asimalizie muda wa magufiuri halafu astaafu
 
Wajumbe, aliyekuwa Rais wa JMT Dk. John Pombe Magufuli alifariki tarehe 17/3/2021 hapo Mzena kisha Samia Suluhu Hassan kutangaza kifo chake saa 5:57 usiku "akiwa ziarani Tanga".

Baada ya hapo aliyekuwa Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan alitawazwa kuwa Rais wa JMT. Katiba yetu inaelekeza kuwa Rais atakuwa madarakani kwa miaka 5 (si minne wala sita) na kama atataka kugombea tena kwa awamu ya pili na ya mwisho basi ataomba ridhaa kwa chama chake.

Katiba imeweka bayana kuwa Rais ataacha Urais kwa (1) kufariki
(2) Kuumwa na kushindwa kutekeleza majukumu yake na (3) kwa kujiuzulu. Katiba haisemi kwamba Rais akipatwa na hayo matatu let's say ndani ya miaka minne basi atakayemrithi atamalizia awamu yake (marehemu).

Naamini hii ndiyo maana uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan umetambuliwa kama Awamu ya Sita na si ya Tano. Kama ni hivyo basi, tutakuwa hatujamtendea haki Rais Samia Suluhu Hassan endapo tutafanya uchaguzi Mkuu Oktoba mwakani Jumapili ya mwisho maana haitokidhi matakwa ya Katiba ya miaka mitano madarakani.

Kwa hiyo tuheshimu Katiba na haki ya Samia tufanye uchaguzi mwezi machi 2026 siku aliyoapishwa. Ova!
Hoja yako siipingi...unataka kusema hata wabunge na madiwani ukomo wao uwe 2026 au kutakuwa na chaguzi 2 ktk kipindi Cha mwaka 1..Endelea kusoma vizuri uelewe.!
 
Samia aligombea Uwenza ili hatimaye aje kuwa Makamu wa Rais si Rais. Samia hamalizii Awamu ya Jiwe mbona hamuelewi? Kwa nini ni AWAMU YA SITA? JPM alitawala awamu ya ngapi?
Wewe katiba huijui na hujui kwamba rais akifariki makamu wa rais anashika kiti cha rais?

Hiyo katiba unayoitajataja umeisoma?

Unaelewa mtu akiwa mgombea mwenza anakuwa makamu wa rais na makamu wa rais anakuwa rais wakati wowote rais akifariki?
 
Naamini hii ndiyo maana uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan umetambuliwa kama Awamu ya Sita na si ya Tano. Kama ni hivyo basi, tutakuwa hatujamtendea haki Rais Samia Suluhu Hassan endapo tutafanya uchaguzi Mkuu Oktoba mwakani Jumapili ya mwisho maana haitokidhi matakwa ya Katiba ya miaka mitano madarakani.
Alishasema kuwa Katiba sio Msaafu, so Acha kuamini upumbavu
 
Wewe katiba huijui na hujui kwamba rais akifariki makamu wa rais anashika kiti cha rais?

Hiyo katiba unayoitajataja umeisoma?

Unaeleea mtu akiwa mgombea mwenza anakuwa makamubwa rais na makamu wa rais anakuwa rais wakati wowote rais akifariki?
Hahahaha wakajipange upya kwa kweli
 
Hahahaha wakajipange upya kwa kweli
Mtu anatajataja katiba katiba, katiba katiba.

Hajaweka hata ibara moja anayoisema tuichambue.

Anakwambia katiba inabakwa.

Unamuuliza, inabakwa vipi, ibara gani?

Anakimbia hata hajibu.

Hata yeye mwenyewe hajui ibara gani anaiongelea, anakurupuka tu kwa hisia, inaonekana hata kuisoma hiyo katiba hajaisoma.
 
Wajumbe, aliyekuwa Rais wa JMT Dk. John Pombe Magufuli alifariki tarehe 17/3/2021 hapo Mzena kisha Samia Suluhu Hassan kutangaza kifo chake saa 5:57 usiku "akiwa ziarani Tanga".

Baada ya hapo aliyekuwa Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan alitawazwa kuwa Rais wa JMT. Katiba yetu inaelekeza kuwa Rais atakuwa madarakani kwa miaka 5 (si minne wala sita) na kama atataka kugombea tena kwa awamu ya pili na ya mwisho basi ataomba ridhaa kwa chama chake.

Katiba imeweka bayana kuwa Rais ataacha Urais kwa (1) kufariki
(2) Kuumwa na kushindwa kutekeleza majukumu yake na (3) kwa kujiuzulu. Katiba haisemi kwamba Rais akipatwa na hayo matatu let's say ndani ya miaka minne basi atakayemrithi atamalizia awamu yake (marehemu).

Naamini hii ndiyo maana uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan umetambuliwa kama Awamu ya Sita na si ya Tano. Kama ni hivyo basi, tutakuwa hatujamtendea haki Rais Samia Suluhu Hassan endapo tutafanya uchaguzi Mkuu Oktoba mwakani Jumapili ya mwisho maana haitokidhi matakwa ya Katiba ya miaka mitano madarakani.

Kwa hiyo tuheshimu Katiba na haki ya Samia tufanye uchaguzi mwezi machi 2026 siku aliyoapishwa. Ova!
Soma tena vizuri katiba kwa kuangazia ibara ya 40 kifungu kidogo cha 4.
Uchaguzi mkuu ni 2025 kwa mujibu wa kifungu hicho. Pia, Rais Dr Samia akigombea 2025 na kushinda, hataruhusiwa tena kikatiba kugombea.
 
Hutoumia kuelewa kwamba Samia anatawala awamu ya ngapi?

1000049215.png
1000049215.png
 
Back
Top Bottom