Tuheshimu Katiba. Uchaguzi Mkuu ufanyike 2026

Tuheshimu Katiba. Uchaguzi Mkuu ufanyike 2026

Mkuu kwa nini twende mzobe mzobe kubaka Katiba?
Makamu wa rais hapigiwi kura na anaweza kuteuliwa siku yoyote, kumbuka makamu wa rais alipofariki nchi haikuingia kwenye uchaguzi bali aliteuliwa mwingine kushika nafasi yake.
Achana na upindishaji wa katiba unaofanywa na CCM.
Makamu wa Rais anachaguliwa na wananchi au anateuliwa na kuthibitishwa na Bunge. Soma ibara hizi za katiba ya JMT 47(2) na 50(4).
 
RAIS SAMIA anaongoza awamu ya NGAPI? Kuna awamu ya miaka minne then mitano? Hivi lojiki yangu inaeleweka? Ya 2026?
Kwanza sioni uchaguzi ukifanyika endapo serikali na ccm yake wanaendelea kuweka pamba masikioni kuhusu mambo ya msingi yanayoibuliwa na wananchi kuhusu uchaguzi,

Anaweza kuachwa hata iyo 2027 ili hali watu waende kwenye uchaguzi wa kuwapata viongozi wao kwa kura halali na sio wiziwizi
 
Kwa kuangalia uzi huu, Watanzania wengi kama mtoa mada hawaelewi dhana ya "ticket".

Wanapiga kura kwa mtu, hawapigi kura kwa "ticket".
 
Samia aligombea Uwenza ili hatimaye aje kuwa Makamu wa Rais si Rais. Samia hamalizii Awamu ya Jiwe mbona hamuelewi? Kwa nini ni AWAMU YA SITA? JPM alitawala awamu ya ngapi?
Leta kifungu cha Katiba kinachoongelea namna ya kuhesabu awamu. Kisha tuendelee na mjadala
 
Wajumbe, aliyekuwa Rais wa JMT Dk. John Pombe Magufuli alifariki tarehe 17/3/2021 hapo Mzena kisha Samia Suluhu Hassan kutangaza kifo chake saa 5:57 usiku "akiwa ziarani Tanga".

Baada ya hapo aliyekuwa Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan alitawazwa kuwa Rais wa JMT. Katiba yetu inaelekeza kuwa Rais atakuwa madarakani kwa miaka 5 (si minne wala sita) na kama atataka kugombea tena kwa awamu ya pili na ya mwisho basi ataomba ridhaa kwa chama chake.

Katiba imeweka bayana kuwa Rais ataacha Urais kwa (1) kufariki
(2) Kuumwa na kushindwa kutekeleza majukumu yake na (3) kwa kujiuzulu. Katiba haisemi kwamba Rais akipatwa na hayo matatu let's say ndani ya miaka minne basi atakayemrithi atamalizia awamu yake (marehemu).

Naamini hii ndiyo maana uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan umetambuliwa kama Awamu ya Sita na si ya Tano. Kama ni hivyo basi, tutakuwa hatujamtendea haki Rais Samia Suluhu Hassan endapo tutafanya uchaguzi Mkuu Oktoba mwakani Jumapili ya mwisho maana haitokidhi matakwa ya Katiba ya miaka mitano madarakani.

Kwa hiyo tuheshimu Katiba na haki ya Samia tufanye uchaguzi mwezi machi 2026 siku aliyoapishwa. Ova!

Nyie ndio mnasababisha bangi inapigwa marufuku kwa huu utoto wenu.
 
Wajumbe, aliyekuwa Rais wa JMT Dk. John Pombe Magufuli alifariki tarehe 17/3/2021 hapo Mzena kisha Samia Suluhu Hassan kutangaza kifo chake saa 5:57 usiku "akiwa ziarani Tanga".

Baada ya hapo aliyekuwa Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan alitawazwa kuwa Rais wa JMT. Katiba yetu inaelekeza kuwa Rais atakuwa madarakani kwa miaka 5 (si minne wala sita) na kama atataka kugombea tena kwa awamu ya pili na ya mwisho basi ataomba ridhaa kwa chama chake.

Katiba imeweka bayana kuwa Rais ataacha Urais kwa (1) kufariki
(2) Kuumwa na kushindwa kutekeleza majukumu yake na (3) kwa kujiuzulu. Katiba haisemi kwamba Rais akipatwa na hayo matatu let's say ndani ya miaka minne basi atakayemrithi atamalizia awamu yake (marehemu).

Naamini hii ndiyo maana uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan umetambuliwa kama Awamu ya Sita na si ya Tano. Kama ni hivyo basi, tutakuwa hatujamtendea haki Rais Samia Suluhu Hassan endapo tutafanya uchaguzi Mkuu Oktoba mwakani Jumapili ya mwisho maana haitokidhi matakwa ya Katiba ya miaka mitano madarakani.

Kwa hiyo tuheshimu Katiba na haki ya Samia tufanye uchaguzi mwezi machi 2026 siku aliyoapishwa. Ova!
Eti nawewe unajiita msomi , waachien walio soma sheria jaman sio kila kitu ni cha kila mtu
 
Awamu imeandikwa wapi kwenye katiba?

Kwanza kabisa, tumalize mzozo wa Samia anaruhusiwa kugombea urais mara ngapi. Kwa kunukuu vifungu vya katiba.

Hii ibara ya 40 (4) ndiyo inamhusu Samia, rais aliyekuwa makamu wa rais awali na kuupata urais baada ya rais wa awali kufariki.

Nanukuu katiba

Ibara ya 40.

(4) Endapo Makamu wa Rais anashika kiti cha Rais kwa mujibu wa masharti ya ibara ya 37(5) kwa kipindi kinachopungua miaka mitatu ataruhusiwa kugombea nafasi ya Rais mara mbili , lakini kama akishika kiti cha urais Rais kwa muda wa miaka mitatu au zaidi ataruhusiwa kugombea nafasi ya Rais mara moja tu.

Mwisho wa kunukuu katiba.

Samia Machi mwaka huu atakuwa kashika urais kwa miaka mitatu. Hivyo hataruhusiwa kugombea urais mara mbili.

Hilo tumemaliza, kwa kifungu cha katiba.

Kwenye miaka ya uchaguzi.

Alivyouawa Karume April 7 1972, Aboud Jumbe Mwinyi alikuja kuchukua urais.

Urais wa Zanzibar ni miaka mitano.

Uchaguzi uliofuata ulikuwa mwaka gani? 1975 au 1977? Ulikuwa mwaka 1975. Hatukusema Aboud Jumbe aendelee kwa miaka mitano kutoka 1972 mpaka 1977.

Kwa nini? Kwa sababu urais ni taasisi, si mtu.

Huu mfumo wa mgombea mwenza katika katiba ya Tanzania tumeutoa Marekani.

Marekani rais anakaa madarakani kwa miaka minne.

Rais Kennedy alichaguliwa mwaka 1960, kipindi chake kilikuwa kinaisha mwaka 1964. Kennedy aliuawa mwaka 1963. Makamu wake Johnson akachukua urais mwaka 1963. Kwa nini Johnson hakupewa urais miaka minne 1963 mpaka 1967, na uchaguzi wa mwaka 1964 ukabaki pale pale?

Kwa sababu urais ni taasisi, si mtu.

Vivyo hivyo, Samia atarudi kwenye uchaguzi mwaka 2025, kwa mara ya mwisho. Akikubaliwa na kudumu kwenye kiti atakuwa rais mpaka 2030. Na huo utakuwa mwisho wa urais wake kwa katiba ya sasa.
Umeeleza vizuri isipokua hapo kwenye mfano wa Jumbe.
Wakati Jumbe anakua Rais wa Zanzibar 1972, Zanzibar haikua na katiba wala Uchaguzi mkuu.

Uchaguzi Mkuu wa kwanza wa Zanzibar ulifanyika 1980.
 
Kwani Samia si alikuwa mgombea mwenza wa Magufuli?na walipoapishwa Magufuli kuwa Rais na Samia Makamu inamaana kipindi chao cha pili kilikuwa kiishe Oktoba 2025;baada ya Magufuli kufariki Samia anaapishwa kumalizia muda uliobaki wa Magufuli;sasa Machi 2026 umeitoa wapi?
Kwahiyo Kwa comment Yako, sa100 ni Awamu ya Tano kipindi Cha pili.
 
Wajumbe, aliyekuwa Rais wa JMT Dk. John Pombe Magufuli alifariki tarehe 17/3/2021 hapo Mzena kisha Samia Suluhu Hassan kutangaza kifo chake saa 5:57 usiku "akiwa ziarani Tanga".

Baada ya hapo aliyekuwa Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan alitawazwa kuwa Rais wa JMT. Katiba yetu inaelekeza kuwa Rais atakuwa madarakani kwa miaka 5 (si minne wala sita) na kama atataka kugombea tena kwa awamu ya pili na ya mwisho basi ataomba ridhaa kwa chama chake.

Katiba imeweka bayana kuwa Rais ataacha Urais kwa (1) kufariki
(2) Kuumwa na kushindwa kutekeleza majukumu yake na (3) kwa kujiuzulu. Katiba haisemi kwamba Rais akipatwa na hayo matatu let's say ndani ya miaka minne basi atakayemrithi atamalizia awamu yake (marehemu).

Naamini hii ndiyo maana uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan umetambuliwa kama Awamu ya Sita na si ya Tano. Kama ni hivyo basi, tutakuwa hatujamtendea haki Rais Samia Suluhu Hassan endapo tutafanya uchaguzi Mkuu Oktoba mwakani Jumapili ya mwisho maana haitokidhi matakwa ya Katiba ya miaka mitano madarakani.

Kwa hiyo tuheshimu Katiba na haki ya Samia tufanye uchaguzi mwezi machi 2026 siku aliyoapishwa. Ova!
Katiba inahusu rais wa kuchaguliwa siyo wa kufiwa. Rais wa bahati mbaya huwa anamalizia kipindi kilichobaki hata kama ni masaa yamebaki nchi haiwezi kuwa bila rais. Sasa rais akifa imebaki mwezi mmoja anayemalizia akae miaka 5?
Wewe chawa mgonjwa kichwani.
 
Wajumbe, aliyekuwa Rais wa JMT Dk. John Pombe Magufuli alifariki tarehe 17/3/2021 hapo Mzena kisha Samia Suluhu Hassan kutangaza kifo chake saa 5:57 usiku "akiwa ziarani Tanga".

Baada ya hapo aliyekuwa Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan alitawazwa kuwa Rais wa JMT. Katiba yetu inaelekeza kuwa Rais atakuwa madarakani kwa miaka 5 (si minne wala sita) na kama atataka kugombea tena kwa awamu ya pili na ya mwisho basi ataomba ridhaa kwa chama chake.

Katiba imeweka bayana kuwa Rais ataacha Urais kwa (1) kufariki
(2) Kuumwa na kushindwa kutekeleza majukumu yake na (3) kwa kujiuzulu. Katiba haisemi kwamba Rais akipatwa na hayo matatu let's say ndani ya miaka minne basi atakayemrithi atamalizia awamu yake (marehemu).

Naamini hii ndiyo maana uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan umetambuliwa kama Awamu ya Sita na si ya Tano. Kama ni hivyo basi, tutakuwa hatujamtendea haki Rais Samia Suluhu Hassan endapo tutafanya uchaguzi Mkuu Oktoba mwakani Jumapili ya mwisho maana haitokidhi matakwa ya Katiba ya miaka mitano madarakani.

Kwa hiyo tuheshimu Katiba na haki ya Samia tufanye uchaguzi mwezi machi 2026 siku aliyoapishwa. Ova!
Tatizo la kuvamia fani za watu. Ndugu yangu waachie wenye uwezo wa kusoma, kuelewa na kutafasili kilichoandikwa ndani ya katiba. Usiendelee kujidhalilisha.
 
Kwa logic ya mtoa maada, nchi inaweza kwenda miaka hata 100 bila uchaguzi wa rais.

Siombei mtu afe, natoa mfano tu.

Magufuli kafa 2021, Samia Makamu wake achukue urais kwa miaka mitano mpaka 2026. Akae miaka mitano ya urais baada ya kifo cha Magufuli.

Bahati mbaya mwanzo hapo 2026 kabla miaka mitano haijafika, Samia naye kafa. Makamu wake Mpango anachukua nchi 2026 mpaka 2031 (bila uchaguzi). Anapewa miaka mitano yake.

2031 kabla Mpango hajafikisha miaka mitano ya urais wake, bahati mbaya sana Mpango naye kafa. Alikuwa kamchagua Makamu wake Makonda. Makonda anachukua urais mpaka 2036, bila uchaguzi.

2036 Makonda naye kapigwa na radi kafariki. Alikuwa kamchagua Makamu wake Sabaya. Sabaya anachukua urais mpaka 2041. Bila uchaguzi.

Nchi inaweza kuendelea hivyo hata miaka 100 bila uchaguzi.

Watu wenye werevu walishaona hilo ndiyo maana wakaweka miaka ya uchaguzi iwe fixed.
Kiranga ,Huo mlolongo uloweka Si Bure,

Magu to Samia

Samia to Mpango,

Mpango to konda,

Konda to Saba ya.


KATIBA mpya kabla ya Uchaguzi ni muhimu mno.
 
Umeeleza vizuri isipokua hapo kwenye mfano wa Jumbe.
Wakati Jumbe anakua Rais wa Zanzibar 1972, Zanzibar haikua na katiba wala Uchaguzi mkuu.

Uchaguzi Mkuu wa kwanza wa Zanzibar ulifanyika 1980.
Katiba zinajengwa kwenye kanuni za logic, hazitokei tu out of thin air.

Kwa hivyo, hata pale pasipo na katiba, kuna logic fulani inatumika kuamua uchaguzi wa rais uwe mwaka gani.

Hapo umeongezea nguvu point ya uchaguzi kufanyika kwenye miaka fixed.

Kwamba, hata pale pasipo na katiba, watu waliona umuhimu wa kuwa na miaka fixed ya uchaguzi, si kuamua uchaguzi kwa kuangalia urais wa mtu unaanzia wapi.

Hapa naona tatizo la siasa za Africa kuangalia watu badala ya sera na mfumo.

Kuna watu wanapenda sana siasa za kuangalia watu, badala ya kuangalia mfumo.
 
Back
Top Bottom