Tuhuma za JWTZ kupiga raia huko Kawe: Tunaomba Waziri wa Ulinzi ajitokezee kukemea, kulaani, na kukataza jeshi kujichukulia sheria mkononi

Siyo kaushamba,hawa ni washamba kabisa, nakumbuka miaka ya nyuma pale Mwenge kwenye magorofa waliyokuwa wanakaa hawa washamba walikuwa wanaweka mapazia ya viroba. Hawa walitakiwa wakae porini tu kwenye makambi yao.
😁😁😁 wewe wakikudaka wanakata hivyo vidole gumba vilivyo-type
 
I think nimekupata kwa namna fulani. Ila basi wajaribu kuwafundisha nidhamu na upendo wa dhati kwa raia.
 
Rais anayesifiwa kwa utendaji wa watu wa chini basi abebe lawama za uzembe wa watu wa chini pia
 
Kumbe kuna kichapo kilitembezwa kawe na hamsemi?
Watu wa dar, kina Maghayo ni wasiri sana
 
Nidhamu iatawekwa na kufuatwa.....
Kama itaachwa hivyo kwamba amemuua mwanajeshi na hajafanywa chochote...Kesho itakuwa wewe
Tatizo tunaloongelea hapa, sio kutaka kuachwa kwa aliefanya tukio. Tatizo ni ile aliefanya tukio ni mungine, na wanaopigwa na hao sojaz ni wengine ambao hawakuwepo na wengine hawakufahamu hata kilichokuwa kimetokea.

Lakini pia sheria zipo na mahakama pia zipo, hivyo wangeiachia polisi na mahakama wafanye kazi yao, na kama polisi wangeshindwa kumkakata basi hapo ndo wangeingia mtaani kumtafuta wenyewe na kisha kumfikisha katika vyombo vya sheria.

Lakin kumbuka kwamba siku hiyo kijana hakukusudia kuuwa mtu. Bali ni ajali iliyosababishwa na marehem mwenyew kwa kuziba njia ambayo ipo kwa ajili ya watu wote wenye vyombo vya usafiri na watembea kwa miguu kupita.

Mjeda alipoombwa kistarab apaki gari lake pemben ili jamaa apite na bajaj yake, ndo hapo mjeda alipoanza kumshambulia jamaa kwa maneno na kisha kumpa makofi kadhaa yaliosababisha hasira kwa kijana (hata wewe kupigwa mbele ya watu na mtu ambae ndio mwenye kosa, usingeweza kuvumilia), hivyo dogo akapandwa hasira na kuamua ku revenge kwa kutumia kisu cha mkunjo kilichosababisha umauti wa soja.

Kama soja angepaki gari yake mahali sahihi au kuamua kupaki pembeni kistaarab kama dogo alivyomuomba, yote hayo yasingetokea.

Hivyo binafsi sifurahishwi na uonevu au mauaji ya aina yoyote ile. Msimamo ni kwamba jeshi halikutakiwa kupiga watu hovyo kwa kosa la mtu mungine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…