Tujenge utamaduni wa kupendeza (kujipenda), kutoka out na kula vizuri

Tujenge utamaduni wa kupendeza (kujipenda), kutoka out na kula vizuri

La Quica

JF-Expert Member
Joined
Dec 19, 2017
Posts
1,009
Reaction score
2,315
Heri ya Pasaka.

Iko hivi, imekuwa kama tamaduni kwetu kuwa siku za sikukuu ndio mtu atavaa vizuri, atakula vizuri na atatoka out.

Jana wakati natoka kwenye mishe zangu nikamuita boda wangu anipeleke home nikaangalie chama langu Liverpool likimenyana na Arsenal.

Jamaa kafika asee alikuwa amevaa amependeza nguo mpya mpya (sio kawaida yake huwa sio msafi sana namtumia tu kwakuwa ni mwaminifu).

Jana yake usiku (juzi) alinipigia kuniomba nimtumie namba ya jamaa yangu ambae huwa ananiuzia kuku wa kienyeji. Akaniambia "bro naomba namba ya yule jamaa wa kuku nimeipoteza nataka home nao wale kuku hii sikukuu"

Sasa jana wakati ananipeleka home njiani ikawa kero kwa kuwa watoto wanakimbia kimbia hovyo barabarani na watu wazima wamejaa sio kawaida. Nikajua tu shida ni hii sikukuu.

Nadhani tuwe na utamaduni wa kujipenda, kula vizuri na kutoka mara kwa mara siku zisizo za sikukuu.

Mimi jana nimerudi zangu home nikala matunda yangu na kulala lakini hizi siku kuna watu wanazichukulia ndio siku za kulewa, kutoka, kufanya ngono na kuvaa vizuri jambo ambalo mimi naona sio sawa kabisa.

Hizi siku huwa ndio siku zenye vurugu nyingi. Ambae hajawahi kunywa atakunywa, wasiotoka watatoka kwahiyo kero ni nyingi. Lakini yote husabaishwa na utamaaduni mbovu kuwa siku za sikukuu ndio za kunywa, kutoka, kuvaa vizuri na kula kuku, nyama na pilau.

Sio sawa.
 
Asee boss unamuonea boda wivu😆😆😆 wacha watu wafanye venye roho zao zinapenda wengine wanakula vizuri tu ila sikukuu lazima panukie kwa sana. Wengine wamekusanya hela zao ili waenjoy siku kama hio tu ww ukiwapangia watoke kila siku hawana huo uwezo
 
Huu utamaduni ulianzia kwa wazazi wetu sasa kizazi kilichofuata na chenyewe kimechukua huo utaratibu wa kuifanya sikukuu kama ndio siku ya mtoko na kufanya mambo mengine ambayo yalikua hayafanyiki. Mfano siku yasikukuu ndio ilikua siku ya kupiga picha kwa sababu ndio ambayo mnavaa nguo mpya na mnakua mmependeza wote

Nguo za sikukuu
Vyombo vya wageni/siku ya sikukuu
Mapochopocho

Huo ni mfano mdogo lakini kadri siku zinaenda huu utamaduni unapotea kidogo kidogo
 
Kwanza ndio maana ikaitwa SIKU KUU, usipopendeza sikukuu na kula vizuri utafanya hayo siku gani?

Kumbuka kwenye sikukuu pia watu hutembeleana na kubadilishana zawadi na vyakula kiufupi ni siku ya kufurahii wewe muombe tu Mungu akuondolee upweke wako uwe na mtu/watu wa kufurahi nao Sikukuu.
 
......kuna watu wengine siku za za sikukuu ndo hawataki kabisa kufanya mitoko......wanasema zinakua zimekaa kishamba coz siku hizo utaona kila mtu kaenda disco, bar, beach etc.......wanasema ukienda huko na wewe unaonekana ni walewale wa sikukuu, wanasema hukawii kukutana na watoto maeneo hayo au hata watu usiowategemea kama vile mamamkwe na mashemeji zako.......Sasa hilo linawaboa wengi so huamua kushinda nyumbani na kuziacha familia au watoto ndo watoke, wao mitoko yao ni siku za kawaida au siku ya pili yake,boxing days, sasa sijui kama ni wengi wenye mtazamo huo au ni vipi.........
 
Huu utamaduni ulianzia kwa wazazi wetu sasa kizazi kilichofuata na chenyewe kimechukua huo utaratibu wa kuifanya sikukuu kama ndio siku ya mtoko na kufanya mambo mengine ambayo yalikua hayafanyiki. Mfano siku yasikukuu ndio ilikua siku ya kupiga picha kwa sababu ndio ambayo mnavaa nguo mpya na mnakua mmependeza wote

Nguo za sikukuu
Vyombo vya wageni/siku ya sikukuu
Mapochopocho

Huo ni mfano mdogo lakini kadri siku zinaenda huu utamaduni unapotea kidogo kidogo
Huo utamaduni hauwezi kupotea na kwanini upotee una shida gani?

Sikukuu ni furaha lazima watu wafurahi pamoja, Duniani kote Sikukuu huunganisha jamii pamoja.
 
Heri ya Pasaka.

Iko hivi, imekuwa kama tamaduni kwetu kuwa siku za sikukuu ndio mtu atavaa vizuri, atakula vizuri na atatoka out.

Jana wakati natoka kwenye mishe zangu nikamuita boda wangu anipeleke home nikaangalie chama langu Liverpool likimenyana na Arsenal.

Jamaa kafika asee alikuwa amevaa amependeza nguo mpya mpya (sio kawaida yake huwa sio msafi sana namtumia tu kwakuwa ni mwaminifu).

Jana yake usiku (juzi) alinipigia kuniomba nimtumie namba ya jamaa yangu ambae huwa ananiuzia kuku wa kienyeji. Akaniambia "bro naomba namba ya yule jamaa wa kuku nimeipoteza nataka home nao wale kuku hii sikukuu"

Sasa jana wakati ananipeleka home njiani ikawa kero kwa kuwa watoto wanakimbia kimbia hovyo barabarani na watu wazima wamejaa sio kawaida. Nikajua tu shida ni hii sikukuu.

Nadhani tuwe na utamaduni wa kujipenda, kula vizuri na kutoka mara kwa mara siku zisizo za sikukuu.

Mimi jana nimerudi zangu home nikala matunda yangu na kulala lakini hizi siku kuna watu wanazichukulia ndio siku za kulewa, kutoka, kufanya ngono na kuvaa vizuri jambo ambalo mimi naona sio sawa kabisa.

Hizi siku huwa ndio siku zenye vurugu nyingi. Ambae hajawahi kunywa atakunywa, wasiotoka watatoka kwahiyo kero ni nyingi. Lakini yote husabaishwa na utamaaduni mbovu kuwa siku za sikukuu ndio zakunywa, kutoka, kuvaa vizuri na kula kuku, nyama na pilau.

Sio sawa.
Apo naona tatizo ni kuona Boda kapendeza na Kala kuku wa kienyeji
 
Kila mtu afanye atakalo.

Mkuu una gubu sana kisa boda boda wako alipendeza kukuzidi na pilau kala kuku sikukuu wakati boss umeishia kula matunda
Shida sio hiyo. Mimi napendeza kila siku nimeshangaa huyu boda kwanini siku ya sikukuu tu ndio anajipenda na sio kila siku?
 
Huo utamaduni hauwezi kupotea na kwanini upotee una shida gani?

Sikukuu ni furaha lazima watu wafurahi pamoja, Duniani kote Sikukuu huunganisha jamii pamoja.
Sijasema utamaduni ni mbaya nadhani hapo umekurupuka. Kuhusu kubadilika ni kutokana na mabadiliko ya hali ya kimaisha hayo mambo upende usipende yatabadilika tu sijui kutunza vyombo kwa ajili ya wageni, kununua nguo za sikukuu wewe mwenyewe unajua hilo.

Mara ya mwisho kumnunulia mtoto wako nguo ya sikukuu ni lini?
 
Asee boss unamuonea boda wivu😆😆😆 wacha watu wafanye venye roho zao zinapenda wengine wanakula vizuri tu ila sikukuu lazima panukie kwa sana. Wengine wamekusanya hela zao ili waenjoy siku kama hio tu ww ukiwapangia watoke kila siku hawana huo uwezo
Kuna haja gani ya kuyokufurahia maisha mpaka siku fulani?
 
Back
Top Bottom