Tujifunze: Kipindi ambacho dini na imani zilianza kupoteza nguvu na kuanguka Ulaya

Tujifunze: Kipindi ambacho dini na imani zilianza kupoteza nguvu na kuanguka Ulaya

Baada ya kuanza kujitambua nlipata kujua mambo mengi na kwa urahisi kabisa.
Fikra zenye uhuru wa kutafakari na kuchanganua mambo.

Japo kwa jamii tunayoishi nayo inaweza isiyaelewe mawazo yangu kirahisi ila natamani siku wafikie hata 10% ya nkiwazacho mimi.

Tusiishi kwa kuridhika na majibu ya kiimani tuliyoyakuta.
Majibu ya kiimani ni ya zama za giza.
Mabadiliko makubwa huletwa kwa matumizi makubwa ya akili pasipo imani kuzingatiwa hii ni falsafa bora ya utatuzi wa changamoto.
 
Je, wafahamu ni kipindi gani hali ya kupoteza nguvu na kuanguka kwa dini ulaya kilianza miaka ipi na karne gani ?

Simple fact:
Tujifunze, wenda hali hii ya sasa ya mataifa mengi ya ulaya kuteteleka katika mambo ya imani na dini yakushanganza na kujenga maswali mengi katika ufahamu wako kuhusu sababu nini na lini hali hii ilianza.

AGE OF REASON
Hiki ndicho kipindi ulaya ili shuhudia mabadiliko makubwa ya kiimani pia kiutawala.

Kipi hiki imani na dini zilipitia wakati mgumu uliopelekea kuanguka kwa kiasi kikubwa katika mataifa mbalimbali ya ulaya tofauti na nguvu iliyokuwa nayo mwanzo

Kipindi hiki kilianza mwanzo mwa karne ya 17 kwenda karne ya 18. Kipindi hiki kilisisitiza matumizi ya akili katika kuchambua masuala ya kidini na kuepesha matumizi ya Imani kwa kiwango kikubwa.

Hiki ndicho kipindi sayansi na utumizi wa falsafa ulichipukia kwa kasi sana ndani ya ulaya. Sayansi na falsafa za kimaisha ziliathiri dini na imani kwa kiwango kikubwa ulaya.

Mapinduzi ya sayansi na teknolojia na uhuru binafsi ulichukua nafasi kubwa kipindi hiki, wanasayansi wengi wakubwa ulaya na duniani walianza kuonekana katika kipindi hiki.
Somo fupi la leo.
Renaissance (Rebirth of culture)
 
Kwa wenzetu wamepitia kipindi Cha kuchambua "faith and reason" Africa vipi?
Kwa kuielezea Afrika tokana na uelewa wangu mfupi kuhusu Afrika. Bado Afrika yakabiliwa na changamoto lukuki za kushindwa kuweka ukuta kati ya matumizi ya imani na akili katika uamuzi na utatuzi wa changamoto
 
Huku Africa sehemu nyingi watu wanaogelea kwenye uchawiuchawi bado.

Hata wasomi bado wana imani hizo.

Mtu ana internet halafu anaamini uchawi.

Tuko nyuma miaka kama 300 kama si zaidi.
Na wanazidi kurudi nyuma tu
 
Kwa kuielezea Afrika tokana na uelewa wangu mfupi kuhusu Afrika. Bado Afrika yakabiliwa na changamoto lukuki za kushindwa kuweka ukuta kati ya matumizi ya imani na akili katika uamuzi na utatuzi wa changamoto
Matumizi ya Imani na akili still bado Sio kwa kiwango kikubwa pia zaidi ya kujiendea tu pasipo vyote hivyo
 
  • Thanks
Reactions: TPP
Sayansi na technology zimewaumbua sana hawa watu wa dini.
Tena haswa imani iliyojengwa kwenye quran.
Quran inamakosa ya wazi kabisa ya geography.
Lakini cha ajabu pamoja na kujinasibu kuwa vitabu vyao vinajitosheleza kabisa ukionesha makosa hayo mtu anakuja na maelezo mengine ya wanazuoni kuongezea hapo.

Wakati mimi natarajia kuwa kitabu kinachojitosheleza hakihitaji maelezo mbadala. Yaani nkisoma tu nielewe.

Sasa watu wanataka kuilinda imani yao kwa nguvu zote.
Hili ni tatzo kubwa.

Imani ni shambulio la akili.
Cha ajabu hii mada wazi wazi inakwepa Rise of Islam ni Europe, hata ukitoa factor ya Migration Uisilamu unakuwa kwa Kasi, pewpewresearch inaonesha by 2050 waisilamu watakuwa 11% ya Ulaya, sababu ya Migration, ila wakaendelea hata Bila Migration Uisilamu utakua 7%.

Zamani miaka 200 ama 300 iliopita Ngumu kukuta Sheikh mzungu, ila sasa hivi Kuna wasomi kibao wa kiisilamu wanaoheshimika Dunia nzima wazungu, kama Sheikh Hamza Yusuf, Abdul hakim Murad, Daniel Haqiqatou, Hamza Tzortis etc.

Na Uisilamu sio illogical, ndio dini pekee unayoweza Kusimama na Atheist na kumpiga ko. Kaangalie Debate Baina ya Hamza Tzortis na professor Lawrence Krauss ambaye ni well known Antitheist kundi moja na Kina Dawkin

 
Cha ajabu hii mada wazi wazi inakwepa Rise of Islam ni Europe
Uanzishwaji wa hili somo fupi si kwa makusudio ya kutokutambua uingiaji wa imani ya dini kiislamu katika himaya ya ulaya hapana lengo ni sote kuelemika kuhusu kipindi cha kuhoji au zama za mwanga ( Age of reason or Enlightenment )

Hivyo si sahihi kuhusisha hili somo na kupinga usambaaji wa dini ya kiislamu mahali popote pale sote twapasa kutambua hilo ili fikra zetu zisiwe na ukwamo mahali popote katika kuchambua jambo hili.

Age of reason haina mahusiano ya moja kwa moja na uwepo wa imani ya dini ya kiislamu katika himaya ya ulaya
 
Uanzishwaji wa hili somo fupi si kwa makusudio ya kutokutambua uingiaji wa imani ya dini kiislamu katika himaya ya ulaya hapana lengo ni sote kuelemika kuhusu kipindi cha kuhoji au zama za mwanga ( Age of reason or Enlightenment )

Hivyo si sahihi kuhusisha hili somo na kupinga usambaaji wa dini ya kiislamu mahali popote pale sote twapasa kutambua hilo ili fikra zetu zisiwe na ukwamo mahali popote katika kuchambua jambo hili.

Age of reason haina mahusiano ya moja kwa moja na uwepo wa imani ya dini ya kiislamu katika himaya ya ulaya
TUJIFUNZE: KIPINDI AMBACHO DINI NA IMANI ZILIANZA KUPOTEZA NGUVU NA KUANGUKA ULAYA

Hio ndio Heading yako, kinachoendelea Ulaya ni dini moja inaanguka na nyengine inakuja, so Uisilamu una fill gape lililoachwa na Wakristo. Hivyo kutumia hoja ya Ukristo Kupungua as if Dini inapungua na ku ignore Uisilamu huoni kama si sahihi?
 
TUJIFUNZE: KIPINDI AMBACHO DINI NA IMANI ZILIANZA KUPOTEZA NGUVU NA KUANGUKA ULAYA

Hio ndio Heading yako, kinachoendelea Ulaya ni dini moja inaanguka na nyengine inakuja, so Uisilamu una fill gape lililoachwa na Wakristo. Hivyo kutumia hoja ya Ukristo Kupungua as if Dini inapungua na ku ignore Uisilamu huoni kama si sahihi?
Umesoma na kuelewa vyema title na kilichomo ndani ?

Ukiweka umakini utatambua kuwa title yakusudia kuzungumzia kipindi na kilichomo ndani ndicho hicho kipindi kilicho zungumwa nacho ni Age of reason. Je, ni jambo gani lakutatiza hapo ?

Wewe ni muislam ? Na je, waona somo hili lawatenga na kutowazungumzia waislam na imani yao ? na uwasambaaji wake ?
 
Umesoma na kuelewa vyema title na kilichomo ndani ?

Ukiweka umakini utatambua kuwa title yakusudia kuzungumzia kipindi na kilichomo ndani ndicho hicho kipindi kilicho zungumwa nacho ni Age of reason. Je, ni jambo gani lakutatiza hapo ?

Wewe ni muislam ? Na je, waona somo hili lawatenga na kutowazungumzia waislam na imani yao ? na uwasambaaji wake ?
Kipindi hicho hicho na Uisilamu nao ukaanza kuenea. Kwenda kwa Sayansi na Technology ulaya kunaenda sambamba na Uisilamu.

Scientist wengi wa Mwanzo walikua Middle East,

Ukiangalia Scientist wa Mwanzo mwanzo Ulaya kama Galileo utakuta vitabu vyao Citation zao wanafanya kwa Scientist wa Middle East.

Hivyo hiyo unayoita Age of Reason nayo pia ni cheche za kueneza Dini nyengine.
 
TUJIFUNZE: KIPINDI AMBACHO DINI NA IMANI ZILIANZA KUPOTEZA NGUVU NA KUANGUKA ULAYA

Hio ndio Heading yako, kinachoendelea Ulaya ni dini moja inaanguka na nyengine inakuja, so Uisilamu una fill gape lililoachwa na Wakristo. Hivyo kutumia hoja ya Ukristo Kupungua as if Dini inapungua na ku ignore Uisilamu huoni kama si sahihi?
Unachanganya madesa, ulaya watu kuona dini ni magumashi si kwamba wanasilimu kutoka Ukristo kwenda Uislamu.

Tena mtu ambaye anaona Ukristo ni magumashi tu mtu huyo hawezi kuwa muislamu Kamwe.
 
Kipindi hicho hicho na Uisilamu nao ukaanza kuenea. Kwenda kwa Sayansi na Technology ulaya kunaenda sambamba na Uisilamu.

Scientist wengi wa Mwanzo walikua Middle East,

Ukiangalia Scientist wa Mwanzo mwanzo Ulaya kama Galileo utakuta vitabu vyao Citation zao wanafanya kwa Scientist wa Middle East.

Hivyo hiyo unayoita Age of Reason nayo pia ni cheche za kueneza Dini nyengine.
Unajaribu kulazimisha imani ya kiislamu ifungamane na age of reason kwa hili haupo sahihi kwa asilimia zozote zile.

Age of reason ilikuwa mbali kabisa na imani ya aina yoyote ile na ilipinga imani kutawala fikra za watu kuliko matumizi ya akili na kufikiri kwa kina.

Unaweza tafuta namna bora zaidi kuelezea historia ya uislam kuingia katika himaya ya ulaya bila kuhusisha Age of reason iliokuwa kinyume na hio hio imani.
 
Kundi kubwa la watu wakisha Acha kutegemea imani fulani wanaanza kufanikiwa , Din zinadumaza akili sana na story zake za kujifariji fariji zinafanya bongo zinategea viumbe wengne .
 
Baada ya kuanza kujitambua nilipata kujua mambo mengi na kwa urahisi kabisa.
Fikra zenye uhuru wa kutafakari na kuchanganua mambo.

Japo kwa jamii tunayoishi nayo inaweza isiyaelewe mawazo yangu kirahisi ila natamani siku wafikie hata 10% ya nkiwazacho mimi.

Tusiishi kwa kuridhika na majibu ya kiimani tuliyoyakuta.
Majibu ya kiimani ni ya zama za giza.
Mkuu umeongea ukweli kabsa katikati ya kundi kubwa la watu waliolala usingizi .
 
Mwafrika ananiacha hoi, "eti namuachia Mungu" unadundwa unasema namuachia Mungu!! Tumia akili, nawe mjibu mara mbili ashike adabu.
 
Dunia ipo the reasoning age, Afrika bado ipo age ya kuamini kama nyumbu bila kutumia ubongo. Kila kitu wao ni imani tu. Imani zenyewe hazimake any sense whatsoever.
 
Back
Top Bottom