Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Nakumbuka enzi hizo kipindi cha mama na mwana cha Debora Mwenda watoto tulikuwa hatukosi. nakumbuka Jumamosi mchana wakati kipindi kipo hewani watoto mmejikusanya wenyewe kwenye radio mbao yenu kunasa hadithi (ua jekundu) ili jumatatu ukaisimulie darasani.
Watoto wa siku hizi sijui hata kama huwa wanasimuliana hadithi huko mashuleni jamani.

Uzuri wa kipindihicho ni kwamba tulikuwa tunafahamu kwamba kikiisha tu yatafuata matangazo ya mpira saa kumi.

Tulikuwa na wakti mzuri sana wa kuburudika, je pamoja na Ua Jekundu, unakumbuka Jadi Mbaharia, Mbaramwezi Nyota begani
na Binti Chura.

Huwezi jua mtu anaweza kutengeneza Filamu hivihivi.
 
Hivi wakulu, Florian Kaiza na Suleiman Kumchaya pia wapo au wamestaafu kazi?

Florian Kaiza alikuwa kisoma taarifa zote za habari za kiingereza na kiswahili. Suleiman Kuchaya pia alikuwa akisoma taarifa za habari.

Walikuwa wakizisoma taarifa zile kwa uhakika na kwa umakini.

Baada ya hapo mzee Salum Seif Mkamba nae akawa anakuja na yake kwenye mazungumzo baada ya habari.

Lakini enzi zile kulikuwa hakuna vituo vingi vya luninga wala redio nchini na dozi za RTD zilikuwa zikitosha kutuliwaza.
 
Hivi wakulu, Florian Kaiza na Suleiman Kumchaya pia wapo au wamestaafu kazi?

.

Kama sikosei, aliendaga (hiki ni kiswahili fasaha??) Idhaa ya Kiswahili ya Radio Japan. Sijui yupo wapi sasa hivi
 
Khalid Ponera - Zilipendwa
Godfrey Mngodo- taarifa ya habari
Chrstopher George- taarifa ya habari
Elly Mboto
Maria Ulimwengu- Your reuest= External service
Mikidadi Mahamood (Brother Miki)
Alex Malumwene
 
Mi namkumbuka Athman Mzigo, maarufu alikuwa kwa usomaji wa taarifa za habari, sauti nzito nzito ,ikikata mawimbi..

Basi, sabasaba iliyopita , nikaenda banda la TBC nikitamani kupata vibwagizo vya zamani, kama ubepari ni unyama, zile jingles kinapotaka kuanza kipindi cha majira , au mahokaa....... , basi nikauliza je naweza kupata michezo ya redio ya akina Havijawa - Mkataa pema pabaya panamwita.. Oh oh huwezi kuamini, wale mabraza men, eti wako marketing ya TBC , wakawa hawajui chochote hata habari hawana, juu ya hizo jingles , vipindi nk.nk .....

Kweli nitaikumbuka Radio Tanzania, walipoiita TBC kila kitu kilipoteza muelekeo....
 
Take a break, na tujikumbushe enzi zile za RTD, ambapo kulikuwa hakuna FMs rado kama sasa. Hakika kulikuwa na watangazaji, vipindi bomba na hata nyimbo za kutambulisha vipindi zilikuwa makini sana. Hebu ngoja niwakumbushe baadhi ya watangazaji wa wakati huo.

1. Nassoro Nsekeli- alikuwa na sauti kama ya mafua hivi alikuwa mtaalamu wa kipindi cha Majira- ndiye aliyetangaza kifo cha Nico Zengekala

2. Bujago Izengo wa Kadago- Kibesi chake kilikuwa safi sana

3. David Wakati (DG) - kipindi cha Nipe habari- Kwaherini wote, mungu awalinde na mmbaki salama, mungu akipenda..............

4, Khalid Ponera- Zilipendwa

5. Ahmed Kipozi- taarifa ya habari

6. Hassan Mkumba- matangazo ya vifo

7. Siwatu Luwanda

8. Salama Mfamao
9. Mohamed Amani (Mohamed Dahman)

10. Salim Seif Nkamba

12. CHisunga Steven- kipindi cha Ugua pole duu

13. Bathoromeo KOmbwa (bati Kombwa) - WAkati wa Kazi

14. Ahmed Jongo- Mpira

15. Christina Chokunogela

16. Dominic Chilambo- Mpira

17. Edda Sanga
18. Debora Mwenda- Mama na Mwana
19. Aloycea Maneno- Ombi lako, cheichei Shangazi, mama na mwana

Duu nawamiss sana hawa watu tofauti na watangazaji wa sasa

Tumemsaha MSHINDO MKEYENGE - aliyekuwa katibu mwenezi wa Yanga enzi hizo
 
Sechelela Balisidya nae alikuwa nani jamani? Jina hilo lilikuwa likitajwa mara kwa mara. Au alikuwa fundi mitambo?
 
Yule wa klab raha leo showwwwwwwww aliitwa nani vile nimesahau!.
 
Hivi mmeshawataja Juma Ngondae na Iddi Rashid Mchata? NaVipindi pia vilikuwa na mashiko sio kama hivi vya leo.
 
Sango Tuo (Mrs Kipozi)
Rose Japhet
Abdul Ngarawa
Irine Msemembo
Julius Nyaisanga (uncle J) pia walikuwepo
 
Bila kumsahau Michael Katembo na kipindi chake cha Asilia Salaam, Tumbuizo asilia na Mkoa kwa mkoa. Jamaa nilikuwa namfill kichizi maana kila mwisho wa ngoma utasikia naye anaimba au anapiga mruzi. Katembooooooooooo.....
 
Nikipindi cha pili cha pili hapa wao sifuri sisi moja na utamsikia tukifungwa timu ya taifa alikuwa hata hasemi goooooooooooo utasikia washatufunga. namna gani hapa jamaa alitakiwa kutumia hata ulimi kuweka ule mpira kimiani. Ahmedi Kampira na mpira lalalalalalalalalaaaaa ah namna gani Juma Mgunda anashindwa kuona milingoti mitatu hapa.
Kwenye maguu kumi nane ana weka mpira ule Edward Chumila na na simba wanafanya mabadiliko namuona kocha mchezaji anaingia hapa heeeee he Chumila kwa guu lake la kushoto anapiga mpira ule anaingiza majalo moja pale ile inaitwa banana chop gooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooo a namna gani hapa mpira unagonga mtambaaaaa panya wasikilizaji ..................... nikikumbuka enzi hizo sipati jibu
 
Hamza kasongo - alitangaza uhuru wa Tanganyika, 1961. Sasa ana kipindi channel 10?
 
Mi nakumbuka taarifa ya habari ikianza tu ile kusikia sauti ya mtangazaji tunaanza kukisia jina lake kabla hajajitambulisha. Yaani ilikuwa kama mchezo fulani hivi burudani tupu enzi hizo.
 
Hamza kasongo - alitangaza uhuru wa Tanganyika, 1961. Sasa ana kipindi channel 10?
hivi hii imekumbukwa kweli kuwekwa kwenye historia? Nasoma mara nyingi ya alipandisha bendera juu ya mlima tu.
 
Baada ya kumaliza na ngwe ya Sumaye kama Press Sec.wake, alirudishwa Maelezo briefly, then amepelekwa wizara ya Habari, nadhari kusubiri kustaafu kwa heshima.
Amestaafu mwaka jana yupo nymbani kwake Msewe anakula bata
 
Back
Top Bottom