Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Siku hizi redio zimekuwa fujo tupu vipindi vyafanana na hujui usikilize redio ipi ilimradi tu tafran,na redio nyingi wanahusudu miziki
Halafu ni special kwa wenye ving'amuzi.Minara ya mawasiliano ime-haribu.Vijijini wenye uwezo mdogo mf wasio na umeme hawapati lolote.Mambo yamebadilika sana. Maisha ni mchaka mchaka[emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125]
 
Mie naona RTD ilibamba AFRICA MASHARIKI kwa umakini na ratiba nzuri za utangazaji.
 
RATIBA ZA UTANGAZAJI NA VIPINDI VYA WAKATI ULE VILI REFLECT MAISHA HALISI YA ZAMA HIZO. KUMBUKENI WIMBO WA MWANAMEKA MPIGAJI AMENITOKA KIDOGO ULIINGIA KWENYE SYLABUS YA KISWAHILI O-LEVEL.
 
Kusema za ukweli siku hizi hakuna watangazaji bali kuna waropokaji na wapiga domo huko studio.......baada ya kuelimika kupitia vyombo vya habari jamii ndio kwanza inahiribiwa........hakuna kipindi chenye manufaa kwenye jamii zaidi ya kuitangaza zinaa na matendo ya ngono.......
Matukio ya wasanii kufanya ngono ndio yanayopewa kipaumbele kuliko matukio mengi ya msingi yanayozinguka jamii zetu.....

Mtangazaji ukimuona mtaani mpaka unashindwa kumtofautisha na watumiaji wa mihadarati kwa jinsi alivyo na muonekano mbaya.....
 

Duh....wee mkali..... umeukumbuka hadi wimbo wa sakina?
Nimesoma maneno tu sauti ikaja....Big up...you made my morning
 
Jumapili saa nane mchana ilikuwaga ni kipindi cha MAMA NA MWANA.

Ilikuwa ni siku ya jumamosi na mama Debora Mwenda akiwa hayupo basi Aleicia Maneno anasimamia kipindi. tulikuwa na club za mama na mwana mashuleni, mkiandika barua yenu siku hiyo ikasomwa kwenye kipindi manajiona niendio nie...lol tumetoka mbali
 
Ilikuwa ni siku ya jumamosi na mama Debora Mwenda akiwa hayupo basi Aleicia Maneno anasimamia kipindi. tulikuwa na club za mama na mwana mashuleni, mkiandika barua yenu siku hiyo ikasomwa kwenye kipindi manajiona niendio nie...lol tumetoka mbali
Nakumbuka mwaka 1983 nikiwa std 7 nikiandika barua yangu kwenye kipindi cha mama na mwana kisha ikasomwa daa kijijini kwetu nilizua ujikooo! niliwachorea zawadi ya bata teh teh teh!![emoji122] [emoji122] [emoji122] [emoji122]
 
radio csssete maarufu enzi hizo ilikuwa ni memory Q!!

Your correct. Nakumbuka nilivyunja mlango wa redio upande wa kuwekea kanda......niliweka kanda, kumbe haijakaa vizuri mie nikang'ang'aniza kufunga mlango, kutahamaki mlango umevunjika, kipigo nilichokipata kutoka kwa mother sitakaa nisahau
 
kipindi hiki ndio hamjataja "mashairi" msomaji Athuman Khalfan saa nane nane mchana!
 

kulikua na idhaa ya biashara, idhaa ya Taifa na external service. hakuna cha zaidi. Jumapili watoto wa geti kali lazima tusikilize "At your request"
watuma salamu kwenye kipindi hiki ni kutoka Oysterbay, Upanga na Chang'ombe kidogo. Uswahili wanatoka Magomeni mikumi.
Namkumbuka sana Jacob Tesha, na sauti yake. Sauti yako ndio qualification yako ya kutangaza radio, vinginevyo unakua fundi mitambo. Kama hujui kutofautisha L na R au H na A, kutangaza radio sahau. Mwenye lafudhi ya kabila lake pia sahau, fanya kwenye mitambo kule, usiharibu shughuli. Ilikua raha sana. Siku hizi hata hamu ya kusikiliza ina bore hasa ukikutana na mtangazaji asiyejua kutofautisha R na L au A na H
 
RATIBA ZA UTANGAZAJI NA VIPINDI VYA WAKATI ULE VILI REFLECT MAISHA HALISI YA ZAMA HIZO. KUMBUKENI WIMBO WA MWANAMEKA MPIGAJI AMENITOKA KIDOGO ULIINGIA KWENYE SYLABUS YA KISWAHILI O-LEVEL.

wimbo wa Marijani Rajab huo
 
Kwa kweli nilikuwa mtoto lakini kuna kipindi cha maigizo cha akina mzee jangala ambapo kuna sauti ilikuwa ikisikika "ung'waaa anhaaa haa dukudukuuu msondo ngoma"
 
1.Michezo na Abdul Omar Masoud na Juma Ngondae
2.Club Raha Leo show na Brother Enock Ngombare
3.Usiku wa Raha na Debora Mwenda/Halima Mchuka
4.Malimwengu
5.Mazungumzo baada ya habari na Salum Seif Mkamba
6.Majira na Mshindo Mkeyenge
7. From me to You (External service)
 
Mazungumzo baada ya habari pamoja na maneno hayoooooo


Hali kadhalika ujumbe wa leo, "......waswahili wa Darisalama wananambia Mwl hatuna pesa, najiuliza pesa nizitoe wapi kama hatutaki kufanya kazi......"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…