Tujuzane na kushauriana ipi gesi bora kwa matumizi ya nyumbani

And that's my sweetheart mwasu...nitainunua mpenzi.
Tena ngoja nianze kutafuta inapopatikana maeneo karibu na hapa ili hii Mihan ikiisha tu nikaichukue fastaaaa.
[emoji39][emoji39][emoji39]
Nitakupa mrejesho dear.
 
Tatizo umeongelea kitaalamu sana mkuu.
Hayo yote naona nyotanyota tu...
Aaarrrggghhh [emoji13][emoji13][emoji13]
 
Kama unamjua mtu anaefanya kazi TPDC
waulize
wana gesi yao ya mtwara nafuu kuliko zote na safe
wafanyakazi wao hasa wanaoishi nyumba za TPDC mikocheni wanaitumia
Aiseeeee naona unataka kunishawishi lakini upatikanaji wake ukoje mkuu?
Maana gas inaweza kuninogea itakapoisha kama ni adimu kitakuwa kimbembe.
Maana nishati kuu niitumiayo ni gas,na ikiisha siwezi kupitisha siku sijanunua tena maana ni shida tupu.
Kama unamjua hata mmoja niunganishe nae pls.

Au kama kuna mfanyakazi wa TPDC aliyeko humu anicheki PM jama [emoji120] ...
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Leo siku yangu imekuwa nzuri sana,I love JF!

Halafu kweli...uzuri sijawahi kuishiwa katikati ya upishi.
Nitaja adhirika hivihivi!
Bora mboga au chochote kile lakini sio ugali...nitafeli.
Huwa ikitaka kuisha naistukia mapema nanunua kabisa wa emergence maana unaweza kuumbuka walah!

Aisee nami nimeshawishika na Manjis, hii ikiisha najaribu Manjis.
 

Pale ubungo linapoishia treni wana kituo chao
anzia hapoo kuuliza
watu wa TPDC kama wanafanya siri
ila Sea Cliff hotel nimesikia pia wanatumia hiyo gas kupikia
 
Huwa ikitaka kuisha naistukia mapema nanunua kabisa wa emergence maana unaweza kuumbuka walah!

Aisee nami nimeshawishika na Manjis, hii ikiisha najaribu Manjis.
Kweli wewe mzoefu,mimi huwa nashtuka imeshapungua nikiitumia kidogo tu inaisha.
Nakimbiaje sasa?

Mwenzangu tuhamie Manjis...japo namsikiliza The Boss hapa naweza kujaribu huko.
 
Pale ubungo linapoishia treni wana kituo chao
anzia hapoo kuuliza
watu wa TPDC kama wanafanya siri
ila Sea Cliff hotel nimesikia pia wanatumia hiyo gas kupikia
Yarabiiiiiii itabidi nipande treni nikawatafute...nitakupa mrejesho mkuu.

Au wapo kwenye majaribio nini?Mbona wanafanya siri?
Hiyo inaonekana itakuwa nzuri.
Maana kibongobongo wakishaanza kupata jina na wateja wengi wanaanza kuchakachua.
 
Kweli wewe mzoefu,mimi huwa nashtuka imeshapungua nikiitumia kidogo tu inaisha.
Nakimbiaje sasa?

Mwenzangu tuhamie Manjis...japo namsikiliza The Boss hapa naweza kujaribu huko.
Huko kwa mtwara khaaaah!! Wanauziana kiukoo au!!
 
Yarabiiiiiii itabidi nipande treni nikawatafute...nitakupa mrejesho mkuu.

Au wapo kwenye majaribio nini?Mbona wanafanya siri?
Hiyo inaonekana itakuwa nzuri.
Maana kibongobongo wakishaanza kupata jina na wateja wengi wanaanza kuchakachua.

Wewe nenda watu 'wanafaidi kimyakimya'
nasikia inauzwa kilo sh 600 ...wafanyakazi wa TPDC hadi magari yao wameyabadilli
wanatumia hiyo gesi
wanatu enjoy tu sisi wengine

mimi kila siku nasema ntaenda huko nasahau
ukienda wewe utanipa feedback
 
Wewe nenda watu 'wanafaidi kimyakimya'
nasikia inauzwa kilo sh 600 ...wafanyakazi wa TPDC hadi magari yao wameyabadilli
wanatumia hiyo gesi
wanatu enjoy tu sisi wengine

mimi kila siku nasema ntaenda huko nasahau
ukienda wewe utanipa feedback
Mkuu The Boss acha masikhara bwana...
Kwahiyo mtungi wa kg 15 kuujaza ni 9,000?
Sasa kununua mpya (complete) si utakuwa 20,000 jamani?
Uwiiiiii hebu ngoja niende nikacheki mie.
Hii sijawahi kuisikia kokote!
 
Mkuu The Boss acha masikhara bwana...
Kwahiyo mtungi wa kg 15 kuujaza ni 9,000?
Sasa kununua mpya (complete) si utakuwa 20,000 jamani?
Uwiiiiii hebu ngoja niende nikacheki mie.
Hii sijawahi kuisikia kokote!

Wewe nenda halafu unipe feedback
ukiteremka na treni fuata tu zile reli hadi zinapoanza
kuingia barabarani utaona petrol station
na ina kibao kabisa kituo cha kujaza gesi
ukifika hapo uliza halafu uniambie PM
labda wapandishe tu kiubishi
sababu project ilikuwa ya majaribio kabla haijasambaza kwa wanancho wote
but siku niliyouliza mimi niliambiwa yeyote anaruhusiwa kununua...
 
Usijali mkuu,nitakwenda.
Kesho ratiba yangu hairuhusu...keshokutwa ndio nitalifanyia kazi hilo.

Asante kwa kushare nasi...nitakujuza bila shaka.
 
Huku ni Orxy,Mihan,O gas na Lake.
Nyingine ni adimu sana.

Sasa sijui nifanyeje na Manji's ndio hasa lengo langu kwa sasa.

Duh,pole sana mkuu.
Mkuu kwani upo wapi mpaka Manjis ziwe adimu?
 
Manjis ni kampuni ya Arusha ndo nyumbani kwao hadi vichochoroni wapo,wameenea sana Arusha hakuna kampuni inayowashinda wao kwa Arusha hata hao Oryx kwa Manjis Arusha wanaisoma namba,pia ni wazuri
kwani mitungi yao inajaa wala hawapunji.
Uko sahihi sana mkuu, kila sehemu lazima uikute.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…