Tukifanya Hivi, Kina Mwamposa na Manabii kuwa Walipa Kodi Wakubwa

Tukifanya Hivi, Kina Mwamposa na Manabii kuwa Walipa Kodi Wakubwa

Kweli Mkuu watu wanapenda kuropoka,kama inalipa na wao si wauze maji yao ya upako!
Wataweza wapi ule ni uchawi usifikiri ni hivihivi, na si kila mtu aweza mambo ya ndumba.
 
Hoja iko hivi?
Kodi hutozwa kwenye mambo matatu tu yaan, business, investment, employment. Chochote nje ya hapo hakitozeki Kodi (out of scope)
Sasa unatakiwa uje na sheria itakayosema na iwe strictly construed ili inmase mwamposa.
No intendment in tax laws, words must clearly be stated.
SASA EBU NISAIDIE HIYO SHERIA ITAKAAKAJE KIASI KWAMBA SADAKA AU MICHANGO kanisan itofautishe na mambo ya mwamposa?
Utaishia kutunga sheria mfu kwan haitaweza kufanya kazi.

Inatakiwa hivi unapowashtaki mwamposas useme ni kivipi arrangement ya transactions zake za maji na mafuta namna ambavyo fall within tax laws na sio kihisia.

Sasa mwamposa si atasena toeni sadaka nitawagawia maji MUNGU alioniruhusu niwagawie...
Wale wa 5,000 watapewa maji , chin ya hapo hatawapo ...hajairuka sheria yeyote
Mkuu watu wanapenda kuropoka kama Mwamposa anapiga hela si na wao wafungue ya kwao wapigie Hela!,kuuza vitu ata makanisha makongwe kama Moravian, KKKT T wanafanya.Kwa mfano Huwa kunakuwa na minada,utakuta mkungu wa ndizi wa 5000,waumini wanauziwa mpaka 50000 na pesa wanaita sadaka ila Mwamposa akiombea maji na kuwauzia waumini wake Ili apate pesa za kuendesha Kanisa lake,wanasema anauza!Kanisa lina Wafanyakazi wanalipwa mishahara,Kuna vibali vya TCRA kulipia matangazo ya Radio,mafuta ya magari nk.
 
Umeandika mengi kitaalamu,sawa.Kumbuka hapo tujikite kwenye kuuza bidhaa.Hayo mengine baki nayo tu.Auze for free?Bila tozo?Kwa nini uiweke akili yako kuwa stugnant kwamba sheria ya kumtoza kodi haitungiki?Umekwama kabla ya kujishughulisha kutafuta aina ya kodi?Na usijikite kwamba kuna kodi fulanifulani tu.Zinaweza kuongezwa muda wowote
Mwamposa ana kiwanda cha maji na duka la kuuzia ayo maji unayoyasema?
 
Yale maji, chumvi au vitambaa ni sadaka au biashara?
Na unadhani kule Kenya mpaka katamka vile (mind you jamaa ni mlokole) hakuifahamu sheria ya kodi kama wewe unayefahamu zaidi?
Hivyo vitu si nao wao wananunua madukani au wana viwanda vya kutengenezea!
 
Akili ya mwafrika ndio tatizo lake. Na huu umaskini unatumiwa na hao wahubiri wa dini kwa kujitajirisha.

Kagame alitumia akili kubwa sana kuwapa masharti ili makanisa yao yakubaliwe Rwanda.

Wanautumia ujinga wa wengi wetu kujitajirisha hawana msaada wowote katika kuleta afadhalii ya kimaisha ni wapigaji tu.
Kwani kqnisa gani ambalo viongozi hawajitajirishi Mkuu?
KKKT wanagombania nini,Biblia?
 
Sacraments ni tofauti na huo utapeli wa wachungaji feki, huuziwi sacrament kanisani unainunua kwa kutoa sadaka mbalimbali. Mapadre wanaishi kwa sadaka zetu za kila misa.

Padre akitaka kununua laptop au kifaa chochote anayo haki ya kuwaambia waumini na wakamnunulia ndio maisha ya useja hayo.

Tofauti na haya makanisa yanayotumia ujinga na ufukara wa waumini katika kutajirisha wachache.

Ni kanisa katoliki lina nidhamu ya uendeshaji na usimamiaji wa kila kinachofanyika huwezi kulinganisha na hayo makanisa ambayo ni mali za watu binafsi.
Kwani Kuna Kanisa ambalo siyo la mtu au taasisi iliyoanzishwa na mtu?.Ata sadaka ya KATOLIKI inaenda Vatican na wewe unabaki na ulofa wako.Bora wakina Mwamposa wanazungusha pesa humuhumu ndani ya nchi!
 
YEHODAYA hebu ngoja kidogo, viwanda vya maji vinalipa kodi kama kawaida na yeye ananunua huko.
Lakini kifuatacho naye anauza nasikia yale maji ya elfu moja anauza elfu 5 mpaka 10. That's where tunasema faida hiyo iwe taxed.
Tupo pamoja mkuu? Hata maduka yetu ya mtaani faida yao ya kuuza maji inatozwa kodi.
Acha uongo yanauzwa kati ya 1000 au 2000 na pesa inaenda kwenye uendeshaji wa huduma za Kanisa.Kuna umeme unawaka pale,Kuna Redio analipia TCRA,Kuna Wafanyakazi na wachungaji wanalipwa pia nk.
Sasa ulitaka pesa atoe wapi?
Mbona kwenye makanisa ya KKKT na Moravian na ata Katoliki Huwa kunakuwa na minada makanisani muumini analeta Kuku wa Tshs 20000 na anauzwa kwa 200000,apo inakuaje Mkuu.Au ndiyo kunywa anye Kuku,akinya Bata kaarisha?
 
Hapo maana yake ni pure biashara,maji yatakuwa yanauzwa kwa 5,000.Sadaka huwa haina kiwango.Kwanini kama ni sadaka basi asiwape hayo maji hata waliotoa shs 100 maana zote ni sadaka.
Kwani hayo maji watu wote wananunua?Sauala la maji ya upako,pia siyo lazima ununue Huwa anaombea ata ya kwako uliyokuja nayo.Kuna kipindi saa tatu usiku kinaitwa "OPERESHENI KOMBOA FAMILIA"mwishoni Huwa anaombea maji na Mafuta yoyote uliyonayo.Kwaiyo tuache uzushi !
 
Kanisa lina utaratibu wa uendeshaji wenye kueleweka kumbuka kanisa katoliki limekuwepo kabla ya uhuru hapa Tanzania huwezi kulinganisha na hayo makanisa yenye anwani za watu binafsi.

Fungukeni akili ili mpige vita huo wizi unaofanywa na hao wachungaji.
Ata Katoliki anauani yake ni Vatican kwa Papa!
Acha uzushi,dini ni Biashara kitambo ila shida inaanza kwasababu wakina Mwamposa wamekuja na njia tofauti ya kuabudu.
 
Sacraments haziuzwi.Utauzaje Sacrament ya Kipaimara ,ubatizo au Komunio? Kama ulimaanisha ile ekarist wanayokula hizo zinatengenezwa Kanisani na masister,huwezi zikuta ziko zinauzwa dukani kama maji,chumvi na mafuta.
Ata maji ya upako yameombewa kanisani au unadhani Yale maji ni ya kawaida Mkuu!
 
Sio chuki ndugu
Anachokifanya kinaonekana kiko kibiashara....awaambe watu waje na maji yao ayaombee warudi nayo makwao.
Vinginevyo inakuwa biashara alipe kodi ikiwa sheria itamwi giza kwenye wigo.
Mapadre , masister, wachungaji walipe Kodi za PAYE
Mkuu umewahi kwenda ukashuhudia akilazimisha watu kununua maji?ninavyojua Huwa anaombea maji yoyote ata ya kwako siyo lazima ya kwake.
 
Nashindwa kuelewa kwanini TRA wanashindwa kuiga kwa Ruto wa Kenya na kuongeza mapato kutoka katika wimbi hili la mitume na manabii walioanzisha biashara ya Maji, chumvi, vitambaa nk wakiviita vya upako na kupata fedha nyingi sana kama biashara isiyo kodi wala cost of production. Msome Rais Ruto alivyoamua.

"Nimeongea na watendaji wa serikali yangu kuhusu baadhi ya wahubiri kucheza na imani za wakenya. Kuanzia sasa yule anataka kuuza maji asajiliwe na mamlaka ya maji, yule anataka kuuza mafuta asajiliwe na food and drugs authority, na yule anataka kuuza mbegu asajiliwe wizara ya kilimo. Watambulike kama wafanyabiashara, na serikali ijue wanauza ngapi kwa siku na walipe kodi. Huku kwa kanisa wabaki wanaoeneza neno la Mungu, sio wafanyabiashara. Hatuwezi kuruhusu imani za wakenya kuchezewa na wakora wachache, wanaotaka kujitajirisha kupitia shida za waumini wetu" William Samoei Ruto, Rais wa Kenya.
Kauli bora kabida kutoka kwa rais wa kenya. Hebu na sisii tanzania serikali ije na uamuxi kudhibiti hawa wakora kwenye imani. Tuige ile ya rwanda kudhibiti uanzishwaji ovyo wa madhehebu za dini na hii ya biashara za kitapeli kuuzia watu bidhaa bila kulipa kodi.
 
Mwamposa ana kiwanda chake binafsi ..Maji yake Yana label yake binafsi na waumini wanauziwa hayo maji....uzembe Tu WA Tra...

Hawatakiwi hata kwenda kabisani..
Waende straight kiwandani kwake
Unaweza kufungua kiwanda bila TRA kujua?
 
Mkuu naona unaingilia madhabahu, hela ya sadaka ni mwiko kukatwa kodi, hela yoyote inayotolewa wakati wa Ibada ni sadaka na ni mali ya kuhani - imeandikwa kwamba Makuhani wote watakula madhabahuni.
 
Upo sahihi sana. Catholic Church imetengeneza mfumo wake wakupata pesa na Mwamposa naye anatengeneza mfumo wake. Wote ni walewale tu.

Kuna dada mmoja alifika hapa kwangu (Arusha) anaomba nimsaidie mchango anadaiwa kanisani (catholic). Nilimuuliza how much? Akaniambia kiasi alichopangiwa ni karibu laki tatu hivi, na document ya church alinionyesha. Nikasema well nimpatie kiasi, lakini nikajiuliza hii si biashara hii? Huyu dada masikini atapata wapi hii pesa? Si atakuwa anasumbua watu wamchangie?

Jambo lakushangaza yeye mwenyewe anatetea kiasi alichopangiwa nakanisa, ambacho hana.

Mwisho tunarudi palepale Catholics na mwamposa wote macho yao ni kwenye fedha. Kila mtu anatumi mbinu zake.
Timu ni ileile ila viwanja ni tofauti![emoji1787][emoji1787]
 
Kauli bora kabida kutoka kwa rais wa kenya. Hebu na sisii tanzania serikali ije na uamuxi kudhibiti hawa wakora kwenye imani. Tuige ile ya rwanda kudhibiti uanzishwaji ovyo wa madhehebu za dini na hii ya biashara za kitapeli kuuzia watu bidhaa bila kulipa kodi.
Ruto atakuwa one term present

Alikuwa kutwa anazurura makanisani kutqfura kura hadi ya vichochoni kumbe tapeli akapata kura kageuka kupiga vita waliompa kura

Akimaliza kipindi chake Uhuru Kenyatta atarudi kwenye madaraka ya uraisi Ruto atakuwa one term president

Wanasiasa hawana loyal members makanisa ndio yanao Ruto ahesabu kuwa atakuwa president kipindi kimoja tu vaada ya hapo kwa heri
 
Hiyo ni income kwa mujibu wa TRA mshahara sio pesa upewayo kila mwezi cha msingi inaingia kwako kwa kazi ufanyayo inahesabika personal income uiite tegemeza padre,sista au askofu ni personal income hayo majina ni porojo tu za kukwepa kodi za PAYE ni mshahara huo kodi ya mapato unatakiwa kulipa kodi ya PAYE

Hayo maneno ya tegemeza Askofu au padre au Sista ni terminologies za kukwepa income tax tu

TRA tueni kanisa katoliki kuna personal income zimefichwa kwenye tegemeza padri,askofu au sista
Unaweza kusema hapa posho wanazolipana wafanyakazi wa serikali even hao TRA kuna wakati hufanya vikao vyao wakajilipa posho huwa zinakatwa kodi?

Una chuki kubwa sana na RC bro kuwachukia hakukuongezei chochote kwenye maisha yako ya kiroho zaidi ya kupoteza muda sasa nakushauri kaa chini kunywa maji kidogo(sijui yatakuwa ni ya mwamposa au vipi utajua mwenyewe) kisha tafakari je ni sahihi kwa mwamposa kuwauzia watu Hill Water 1litre ya Tsh 500/= mtaani kwa gharama ya 5,000/= hapo Kawe na popote kwenye matamasha yake?
 
Back
Top Bottom