Tukifuata ushauri wa Professor Janabi tutaangamia kwa njaa

Tukifuata ushauri wa Professor Janabi tutaangamia kwa njaa

Wasalaam wakuu!

Kwanza kabisa Nakubaliana na ushauri wote wakitabibu kuhusu aina sahihi ya chakula na namna nzuri ya ulaji kutoka kwa Daktari bingwa na mkuu wa kitengo cha magonjwa ya moyo professor mohamed Yakub Janabi.

Namimi baada yakumsikiliza na kuanza kufuatilia miongozo yake nikaamua kubadili aina yangu ya ulaji ili niendane na matakwa ya msomi huyu. Na sasa ni wiki ya 3 tangu nianze kufuatana na miongozo ya Janabi na nasema wazi kuwa nimenyoosha mikono juu [emoji119], hii ni Baada ya kuzidiwa na njaa kisha kupata kizungu zungu na kuanguka ghafla ofisini.

Baadhi ya miongozo ya Professor huyu msomi

1.Kunywa bia moja masaa yasiyopungua mawili na usiongee wakati unainywa hiyo bia

2.kula mara moja tu, ukizidisha iwe mara mbili na chakula kisizidi ujazo wa kiganja cha mkono wako.

3. ugali ni hatari kwa afya ya moyo na unadumaza akili

4. Professor anasema yeye hajanywa juice ya aina yoyote miaka zaidi ya 15, lakini anasema tusile sukari, chumvi, nyama nyekundu, nyama nyeupe tule kwa kiasi kidogo sana , samaki wasio na magamba wanamafuta mbaya, lakini samaki wa maji chumvi nao ni tatizo kwa moyo. Janabi anaenda mbali nakushauri mboga zote za majani ziliwe zikiwa mbichi. "Kweli kisamvu nikitafune kikiwa kibichi professor?"

Literally ni kama professor Janabi yupo katika kampen ya #kataa chakula sababu anapingana na kila mlo uliozoeleka kwa WaTanzania. Nashauri asipuuzwe ila asitiliwe maanani sana.
Hivi huyu doctor yupo sawa kweli? Maana haya anayoshauri naona kama anataka watu tusile anaona tunafaidi
 
mnawezahisi profesa yuko serious kumbe yuko ktk kampeni ya kuzuia wageni nyumbani kwake😀😀😀.

fikiria huyu ni shemeji yako au baba yako mdogo,ukienda kwake utakaa siku ngapi🤣🤣🤣
Mwenyewe na familia yake hawataki kula Mimi niende ili nikajisababishie vidonda vya tumbo?
 
Literally ni kama professor Janabi yupo katika kampen ya #kataa chakula sababu anapingana na kila mlo uliozoeleka kwa WaTanzania. Nashauri asipuuzwe ila asitiliwe maanani sana.
Professor Janabi yupo sahihi ukila hata mara 1 kwa siku Mwezi mzima haufi, na hautaumwa magonjwa yasiyoambukiza
 
Kama video yenyewe ndio hii mkuu itoshe kusema uelewa wa binadamu wengine ni mdogo sana kuchakata mambo mepesi. Janabi ameongea clear sana bila utata wowote na msisitizo ameuweka kwenye kukojoa damu sio hata mkojo wa povu!
Pia anasema "dalili hizi'', sio mojawapo tu ya ya hizi!
Janabi hajaongea clear bila utata.

Labda standards zako za clear bila utata na zangu ni tofauti. Labda una very low standards.

Na siwezi kushangaa.

Kwa sababu, Watanzania wengi mna vipaji vya kufanya kazi na unclear, vague communication, msielewane, halafu wote mkaona mmeelewana.

Mnarahisisha mambo tu kuyaita mepesi kama ulivyofanya wewe.

No nuance.

Daktari anasema hizi ni dalili za ugonjwa wa figo. Ukiona hizi dalili ugonjwa uko advanced stage tayari.

Hajasema ukiona dalili yoyote kati ya hizi, ukiona dalili zote 15, au ukiona dalili tano kati ya hizi 15.

Unasema vipi kuwa daktari kasema kitu clear hapo?
 
Mwenyewe na familia yake hawataki kula Mimi niende ili nikajisababishie vidonda vya tumbo?
Hauumwi hata hivyo vidonda vya tumbo inategemea unakula nini, na alishaelezea unachotakiwa kula ni nini sio unakulakula tu tatizo hamsikilizi kwa makini
 
Janabi alikuwa anazungumzia utambuzi wa matatizo ya figo kwa kutaja dalili kadhaa kwa pamoja, zilikuwa nyingi mojawapo ikiwa mwili kuchoka sana, kuvimba miguu, kupumua n.k alichomaanisha ni kama mtu anazo hizi dalili kwa pamoja, sio moja moja. Yani sio tu kwamba ukiwa mchovu wakati wote una dalili za figo ila kwa sababu tumekuwa nchi ya mizaha na utani sana watu wakakuruka na hiyo ya mkojo tu.
Kuna haja ya kumsikiliza Mimi mwenyewe huyu doctor inawezekana watu wanapindisha uwasilishaji humu mitandaoni au wanachukua kipande kimoja na kuacha vingine
 
Hauumwi hata hivyo vidonda vya tumbo inategemea unakula nini, na alishaelezea unachotakiwa kula ni nini sio unakulakula tu tatizo hamsikilizi kwa makini
Nahitaji nimsikilize mwenyewe maana humu mitandaoni nimeshagundua watu wanaleta taarifa isiyokamilika.
Tatizo ni kwamba sijui napataje haya mafunzo yake.
 
Nahitaji nimsikilize mwenyewe maana humu mitandaoni nimeshagundua watu wanaleta taarifa isiyokamilika.
Tatizo ni kwamba sijui napataje haya mafunzo yake.
Ingia YouTube andika Jina lake Prof Janabi video zinakuja angalia anavyoeleza
 
Cha msingi kabisa
Ni kujitambua. Kila mtu awe na self awareness ya mwili wake. Ajue metabolic rates, Calories anazohitaji kulingana na shuguli anazofanya.
Baada ya hapo ndio atumie hizi insights za Profesa.

Tatizo kubwa wengi hatuna utamaduni wa kupima kabisa ili tujue miili yetu. Lakini Profesa yupo sahihi sana Guys gharama za matibabu ni kubwa mno. Surgery tu ya moyo India ni karibu milioni 60 (Angalau kidogo JKCIA Wameanza kufanya)
Ukila kwa usahihi wake utaondoa matatizo mengi sana hapo baadae.
 
Hivi nani kasema tunatakiwa kula mara tatu kwa siku? Ni makampuni sio Madaktari na ubongo unakumbuka na ndiyo maana unapata njaa. Lakini milo inatakiwa kula miwili tu. Saa nne au saa tano asubuhi na jioni kabla ya saa mbili. Baada ya chakula cha jioni kama ni chai au kahawa iwe ya rangi bila sukari wala maziwa mpaka asubuhi saa nne au saa tano yaani masaa 14-16 kila siku. Nimefanya hivi kwa miaka zaidi ya miwili sasa na madaktari wengi wanashauri hivi. Njaa ni akili yako tu ukishafanya wiki moja mwili unazoea. Usikofanya hivi hasa kuanzia 45 years unahatari ya kupata kisukari
Unafanya kazi gani??
Umeshwahi kuona au kusikia wafanyakazi wa kiwanda cha bakhresa pale buguruni wanavyohenyeka kila siku??
Halafu baada ya hiyo kazi ngumu ya kupakia viroba eoli zaidi ya 20 kwa siku aje anywe gahwa, mtaua watu aisee.
Kiranga hapo juu kaua winga, kula kulingana na shughuli zako na uahauri wa dkt.
 
Wasalaam wakuu!

Kwanza kabisa Nakubaliana na ushauri wote wakitabibu kuhusu aina sahihi ya chakula na namna nzuri ya ulaji kutoka kwa Daktari bingwa na mkuu wa kitengo cha magonjwa ya moyo professor mohamed Yakub Janabi.

Namimi baada yakumsikiliza na kuanza kufuatilia miongozo yake nikaamua kubadili aina yangu ya ulaji ili niendane na matakwa ya msomi huyu. Na sasa ni wiki ya 3 tangu nianze kufuatana na miongozo ya Janabi na nasema wazi kuwa nimenyoosha mikono juu [emoji119], hii ni Baada ya kuzidiwa na njaa kisha kupata kizungu zungu na kuanguka ghafla ofisini.

Baadhi ya miongozo ya Professor huyu msomi

1.Kunywa bia moja masaa yasiyopungua mawili na usiongee wakati unainywa hiyo bia

2.kula mara moja tu, ukizidisha iwe mara mbili na chakula kisizidi ujazo wa kiganja cha mkono wako.

3. ugali ni hatari kwa afya ya moyo na unadumaza akili

4. Professor anasema yeye hajanywa juice ya aina yoyote miaka zaidi ya 15, lakini anasema tusile sukari, chumvi, nyama nyekundu, nyama nyeupe tule kwa kiasi kidogo sana , samaki wasio na magamba wanamafuta mbaya, lakini samaki wa maji chumvi nao ni tatizo kwa moyo. Janabi anaenda mbali nakushauri mboga zote za majani ziliwe zikiwa mbichi. "Kweli kisamvu nikitafune kikiwa kibichi professor?"

Literally ni kama professor Janabi yupo katika kampen ya #kataa chakula sababu anapingana na kila mlo uliozoeleka kwa WaTanzania. Nashauri asipuuzwe ila asitiliwe maanani sana.
Huyu Prof ni mgonjwa na ndiyo maana kakauka utadhani anakula sementi. Anataka kutu preempt tusihoji hali yake kiafya. Yuko kwenye grid ya Taifa kitambo huyo
 
Mkuu,

Nakumbushia tu historia ya Upanga ya tangu enzi hizo Yoweri Museveni anakodi teksi kurudi kwake halafu akakimbia kulipa bill.

Leo nikimuona Museveni rais wa Uganda anazingua miaka yote hii nacheka sana jinsi maisha yanavyobadilika.

Leo nikirudi mimi Upanga naonekana mgeni
Ndugu yangu naomba kama una nyimbo za #jkalikawe hasa ile album ya usimdharau
 
Marehemu Justine kalikawe nilikuwa namkubali Sana lifestyle yake MTU wa watu humble alikuwa akija home by that time kabla kifo chake the guy was nice guy


Kiranga unaibuaga mambo 🙌🏽
Namkubali sana Justin Kalikawe
Nakumbuka kuna album nyingi niliwahi kuwa nazo ila katika harakati za utafutaji nikajikuta nipo nje ya mfumo kuja kurudi tape zote zimeharibika
Nikiingia mtandaoni nakutana na nyimbo chache sana
Sijui ndugu kama waweza kusaidia kupata hata kupitia familia yake nilipie
 
Ushauri wowote wa jinsi ya kula chakula, jinsi ya kufanya mazoezi, jinsi ya kula dawa, na mambo mengine muhimu yoyote ya kiafya ya jamii, hautakiwi kutolewa kiujumla.

Ndiyo maana wenzetu baada ya kutoa ushauri, husisitiza sana suala la kwamba kila mtu yuko tofauti, usiufanyie kazi ushauri kabla ya kuongea na daktari wako.

Kila mtu ana tofauti, na hivyo, anaweza kuhitaji mbinu tofauti.

Mfano, mtu mwenye uzito uliozidi, anayefanya kazi ofisini, anayekaa sana kwenye kiti, mwenye gari, ambaye hana mizunguko mingi kwa siku, anaweza kuangaliwa na daktari wake akaambiwa aongeze mazoezi na kupunguza caloric intake na ushauri huu ukamsaidia.

Lakini, mtu ambaye yuko underweight, analima kwa kutumia nguvu kubwa sana siku nzima, ana mizunguko mingi, kazi yake tu ni sawa na mazoezi, inahitaji nishati kubwa sana, na yeye utamwambia apunguze kula na aongeze mazoezi? Hai make sense.

Dr. Janabi anapotoa ushauri, huwa anasisitiza watu waongee na madaktari wao kwanza kabla ya kupanga jinsi ya kula au kufanya mazoezi?
Point sana
 
Wasalaam wakuu!

Kwanza kabisa Nakubaliana na ushauri wote wakitabibu kuhusu aina sahihi ya chakula na namna nzuri ya ulaji kutoka kwa Daktari bingwa na mkuu wa kitengo cha magonjwa ya moyo professor mohamed Yakub Janabi.

Namimi baada yakumsikiliza na kuanza kufuatilia miongozo yake nikaamua kubadili aina yangu ya ulaji ili niendane na matakwa ya msomi huyu. Na sasa ni wiki ya 3 tangu nianze kufuatana na miongozo ya Janabi na nasema wazi kuwa nimenyoosha mikono juu [emoji119], hii ni Baada ya kuzidiwa na njaa kisha kupata kizungu zungu na kuanguka ghafla ofisini.

Baadhi ya miongozo ya Professor huyu msomi

1.Kunywa bia moja masaa yasiyopungua mawili na usiongee wakati unainywa hiyo bia

2.kula mara moja tu, ukizidisha iwe mara mbili na chakula kisizidi ujazo wa kiganja cha mkono wako.

3. ugali ni hatari kwa afya ya moyo na unadumaza akili

4. Professor anasema yeye hajanywa juice ya aina yoyote miaka zaidi ya 15, lakini anasema tusile sukari, chumvi, nyama nyekundu, nyama nyeupe tule kwa kiasi kidogo sana , samaki wasio na magamba wanamafuta mbaya, lakini samaki wa maji chumvi nao ni tatizo kwa moyo. Janabi anaenda mbali nakushauri mboga zote za majani ziliwe zikiwa mbichi. "Kweli kisamvu nikitafune kikiwa kibichi professor?"

Literally ni kama professor Janabi yupo katika kampen ya #kataa chakula sababu anapingana na kila mlo uliozoeleka kwa WaTanzania. Nashauri asipuuzwe ila asitiliwe maanani sana.
Fanya kitu kulingana na uwezo wako na mazingira yako,si kila ushauri wakufuata
 
Back
Top Bottom