Tukio kwenye mataa ya Mwenge: Tofauti ya Wazungu na Waafrika

Tukio kwenye mataa ya Mwenge: Tofauti ya Wazungu na Waafrika

Kuthamini kazi kama hizo ni kuendeleza kudumaza akili za wahusika
Sipingani nawe lakini sidhani kama ni sahihi. Kuna watu hufanya kazi za kubeba takataka na kuenda kuzitupa. Vipi hao nao kuthamini kazi zao ni kuwadumaza akili?! Wasipokuwepo kazi hizo zifafanywa na nani?! Kuna watu huokota makopo mifaani, tukisema wasifanye kopo zitaokotwa na nani?!

Nadhani kila kazi ina umuhimu wake na watu wanaopaswa kufanya. Ikiwa ni kazi ya halali na inampatia kipato kinacho mtosheleza kwa mahitaji yake na familia basi na tuache afanye. Tumuunge mkono maana soko la ajira Afrika bado changa. Usipojiajiri na kuwa mbunifu katika ajira yako huwezi toboa.
 
Watu wa Asia kamwe siwezi fanya kazi naye isipokuwa Mwisrael kidogo ana tofauti kubwa
Hivi unajua Ulaya watu hufanya kazi kwa masaa, yaani ikiwa muda wako wa kazi ni saa 1 asbh hadi saa 10 jioni utalipwa kutokana na huo muda. Na ikiwa uta over time pia ufalipwa. Sasa njoo Afrika uone, utafanya kazi mchana na wakati mwingine hadi usiku lakini malipo ni yale yale. Na unalipwa kwa tabu sana, hadi udanganye kuwa una tatizo ndio pengine utawahishiwa malipo yako.
 
Sipingani nawe lakini sidhani kama ni sahihi. Kuna watu hufanya kazi za kubeba takataka na kuenda kuzitupa. Vipi hao nao kuthamini kazi zao ni kuwadumaza akili?! Wasipokuwepo kazi hizo zifafanywa na nani?! Kuna watu huokota makopo mifaani, tukisema wasifanye kopo zitaokotwa na nani?!

Nadhani kila kazi ina umuhimu wake na watu wanaopaswa kufanya. Ikiwa ni kazi ya halali na inampatia kipato kinacho mtosheleza kwa mahitaji yake na familia basi na tuache afanye. Tumuunge mkono maana soko la ajira Afrika bado changa. Usipojiajiri na kuwa mbunifu katika ajira yako huwezi toboa.
Kuokota makopo au kubeba taka hizo kazi ni nzuri na nitawaunga mkono lakini hiyo ya kuosha gari sehemu za makutano ya magari ni kuchochea ajali pia . Chukulia watu kama wanaweza kupata hela nzuri hapo kwenye makutano ya magari hali itakuwaje. In short hapo siyo sehemu rafiki kwa kazi hiyo
 
Dah ulivyowasifia wazungu, hawa ambao waliwafanyisha kazi mababu zetu kama punda na kuwalipa kwa mijeledi...kwa kufanya generalisation ya tukio moja huwezi ukawamiminia sifa zote hizo.

Wengi wao ni mabahili na wala hawatuthamini watu wenye rangi nyeusi, kwenye nchi zao kupata nusu ya walichonacho inabidi ufanye kazi na uwe vizuri katika unachokifanya mara mbili yao.
Ukizungumzia hilo nakataa sababu kibongo bongo you will never be as fortunate as ukifanya kazi na mzungu!

Fanya kazi na wadosi,wabongo,wachina non of them care..Hawa watu hawana utu kabisa yani. Anakufanya kama punda wake tu. Fanya kazi masaa 12 akuhenyeshe na lugha mbovu mitusi juu ila by the end of the day akupe buku 5-7 kwa hali ya sasa na hajali umekula hujala yeye kazi yake ufanye tu! Na unafanyishwa mikazi hata nje ya scope ya makubaliano.

Ila siku ukipata kazi ya mzungu ndio utaelewa, system ya kazi iko straight utafanya jambo a,b,c kwa masaa 8! Baada ya masaa hayo ujira wako ni 80K au anakwambia kila lisaa limoja nitakulipa elfu 10...On top of that kuna buffet kwa ajili ya wafanyakazi mtakula through the day kisha
kuna transport allowance utachukua kila siku ni 10K. Natumai kazi itaenda vizuri ambapo kuna ugumu basi muombe kuelekezwa mumuone flani.

Unakuta kazi ni ya miezi mitatu tu ila mpaka kazi imeisha una kiwanja mahali. Achana na mzungu wewe!!!

Bongo sijawahi kutana na kazi ya mzungu ambayo haina maslahi, wanaoharibugi maslahi ni wabongo wenzetu walioko top management ambao wao wanachofanyaga ni kupiga panga salio tofauti na mikataba anayotoa mzungu mwenyewe!
 
Sijui hata niseme vipi?!.

Kwa lugha nyepesi tu naweza kusema wenzetu WAZUNGU wameumbwa tofauti kabisa na sisi (ngozi nyeusi) WAAFRIKA. Sitaki kutumia maneno yanayoweza kufanya nikufuru, lakini ninachoweza kusema ni kwamba Mwenyezi Mungu aliwaumba wazungu kwa namna ya pekee sana. Kusema hivi wala sio utumwa kama wengine mnavyoweza kudhani, bali ni ile hali ya kukubali (appreciating) jamii ya watu fulani pasi na kujali dini zao, rangi zao, wala asili zao. Kukubali katika jambo jema na zuri ni busara zaidi kuliko kukataa tu hata kama ni jambo jema na lina manufaa.

Ninapozungumzia wazungu simaanishi ngozi nyeupe, hapana. Sizungumzii waraabu, sizungumzii wachina, wala sizungumzii wahindi. Nazungumzia WAZUNGU, watu wenye asili ya kutoka bara la Ulaya wenye rangi nyeupe (the white people).

Kuna Kijana anafanya kazi ya kufuta vioo vya magari katika makutano ya barabara ya kutoka Tegeta kuja Mwenge. Ni pale kwenye taa za barabarani (trafic light). Gari zinapo simama tu kwenye foleni kijana huyu humwaga povu la sabuni kwenye kioo cha mbele, kisha hutumia kifaa chake maalumu kufuta lile povu ili kuondoa vumbi. Kazi hii huifanya kwa uharaka sana na kwa ustadi wa hali ya juu. Ndani ya dakika moja na sekunde kadhaa atamwaga povu, atasafisha kioo, kisha atafuta povu na kuacha kioo cha gari yako kikiwa kisafi.

Kazi hii imekuwa ikifanywa na vijana wengi katika miji mbali mbali hapa barani Afrika.

Akishafanya hiyo kazi, wewe dereva unampatia kipande kidogo cha pesa. Kiasi cha pesa cha kumpa unapanga wewe mwenyewe. Wengi waliopata huduma ya kijana huyu walikausha kimya bila kulipia chochote na wala haikuwa kesi. Na wapo baadhi yao (wachache) walilipia shilingi 100 hadi 200 hivi.

Kuna gari aina ya CROWN iliyokuwa ikiendeshwa na Mzungu. Alionekana kama sio raia wa Uingereza basi atakuwa anatokea Wiles au maeneo ya jamii hiyo.

Kijana ni kama alijua vile. Na inaonyesha ana uzoefu wa kutosha wa malipo ya wateja anao wahudumia. Alisafisha kioo cha ile gari chap chap, kisha akasogea dirishani kwa dereva ili apate ujira wake. Yule dereva Mzungu akatoa noti ya shilingi 10,000 na kumpatia yule dogo. Daaah! Dogo alimshukuru sana kana kwamba yule Mzungu alikuwa amemfanyia kitu kikubwa sana kwenye maisha yake.

Taa ziliporuhusu ile gari ilipokuwa ikiondoka bado dogo aliendelea kumshukuru tena kwa kumpigia "saluti" yule Mzungu kuonyesha ame-appreciate kile alichofanya. Kama ilivyo utaratibu, yule Mzungu nae alijibu ile saluti ya dogo nae kwa kupiga Saluti.

Lilikuwa tukio la kipekee sana lililo onyesha namna sisi watu weusi (waafrika) na wenzetu wazungu tulivyo tofauti. Ni tukio lililompa yule kijana FARAJA NDANI YA MOYO. Mbali na kiasi cha pesa alicholipwa na yule Mzungu lakini kwa kijana aliona thamani ya kile anachofanya (kazi yake). Thamani ya kazi ya halali inayofanywa na mikono yake. Pengine kijana yule angekuwa mwizi au kibaka akikwapua mali za watu kwenye yale makutano ya ile barabara, leo hii thamani ya kazi yake asingeiona. Na zaidi ya yote angekuwa adui mkubwa mbele ya jamii na hasa watumiaji wa ile barabara.

Ni kawaida kwa wenzetu wazungu ku-appreciate kazi ya mtu pasi na kujali ni kazi ya aina gani. Ikiwa ni kazi ya halali na unaifanya kwa ustadi basi ataiheshimu kazi yako katika kiwango kinacho stahili. Hii ni tofauti kabisa na sisi Wafrika.

Sisi waafrika ni watu ajabu sana. Mtu unafanya kazi ngumu, nzito tena inayo "RISK" maisha yako, inapofika wakati wa kukulipa anakulipa isivyostahili. Na pengine asikulipe kabisa, au akakudhulumu kwa kukulipa kidogo tofauti na ilivyopaswa. Kama huamini, mtazame Meneja au Muhasibu hapo ofisini kwako. Amepewa mamlaka ya kuwalipa mishahara yenu. Lakini swali ni Je, anawalipa kwa wakati?!. Na je, ikifika wakati wa malipo anawalipa tu, au anasubiri hadi usingizie mtoto au mke/mume kuugua ndio aidhinishe malipo yako?!.

Kwakuwa yupo kwenye mamlaka ya kukulipa basi atakulipa atakavyo yeye.

Nadhani hapo utakuwa umenielewa vizuri kile ninacho maanisha. Akiwa Muhasibu au Bosi anaye idhinisha malipo yenu kuna wakati atasubiri hadi ifike tarehe 38 ndio awalipe malipo yenu. Hatari sana.

Naomba leo niwakumbushe kitu muhimu. Ni dhambi kubwa sana mbele ya dunia na mbele ya Mungu kudhulumu jasho la anaye pigana kwa haki. Jasho la mpiganaji daima huwa halipotei bure. Mungu wetu mlezi anasema "walipeni watumishi ujira wao kama vile inavyo stahili". Tambua kuwa athari za kuchelewesha mshahara wa mfanyakazi wako zinaumiza watu wengi sana. Kuchelewa kumlipa mfanyakazi wako kunaumiza watoto wake, mke/mume wake, wazazi wake, ndugu zake na hata jamaa zake. Anapochelewa kupata malipo yake hata Mangi dukani anakosa pesa, kwani pengine huyo ni mmoja katika wateja muhimu sana pale dukani.

Ndugu yangu, ikiwa umepewa dhamana ya kulipa ujira wa mtu anayemwaga jasho lake, basi mlipe katika wakati sahihi. Na ikiwa unadaiwa, basi lipa deni lako katika wakati mliokubalina.

Mwenyezi Mungu awabariki sana.

Na Hilal Kanal
0718022322
Dar es Salaam
View attachment 1858654
Hawa ni miongoni mwa watu wansotakiwa kupigwa marufuku mijini!!! Waje vijijini tulime tufuge waachana na ujinga huo wa kufuta magari ya watu!!
 
Mkuu, mbona wazungu ni wengi wanaendesha gari za kawaida.kuna mzungu ana drive subaru yupo kenya na ana pesa. Hapa jirani yangu kuna wazungu wanapanda boda boda. Na wengine wana NOAH
Ukimsoma mleta mada vizuri utamuelewa
Asante kwa kunielewa. Na katika hii mada kuna logic, wala ishu sio aina ya gari. Mshikaji anapaswa afikiri zaidi ili apate kuelewa nimelenga nini katika mada hii.
 
Kuokota makopo au kubeba taka hizo kazi ni nzuri na nitawaunga mkono lakini hiyo ya kuosha gari sehemu za makutano ya magari ni kuchochea ajali pia . Chukulia watu kama wanaweza kupata hela nzuri hapo kwenye makutano ya magari hali itakuwaje. In short hapo siyo sehemu rafiki kwa kazi hiyo
Mkuu. Hata trafiki nao hufanya kazi barabarani tena all the time na luna wakati ajali huwakuta vile vile, lkn bado hilo haliwafanyi kuacha kufanya kazi yao. Vijana hawa wapo makini sana na wanatambua kuwa kuna ajali, ndio maana hufanya kazi zao wakati taa nyekundu zimewaka na gari zimesimama. Taa zinaporuhusu tu utaona wakikaa kando ya barabara.
 
Mkuu. Hata trafiki nao hufanya kazi barabarani tena all the time na luna wakati ajali huwakuta vile vile, lkn bado hilo haliwafanyi kuacha kufanya kazi yao. Vijana hawa wapo makini sana na wanatambua kuwa kuna ajali, ndio maana hufanya kazi zao wakati taa nyekundu zimewaka na gari zimesimama. Taa zinaporuhusu tu utaona wakikaa kando ya barabara.
Sawa mkuu lakini barabarani siyo sehemu ya kuoshea magari. Hao walitakiwa wapigwe marufuku
 
Sema kwenye suala la kutoa kwa moyo na ku appriciate nadhani inatokana na moyo wa mtu na mood aliyo nayo kwa muda huo, Wala sio wazungu wote na pia ata Africans tupo pia wenye moyo wa kutoa
 
Sema kwenye suala la kutoa kwa moyo na ku appriciate nadhani inatokana na moyo wa mtu na mood aliyo nayo kwa muda huo, Wala sio wazungu wote na pia ata Africans tupo pia wenye moyo wa kutoa
Yes, ni kweli lakini ni wachache cos sio asili yetu kusaidiana. Asili ya mtu haipotei Mkuu.
 
Africans bana.

Mzungu ni neno ambalo sipendi kulitumia.
Lakini hii mada kila mtu anajadili kuhusu mzungu kama miungu au aina fulani hivi ya demigods.

Ni akili tu ya kibinadamu pia wapo africans wengi wanaofanya hivyo ila kwakua ni mtu mwenye asili ya nje afrika basi ikawa sababu ya sifa zote hizi.
Na nina uhakika kama muafrika angefanya hivyo usingeandika hii thread.

Sina uhakika lakini ni vizuri ukasoma history ili kujua ni nani aliyefanywa mtumwa na nani aliyemfanya mwenzake mtumwa.
Kwa kuwaua,kuwatumia kama punda pia kuwafunga minyororo kama mbwa, kuwatesa na kuwadharirisha.
Bila kusahau yule jamaa mweusi aliyepigwa kabali ya goti mpaka kifo na polisi mweupe.
Pia bila kusahau ubaguzi juu ya mtu mweusi huko nje.

Alafu unasema wamweumba tofauti really?
Huyo aliyewaumba labda alikuwa high at the time.


Ni ajabu Africans mpaka leo bado wana ile low self esteem na inferiority mbele ya mzungu iliyotokana na history ya nyuma na kusahau kwamba wote ni binadamu waliotofautiana utashi na rangi iliyotokana na mazingira.

Mimi sioni cha ajabu hapo zaidi ya sign za low self esteem na inferiority complex.
 
Back
Top Bottom