Tukumbuke Zamani: Historia ya Taifa letu katika picha

Tukumbuke Zamani: Historia ya Taifa letu katika picha

...Saana, Pecos na Raizon kwa kwenda mbele! Ama kweli tulifaidi jamani!

Mkuu huyu mkulu ni Balozi Weddy Mwasakafyuka (RIP), enzi zake akiwa ofisa pale Foreign, hata kwenye picha ya Mbaraka Mwinshehe (RIP), naye pia ampigilia pekosi!
 
Mkuu Invisible na Mods,

Tafadhali naomba mzifungue hizi picha hapo kwa Mkuu Ochu, maana kuna picha muhimu na safi sana,

Mkuu Ochu,

Kofia chini na heshima mbele kwa uzalendo wako, ubarikiwe tu! Ndio maana ninaiheshimu sana JF mawe mazito hutokea kila kona, tena bila habari!

attachment.php


attachment.php


attachment.php


attachment.php


attachment.php
 
Field Marshall uliyeanzisha thread hii, na wengine wote walioleta picha,

Mbarikiwe! Imekuwa burudani tosha na imetukumbusha mbali sie wa mwaka 47!
 
Mkuu Kibunango,

1. Heshima mbele bro, naona hapo mstari wa mbele kuna marais wa zamani kuanzia kushoto ni Ngwabi wa Congo Brazaville, Bokassa wa Central Afrika, Haile Selassie Wa Ethiopia, Kenyatta wa Kenya, Siaka Stevens wa Siera Leone, na Mobuttu wa Zaire,

2. Mstari wa Nyuma ni Kayibanda wa Rwanda, Obotte wa Uganda, Mwalimu Baba Wa Taifa letu Tanzania, Kaunda wa Zambia, hao wengine wawili siwakumbuki kabisaa, ninaomba msaada na ninaweza kuwa nimewakosea wengine pia!

3. Huko chini ni rais wetu Jakaya Mrisho Kikwete, ahsante kwa kuziweka kwa chini ya wazee wa kazi.

Mkuu Kibunango, ahsante sana kwa ufundi na maarifa yako mazito sana, na Mkulu Ochu, ubarikiwe.
 
nani kakwambia kama Nyerere hakulimbikiza mali ,kama unaijua sababu ya Mkapa kufungua genge la biashala ikulu ,usingesema hayo ?
Kifo cha Nyerere kinajulikana ni ni baada ya kufa Jamal ambae ndie aliekuwa anahifazi feza ya Nyerere kwa jina lake,ghafla Jamal alipofariki Nyerere akafunga safari hadi kwa mke wa Jamali na kuulizia ela yake ,mke wa Jamali akamjibu Bana haikuacha kitu kwa jina lako ,hapo ndipo ugonjwa ulipoanza kumtambalia Mwalim na kumuondoa duniani.


What a plonker!!
 
Nadhani kuna watu hatambui kuwa Mzee kawawa alikuwa ni mmoja wa kuruta wa kwanza kwanza wa JKT pale Ruvu. Kwenye picha hii Mzee Kawawa ni huyu wa pili kwenye msitali wa mbele, mfupi na mwenye kitumbo kikubwa kuliko wote. Pich hii ilipigwa wakati wa pass-out parade, sikumbuki mwaka gani lakini ni kati ya mwaka 1968 na 1970 hivi.

attachment.php
 

Attachments

  • c4.jpg
    c4.jpg
    46 KB · Views: 1,475
Mkuu Kichuguu,

Heshima tena mkuu, hii picha kwa kawaida huwa ipo katika kila nyumba ya kiongozi wetu wa taifa wa zamani, ninaowakumbuka kwenye hiyo picha ni

Wa kwanza ni John Rupia (Ambaye ndio kwanza alikuwa amerudi bongo kutoka NY, US ambako alifuzu shahada ya Masters katika College maarufu ya NYU), Mheshimiwa Kawawa, Spika Sitta, Marehemu Spika wa Zamani Adam Sapi, na anayefuatia ni Balozi Mwakawago.

Again heshima mbele mkuuu kwa huu ukumbusho mzito sana.
 
Vile vile kumbukeni cabinets za kwanza. Hii hapa ni cabineti baada ya uhuru: Ninawakumbuka akina Nsilo Swai, George Kahama, Amil Jamal, Rashid Kawawa, Oscar Kambona, Bhokhe Munanka. Je Marshall unaweza kutukumbusha majina ya wengine??

attachment.php


Na hii hapa ni cabinet mara baada ya Muungano

attachment.php
 

Attachments

  • DSC04445.jpg
    DSC04445.jpg
    139.6 KB · Views: 1,282
  • Cabinet1.jpg
    Cabinet1.jpg
    55.2 KB · Views: 1,283
Mkuu ninaweza kuwakumbuka wachache wao,

1. Ile picha ya juu ni waliosimama toka kushoto ni, Lusinde, Kawawa, Swai, Kambona, Lawi Sijaona, na Derek Bryson,

2. Waliokaa chini ni toka kushoto Bomani, Mwalimu, na mwisho ni Amir Jamal.

Naweza pia kuwa nimekosea, maana nilikuwa mdogo sana mkuu ila ni viongozi ninaowakumbuka sana katika sherehe sherehe za hapa na pale.
 
Kichuguu,
Kwenye hiyo picha ya kwanza juu George Kahama hayumo.Nyuma ni Lusinde, Kawawa, Swai, Kambona, Said Tewa na huyo mzungu jina limetoka lakini alikuwa ni Secretary to the Cabinet. Mbele ni Bomani, Fundikira, Nyerere, Ernest Vassey na Jamal
 
Kichuguu,
Kwenye hiyo picha ya kwanza juu George Kahama hayumo.Nyuma ni Lusinde, Kawawa, Swai, Kambona, Said Tewa na huyo mzungu jina limetoka lakini alikuwa ni Secretary to the Cabinet. Mbele ni Bomani, Fundikira, Nyerere, Ernest Vassey na Jamal

Mkuu Jasusi

Nashukuru kwa kuweka rekodi sawa. Unajua wakati huo mimi nilikuwa fundi wa kutengeneza magari ya mabua yanayoendeshwa kuvutwa kamba, injini ikiwa mdomoni mwa mwendeshaji (utamsikia ziiiiiii, mara pipii); kwa hiyo sikuweza kuwajua hawa wote sawasawa kwa sura isipokuwa Nyerere tu ambaye alikuwa wimbo wa kila siku.
 
Mkuu Jasusi,

Heshima mbele huyu wa pili sio Sitta, au?

Hapana, Sita alikuwa hajawa mwanasiasa wakati huo; nadhani alikuwa mwanafunzi wa middle school. Sitta asingefurukuta wakati huo kwa vile Jimbo la Tabora lilikuwa chini ya wazito wa nchi akina Chifu Fundikira na Kasela Bantu.
 
Huyo wa pili nadhani ni Hashim Mbitta, lakini sina uhakika wa 100%
 
FMES,Bubu-ataka-Kusema,Jasusi,Kichuguu,...

..samwel sitta alikuwa mwanafunzi miaka hiyo. nina hakika hata chuo kikuu alikuwa hajaanza.

..samwel sitta na wilfred mwabulambo waliongoza mgomo wa UDSM ambapo walibeba mabango yaliyosema "bora mkoloni kuliko serikali ya kizalendo."

..maneno hayo yalimkasirisha sana Baba wa Taifa. samwel sitta na mwabulambo walichapwa viboko kama adhabu kabla hawajaruhusiwa kuendelea na masomo.

..Hashim Mbitta hajawahi kushika nafasi ya uwaziri. nadhani alianzia kwenye tanu, baadaye akawa mwandishi wa habari wa raisi, halafu akawa katibu wa kamati ya ukombozi ya OAU.

NB:

..kama sijakosea Samwel Sitta ana undugu na Chief Fundikira[r.i.p].

..labda hiyo ndiyo sababu Bubu anawafananisha.
 
sokoinebc%5B1%5D.jpg

Edward Moringe Sokoine: The Prime Minister people loved "...Edward Moringe Sokoine was then Prime Minister, and what a Prime Minister he was. He commanded and won respect from over 98 per cent of all Tanzanians. He deservedly won the respect of the then President, the late Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Edward Moringe Sokoine was a darling to all patriots because he was a great patriot, to all honest people because he was the most honest man, to all hard working people because he was himself the epitome of hard work, to all practical people because he was a man of few words. He was action-oriented. He wanted to see things done and done now, not tomorrow. But Edward Moringe Sokoine was a terror to majambazi (bandits) because he hated them like poison, he was poison itself to embezzlers; and saboteurs feared him like death. He was no friend to lazy indecisive workers and managers alike. He was a man of the people, indeed. Sokoine died in a horrible road accident in mysterious circumstances at Dakawa area on the Dodoma - Morogoro Road that dark April day in 1984 at the tender age of 56 short years.
 
View attachment 2079

View attachment 2080

View attachment 2081

View attachment 2082

View attachment 2083




nayo ni historia hii

...enzi hizo unapewa shillingi mia tatu kwenda nazo boarding school, zinatosha half term! ...thumni, inatosha kununua bhajia na mihogo ya kukaanga shule

...enzi hizo David Wakati na mazungumzo baada ya habari,

...enzi hizo Idi Amin alikuwa anasifika kwa majina kama nduli, joka kuu!...

...enzi hizo saa tatu usiku katika kipindi cha majira Ben Kiko alikuwa hewani kutuhabarisha,...

...nasisimkwa mwili nikikumbukia siku hiyo Mwalimu JK Nyerere alipolihutubia taifa,

..." NDUGU WATANZANIA, ASKARI WETU WAPO KWENYE UWANJA WA MAPAMBANO, IDI AMINI AMETUVAMIA... NIA YA KUMPIGA TUNAYO, SABABU YA KUMPIGA TUNAYO, NA UWEZO WA KUMPIGA TUNAO!",...
 
Enzi hizo pesa zetu zilipokuwa na nguvu kabla ya kushushwa thamani na Mkapa ukiwa na hizo nyekundu 10 wewe tajiri mkubwa 🙂 unaweza kukusanya marafiki na kushuka nao sehemu sehemu na kumwambia mhudumu lete kama tulivyo 🙂
 
nyerere13bc.jpg

Baba yetu wa Taifa, pamoja na kuwa alikuwa na huruma kamwe asingeyafanya haya yanayofanywa na Kikwete ya kuwapigia magoti mafisadi warudishe mabilioni waliyokupua huku wakiendelea kupeta mtaani. RIP Mwalimu.
 
Back
Top Bottom