Tukumbuke Zamani: Historia ya Taifa letu katika picha

Tukumbuke Zamani: Historia ya Taifa letu katika picha

Small nations are like indecently dressed women. They tempt the evil-minded."
Julius K. Nyerere

"Freedom to many means immediate betterment, as if by magic. Unless I can meet at least some of these aspirations, my support will wane and my head will roll just as surely as the tickbird follows the rhino."
Julius K. Nyerere

"African nationalism is meaningless, dangerous, anachronistic, if it is not, at the same time, pan-Africanism"
Julius K. Nyerere

"Violence is unnecessary and costly. Peace is the only way."
Julius K. Nyerere

Source: http://thinkexist.com/quotes/julius_k._nyerere/

RIP Nyerere

Love from my heart

Kalenge
 
FMES,
Kenyatta hakuwa na fimbo peke yake. Alikuwa pia na ule mkia wa ng'ombe uliosukwa kwenye fimbo. Wenyewe wanaita whisk. Ningekuwa na hiyo picha nigeiweka hapa.

Kenyatta na bakora na ki whisk.JPG
Hapa Mzee Kenyatta ameshika fimbo pamoja na whisk
Hii ilikuwa 30th March 1965, Akimpa degree ya heshima ya udaktari wa falsafa


kenyatta.jpgkenyatta.gif
 
nimependa sana hii thread kwa kweli inatupa changamoto
attachment.php

Asante kwa picha nzuri.
Je hapa ni wapi? Je ni Ikulu? kusema kweli Mwalimu alikuwa hana makuu, hapa yuko more than relaxed na wananchi wake. Yes, policy zake hazikufanikiwa, lakini kwa mtazamo wangu kama mtu wa watu alijitahidi.
 
Mzeeba,

..nadhani hapo alipokaa Mwalimu ni nje Karimjee Hall.
 

Hii picha imenipa huzuni sana...hayo maneno ya Mwalimu Nyerere yalikuwa na nguvu sana.

YAP! Nakubalina na wewe, pia sikuwahi kujua kama maneno haya Mwalimu aliyasema wakati akitoa hotuba ya kwanza siku ya uhuru. Ama kweli Mwalimu alinuia kuwafikisha Watanzania kwenye nchi ya ahadi.
 
Kuna hii movie ya Michael Douglas inayohusu Simba wa Tsavo ( au Nyamaume wa Tsavo) ambayo hata sikumbuki jina lake tena. Tuliingalia sana na familia yangu kipindi cha mwaka 2004 na 2005 ikihusu ujenzi wa reli huko kenya. Kweli yule simba aliwatesa sana mpaka wakaamua kuwaajili morani wa kimasai kumuwinda.

Ni kweli kuwa hakuna rekodi sawasawa kuhusiana na ujenzi wa reli zetu zote tatu za Tanga, Kati na kusini zilizojengwa wakati wa mkoloni. Ila kama ilivyo kwenye major construction yoyote ile, ni lazima relie hizi zilikwenda na maisha ya watu wengi sana, hasa ndugu zetu ambao wakati ule walikuwa wakionekana kama vile hawana thamani.

Nimejaribu kuangalia tovuti ya TRC nikijua walau ntapata historia kidogo, wapi!!! wao mbali kabisa... ni kuanzishwa TRC 1977. Tutangojea kuandikiwa historia yetu mpaka lini? Tatizo kubwa nadhani (sio kwa serikali tu, hata watu binafsi) hatuna tabia ya kujiwekea kumbukumbu kwa ajili yetu na vizazi vijavyo. Au kwa vile tumezoea kupeana historia zetu kwa hadithi za kusimuliana? Vyovyote vile, tuna takiwa kuandika historia zetu na za taifa letu
 
Vile vile kumbukeni cabinets za kwanza. Hii hapa ni cabineti baada ya uhuru:
attachment.php


Na hii hapa ni cabinet mara baada ya Muungano
attachment.php

Hii ni miaka 40 baadae
2005.jpg

Na hii 2008
new_cabinet ya sasa.jpg

Je Historia katika huu mtiririko inakuonyesha nini?

Mwenye baraza la wakati wa Raisi Mwinyi na Raisi Mkapa aweke hapa nadhani nachoongelea tutakiona vizuri
 
Unajua the sad news ni kwamba ni Nkurumah, ndiye aliyepigana sana kuiuwa EAA, na aliweza kum-recruite Njonjo akishirikiana na Makaburu wa Africa Kusini, na Muingereza Tiny Rowland,

Nkurumah, alitaka kuwe na muungano wa Afrika nzima, huku yeye akiwa rais wake wa kwanza, Mwalimu akawa a big competititor wake kwa sababu, tayari Mwalimu alikuwa na Muungano wa Tanzania, na EAA hivyo viongozI wengi wa Africa, walikuwa wako radhi kumsikiliza Mwalimu zaidi on this ishu ya muungano kuliko Nkurumah, ambaye hakuwa na any experience. Kuona hivyo Nkurumah akaanza hizo njama, ambazo baadaye zilizaa matunda ya kuvunjika kwa Jumuiya, ambako Kenya ndio waliofaidika sana na matokeo kwa sababu waliweza ku-retain mali nyingi sana za Jumuiya kuliko nchi zingine yaani sisi Tanzania na Uganda.
FMES,

Heshima yako Mkuu.

Kuhusu Nkurumah kuhusika na kuua EAA, ninadhani huenda siyo sahihi kwa sababu jamaa huyu alipinduliwa kutoka madarakani na General Joseph Ankrah mwezi February mwaka 1966, ikiwa ni miaka miwili tangu tuwe na muungano wa Tanzania. East african Community ilizaliwa 1967 wakati Nkurumah hayupo madarakani kabisa. Ingawa EAAC ilikuwapo tangu mwaka 1948 ikiwa inaendeshwa kama branch ya BOAC (British Overseas Airways Corporation), haikuwa mali ya serikali za afrika ya mashariki wakati huo hadi baada kuanzishwa kwa EAC mwaka 1967, ambapo Nkurumah alishaishia kusikojulikana. Kati ya mwaka 1967 hadi mwaka 1972, EAA ilikuwa inaendeshwa vizuri sana wala hakukuwa na matatizo yoyote. Ni katika kipindi hicho walipoweza kununua ndege za jet kama vile Comet na VC10


lgw43.jpg


scan0061.jpg


Matatizo yalianza mwaka 1974 baada ya Amini kuwa madarakani huko Uganda, na vile vile uchumi wa Tanzania kuanza kuyumba pole pole baada ya zoezi la kuhamisha watu kwa nguvu kwenda kwenye vijiji vya ujamaa na hivyo kupunguka kwa uzalishaji wa chakula, jambo lililosababisha kuyumba sana kwa uchumi kufuatia njaa ya mwaka 1974, ndipo Kenya walipodai wawe na sauti kubwa kwenye jumuia ile kwa vile uchumi wao ulikuwa imara. Sasa kuwepo kwa madai haya ya Kenya huku Nyerere na Amini hawakai meza moja ndiko kulikuyumbisha sana jumuia hadi ikafa.


Mkuu Kichuguu, Ahsante kwa hizo picha kati ya hao ma-Air Hostess wa EAA, kuna mama mmoja ninaishi naye karibu sana, yaani hata leo akisema kuwa aliwahi kuwa one of hao kina mama huwa tunakufa sana na kucheka na hata yeye mwenyewe hucheka sana, lakini off course ujana na uzee ndio maisha na owte siku moja tutakuwa hivyo, kama tutafanikiwa kuishi kwa muda mrefu maana kila siku life expectency huku kwetu Africa inazidi kushuka tu, nafikiri kama sikosei mara ya mwisho ilikuwa ni miaka 37 tu! Damn it!

Sote tunaelekea kumoja. Huko nyuma niliwaambia nilikuwa fundi wa kutengeneza magari ya mabua. Je unadhani naweza kufanya kazi hiyo tena kwa leo?
 
FMES,

..Kenya walibakiwa na mali nyingi zipi hizo?

..Makao Makuu ya EAC yalikuwa Arusha.

..pia kulikuwa na msuluhishi wa mgawanyo wa mali za EAC, akiitwa Dr.Victor Umbrich.

..kuna uwezekano Kenya walionekana na ahueni kwasababu uchumi wao ulikuwa imara from the beggining kwasababu za KIHISTORIA.

Kichuguu,

..kwa mtizamo wangu EAC was bound to collapse.

..Tanzania ilikuwa ikinung'unika kutokana na disparity ya maendeleo ya kiuchumi kati yake na wenzake. nitajaribu kukuletea chanzo cha habari hiyo.

..vilevile nadhani Wakenya walikuwa wanataka kuendeleza ile status quo ya kiuchumi iliyoachwa na mkoloni EAC.

..nina wasiwasi kwamba Muungano mpya tunaojaribu sasa hivi utakuwa na matatizo yaleyale ya kama ule uliovunjika.

NB:

..Nyerere pia alikuwa amezidi kumchokonoa Iddi Amini.

..baada ya Obote kupinduliwa akiwa ng'ambo, alikuja na kukaa ikulu ya Tanzania. Nyerere aliendelea kupeperusha bendera ya Raisi wa Uganda kwa kipindi chote Obote alichokaa ikulu ya dsm.

..pia Nyerere ali-host wakimbizi wengi tu waliokuwa wakimpinga Amini na kuwapa mafunzo na misaada ya kijeshi.
 
huyu mwingereza,TINY ROWLAND,amezivuruga sana serikali za africa,ametumia sana mali za LONRHO kuziyumbisha nchi za kiafrika,in fact this man was almost a behind the scenes president of many african countries,coup de tat nyingi africa,his name cropped up.HATA nyerere,tough as he was,amewahi kuwa cornered na TINY.in one of his speeches,nyerere amewahi kusema 'aka kaTINY kana mambo makubwa kuliko jina lake'


All this goes back to Cecil Rhodes aliyeakuwa mwanzilishi wa Rhodesia an kuleta ile ambition project the Cairo to Cape Town, exploring and exploiting Africa from one point north the the south point, Cape Town!

Sasa LonRho wao wakaja na Tiny Rowland ambaye kama kumbukumbu zangu ni nzuri, waliwahi kufukuzwa na Mwalimu ingawa walirudi baadaye na wame-invest kwenye mashamba ya Chai!
 
kazi nzuri wakuu......Mimi naomba kama anaweza kujua majina ya hawa vijana walioshika hilo bakuli ambalo mwalimu anachanganya mchanga huo na bado wako hai?mbona sijawahi kusikia wakikumbukwa.......pia hao akina mama kushoto ni akina nani na huyo mzee kushoto anaepiga makofi......
attachment.php
 
Hao walioshika mabakuli ya udongo na hao akina mama inasemekana wako hai. Kama sikosei last week walitwa bungeni wakati mjadara wa muungano unazungumziwa na majina yao yalitoka kwenye one of the papers, nafikiri nipashe. Jaribu kucheck kwenye mtandao wa nipashe for the past week unaweza ukawaona.
 
Unajua the sad news ni kwamba ni Nkurumah, ndiye aliyepigana sana kuiuwa EAA, na aliweza kum-recruite Njonjo akishirikiana na Makaburu wa Africa Kusini, na Muingereza Tiny Rowland,

Nkurumah, alitaka kuwe na muungano wa Afrika nzima, huku yeye akiwa rais wake wa kwanza, Mwalimu akawa a big competititor wake kwa sababu, tayari Mwalimu alikuwa na Muungano wa Tanzania, na EAA hivyo viongozI wengi wa Africa, walikuwa wako radhi kumsikiliza Mwalimu zaidi on this ishu ya muungano kuliko Nkurumah, ambaye hakuwa na any experience. Kuona hivyo Nkurumah akaanza hizo njama, ambazo baadaye zilizaa matunda ya kuvunjika kwa Jumuiya, ambako Kenya ndio waliofaidika sana na matokeo kwa sababu waliweza ku-retain mali nyingi sana za Jumuiya kuliko nchi zingine yaani sisi Tanzania na Uganda.

Mkuu Kichuguu, Ahsante kwa hizo picha kati ya hao ma-Air Hostess wa EAA, kuna mama mmoja ninaishi naye karibu sana, yaani hata leo akisema kuwa aliwahi kuwa one of hao kina mama huwa tunakufa sana na kucheka na hata yeye mwenyewe hucheka sana, lakini off course ujana na uzee ndio maisha na owte siku moja tutakuwa hivyo, kama tutafanikiwa kuishi kwa muda mrefu maana kila siku life expectency huku kwetu Africa inazidi kushuka tu, nafikiri kama sikosei mara ya mwisho ilikuwa ni miaka 37 tu! Damn it!

FMES,
Ni kweli Nkrumah hakutaka EA Federation ifanikiwe kwa sababu hii ingeua
hoja yake ya instant African federation. Hata katika kikao cha OAU 1963 walibishana sana na Mwalimu lakini at the end of the day Nkrumah akaishia kumpigia Mwalimu makofi kwa sababu ya nguvu za hoja zake kuhusu mwungano wa hatua kwa hatua. Lakini khasa khasa aliyeua mipango ya EA Federation alikuwa ni Mwingereza. Mwalimu alikuwa tayari kumpisha Kenyatta awe rais wa kwanza wa Federation. Obote naye alikuwa amekwishakubali. Lakini kwa sababu ya age Waingereza wakatambua kuwa eventually Mwalimu angekuwa kiongozi na hawakumwamini kwa sababu hawakuweza kumtumia kama walivyokuwa wanamtumia Kenyatta. Basi wakamshawishi Kenyatta kuwa asikubali, and that was the end of it.
 
Hao walioshika mabakuli ya udongo na hao akina mama inasemekana wako hai. Kama sikosei last week walitwa bungeni wakati mjadara wa muungano unazungumziwa na majina yao yalitoka kwenye one of the papers, nafikiri nipashe. Jaribu kucheck kwenye mtandao wa nipashe for the past week unaweza ukawaona.


Ni kweli, bado wapo hai.

Hoja ya Muungano yawagawa wabunge

2008-08-21 09:16:17
Na Beatrice Bandawe, Dodoma


Hoja ya Muungano jana iliwagawa wabunge wa kutoka Tanzania Bara na wale wa Visiwani huku wa Bara wakiiunga mkono kwa kutaka uongelewe U-Tanzania zaidi na wale wa Visiwani wakionyesha kutokubaliana nao.

Bila kujali itikadi zao za vyama, wabunge wa Visiwani walionekana kuwa na msimamo mmoja wa kung\'ang\'ania kuwepo kwa serikali tatu na baadhi kudiriki kusema Wazanzibari hawako tayari kuwa na serikali moja.

Hoja hiyo iliingiliwa kati na Spika wa Bunge, Bw. Samuel Sitta, aliyesema kuna haja ya kutafuta nafasi ya kufanya semina kuhusu Muungano kwa kuwa dhana hiyo inapotoshwa na baadhi ya wabunge.

``Tunahitaji wazee wetu tusaidiane, kama mzee wetu Kingunge,`` alisema Spika Sitta.

Wakichangia mjadala wa hotuba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Bw. Mohammed Seif Khatib, ambao uliendelea kwa siku ya pili jana, wabunge hao walionekana kupangwa kwa utaratibu wa kuchangia kwa mbunge wa Tanzania Bara kufuatiwa na kutoka mbunge kutoka Visiwani.

Mjadala huo pia ulihudhuriwa na mashuhuda wa Muungano wa mwaka 1964, ambao ndio waliobeba vibuyu vya udongo kutoka Tanganyika na Zanzibar na baadaye kuchanganywa na waasisi wa Muungano, Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Mzee Abeid Amani Karume.

Mashuhuda hao ni Bi. Khadija Abbas Rashid ambaye wakati huo alikuwa na umri wa miaka 16, Bw. Hassan Omar Mzee, naye alikuwa na miaka 16 na Bi. Sifael Shuma, aliyekuwa na miaka 30, wakati huo.

Mbunge wa Viti Maalum (CHADEMA), Bi. Anna Komu, alikataa kuunga mkono hoja ya wizara kwa madai kuwa mpaka aelezwe Zanzibar inasaidiwa vipi kiuchumi kwa kuwa maisha ya Wazanzibari ni magumu.

Bw. Job Ndugai, Mbunge wa Kongwa (CCM), alisema linapokuja suala la Muungano, upande mmoja kazi yake ni lawama tu na kuhoji hivi ni kweli Bara kazi yake ni kuionea Zanzibar.

``Kwa nini mnajidharau wenyewe, wakati Zanzibar ina maendeleo kushinda Bara,`` alisema.

Mbunge wa Nkasi (CCM), Bw. Ponsian Nyami, ambaye alikuwa akinukuu vifungu vya Katiba kila alipokuwa akitoa hoja zake, aliwataka Wazanzibari kuongelea U-Tanzania zaidi kwa kuwa Tanzania ni nchi moja tu na si vinginevyo.

Akipinga kuwepo kwa serikali moja, Mbunge kutoka Baraza la Wawakilishi, Bw. Aboubakar Khamis Bakar (CUF), alisema Wazanzibar hawako tayari kuwa na serikali moja.

Naye Mbunge wa Kilwa Kaskazini (CCM), Dk. Samson Mpanda, alihoji wanachokitaka hawa (akimaanisha Wazanzibari) kipo.

``Mimi sijui ni kitu gani lakini kipo wenyewe wanakijua,`` alisema na kuongeza kuwa wasioutaka Muungano walie tu.

Hata hivyo, Mbunge wa Konde (CUF), Bw. Ali Tarab Ali, alisema wakati umefika wa kuwashirikisha wananchi kwa kuibua mijadala waeleze wanataka aina gani ya muungano.

Mbunge wa Mchinga (CCM), Bw. Mudhihir Mudhihir, alisema mtafaruku unaojitokeza ndani ya Bunge Watanganyika na Wazanzibari ni wa kawaida na kuonya kuwa hakuna sababu ya kugombea majina ya Tanganyika na Zanzibar bali jukumu la wabunge ni kuangalia wananchi wa pande zote mbili.

Alisema muingiliano wa watu wa Bara na Visiwani ulianza tangu mwaka 1964 ndio maana ukienda Zanzibar unawakuta Wamakonde na Wanyamwezi na ukienda Bara unawakuta Wazanzibari.

Alisema kuvunjika kwa Utanganyika kumezuia ukanda na ukabila na kwamba ingekuwepo Tanganyika leo watu wangeshuhudia yanayotokea Zanzibar na Pemba.

Alisema dawa ya kero ya Muungano si vurugu bali ni kuelekea kwenye serikali moja.

Akichangia mjadala huo, Mbunge wa Jang`ombe (CCM), Bw. Mohamed Rajab Soud, alisema anapendekeza Ofisi ya Makamo wa Rais (Muungano) ibadilishwe iwe Kamati ya kushughulikia Muungano.

Naye Mbunge wa Kitibi (CCM), Bw. Adul Marombwa, alisema hata watu wa Bara wana kero zao za Muungano na kutoa mfano kuwa wakati Mbunge wa Bara anawapiga kura 70,000, wa Zanzibar anawapiga kura 5,000 lakini posho inayotolewa kwa wabunge ni ile ile haijali kama unawapiga kura wengi au wachache.

Bw. Hafidh Ali Tahir, Mbunge wa Dimani (CCM), alisema kuna watu wanaojifanya wana hatimiliki ya Muungano.

``Muungano una matatizo kwa sababu kuna mambo ya kudanganya danganya,`` alisema.

Wakitoa maoni yao kuhusu mjadala huo, mashuhuda wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, walisema wao wanaona Muungano ni mzuri na uendelee.

Bw. Rashid, alisema tofauti zinazoonekana sasa hivi, ni mawazo tu ya watu lakini wakikaa pamoja na kutafuta suluhu wataelewana.

Alisema hivi sasa wabunge wana uhuru wa kusema na kutoa maoni yao na kwamba elimu ni muhimu ya kujua mazingira ya Muungano huo.

``Mimi sio mwanasiasa, siwezi kushauri kitu, isipokuwa kwa upande wangu Muungano ni mzuri uendelee,`` alisema.

Mapema juzi, kambi ya upinzani ilisema kuna haja ya kufikiria upya wazo la kurejesha serikali ya Tanzania Bara.

Akiwasilisha hotuba ya Kambi ya Upinzani Bungeni, Waziri Kivuli wa wizara hiyo, Bi. Riziki Omar Juma, alisema Jamhuri ya Muungano wa Tanzania maana yake ni nchi mbili, Tanganyika na Zanzibar na kwamba katiba ya Tanzania ilipata pigo kubwa na hivyo kujeruhi mkataba wa Muungano.

``Pigo hilo ni mabadiliko ya 14 ya katiba yaliyomuondolea Rais wa Zanzibar nafasi ya kuwa Makamu wa Rais wa Tanzania,`` alisema.

Alisema leo hii, Rais wa Zanzibar ni waziri wa kawaida katika Serikali ya Muungano na kwamba makubaliano ya Muungano yamevunjwa na kupotoshwa kwa kiwango alichoita ``cha kupindukia``.

Akizungumzia akaunti ya pamoja ya fedha, kama mfano wa hoja yake, alisema Ibara ya 133 cha Katiba inasema akaunti hizo za pamoja zinawekwa fedha za serikali mbili kwa viwango vitakavyowekwa na Tume ya Pamoja ya Fedha.

``Kwa hiyo, kikatiba ni Serikali ya Muungano wa Tanzania na ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) zina wajibu wa kuchangia huduma na uendelezaji wa Muungano.

Tanzania Bara haichangii wala haiwajibiki kwa mujibu wa katiba,`` alisema na kuongeza: ``Ni hapa ndipo sasa unapoona kwamba kumbe kulitakiwa kuwepo na Serikali Tatu; Tanzania Bara, Muungano na SMZ.``

Kambi hiyo ilisema Bunge lina historia kuwa chombo kilichotumiwa na wabunge 55 wa Bara kudai Serikali ya Tanganyika.

``Ni maoni ya kambi kuwa hoja ile ilikuwa sahihi kama ilivyo sahihi leona itakavyokuwa sahihi kesho,`` alisema.

Aliongeza kuwa Tanzania inahitaji muungano wenye serikali tatu ili kuondoa manung`uniko yasiyokwisha, tume zisizokuwa na mwisho, vikao visivyokwisha, mambo alisema yanapoteza fedha za walipa kodi zinazowezesha kukaa na kujadili masuala ya maendeleo na mustakabali wa nchi.

``Tunajidanganya kuamini kuwa Tanzania Bara si serikali,`` alisema.

SOURCE: Nipashe

Tuma Maoni Yako
 
FMES,

..Kenya walibakiwa na mali nyingi zipi hizo?

..Makao Makuu ya EAC yalikuwa Arusha.

..pia kulikuwa na msuluhishi wa mgawanyo wa mali za EAC, akiitwa Dr.Victor Umbrich.

..kuna uwezekano Kenya walionekana na ahueni kwasababu uchumi wao ulikuwa imara from the beggining kwasababu za KIHISTORIA.

Kichuguu,

..kwa mtizamo wangu EAC was bound to collapse.

..Tanzania ilikuwa ikinung'unika kutokana na disparity ya maendeleo ya kiuchumi kati yake na wenzake. nitajaribu kukuletea chanzo cha habari hiyo.

..vilevile nadhani Wakenya walikuwa wanataka kuendeleza ile status quo ya kiuchumi iliyoachwa na mkoloni EAC.

..nina wasiwasi kwamba Muungano mpya tunaojaribu sasa hivi utakuwa na matatizo yaleyale ya kama ule uliovunjika.

NB:

..Nyerere pia alikuwa amezidi kumchokonoa Iddi Amini.

..baada ya Obote kupinduliwa akiwa ng'ambo, alikuja na kukaa ikulu ya Tanzania. Nyerere aliendelea kupeperusha bendera ya Raisi wa Uganda kwa kipindi chote Obote alichokaa ikulu ya dsm.

..pia Nyerere ali-host wakimbizi wengi tu waliokuwa wakimpinga Amini na kuwapa mafunzo na misaada ya kijeshi.

jokaKuu,
Ukweli ni kwamba Tanzania ndiyo ilikuwa common market kwa bidhaa zote zilizotengenezwa Kenya. Na sisi ndio tuliowafungulia mlango wa kuingia katika soko la Zambia na Malawi. Kulikuwa na maelewano kwamba kuweko aina fulani ya parity kati ya hizi nchi tatu, ndio maana mamlaka ya bandari yalihamishiwa Dar na shule ya kuendesha ndege ikahamishiwa Uganda. Lakini uchoyo wa Waingereza kwa kutumia watu kama vile Njonjo, zaidi ya tofauti baina ya Nyerere na Idi Amin, ulichangia zaidi kuivunja EAC. Unakumbuka wakati Nyerere alipofunga mpaka na Kenya nani alikuja kulalamika Tz? Alikuwa ni Mwingereza kwa sababu ya biashara zake za utalii.
 
Ni kweli, bado wapo hai.
Mkuu hapo sijui ni macho yangu hao walioshika vikapu ni wavulana......na hao akina mama wawili wa upande wa kushoto....naona wametajwa watatu tu......
 
Mkuu hapo sijui ni macho yangu hao walioshika vikapu ni wavulana......na hao akina mama wawili wa upande wa kushoto....naona wametajwa watatu tu......

Hapana, walioshika kikapu kile kuna mvulana mmoja na msichana mmoja: msichana yupo upande wa kulia wa Nyerere, wakati mvulana yupo upande wa kushoto wa Nyerere. Nadhani hawa ndio waliokuwa na miaka 16 wakati huo, halafu yule anayeonekana kama mama ambaye yuko mbele kabisa ya picha akiwa amevaa khanga yenye mapambo ya vibuyu ndiye yule mwanamke ambaye alikuwa na miaka 30 wakati huo.
 
Ni kweli Nkrumah hakutaka EA Federation ifanikiwe kwa sababu hii ingeua
hoja yake ya instant African federation. Hata katika kikao cha OAU 1963 walibishana sana na Mwalimu lakini at the end of the day Nkrumah akaishia kumpigia Mwalimu makofi kwa sababu ya nguvu za hoja zake kuhusu mwungano wa hatua kwa hatua. Lakini khasa khasa aliyeua mipango ya EA Federation alikuwa ni Mwingereza. Mwalimu alikuwa tayari kumpisha Kenyatta awe rais wa kwanza wa Federation. Obote naye alikuwa amekwishakubali. Lakini kwa sababu ya age Waingereza wakatambua kuwa eventually Mwalimu angekuwa kiongozi na hawakumwamini kwa sababu hawakuweza kumtumia kama walivyokuwa wanamtumia Kenyatta. Basi wakamshawishi Kenyatta kuwa asikubali, and that was the end of it.

Mkuu Jasusi,

Heshima mbele sana, nimewahi kuongea na mkulu mmoja aliyehudhuruia hicho kikako OAU, kule Adis ambako Nkurumah alikuwa amepania sana kuanzisha huo muungano wa Afrika na jinsi alivyokuwa akumuona Mwalimu kama ni tatizo katika hiyo ndoto yake ya kuwa rais wa kwanza wa huo muungano,

Nkurumah alifanya mambo mengi ya aibu sana kwenye hicho kikao, akijaribu kummshusha hadi Mwalimu, lakini Mwalimu hakuonyesha kuwa na wasi wasi naye wala kugombea hiyo power kama Nkurumah alivyofikiri, mkulu aliniambia kuwa katika hiyo kiu ya power Nkurumah alisafiri sana kuonana na Wareno, watawala wa Then Mozambique, katika kutafuta njia za kuiua EAA,

Anyways, ninakushukuru sana mkuu kwa kuweka habari hii sawa, kwa kweli tunakula elimu nzito sana hapa.
 
..Kenya walibakiwa na mali nyingi zipi hizo?

Ninaamini sana kuwa katika kuvunjika kwa EAA, Kenya walituzidi ujanja kwa sababu wao walishapanaga kuiua Jumuiya kabla hata sisi hatujajua nia yao, waliilimbikiza madeni kwa EAA, kwa makusudi ambayo baadaye yalihesabiwa kuwa ni madeni ya Jumuiya, Siku EAA inakufa ndege karibu zote zilikuwa nchini kwao, na hata Treni pia,

Ndio maana hata SADC ilipoanzishwa Tanzania ilituchukua muda sana kujiunga, kwa sababu ambazo tulizisema wazi kuwa baada ya kuumizwa kwenye EAA, hatuwezi kurukia rukia tena miungano au jumuiya, bila ya kuwa na uhakika na tunachofanya,

Tanzania tulikuja kushituka mwishoni sana kuwa tumeibiw ana wa-Kenya, ndio Rais Mwinyi, akamtuma Malecela ambaye alikuwa amewahi kuifanyia kazi sana EAA, kwenda kusimamia mgawanyo wa mali zake na madeni yake, lakini ilikuwa too late, wa-Kenya walikuwa wameshatuzidi akili.
 
Back
Top Bottom